Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
HADITHI ZA IMAMU MUHAMMAD TAQI [a]

  1. Yeyote yule amsaidiaye mshari (kwa namna yoyote ile) katika vitendo vyake ni mshiriki wake.
  2. Siku ya "Uadilifu" (mdhuIumiwa kulipiziwa kisasi) ni ngumu zaidi kwa mshari (huyo aliyedhulumu) kuliko siku aliyomfanyia shari mdhulumiwa.
  3. Mtu afanyaye kitu bila ya elimu ya kukifanyia kitu hicho, hukiharibu badala ya kukitengeneza.
  4. Uchamungu huleta heshima, kujifunza ni hazina, ukimya humpa mtu hekima.
  5. Hakuna kitu kibaya kwa dini kupita 'bid'at' (uzushi wenye maana mbaya) na hakuna kitu kiharibucho heshima kama tamaa.
  6. Kuwatengeneza raia hutokana na mtawala na dua huzuia maovu.
  7. Anayetumia maneno mabaya hulipwa maneno mabaya na afanyaye jambo bila akili huumia.
  8. Mkarimu huwa mwangalifu kwa ukarimu wake kuliko wale wafaidikao kwa ukarimu huo. Ukarimu wake humlipa na humletea heshima na utukufu.
  9. Yeyote ategemeaye upendeleo fulani toka kwa mtu mwingine pia humuogopa mtu huyo. Na yeyote asiyekielewa kitu fulani hukiona ni kibaya.
  10. Kuachwa kwanza (kutoadhibiwa mara moja) ni kitu kipoteacho mara moja tu.
  11. Anayetaka kuokoka lazima awe na moyo wa uvumilivu katika shida.
  12. Ampandaye farasi wa uvumilivu huipata barabara ya kwendea kwenye uwanja wa ushindi.
  13. Vitu vinne humuongoza mtu kwenye matendo mazuri, afya, utajiri, elimu na Neema za Mwenyezi Mungu.
  14. Kumwamini Mwenyezi Mungu ni kuokokana na maovu yote na ni kinga kutokana na kila adui.