 |
Hussein Amefariki
|
Hakika ni ujahili |
Uovu na ukatili |
|
Kuuwa pasi kujali |
Bila ya kuzingatia |
| |
|
|
Asikiyae Hakika |
Moyo utasikitika |
|
Ma machozi yatatoka |
Bila yakufikiria |
| |
|
|
Kwa huyu mtoto wake |
Hussein kina chake |
|
Muda kiu imshike |
Maji akihitajia |
| |
|
|
Kufika kwa makafiri |
Hussein alopojiri |
|
Na mwana huyu saghiri |
Maji alimuombea |
| |
|
|
Maadui wasijibu |
Kwa kuwazidi ghadhabu |
|
Mmoja wao kajibu |
Mshale kuutumia |
| |
|
|
Jibu lake ni mshale |
Kumfunma mwana yule |
|
Akafia pale pale |
Kifo cha kukusudia |
| |
|
|
Hapo ndipo Hussein |
Kwa uchungu wamoyoni |
|
Akaingia vitani |
Bila tena kungojea |
| |
|
|
Hussein akapigana |
Kishujaa kukazana |
|
Akauwa wengi sana |
Kwa nguvu zake jalia |
| |
|
|
Naye mwisho kifo chake |
Afanyeje peke yake |
|
Akafa hali yu pweke |
Shahidi akajifia |
| |
|
|
Hussein amefariki |
Hali yukatika haki |
|
Na hao ni yao dhiki |
Walomtenda ubaya |
|