Sura Ya Hamsini Na Tano: Ar-Rahman
Ina Aya 78.
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.
الرَّحْمَٰنُ {1}
Mwingi wa Rehema.
عَلَّمَ الْقُرْآنَ {2}
Amefundisha Qur’an.
خَلَقَ الْإِنْسَانَ {3}
Amemuumba mtu,
عَلَّمَهُ الْبَيَانَ {4}
Akamfundisha ubainifu.
الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ بِحُسْبَانٍ {5}
Jua na mwezi ni kwa hisabu.
وَالنَّجْمُ وَالشَّجَرُ يَسْجُدَانِ {6}
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
وَالسَّمَاءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ الْمِيزَانَ {7}
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
أَلَّا تَطْغَوْا فِي الْمِيزَانِ {8}
Ili msidhulumu katika mizani.
وَأَقِيمُوا الْوَزْنَ بِالْقِسْطِ وَلَا تُخْسِرُوا الْمِيزَانَ {9}
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
وَالْأَرْضَ وَضَعَهَا لِلْأَنَامِ {10}
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
فِيهَا فَاكِهَةٌ وَالنَّخْلُ ذَاتُ الْأَكْمَامِ {11}
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
وَالْحَبُّ ذُو الْعَصْفِ وَالرَّيْحَانُ {12}
Na nafaka zenye makapi, na mrehani.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {13}
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu mnayoikanusha nyinyi wawili?