Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
HADITHI CHACHE ZA IMAMU HUSAYN [a]

  1. Baadhi ya watu humwabudu Mwenyezi Mungu kwa matumaini (ya kupata Pepo); hiyo ni ibada iliyo kama ile ya wafanyi biashara; baadhi ya watu humwabudu Mwenyezi Mungu kwa sababu wanamwogopa; hiyo ni ibada ya watumwa; na wengine humwabudu kwa shukrani; hiyo ndio ibada ya mtu kamili.
  2. Kama kusingalikuwa na vitu vitatu mwana Adamu asingelitii kitu cho chote - umasikini, maradhi na kifo.
  3. Bahili (mbaya) sana ni yule anayefanya ubahili katika salamu.
  4. Usiwe mbaya kwa mtu asie (saidiwa) na mtu yeyote yule dhidi yako ila Mwenyezi Mungu.
  5. Jihadhari na vitendo vinavyotaka uombe msamaha; kwa kuwa mtu mwaminifu hafanyi maovu na mnafiki hufanya.
  6. Katika mafungu sabini ya neema, mafungu sitini na tisa ni ya yule aanzae kitu kizuri na (fungu) moja ni kwa wale wanaofuatia.
  7. Wakati maskini anapoitoa mhanga heshima yake katika kukuomba, ilinde heshima yako kwa kujizuia usimuudhi.
  8. Kosa kubwa Ia wafalme ni woga mbele ya adui, ukatili kwa wanyonge na kutokuwa na ukarimu.
  9. Kama utajiri wako hauwezi kukuhudumia utauhudumia wewe, hivyo usiuweke wote, kwa sababu hautakuweka mzima; utumie kabla haujakutumia.
  10. Yoyote yule aupokeaye ukarimu wako hukusaidia katika kuwa mtu bora.
  11. Ukweli ni heshima, uwongo ni kukata tamaa, siri ni dhamana, ujirani ni udugu; msaada ni urafiki, vitendo ni ujuzi, wema ni Ibada (kwa Mwenyezi Mungu), kunyamaza (kukaa kimya) ni pambo, ubahili ni umasikini, na huruma ni hekima, ukarimu ni ustawi.
  12. Kufa kwa heshima, ni bora kuliko kuishi kwa aibu.
  13. Wakati Imamu [a] alipoulizwa, kwa nini Mwenyezi Mungu aliamrisha watu kufunga, alijibu: "Ili kwamba tajiri ajue jinsi njaa ilivyo na aweze kuwa na huruma kwa maskini."
  14. Yavumilie mabaya kwa kuufuata Ukweli na vumilia kutengana na vitu uvipendavyo kwa kuitika mwito wa Akili.
  15. Mojawapo ya mambo yaliyo bora kwa mtu ni kuliacha lile jambo Iisilomhusu.
  16. Nyingi ya dhambi (azifanyazo mwanadamu) ni bora kuliko toba zao.
  17. Kutafuta elimu ni njia ya kuutambua Ukweli; upana wa maarifa ni ukamilishaji wa hekima; ubora huambatana na uchamungu; kutosheka ni usalama wa miili; ye yote yule akupendae atakuzuia (usifanye maovu) na adui yako atakushawishi kufanya maovu.
  18. Wanadamu ni watumwa wa Ulimwengu. Dini ni kama chakula kupendeza kwa ndimi zao na binadamu huishikilia (hiyo dini) kwa muda mrefu wa kadri itakavyowapa uwezo wa kujipatia riziki zao. Na kila wanapopatwa na tatizo lo lote lile, ni wachache sana wanaobakia katika dini.
  19. Kama mtu ye yote akimwabudu Mwenyezi Mungu kama ipasikavyo, Mwenyezi Mungu humpa zaidi ya mategemeo yake na mahitaji yake.