Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
SIFA ZA IMAM HASSAN NA IMAM HUSAIN (A.S.)

Nawapa na taarifa

Japo kuwa walikufa

Walikuwa wana sifa

Njema ilotimilia

   

Walikuwa watukufu

Tena ni waaminifu

Walo na njema sharafu

Alowajazi Jalia

   

Walikuwa Maimamu

Kuongoza Isilamu

Mashujaa walotimu

Dini kuipigania

   

Walikuwa watu wema

Vijana wenye heshima

Akiwapenda Hashima

Wajukuu wa Nabiya

   

Walikuwa wenye dini

Maovu hawathamini

Na nyingi mno imani

Nyoyoni ilowangia

   

Walikuwa na huruma

Isilamu wenye hima

Toka kwa watu wazima

Na vijana wote pia

   

Walikuwa wasifika

Duniani kutukuka

Tena waliyoumbia

Kwa uzuri na tabia

   

Walikuwa makarimu

Huwezi kuwalaumu

Kisha ni wenye ilimu

Ya dini na ya dunia

   

Walikuwa wafalume

Wajukuu wa Mtume

Mashujaa wenye tume

Vitani kushambulia

   

Sifa zao ni kathiri

Tena zote ni nzuri

Wala hazina akhiri

Wallahi zimezidia