Ya Husaini Bin Ali niwe nikihadithia
Na Madina mji mwema, ndiko aliko zaliwa
Akiwapenda amini, kisha akiwa sifia
Na mwingine ni Hasani, Peponi wataingia
Subhana maulana, wote amewaridhia
Na siku yake yakini, ni jumanne sikia
Na siku ya saba mara, kamwakikiya Nabia
Kinywa kamsugulia, kwa mate alafunua
Sura kama ya Bashiri, kwani kamshabihia
Hajali nini na nini, ila dini ya jalia
Kuwa aende haraka, Iraqi kum-baiya
Aliwambia Husseini, Nao wakafuatia
Twakusihi kusikia, Huko hapatakufaa
Zao japo wafuasi, Japo na watoto pia
Bwana kwa hisani yako, Shika ninayo kwambia
Litalonipata nijema, Mimi nimesafi nia
Kwani nimesafi nia, Dini kuisimamia
Sio mimi niofie Niache kupaendea
Na watu wake sabini, Wote wakamfatia
Wengine arubaini, Kwa miguu ilikuwa
Mia moja khamsini, Ndio waliozidiya
Hawakumfata Husain, Hadi Iraqi sikiya
Na taabu iwafike, Kwa humo Karbala
Alizuiwa ajabu, Na maadui kutumia
Kambi akajipigia, Bwana Husseini sikia
Watoto wanalalama, Kwa vile wanaumia
Na maji yasitumike, Kunywewa na watu hawa
Watoto walalamika, Baba! Baba! twaumia
Husseini kukaribia, Maji yale kutumia
Kati yao alikuwa, Mtoto mdogo pia
Zeinabu binti Ali, Sanasana alilia
Akayafonza hakika, Mtoto kujimezeya
Kwa ala kulihali, Machozi maji yakawa
Muharamu ndio mara, Wakaanza kuuwawa
Alibaki ye na chake, Kijitoto kikilia
Hivyo maji angepata, Yangali msaidia
Na mtoto pale pale, Aliiaga dunia
Wakamuuwa hakika, Nae kaaga dunia
Hata wakawachukua, Banati zake Nabiya
Huko Kufa kupafika, Bila kuwahurumia
Gavana wake Yazidi, Yeye ndie alikiuwa
Kumuuwa mwenye haki, Kipenzi chake Nabia
Katu haiwezekani, Machozi kuyazuia
Kwa kipenzi msifika, Kinyume alofanyiwa
Kwa kupigania dini, Peponi wenda ingia
Allahu Mola wadudi, Shahidi kakwandikia
Na Husseini Muadhamu, Na walio bakiya
Na: Saidi Musa
ALLAMAH SAYYID SAEED AKHTAR RIZVI ASEMA: Husain (a.s.) wameuhurisha Uislamu kutokana na utumwa wa Wafalme na hivyo basi, wameuhifadhi kutokana na uharibifu daima. Wafalme watakuja, na Wafalme watakwenda, lakini Uislamu utadumu milele. Kwa Uislamu, majina matakatifu ya Hassan na Husain yataangaza milele. |