Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
(33). KUZINI NA MWANAMKE MKRISTO AU MYAHUDI

Bwana Muhammad bin Abu Bakr alimwandikia Imam Ali a.s. akimwulizia adhabu kwa mwanaume Muislamu kuzini pamoja na mwanamke mkristo au Myahudi.

Imam Ali a.s. alimjibu: "Iwapo mwanamme wa Kiislamu ameoa, basi arajimiwe, na iwapo bado hajaoa, achapwe viboko mia moja. Ama mwanamke wa kikristo au Kiyahudi, apelekwe uhamishoni.