 |
Kwa Mwezi wa Muharram
|
Naanziliza kauli |
Kwa jina lake jalali |
|
Na Swalawati Rasul |
Na-ali zake pamoja |
| |
|
|
Mswiba ulo adhimu |
Kwa mwezi wa Muharramu |
|
Dhuriya zake Hashimu |
Karbala wakingiya |
| |
|
|
Hadithi imetuwambiya |
Rasuli ameuswiya |
|
Wapendwa wake dhuriya |
Kinyume wakatumiya |
| |
|
|
Umati walibadili |
Mahabba yao kwa Ali |
|
Ikawa ni kuwadhili |
Na maji kuwaziwiya |
| |
|
|
Yasitoshe walofanya |
Ya Mtume kuyakanya |
|
Dhuluma wakamuonya |
Vijana kumuuliya |
| |
|
|
Hawakujali hishima |
Ya Sayyidati Fatima |
|
Vijana waliye wema |
Wa Haidari Aliya |
| |
|
|
Sina budi nitalia |
Kukosa kuwatetea |
|
Iwe kwetu mazoweya |
Ashura ikingiliya |
| |
|
|
Hadithi walisahau |
Mapenzi wakadharau |
|
Wakawauwa na kiu |
Furati wakangaliya |
| |
|
|
Walikunwa Kauthari |
Maji mema ya fakhari |
|
Pamoja na Answari |
Dini waloitetea |
| |
|
|
Yalopita tayakidhi |
Kwa Tumwa nipate radhi |
|
Na kwa Mungu ni fawidhi |
Na Aya kiisomeya |
INNA LILLAHI WA INNA ILAIHI RAJEUN
Sharif Mohammed Ahmed Al-Huseini
Jomvu Station, Mombasa
|