Subject Index 
Search
Announcements
Feedback
WAPINZANI WANYAMAZA

Hebu tuyaangalie maisha ya Mtume wa Islamu [s]. Tunaona kuwa katika umri wa ujana wake aliridhika kuwa na mke mmoja aliyekwishakuwa mjane mara mbili na mwenye umri mkubwa na wala (Mtume [s]) hafikirii mwanamke mwingine. Kisha tunaona kuwa, katika miaka 10 ya mwisho ya maisha yake, akiwa na umri wa zaidi ya miaka 50, akiwa katika uzee wake na akiwa amezungukwa na matatizo mgumu sana ya dola mpya ya Kiislamu, alianza kuoa wake wengi.

Hebu waulize waandishi hawa wa Kikristo, "kwa nini itukie hivi?"

Ni jibu gani la kihoja wapinzani hawa wawezalo kulitoa kwa swali zuri kama hili?

Je, si jambo gumu na mzigo mzito kuoa wajane na kuwatunza yatima? Je, lilikuwa jambo rahisi kwa mtu mwenye hekima kama Mtume Muhammad [s] kuoa wanawake wa maumbile mbali mbali, tabia na wa makabila tofauti na kati yao wakiwemo wanawake vijana mno ambao bado hawauelewa wajibu wa maisha?

Hebu natulifikirie jibu lifuatalo ambalo limeelezwa na Mwanahistoria wa nchi za magharibi Bwana Thomas Carlyle kuyajibu maswali hayo hapo juu, katika kitabu chake kiitwacho "Heroes and Heroes Worship" Yeye anasema kinyume na vile maadui wake Mtume [s] wanavyomshitaki. Anasema, "Muhammad hakuwa na tamea ya kiashiki, hivyo ulikuwa usingizio utokanao na chuki na hakika huu ni udhalimu mkubwa".

Bwana John Devenport anasema, "na, mtu anaweza kuuliza kama inawezekana kwa mtu mwenye tamaa za kimwili, wa nchi ambayo tabia ya kuoa wake wengi ilikuwa ni jambo la kawaida, na katika muda wa miaka hamsa-wa-ishirini ni ambaye yu mkubwe kuliko yeye mwenyewe kwa umri wa miaka kumi na mitano."