 |
HADITHI ZA IMAMU MUHAMMAD TAQI [a]
- Yeyote yule amsaidiaye mshari (kwa namna yoyote ile) katika vitendo vyake ni mshiriki wake.
- Siku ya "Uadilifu" (mdhuIumiwa kulipiziwa kisasi) ni ngumu zaidi kwa mshari (huyo aliyedhulumu) kuliko siku aliyomfanyia shari mdhulumiwa.
- Mtu afanyaye kitu bila ya elimu ya kukifanyia kitu hicho, hukiharibu badala ya kukitengeneza.
- Uchamungu huleta heshima, kujifunza ni hazina, ukimya humpa mtu hekima.
- Hakuna kitu kibaya kwa dini kupita 'bid'at' (uzushi wenye maana mbaya) na hakuna kitu kiharibucho heshima kama tamaa.
- Kuwatengeneza raia hutokana na mtawala na dua huzuia maovu.
- Anayetumia maneno mabaya hulipwa maneno mabaya na afanyaye jambo bila akili huumia.
- Mkarimu huwa mwangalifu kwa ukarimu wake kuliko wale wafaidikao kwa ukarimu huo. Ukarimu wake humlipa na humletea heshima na utukufu.
- Yeyote ategemeaye upendeleo fulani toka kwa mtu mwingine pia humuogopa mtu huyo. Na yeyote asiyekielewa kitu fulani hukiona ni kibaya.
- Kuachwa kwanza (kutoadhibiwa mara moja) ni kitu kipoteacho mara moja tu.
- Anayetaka kuokoka lazima awe na moyo wa uvumilivu katika shida.
- Ampandaye farasi wa uvumilivu huipata barabara ya kwendea kwenye uwanja wa ushindi.
- Vitu vinne humuongoza mtu kwenye matendo mazuri, afya, utajiri, elimu na Neema za Mwenyezi Mungu.
- Kumwamini Mwenyezi Mungu ni kuokokana na maovu yote na ni kinga kutokana na kila adui.
|