Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
SWALI LA TATU

Kwa Mashia, Yazid na wauaji wengine wa Imamu Husayn (a.s.) ni Kafir na hivyo wamejitakia laana ya Allah iwe juu yao na juu ya wote wenye kuyafurahia matendo yao; na huwahesabu wote hao kuwa ni watu wa motoni. Mahanafiya, Mashafii na Mahambaliya wapenda haki nao humchukia Yazid na wauaji wengine wenye kustahili karipio kali zaidi.

Lakini Mawahhabiya na Manasibi huwapinga Mashia waziwazi kwa kuwa wanawahesabu wauaji wa Imamu Husayn (a.s) kuwa ni wenye kustahili sifa. Miongoni mwa wauaji hawa, baadhi yao waliweza hata kujinyakulia Ukhalifa na wengine wakapewa majina ya heshima kama vile "Saduq" (Mkweli zaidi) na "Thiqah" (Mwaminifu), na watu kadhaa miongoni mwao wamekuwa wapokeaji wa Ahadith za Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwenye "Sihah Sitta" na kutokana na maelezo yao watu hujichukulia hukumu za kidini.

Sasa tutawataja hapa chini kila mmoja wao kwa jina na kumwonyesha alikuwa ni mtu wa aina gani.