Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
Mzuri sana Husaina

Kiitikio

Mzuri sana Husaina Wallahi na kuapia

Giza ilitueneya hapo ulipouliwa

  1. Ee mwema mwana amani, umekufa kishahidi
    Kunusuru hasa dini, ya wetu Mola wadudi
  2. Umejitolea muhanga, ewe mwana wa Hashima
    Ili kuhifadhi mwanga, Nuru kubwa ya Karima
  3. Kila lote la azizi, kwa Rabuna umetoa
    Bila kujali ajizi, hadi kufa kuokoa
  4. Wanao wenye tohara, Nduguzo waso kifani
    Masahaba we imara, umetoa uwanjani
  5. Kunusuru haki kweli, mfano wako kuiga
    Ujabali wenye dhili, kupambana bila woga
  6. Kuishi na madhalimu, kamwe neema hapana
    Ni kudhili jahanamu, maisha hayana maana