Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
POTE LENYE KUOKOKA

Amesema Mtukufu Mtume (s.a.w.) "Watafarakana umma wangu makundi sabini na tatu, kundi moja tu kati ya hayo litaokoka, na yaliyobaki yatatiwa motoni. Ali akauliza: "Ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu! Kundi gani litakalookoka? Mtume (s.a.w.) akajibu: "Wewe na watu wako".

Taz: Ithbatul Hudat J. 2 Uk. 260

Mfarakano kwa mara ya kwanza ulitokea kwa Waislamu pale tu alipofariki Mtume Muhammad (s.a.w.). Mtume (s.a.w.) kabla ya kufariki dunia, aliweka sera kamili ya uongozi katika Uislamu. Iliposhuka Aya: "Hakika wale walioamini na wakatenda mema, basi hao ndio wema kushinda viumbe vyote" 98:7. Mtume (s.a.w.) akamwambia Ali: "Wewe Ali na kundi (pote) lako".

Taz: Tafsirut Tabari J. 30 Uk. 171

Mtume (s.a.w.) amesema: "Ali yu pamoja na Qur'an, na Qur'an ipamoja na Mi, hawataachana mpaka wanifikie katika Haudh".

Taz: Faidhul Qadir J. 4 Uk. 358

Musnad Ahmad J. 5 Uk. 31

Alfat'hul Kabir J. 2 Uk.21

Tarikhul Khulafai Uk. 174

Majmauz Zawaid J. 9 Uk. 134

Kifanyatut Talibi Uk. 399

Asnal matalibi Uk 136

Mtume (s.a.w) amesema: "Mimi ninakuachieni vizito viwili ambavyo mkishikamana navyo hamtapotea baada yangu, Qur'an na Ahlul Bayt wangu, viwili hivi havitaachana mpaka vitakaponifikia katika Haudh".

Taz: Tafsir ibn Kathir J. 4 Uk. 122

Tafsir ul Kazin J. 1 Uk. 4

Tarikhu Bughdad J. 8 Uk. 442

Sahihi Muslim J. 4 Uk. 1873

Jamiul Usul J. 1 Uk. 187

Albidayatu Wannihaya J. 7 Uk. 362

Majmauz Zawaid J. 9 Uk. 163

Musnad Ahmad J. 2 Uk. 17-26

Al Mustadrak J. 4 Uk. 109

Imam Ali (a.s.) mmoja katika Ahlul Bayt wa Mtume (s.a.w.) tazama pale iliposhuka Ayatut Tat'hir: "Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu watu wa nyumba (ya Mtume) na (anataka) kukutakaseni sana sana" 33:33. Na mke wa Mtume (s.a.w.) (Ummu Salama) alipotaka kuingia katika nguo hiyo Mtume akamzuia!!

Taz: Sahihi Muslim J. 4 Uk. 127

Sahihi Tirmidhi J. 4 Uk. 304

Alkhasais Uk. 4

Tarikh Bughdad J. 9 Uk. 126

Al' Isaba J. 1 Uk. 27

Usudul Ghaba J. 5 Uk. 521

Al Mustadrak J. 2 Uk. 416

Tafsirut Tabari J. 22 Uk. 5-7

Tafsirul Khazin J. 5 Uk. 259

Addurrul Manthur J. 5 Uk. 198