Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
2. Shimr Ibn Dhil-Jaushan

Huyu ndiye mchinjaji hasa wa Imamu Husayn (a.s.). Ibn Ziad alimfanya mtu huyu kuwa kapteni wa jeshi madhubuti la watu elfu nne, na akampa maagizo ya kwamba iwapo 'Umar Ibn Sa'd atasitasita kumshambulia Imamu Husayn (a.s.) basi amnyang'anye uamiri-jeshi wa jeshi hilo na auchukue yeye. Huyu naye yu kiongozi wa wapokeaji wa Ahadithi wa Mawahhabiya. Kwenye kitabu kiitwacho "Tahdibut Tahdhib" imeandikwa hivi:

"Shimr ibn Dhil-Jaushan Abu Nabighah Dhubyani amepokea Ahadithi kutoka kwa baba yake, na kutoka kwa Shamr amepokea (Ahadithi hizo) Abu Ishaq Sabi'i."

Hayo yameandikwa kwenye kitabu kiitwacho Mizanul I'tidal na kwenye kitabu kingine kiitwacho Isti'ab. Kwenye Tadhkiratul Hufadh inaelezwa zaidi hivi:

"Na kutoka kwake amepokea A'mash na Shu'bah na Thawri na Israil na Abul Ahwas na Abu Bakr Ibn Ayyash na Sufyan bin Ayniyah."

Maelezo ya Abu Ishaq Sabi'i (ambayo ndani yake ameeleza udhuru wa kutomlaumu Shimr) ni haya yafuatayo:-

"Shimr alikuwa akisali pamoja nasi, na alikuwa kila mara akisema: Ee Allah! Unajua kuwa mimi ni mtu mtukufu, basi unisamehe."

Abu Ishaq anasema: "Nilimwuliza: Ni vipi Allah Angeweza kukusamehe wakati wewe umeyasaidia mauaji ya mwana wa Mtume? Shimr akajibu: Ole wako! Ningefanyaje? Viongozi wetu wametuamrisha kufanya hivyo nasi hatukuwaasi! Kama tungewaasi, hali zetu zingekuwa mbaya zaidi kuliko kumwua Husayn."