Baada ya kifo cha mke wake wakwanza Bibi Khadija [a] Mtume [s] alioa wanawake wafuatayo: (1) Saudah, (2) Ayisha, (3) Umus-Salamah bint Khuzaimah, (4) Zainabu Binti Jahash, (5) Ummu-Habibah (Ramla), (6) Mayimunah, (7) Zainab bint Umais, (8) Juwairiyah, (9) Safiyyah na (10) Khaulah binti Hakim. Hebu tuyechunguze matukio na hali zisizosababisha ndoa hizi kufungwa. Ukweli ni kuwa, tunaweza kusema kuwa ndoa hizi zilifungwa kwa moja au zaidi ya sababu hizi zifuatazo:
Kwa mfano Bibi Saudah (r.a.) alihamia Uhabeshi na huko mume wake alifariki, hivyo alikuwa hana msaidizi ye ypte. Wakati huo ambapo Mtume [s] naye alikuwa keshafiwa na mkewe wa kwanza Bibi Khadija [a], hivyo alimuoa Bibi Saudah (r.a.). Vivyo hivyo, Bibi Zainabu binti Khuzaim (r.a.) naye alikuwa mjane mwenye umri mkubwa ambaye baada ya kufiwa na mume wake alibaki katika hali ye umaskini, ingawa alikuwa mwenye tabia njema na aliyejulikana sana kwa jina la "Ummul-Masaakin (Mama wa maskini)". Mtume [s] alimuoa Bibi Zainab (r.a.) ili kuendeleza hadhi yake na baadaye Bibi huyu alifariki kwa uzee, miaka miwili tu tangu kuolewa na Mtume [s].
Kwa bahati mbaya, kwa sababu ya majivuno ya Bibi Zainab (r.a.) kuhusu ubora wa familia yake, Bwana Zaid hakuweza kuishi na mke huyo, ingawaje Mtume [s] aliwasihi ndoa yao iendelee. Tofauti hizo zilizaa talaka. Wakati huo, mtindo wa watoto wa kulea ulikuwa umekatazwa na Mwenyezi Mungu (Qur'ani 33:45). Kwa hiyo, Bwana Zaid (r.a.) alipomtaliki Bibi Zainab (r.a.), Mtume wa Islamu [s] kwa amri ya Mwenyezi Mungu, (Qur'ani 33:37) alimuoa Bibi Zainab (r.a.), na hivyo basi aliiulia mbali imani iliyokuwepo isemeyo kuwa watoto wa kulea walikuwa sawa na watoto wa kuzaa na kuwa wake au wajane wa watoto wa kulea walikuwa sawa na wakawana wa watoto wa kuzaa.
Mtume [s] alimuoa Bibi Ayesha bint Abu-Bakar (Abdul Kaabah au Abdallah bin Abi Quhaafah) kutoka katika kabila la Bani Taim, Bibi Hafsa (r.a.) binti Umar bin Khattab kutoka kabila la Adi, Bibi Ummu Habibah (r.a.) binti Abu Sufyani toka katika kabila la Umayya, Bibi Safiyyah (r.a.) binti Huaiy bin Akhtab wa kabila la Kiyahudi la Bani Nazir, na Bibi Mayimuunah (r.a.) kutoka kabila la Bani Makhzuum. Bibi Ummu-Habibah (r.a.) (Ramla) alikuwa mtoto wa Abu Sufyan wa kabila la Banu Umayya ambaye alikuwa adui mkubwa wa Mtume [s] na alipigana naye mara nyingi. Bibi Ummu Habibah (r.a.) baada ya kusilimu alikuwa katika hali mbaya sana kwani alikuwa ameachwa na mume wake wa kwanza (aliyeingia dini ya Kikristo huko Uhabashi) na wakati huo huo baba yake alikuwa adui mkubwa wa Uislamu. Mtume [s] alipomuona Bibi huyu katika hali ile, akiwa hana msaada wo wote toka kwa wazazi wake na mume wake kamtaliki, alimuoa kwa kumuonea huruma. Ndoa hii pia ilitowa mfano kwa watu wa Bani Umayya kuilegeza mioyo yao kwa dini ya Kiislamu. Bibi Safiyyah (r.a.) alikuwa mjane na binti wa Bwana Huaiy bin Akhtab, mmoja wa watemi wa kabila la Kiyahudi la Bani Nazir. Mateka wa kabila hili walipoachiliwa na Waislamu, Mtume [s] alimuoa Bibi Safiyyah (r.a.) kwa madhumuni ya kulinda hadhi ya bibi huyu na pia kwa kufanya hivyo Mtume [s] akajihusisha na moja ya makabila makubwa ya Kiyahudi ya wakati huo na kuyasogeza karibu na Islamu. Bibi Mayimuunah (r.a.) ambaye Mtume [s] alimuoa katika mwaka wa 7 baada ya Hijja, akiwa na umri wa miaka 51 na alitoka katika kabila maarufu sana la Bani-Makhzuum. Historia iliyoelezwa hapo juu, ya ndoa za Mtume [s] inaonyesha wazi umuhimu wa madhumuni hayo ya kuoa wanawake kadhaa. Si ngumu hata kidogo kuona kuwa hakuna hata ndoa moja ambayo madhumuni yake yalikuwa kuridhisha tamaa za kimwini za kibinafsi kama wasemavyo waandishi wa Kikristo wanaomlaumu Mtume [s] . Pia ni muhimu kukumbuka kuwa ndoa hizi zote, ila ile ya Bibi Ayesha (r.a.), zilifungwa na wanawake waliokuwa wajane, si mara moja tu bali mara mbili au tatu.
|