Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
7. Marwan Ibn al-Hakam

Baba yake aitwaye Hakam alifukuzwa mjini Madina na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ambaye alimwita "guruguru mwana wa guruguru". Mwenye Isti'ab imeelezwa hivi:

"Ayisha alisemo. "Ewe Marwan! Ninashuhudia ya kwamba Mtume alimlaani baba yako ulipokuwo (bado u mbegu za uzazi) mwenye kiuno chake (hivyo basi wewe nawe umo kwenye laana hiyo)."

Marwan alikuwa na kawaida ya kumlami Amiirul Mu'minnin Ali (a.s.) mbele ya Imamu Hassan (a.s.) na akamzuia Imamu Hassan (a.s.) asizikwe karibu na kaburi la babu yake Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Walid (gavana wa Yazid mjini Madina wakati ule) alipomwita Imamu Husayn (a.s.) kula kiapo cha utii kwa Yazid na Imamu (a.s.) akaamua kuwa jambo hilo liahirishwe hadi siku ifuatayo, ni huyu Marwan ibn Hakam aliyemwambia Walid kuwa kama atamwachia Imamu (a.s.) aende, katu hataweza tena kumkamata na akamhimiza amwue Imamu (a.s.) pale pale. Huyu Marwan aliyefukuzwa mjini Madina na akafahamika kwa majina ya "Mfukuzwa wa Mtume (s.a.w.w.)" na "guruguru mwana wa guruguru" na aliyemshawishi gavana wa mjini Madina kumwuua Imamu Husayn (a.s.), alipandishwa cheo hadi kukifikia cheo cha Ukhalifa na akawa anazungumziwa kuwa yu mpokeaji Ahadithi wa kuheshimika. Kitabu kiitwacho Taqribut Tahdhib kinaandika hivi:

"Marwan aliushika Ukhalifa mnamo mwaka wa 64 Hijiriya."

Kwenye kitabu kiitwacho Tahdhibut Tahdhib imeandikwa hivi:-

"Marwan ibn Hakam amepokea Ahadith kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ingawa inadhihirika wazi wazi kuwa katu hakuzisikia hadithi hizo moja kwo moja kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) mwenyewe. Vile vile amepokea Ahadithi kutoka kwa 'Uthman na Ali (a.s.) na Zaidi bin Thabit, na Abu Huraira, na Bushra binti Safwan na Abdulrahman bin Aswad bin Abd Yaghuth. Na mwanawe 'Abdul Malik na Sahl bin Sa'd Sa'idy (ambaye yu mtu mzima kuliko Marwan), Sa'id ibn Musayyab, Urwah bin Zubair, Abu Bakr bin Abdulrahman bin Harith, Ubaidullah bin 'Abdullah, bin 'Utbah Mujahid na Abu Sufyan (Mawla wa Ibn Abi Ahmad) wamepokea Ahadith kutoka kwake. Marwan alikuwa ni Katibu wa Khalifa 'Uthman bin Affan na mwenye utawala wa Mu'awiya alifanywa gavana wa Madina. Baada ya kufariki dunia kwa Mu'awiya bin Yazid bin Mu'awiya watu walikula kiapo cha utii kwa Ukhalifa wake. 'Urwah bin Zubair alisema kuwa Marwan hatiliwi shaka kwenye mapokezi yake."

Mtu ahitaji kusema mengi zaidi baada ya kuiona hiyo orodha ndefu ya watu waliopokea Ahadith kutoka kwa mtu huyu? Haishangazi kumwona mtu huyu akizipamba kurasa za Sahih Bukhari, Sahih Muslim, na Sunan Abi Dawuud