Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
9. Dhahhaka bin Qais na Ziad bin Sumaiyya n.k.

Zaidi ya hapo Dhahhak bin Qais na Ziad bin Sumaiyya na wengineo waliokuwa na uhusiano maalum na Yazid ni miongoni mwa wale ambao mapokezi yao yanahesabiwa na Mawahhabiya kuwa ni yenye kutegemeka.

Mpaka hapo tumetoa upande nimoja wa picha hii. Upande mwingine wa picha hii ni wa yule mtu ambaye kwa kusukumwa na nguvu ya huba yake kwa Ahlul Bayt (a.s.) aliwakamata wale waliomchinja Imamu Husayn (a.s.) na akawaua, anatukanwa na kulaumiwa. Hivyo basi, Mukhtar ibn Abu 'Ubaidah Thaqafi Rahmatullahi Alaih) anatukanwa kama ifuatavyo:

"Mukhtar ibn Ubaidah alikuwa mwongo mkubwa. Haifai kuyakubali mapokezi yake yoyote ya Ahadith kwa kuwa sio tu kwomba alijipoteza, bali vile vile alijaribu kuwapoteza watu. Alidai kwamba Jibrili alimjia. Mukhtar yu mwovu kama Hajjal au yu sawa na yeye. Inasemekana kwamba yeye yu mwongo ambaye Hadith ya Mtume ilimzungumzia kwamba kutokana na kabila la Thaqaf atajitokeza mtu mwongo na mchochezi. Hadithi hii imo kwenye Sahih Muslim" (Taarifa hii imechukuliwa kutoka kitabu Lisanul Mizan).

Maelezo haya yanaweza kumfanya mtu kufikiria kwamba pengine Bwana Mukhtar alikuwa na tabia za namna hiyo hasa na hivyo Ulama wa Rijal wakamfanyia upinzani. Lakini tunapoyatazama maelezo yaliyomo kwenye Isti'ab tunaona kwamba chuki yote hii inatokana na kwamba Bwana Mukhtar aliwaangamiza wauaji wa Husayn (a.s.). Hii ndio sababu iliyowafanya wale walioyachukia matendo yake walitwae rungu na kumsema kwa maneno ya uovu. Hicho kitabu kiitwacho Isti'ab kimeandika hivi:

"Mukhtar alidai kwamba katika kuilipizia kisasi damu ya Husayn (a.s.) alikuwa yu mjumbe wa Muhammad ibn Hanafiyyah. Hivyo akaomba msaada wa Ibrahim ibn Malik Ashtar na akawarukia wauaji wa Imamu Husayn (a.s.) na akawaua. Allah aliwafanya wengi wa wauaji wa Husayn (a.s.) kufa mikononi mwa Mukhtar; na ni kwa amri yake kuwa 'Ubaidullah ibn Ziad aliuawa na Ibrahim. Hii ndio sababu kwamba Waislamu wengi wanampenda na wale wasiozipenda itikadi zake humtukana na kumtusi."

Kwa kauli nyingine ni kuwa kiini cha maelezo haya ni kwamba wafuasi na wapenzi wa wauaji wa Imamu Husayn (a.s.) humtukana Bwana Mukhtar.

Kutokana na maelezo hayo hapo juu ni rahisi kuamua kuwa, Mawahhabiya huwatukuza wauaji wa Imamu Husayn (a.s.). Kila kiongozi wajeshi hili la wauaji amezipamba kurasa za Sihah. Wengi wao wamepewa vyeo vya kuwa wakweli, ukweli na kukubalika. Kwa upande mwingine, licha ya kuwa wauaji, wachochezi wa mauaji ya Imamu Husayn (a.s.) na kufukuzwa na Mtukufu Mtume wamefanywa kuwa Makhalifa. Kwa upande mwmgine, mwenye kuilipizia kisasi damu ya Imamu Husayn (a.s.) kama vile Bwana Mukhtar Thaqafi anashu-tumiwa kwa kupotoka na kuwa-poteza watu na kuwa mwongo na kuwa mwovu zaidi ya Hajjaj - na Allah anajua ni yapi mengineyo wayasemayo juu yake.