Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
3. Hasin ibn Numayr

Mlaaniwa huyu aliongoza jeshi la askari elfu nne huko Karbala. Baada ya kuuawa kwa Bwana Muslim Ibn Aqiil, Ibn Ziad alimfanya Hasin ibn Numayr kuwa kiongozi wa jeshi la kufunga mipaka ya Kufah ili kuweza kumkamata Imamu Husayn (a.s.) atakapokuja huko. Hurr alikuwa na afisa wa chini yake. Baada ya masaibu ya Karbala, wakati wa kuzingirwa kwa mji wa Madina na Harram, alikuwa kiongozi wa Jeshi sababu kiongozi wa jeshi hilo aliyeitwa Muslim ibn Uqbah alikuwa mgonjwa; baada ya kuuteka mji wa Madina Muslim ibn Uqbah alipofariki, akawa kiongozi hasa wa jeshi lililouzingira mji wa Makkah. Yeye nae yu mpokeaji wa Ahadith kwenye Sihah. Kwenye kitabu kiitwacho Tahdhibat Tahdib imeelezwa hivi:

"Mwenye mazingira ya mji wa Madina alikuwa mmoja wa maamiri-jeshi wa Yazid ibn Mu'awiyah. Kisha mwenye kumzingira Ibn Zubair alikuwa amiri jeshi wa jeshi la Yazid. Yeye yu mtu maarufu".

Kwenye Mizanul-Itidal imeandikwa kuwa yeye kapokea Ahadithi chache tu, lakini halaumiwi kwa kuwa mmoja wa wauaji wa Imam Husayn (a.s.). Zaidi ya hapo, Bukhari, Abu Dawuud, Tirmidhi, na Nasai wapokeaji wanne maarufu sana wamezinukuu kwa uhakika Ahadithi zake kwenye vitabu vyao ambavyo ni miongoni mwa Sihah Sitta ambavyo Ahadithi zote zilizoandikwa humo zahesabiwa kuwa ni sahihi kabisa.