 |
Machozi yamiminika
|
Kwa Jina Ia Rahmani |
Na Muhammad Amini |
|
Na Anza nudhumuhini |
Kwa Machungu na Kuliya |
| |
|
|
Siku hizi za Ashura |
Twazitaja kila mara |
|
Kwa kubwa mno hasara |
Maadui walotiya |
| |
|
|
Kiswache cha tuumiza |
Na roho kutuunguza |
|
Hatuwezi kunyamaza |
Mashingo kuvumiliya |
| |
|
|
Twadhihirisha Majonzi |
Kwa Imamu na kipenzi |
|
Na nyoyo zina simanzi |
Kwa haya yalotokea |
| |
|
|
Twakumbuka siku hini |
Ya vilio na huzuni |
|
Ya kuuwawa Huseini |
Mjukuu wa Nabiya |
| |
|
|
Wallahi Tunakatika |
Machozi ya miminika |
|
Mitilizi inashuka |
Hatuna budi kuliya |
| |
|
|
Huseini kudhulumiwa |
Kwa machungu kuuliwa |
|
Kanyimwa maji kupewa |
Yeye na wake dhuriya |
| |
|
|
Hata watoto wachanga |
Wasibali kuwanyonga |
|
Kwa mishale kuwadunga |
Na maji kuwazuwiya |
| |
|
|
Wakamchinja Huseini |
Bila kite na imani |
|
Mjukuu wa Amini |
Pasina kuzingatiya |
| |
|
|
Na kicha kukitundika |
Kwa shangwe wakizunguka |
|
Kwa mizozo na dhihaka |
Kwa kipenzi cha Nabiya |
| |
|
|
Tuliye kiliyo gani |
Tudhihirishe Imani |
|
Kwa kiongozi wa dini |
Huyu walo tuuliya |
| |
|
|
Walomuuwa Imamu |
Wakashika yake damu |
|
Hao ndio madhalimu |
Tarikhi inatwambiya |
| |
|
|
Bila shaka yupeponi |
Yeye na tumwa Amini |
|
Owe nao makhaini |
Huseini kutuuliya |
| |
|
|
Kula alo muumini |
Atajawa na huzuni |
|
Kwa kifo chake Huseini |
Kipenzi cha Hashimiya |
| |
|
|
Na mengi tukiyaeleza |
Maovu ya kuchukiza |
|
Ya akili kushangaza |
Na moyo kutosheya |
| |
|
|
Tumefika kikomoni |
Tushukuru Manani |
|
Atupe nyingi Imani |
Ya dini kusimamiya |
| |
|
|
Muliyoko Hadhirani |
Amina kikieni |
|
Rabi atiye auni |
Dini kuipiganiya |
Umetungwa na:
Sheikh Ahmed Sheikh Nabhany
P.O. Box 86876
Mombasa, Kenya
|