 |
Husseini Mwana wa Ali
|
Naanziliza kwajina |
Lake yeye Subhana |
|
Mola asiye kijana |
Wala mke asiliye |
| |
|
|
Ndie watangu natangu |
Kabula ya ulimwengu |
|
Muumba nchi na mbingu |
Milele Atabakiya |
| |
|
|
Asie na mshirika |
Na wala hakuzalika |
|
Ameketi pasi shaka |
Enzie imetimiya |
| |
|
|
Sasa penda kuweleza |
Kisa kenye kuchukiza |
|
Na moyo nitaukaza |
Hadi mwisho kufikiya |
| |
|
|
Ni rafiki wa Rasuli |
Muhammadi mur sali |
|
Husseini mwana wa Ali |
Na Fatuma Hashimiya |
| |
|
|
Kipenzi chake Nabiya |
Kuliko viumbe piya |
|
Uhai wake sikia |
Husseini akimwambiya |
| |
|
|
Wewe mtu wa peponi |
Huna shaka asilani |
|
Apendae kubaini |
Namtizame Husseini |
| |
|
|
Baada kufa Rasuli |
Muda ulipotawili |
|
Na Alii mjamali |
Mipoaga duniya |
| |
|
|
Kukazidi wasiwasi |
Ulimwengu ukahisi |
|
Pasiwe mwenye nafasi |
Matumbo kupiganiya |
| |
|
|
Baada yote kufika |
Na damu zikimwaika |
|
Waso haya wakatoka |
Vita wakaandaliya |
| |
|
|
Vikaandaliwa vita |
Na mengi mno matata |
|
Umbea nausalata |
Vigaro vikatimiya |
| |
|
|
Vigaro vya mahasidi |
Nyoyo zenye ufisadi |
|
Chini ya yeye yazidi |
Vitani wakaingia |
| |
|
|
Husseini yuko ndiani |
Kutaka ihami dini |
|
Kuwapinga mashetani |
Nakuituza duniya |
| |
|
|
Kwa moyo uso imani |
Majeshi yakawa kani |
|
Na damu waitamani |
YaHusseni na dhuriya |
| |
|
|
Wakawa wajikatakata |
Watakayo washapata |
|
Naimamu washamwita |
Mjini kwao kungiya |
| |
|
|
Habari hiyo hanayo |
Amekaza wake moyo |
|
Kumbe mambo sasa siyo |
Mauti yamngojea |
| |
|
|
Yunjiani enda zake |
Akaweta watu wake |
|
Waume na wanawake |
Na radhi akawiliya |
| |
|
|
Kuwajuza kwa yakini |
Hila zote kwa makini |
|
Pasipo matumaini |
Iraqi kufikiliya |
| |
|
|
Kawambiya kimbieni |
Atakae samahani |
|
Ela mini niwacheni |
Nimuhali kukimbiya |
| |
|
|
Baada yeye kukuli |
Wengi hawakuhimili |
|
Kama vile mafahali |
Nyumbani wakarudia |
| |
|
|
Akabakiya Husseini |
Na dhuriya wa nyumbani |
|
Na baadhi ikhiwani |
Akali wakasaliya |
| |
|
|
Alipofika Iraqi |
Jamii ya halaiki |
|
Furaha na kujinaki |
Jeshi likamwingilia |
| |
|
|
Akawa hana namna |
Pande zote amebanwa |
|
Pamwe na wake vijana |
Wapi watakimbiliya |
| |
|
|
Akasema kwa lafudhi |
Ka fasaha na mahadhi |
|
Adui kuwapa radhi |
Kuwatajia Jalia |
| |
|
|
Akawaonya mifano |
Hati zao za mkono |
|
Barua zilizo nono |
Walizo kumwandikia |
| |
|
|
Kayesha yote maneno |
Wala pasipo usono |
|
Yote yasiwe ni neno |
Yao wakashikilia |
| |
|
|
Wakamuonya adhabu |
Na nyingi mno sulubu |
|
Zimewaingia ghadhabu |
Bila sababu ya njia |
| |
|
|
Adui pasi kuchoka |
Wakamwandama M-maka |
|
Karbala wakafika |
Kusudi wa mwandamiya |
| |
|
|
Furati wakaushika |
Pasi nafasi kutoka |
|
Mto wakauzunguka |
Na maji wakijinyweya |
| |
|
|
Kiu ikazidi sana |
Najoto likawabana |
|
Imamu na wake wana |
Dhiki ikawadhidiya |
| |
|
|
Ikawa hakuna budi |
Dhiki imeshawazidi |
|
Wazee kwa auladi |
Roho zikiteketea |
| |
|
|
Kiu ilo kubwa mno |
Joto lisilo kifani |
|
Vijana wazi midomo |
Maji wanahitajiya |
| |
|
|
Maji wanywayo wanyua |
Punda farasi na kima |
|
Mjukuu wa Hashima |
Adui akawendeya |
| |
|
|
Akenda kwao salama |
Karibu roho kutema |
|
Abdallah anawana |
Kwa kiu kumzidiya |
| |
|
|
Kile kijana swaghiri |
Imamu wetu Amiri |
|
Tamaa hakukasiri |
Ya mali kumpatiya |
| |
|
|
Adui wasikubali |
Japo lau tone mbili |
|
Mahali wakaratili |
Pasi imani kuingiya |
| |
|
|
Mipo akikariri |
Imamu akihubiri |
|
Alipata takisiri |
Chembe wakamrushiya |
| |
|
|
Wakamba ha ndiyo maji |
Katu huyaonji maji |
|
Mnyweshe yamfereji |
Ni leo mtatubiya |
| |
|
|
Kijana kikalalama |
Chembe limeshika nyama |
|
Na damu mwili nzima |
Mikononi kikafiya |
| |
|
|
Mikononi mwa Imamu |
Yote ikajaa damu |
|
Na roho yake ghulamu |
Ikaiaga duniya |
| |
|
|
Katu wakamba adui |
Maji yetu situmai |
|
Mtayaona jamii |
Kanwani hamtotiya |
| |
|
|
Ukazidi ukaidi |
Kwa jeshi la mafisadi |
|
Ikawa hapana budi |
Roho zikiteketeya |
| |
|
|
Basi huu ndiyo mwanzo |
Wakazidisha mikazo |
|
Pasiwe hata pumbazo |
Vitoto vikiumiya |
| |
|
|
Kajaribu kwa upole |
Kuwaeleza walo pale |
|
Maji yote yako tele |
Japo tone kutumiya |
| |
|
|
Akenda huko karibu |
Kiu ilimughilibu |
|
Alipotaka jaribu |
Chembe kikamuingiya |
| |
|
|
Kikamwingia Imamu |
Chembe chao mahasimu |
|
Mdomoni kikadumu |
Na damu ikamweneya |
| |
|
|
Huku kiu imemshika |
Damu ikichirizika |
|
Msiba umemfika |
Hana pakukimbiliya |
| |
|
|
Kakishika kakizuwa |
Kwa nguvu akakitowa |
|
Kamshukuru Moliwa |
Muumba wa waja piya |
| |
|
|
Zikazidishwa sulubu |
Mno na nyingi taabu |
|
Rafikize wakaghibi |
Mauti kuyandamiya |
| |
|
|
Rafiki wakaanguka |
Imamu kumzunguka |
|
Na damu zikimwaika |
Akawa aogeleya |
| |
|
|
Katikati kwenye damu |
Adui wakakalimu |
|
Katu yako hayatimu |
Mauti yakungojea |
| |
|
|
Mauti yenye taabu |
Usumbufu na adhabu |
|
Yatakufika karibu |
Kaa ukiliadhania |
| |
|
|
Ni leo, leo ni leo |
Utaiona kwa leo |
|
Na wote hao watu |
Wote tutawalemeya |
| |
|
|
Kakalimu muungwana |
Kamshukuru Rabana |
|
Na Molawe kalingana |
Na dua kujiombeya |
| |
|
|
Akatamka Husseini |
Kamwambia Mola manani |
|
Kwako wewe shukrani |
Nyoyo zimefurahiya |
| |
|
|
Hatuna katu huzuni |
Kwa ulio yasaini |
|
Mauti twayatamani |
Kuliko kuangukia |
| |
|
|
Vita vikauma sana |
Pasipo kusemeyana |
|
Na Imamu akawana |
Pasi nyuma kurejeya |
| |
|
|
Lakini ifae nini |
Kwa adui elfeni |
|
Na ziyada ilondani |
Husseini akalegeya |
| |
|
|
Akalegeya kwa dhiki |
Aloikuta hilaki |
|
Asimpate rafiki |
Huruma kumuonea |
| |
|
|
Ukweli ulodhihiri |
Ikakabili ni shari |
|
Haikuweko ni siri |
Shida zikawachachiya |
| |
|
|
Kutamka kwa upole |
Pasipo nyingi kelele |
|
Sahibuze kuwambile |
Atakaye kukiribiya |
| |
|
|
Usiku huo gizani |
Kawambia kimbiyani |
|
Namimi radhi moyoni |
Na dua nawaombea |
| |
|
|
Jamii wakakataa |
Heri kwao kujifia |
|
Kuliko kuyakimbia |
Mauti wakaridhiya |
| |
|
|
Adui likadhihiri |
Moyo umetahayari |
|
Na upesi ikaswiri |
Imamu kumjiliya |
| |
|
|
Mtoto wake Husseini |
Naye alipobaini |
|
Karuka pasi makini |
Amie kumteteya |
| |
|
|
Pasi khofu wala shaka |
Adui akamshika |
|
Na maneno katamka |
Msihaya kamwambiya |
| |
|
|
Kamwambiya huna haya |
Bure wayatenda haya |
|
Utaikuta hizaya |
Mbele ya Mola jaliya |
| |
|
|
Adui likazunguka |
Mtoto akamshika |
|
Husseini akimtaka |
Kijana kumuusiya |
| |
|
|
Huku mepiga pambaja |
Na adui huko waja |
|
Na huku akiwapiga |
Mpaka mwisho kufikiya |
| |
|
|
Yakamzidi machungu |
Akamsabihi Mungu |
|
Akaaga Ulimwengu |
Mjukuu wa Nabiya |
| |
|
|
Ghafula akijiliwa |
Roho yake ikatwawa |
|
Adui lake Moliwa |
Imamu akamwendeya |
| |
|
|
Akamwendeya kwa dhati |
Akamendesha mauti |
|
Jiadui afiriti |
Dharuba kumwemezeya |
| |
|
|
Alipokufa Husseini |
Yalitimu thelathini |
|
Na tatu yaliyo ndani |
Mafumu yalowingiya |
| |
|
|
Kuna tena thethini |
Na nne mwake mwilini |
|
Panga za hao wahuni |
Mwilini zimesaliya |
| |
|
|
Mbali mengi majaraha |
Kuyataja ni karaha |
|
Moyo hauna furaha |
Kwa Imamu kujifiya |
| |
|
|
Ndio huo mwisho wake |
Hiki ndicho kisa chake |
|
Cha Imamu tusichoke |
Milele kujisomeya |
| |
|
|
Walipokwisha saini |
Adui wakabaini |
|
Sasa hii ni yakini |
Ushindi umewajiya |
| |
|
|
Wakendewa majohari |
Mabanati wa Amiri |
|
Matekani wakaswiri |
Huku wakiwachezeya |
| |
|
|
Pasi haya za uso |
Wakaona ni kifani |
|
Kuwatia taabani |
Jamaa zake Nabiya |
| |
|
|
Wakazidisha jeuri |
Wala pasipo na siri |
|
Na kichwa chake Amiri |
Fumoni wakakitiya |
| |
|
|
Huku wakikichezeya |
Na huku wakiimbiya |
|
Pasi imani kuwaingia |
Wote wamefurahiya |
| |
|
|
Njiani walikipita |
Nyoyo zao mezipata |
|
Zimekwisha jaa vita |
Shetwani amewaingia |
| |
|
|
Alipopata habari |
Kwa ambayo yamejiri |
|
Yazidi akaamuri |
Ili kwehwa kumwiliya |
| |
|
|
Furahani vibaraka |
Haraka kukipeleka |
|
Kwa Yazidi kikafika |
Meyowe kufurahiya |
| |
|
|
Akawa kukitozeya |
Na vijiti kukitiya |
|
Huku akimbiliya |
Chini kukiumbiriya |
| |
|
|
Msihaya wake dini |
Yazidi akatamani |
|
Uchunguwe wa moyoni |
Utatowa kwa duniya |
| |
|
|
Na huku akikigota |
Meno akiyaambata |
|
Uovu na usalata |
Hakuna alodhaniya |
| |
|
|
Ajabu hii ajabu |
Kwa kijanache swahibu |
|
Kumfikiya ikabu |
Wala pasipo hatiya |
| |
|
|
Muili ukiwa mbali |
Kijana cha Murisali |
|
Wakawachiwa mahuli |
Na nyama kukitezeya |
| |
|
|
Basi haya ni mauti |
Walotenda asherati |
|
Lakini kwao laiti |
Milele wamejutiya |
| |
|
|
Walitenda pasi haya |
Dini kutotegemeya |
|
Ya Mola kuyachezeya |
Pasi nyuma kurejeya |
| |
|
|
Yapasa tuyalilie |
Mauti yake Husseini |
|
Islamu natulie |
Kwa kifo chake Husseini |
| |
|
|
Hapa napenda kukoma |
Hadithie kuisoma |
|
Bali mengi sikusema |
Dhiki nikiisikiya |
| |
|
|
Kisomoni waungwana |
Majumbani na vijana |
|
Mpate jua maana |
Mambo yaliyo tukiya |
| |
|
|
Yatupasa Isilamu |
Machozi hadi ya damu |
|
Kumliliya Imamu |
Kwetu imetupasiya |
| |
|
|
Rabi atamtukuza |
Peponi kum-bakiza |
|
Kuzidi akimjaza |
Neema kumshushiya |
| |
|
|
Hapa naweka kalamu |
Nimefikiya makamu |
|
Wala mbele siyo tamu |
Hapa nitakomeleya |
YAPASA TUYALILIE MAUTI YAKE HUSSEIN
Na: Masoud Abdallali Muh'd,
Mombasa - Kenya
IMAM SHAFII ASEMA:
- Hussein! aliuliwa shidi pasi na makosa yoyote na kanzu yake ikatapakazwa wekundu.
- Ikiwa dhambi zangu ni kuwapenda watoto wa Mtume Mohammad (s.a.w.) basi ni dhambi ambazo sitatubiya.
- Kwa sababu ya Ahlil-Beit wa Mtume (s.a.w.) Ulimwengu mzima ulitetema na majabali na milima ilikaribia kuyeyuka.
- Ni nani atakayemfikishia Hussein ujumbe wangu na hata kama nyoyo zatukia?
|