Al-Islam.org
Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org)

Home > Al-Kashif-Juzuu Ya Thalathini

Al-Kashif-Juzuu Ya Thalathini

  • 4050 views

Author(s):

  • Muhammad Jawad Mughniyya [1]

Publisher(s):

  • Al-Itrah Foundation [2]

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu waliojitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Get PDF [3] Get EPUB [4] Get MOBI [5]

Translator(s):

  • Hassan Ali Mwalupa [6]

Utangulizi Wa Mchapishaji

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu waliojitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Kama lilivyo jina la Tafsiri ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo.

Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyoviandika katika maudhui mbalimbali na hivyo kujipa­tia wasomaji wengi sana.

Msomi huyu, mwenye fikra huru na anayetetea kile anachokiamini, ni mtu mwenye mawazo mapana na kuyaangalia mambo kwa undani sana, kipaumbele chake ni katika maslahi ya umma huu na amejaribu sana kwen­da na wakati.

Sifa kubwa pekee ya mwanachuoni huyu ni kuwa yeye hakujihusisha sana na kung'ang'ania madhehebu fulani tu, labda hii yatokana na wadhifa wake wa ukadhi aliokuwa nao katika nchi ya Lebanon ambayo ina madhehebu mengi, ambapo sula la madhehebu ni nyeti nchini humo, hata hivyo yeye aliweza kuamua matatizo ya watu kwenye ofisi yake kulingana na madhe­hebu yao pale walipomwendea. Hiyo ilimsaidia sana hata kuweza kutoa kitabu kitwacho Al-Fiqh a'laa madhaahabil-khamsah (Fikhi ya madhehe­bu matano) yaani ya Hanafi, Maaliki, Shafi, Hambali na Shia (ambacho twataraji kitatoka kwa lugha ya kiswahili hivi karibuni Inshaallah).

Jambo lililotupa msukumo wa kukifasiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ni zile faida nyingi atakazozipata msomaji na kujua mambo mengi na ya ajabu yaliyo mapya kwake ambayo si rahisi kuyapata kwa wafasiri wengine.

Msomaji atapata faida katika fani za Sayansi, Siasa, Historia, Mashairi, visa vizuri, na Saikolojia miongoni mwa mengine; ndiyo maana msomaji atashangaa kidogo anapoisoma Tafsiri hii atakapoona mwandishi ame­wataja na kuwanukuu watu kama kina Mfalme Edward, wanasayansi kama kina Enstein, wasanii kama Charlie Champlin (Mchekeshaji maarufu), na wengineo, hali inayoifanya tafsiri hii kuwa ni ya kipekee kabisa.

Mtindo alioutumia mwandishi ni sahali uliokusudiwa watu wa tabaka mbalimbali, wanavyuoni na watu wa kawaida. Nia yetu ni kukigawanya kitabu hiki bure lakini tumelazimika kukiuza kwa bei nafuu ili kurudisha gharama za uchapishaji. Mwisho: Shukrani kubwa iwaendee bila ya kuwataja watu waliojitolea usiku na mchana, jopo la wafasiri, wahariri, wachapaji, waliotupa moyo na kutoa maoni yao na walioisimamia ili kuhakikisha kwamba kitabu kimem­fikia msomaji.

Makosa Ya Chapa

Sikumbuki kama nimewahi kusoma kitabu kilichotoka kupigwa chapa, cha zamani au cha sasa, bila ya kukuta makosa ya chapa. Nafikiri sitasoma kitabu kisichokuwa hivyo. Nimejaribu sana kuliepuka hilo katika tungo zangu, lakini sikufanikiwa.

Nilikuwa sifikirii kama ninaweza kuona makosa haya katika maandishi ya msahafu mtukufu, kama yale yaliyo katika baadhi ya chapa; kwa mfano neno yabswutu kwa swad, badala ya yabsutu kwa sin, na katika chapa ya Tafsir Arrazi ya Misr ya mwaka 1935, Sura ya (2:146). Imeandikwa a Ya'alamuun, (hawajui) badala ya Ya'alamuun (wanajua). Mfano wa makosa haya hausameheki.

Katika Tafsir Al-anar, chapa ya Pili, sura (5:212), imeandikwa Fawqahum ila yawmil qiyama badala ya Fawqahum yawamal qiyama. Hatuwezi kusema kosa hili ni kubwa zaidi kuliko lile. Lakini mkosaji atatuletea udhuru kwa msemo mashuhuri huko kwetu Jabal amil 'Makosa ya chapa.' Katika Tafsiri Majmau chapa ya Urfan, Sura (46:15), imeandikwa: Hatta idha balagha arbai' na sanah badala ya: Hatta idha balagha ashuddahu arbai ' na sanah!

Kusema hivi sio kama ninajitetea kutokana na makosa ya chapa atakayoy­akuta msomaji katika kitabu hiki, ijapokuwa naomba msamaha kama lita­tokea hili, lakini makusudio yangu hasa ni kumwambia yule atakayefungua macho yake kwenye makosa ya matamko na kuufungia macho uzuri wa maana. Vilevile ninamwambia yule ambaye siku moja aliniambia: "Vitabu vyako vimejaa makosa ya chapa.” Kama kwamba hakuna kitu chochote katika vitabu hivyo isipokuwa makosa ya chapa tu. Wote hao ninawaam­bia: Mungu awasamehe na aniongoze mimi na nyinyi.

Vyovyote iwavyo, mimi ninaomba msamaha kutokana na makosa ya kifikra na ya chapa. Anasema Amirul Muminiin (a.s): "Watu wote ni wapungufu wenye kuchanganyikiwa, isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mwenyezi Mungu." Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye jukumu la kunikubalia yale niliyoyapatia na kunisamehe niliyakosea, kwa jaha ya Mtume na kizazi chake, ziwashukie rehema na amani (Amin).

MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYAH

  • 1420 views

Sura Ya Sabini Na Nane: An-Nabai

Imeshuka Makka Ina Aya 40.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

عَمَّ يَتَسَاءَلُونَ {1}

Ni lipi waulizanalo.

عَنِ النَّبَإِ الْعَظِيمِ {2}

Ni ile habari kubwa,

الَّذِي هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ {3}

Ambayo kwayo wanahitalifi­ana.

كَلَّا سَيَعْلَمُونَ {4}

Si hivyo! Punde tu watajua.

ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ {5}

Tena si hivyo! Punde tu wata­jua.

أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ مِهَادًا {6}

Kwani hatukuifanya ardhi kuwa ni tandiko?

وَالْجِبَالَ أَوْتَادًا {7}

Na milima kuwa ni vigingi?

وَخَلَقْنَاكُمْ أَزْوَاجًا {8}

Na tukawaumba kwa jozi.

وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًا {9}

Na tukaufanya usingizi wenu ni kufa?

وَجَعَلْنَا اللَّيْلَ لِبَاسًا {10}

Na tukaufanya usiku ni vazi?

وَجَعَلْنَا النَّهَارَ مَعَاشًا {11}

Na tukaufanya mchana ni maisha?

وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًا شِدَادًا {12}

Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?

وَجَعَلْنَا سِرَاجًا وَهَّاجًا {13}

Na tukafanya taa yenye mwangaza na joto kali?

وَأَنْزَلْنَا مِنَ الْمُعْصِرَاتِ مَاءً ثَجَّاجًا {14}

Na tukateremsha maji yenye kububujika kutoka kwenye yanayokamuliwa.

لِنُخْرِجَ بِهِ حَبًّا وَنَبَاتًا {15}

Ili tutoe kwayo nafaka na mimea.

وَجَنَّاتٍ أَلْفَافًا {16}

Na mabustani yenye miti iliy­ofungamana?

Aya 1- 16

Maana

Ni lipi waulizanalo. Ni ile habari kubwa, ambayo kwayo wanahitalifi­ana.

Misingi ya kuamini Uislamu ni mitatu: Kuamini umoja wa Mwenyezi, utume wa Muhammad na Siku ya Mwisho. Kaumu ya Mtume (s.a.w.) ilikuwa mbali kabisa na misingi hii mitatu; kwa hiyo waliulizana kwa mshangao wakisema:

أَجَعَلَ الْآلِهَةَ إِلَٰهًا وَاحِدًا ۖ إِنَّ هَٰذَا لَشَيْءٌ عُجَابٌ {5}

“Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili kweli ni jambo la ajabu.”
Juz. 23 (38:5).

Vile vile walizidisha mshangao kwa Muhammad kuwa Mtume, si kwa lolote ila kwa kuwa ni fukara wa mali, wakasema miongoni mwa waliyose­ma:

 لَوْلَا أُنْزِلَ عَلَيْهِ كَنْزٌ  {12}

“Mbona hakuteremshiwa hazina?” Juz. 12 (11:12).

Kuhusu ufufuo wakasema:

أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَدِينُونَ {53}

“Ati tukishakufa tukawa udongo na mifupa, ndio tutahisabiwa?” Juz. 23 (37:53).

Misingi hii mitatu ndiyo iliyokuwa habari kubwa ambayo washirikina walikuwa wakiulizana. Kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.): ‘ambayo kwayo wanahitlaifiana,’ inaashiria kuwa miongoni mwao kuna waliosadi­ki kwa ndani bila ya kujionyesha na waliokadhibisha kwa ndani na nje au kutaradadi.

Si hivyo! Punde tu watajua. Tena si hivyo! Punde tu watajua.

Hii ni kuurudi ukanusho wao na kuwahadharisha na inadi yao. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameisisitiza hadhari hii kwa kuikariri, kisha akabainisha dalili za uweza wake na ishara za hikima yake, asaa wapinzani warejee kwenye uongofu na wahofie siku ya hisabu na malipo, ambayo amewa­hadharisha nayo Mtume; ndipo akasema mtukufu wa wasemaji:

Kwani hatukuifanya ardhi kuwa ni tandiko?

Yaani hamuoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyoitiisha ardhi mnufaike nayo na kuitandika kama mnavyotandika kitanda cha mtoto.

Na milima kuwa ni vigingi?

Milima kwa ardhi ni kama vigingi kwenye hema; lau si hivyo basi ardhi ingelitingishika na kuwagonganisha wakazi wake.

Na tukawaumba kwa jozi, mwanamume na mwanamke, ili kuhifadhi kizazi na kujenga jamii.

Na tukaufanya usingizi wenu ni kufa? Kwa sababu usingizi ni aina ya mauti. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

وَهُوَ الَّذِي يَتَوَفَّاكُمْ بِاللَّيْلِ {60}

“Naye ndiye anayewafisha usiku.” Juz. 7 (6:60).

Usingizi ni lazima kwa ajili ya roho na mwili; wala uhai hauwezi kuwa bila ya huo; hata hivyo haipendekezwi kuuzidisha. Mtume wa Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: “Jihadharini na kulala sana, kwani mwenye kufanya hivyo ni fukara siku ya Kiyama.” Imam As-sadiq (a.s.) anasema: “Usingizi unaondoa dini na dunia.”

Na tukaufanya usiku ni vazi?

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameufananisha usiku na vazi kwa vile unamsi­tiri mtu na yale asiyotaka yaonekane.

Na tukaufanya mchana ni maisha?

Yaani wakati wa harakati na kufanya kazi kwa ajili ua uhai. Kwenye Aya nyingine, Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anasema:

 وَجَعَلَ النَّهَارَ نُشُورًا {47}

“Na akaufanya mchana ni wa mtawanyiko.” Juz. 19 (25:47).

Kwa hiyo usingizi ni kama mauti na mchana ni kama kufufuka kuwa hai.

Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu? Makusudio ya saba hapa ni sayari saba zilizo maarufu kwa watu; vinginevyo ni kuwa mbali ya hizi ziko nyingine zisizo na idadi.

Mwenyezi Mungu amezipa sifa za kuwa na nguvu kwa vile zimepangiliwa vizuri. Tumeyazungumzia kwa ufafanuzi haya katika Juz. 28 (65:12).

Na tukafanya taa yenye mwangaza na joto kali. Makusudio ya taa hapa ni Jua ambalo mwangaza wake unatumika kwa viumbe kwa ajili ya maisha yao.

Na tukateremsha maji yenye kububujika kutoka kwenye yanayoka­muliwa.

Yanayokamuliwa hapa ni mawingu. Yameitwa hivyo kwa sababu upepo unayakamua mpaka yanatoa maji hayo yanayobubujika. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu ameteremsha mvua kutoka mawinguni.

Ili tutoe kwayo nafaka na mimea.

Ardhi inapata uhai kwa maji baada ya kufa kwake na inatoa chakula cha binadamu, wanyama na wengineo. Mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

كُلُوا وَارْعَوْا أَنْعَامَكُمْ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِأُولِي النُّهَىٰ {54}

“Kuleni na mchunge wanyama wenu. Hakika katika hayo zipo ishara kwa wenye akili.”
Juz. 16 (20:54)
.

Na mabustani yenye miti iliyofungamana.

Yaani matawi yake yameingiliana kwa sababu ya kukurubiana miti. Hakuna mwenye shaka kwamba mwenye kuyaweza maajabu haya basi anawa uwezo zaidi wa kuwafufua wafu.

Maana haya yamekaririka mara nyingi; ikiwemo ile isemayo:

حَتَّىٰ إِذَا أَقَلَّتْ سَحَابًا ثِقَالًا سُقْنَاهُ لِبَلَدٍ مَيِّتٍ فَأَنْزَلْنَا بِهِ الْمَاءَ فَأَخْرَجْنَا بِهِ مِنْ كُلِّ الثَّمَرَاتِ ۚ كَذَٰلِكَ نُخْرِجُ الْمَوْتَىٰ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ {57}

“Hata zinapobeba mawingu mazito tunayasukuma kwa ajili ya mji ulioku­fa. Kisha tunateremsha hapo maji. Kwa hayo tukaotesha kila matunda. Kama hivi tutawafufua wafu ili mpate kukumbuka.” Juz. 8 (7:57)

إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ كَانَ مِيقَاتًا {17}

Hakika Siku ya upambanuzi imewekewa wakati.

يَوْمَ يُنْفَخُ فِي الصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًا {18}

Siku itakapopulizwa para-panda nanyi mtakuja makun­di makundi.

وَفُتِحَتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ أَبْوَابًا {19}

Na mbingu zitafunguliwa ziwe milango.

وَسُيِّرَتِ الْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا {20}

Na milima itaondolewa iwe sarabi.

إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًا {21}

Hakika Jahannam inangoja!

لِلطَّاغِينَ مَآبًا {22}

Kwa walioasi ndio marejeo.

لَابِثِينَ فِيهَا أَحْقَابًا {23}

Wakae humo siku nyingi.

لَا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًا وَلَا شَرَابًا {24}

Hawataonja humo baridi wala kinywaji.

إِلَّا حَمِيمًا وَغَسَّاقًا {25}

Isipokuwa maji ya moto na usaha.

جَزَاءً وِفَاقًا {26}

Ni malipo muwafaka.

إِنَّهُمْ كَانُوا لَا يَرْجُونَ حِسَابًا {27}

Hakika wao walikuwa hawatarajii kuhisabiwa.

وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كِذَّابًا {28}

Na wakazikadhibisha Ishara zetu kuzikadhibisha.

وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ كِتَابًا {29}

Na kila kitu tumekidhibiti kwa kukiandika

فَذُوقُوا فَلَنْ نَزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا {30}

Basi onjeni! Hatutawazidishia ila adhabu!

Aya 17 – 30: Siku Ya Upambanuzi

Maana

Hakika Siku ya upambanuzi imewekewa wakati.

Siku ya upambanuzi ni Siku ya Kiyama; ndani yake itapambanuliwa haki na batili na ina wakati maalum, lakini haujui isipokuwa Mwenyezi Mungu. Wakati huo ndipo ulimwengu utaisha na viumbe hai na waliokufa watagur­ishwa kupelekwa kwenye ulimwengu mwingine usiofanana na dunia yetu na chochote. Ulimwengu usiokuwa na batili wala kwisha, wala kuwa na kazi au maombi.

Hakuna chochote isipokuwa neema kwa mwenye kufanya wema na moto kwa mwenye kufanya uovu. Miongoni mwa dalili zake ni aliyoaashiria Mwenyezi Mungu kama ifuatavyo:-

Siku itakapopulizwa parapanda nanyi mtakuja makundi makundi.

Parapanda ni baragumu lenye sauti kubwa. Hatujui kuwa Mwenyezi Mungu amekusudia maana yake halisi au ni kinaya tu cha kufufuliwa waliomo makaburini? Vyovyote iwavyo, sisi hatukukalifishwa kuitafuta ilimu hii, wala haina uhusiano na maisha yetu kwa mbali wala karibu.

Na mbingu zitafunguliwa ziwe milango.

Hiki ni kinaya cha kuparaganyika ulimwengu wa juu, zikiwemo nidhamu za sayari na kuondoka mshikamano wake. Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Inawezekana kuwa mbingu ziwe ni milango kwetu, tuuingie ule tunaoutaka kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.”

Na milima itaondolewa iwe sarabi; yaani iwe kama hakuna kitu; kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَبُسَّتِ الْجِبَالُ بَسًّا {5}

فَكَانَتْ هَبَاءً مُنْبَثًّا {6}

“Na milima itaposagwasagwa, iwe mavumbi yanayopeperushwa.” Juz. 27 (56:5-6).

Yaani itavurugika iwe kama uji, au kama vumbi linalokwenda na upepo.

Hakika Jahannam inangoja, kwa walioasi ndio marejeo.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kutaja dalili za uweza wake, sasa anawahadharisha wale wanopinga utume wa Muhammad (s.a.w.) kuwa Jahannam inawangojea nayo ndio makazi yao pekee na marejeo yao.

Wakae humo siku nyingi.

Neno siku nyingi tumelifasiri kutokana na neno la Kiarabu Ahqab lenye maana ya muda usiojulikana mwisho wake. Imesemekana kuwa maana ya neno hilo ni miaka thamanini. Maana ni kuwa watakaa muda usiokuwa na kikomo wala mwisho.

Hawataonja humo baridi wala kinywaji.

Kwani maji yanaweza kuwa pamoja na Moto?

Isipokuwa maji ya moto na usaha.

Huku ni kuvua kunakoambatana na kinachovuliwa, kwa sababu mwili ndio maji yanayotokota motoni na usaha unaomiminika kutoka kwenye mwili unaounguzwa na Moto.

Ni malipo muwafaka.

Adhabu inaafikiana na matendo yao na maovu yao katika maisha ya dunia:

وَجَزَاءُ سَيِّئَةٍ سَيِّئَةٌ مِثْلُهَا ۖ {40}

“Na malipo ya uovu ni uovu mfano wa huo.” Juz. 25 (42:40).

Hakika wao walikuwa hawatarajii kuhisabiwa, na wakazikadhibisha Ishara zetu kuzikadhibisha.

Starehe za dunia zilipofua macho na akili zao, vipi watatarajia kukutana na Mwenyezu Mungu na hali wanaona ishara na ubainifu wake kisha wanaukadhibisha?

Na kila kitu tumekidhibiti kwa kukiandika.

Hakifichiki kwa Mwenyezi Mungu chochote kilicho kwa waja wake, wali­chokifanya usiku au mchana; hata kile wanachokiwazia katika nafsi zao na kinachowapitia katika dhamiri zao.

Basi onjeni! Hatutawazidishia ila adhabu!

Hamna chochote isipokuwa adhabu, wala msiwe na matumaini isipokuwa kuongezewa.

إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا {31}

Hakika wenye takua wana pa kufuzu.

حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا {32}

Mabustani na mizabibu.

وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا {33}

Na wasichana walio marika mamoja.

وَكَأْسًا دِهَاقًا {34}

Na bilauri zilizojaa.

لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا {35}

Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo.

جَزَاءً مِنْ رَبِّكَ عَطَاءً حِسَابًا {36}

Malipo kutoka kwa Mola wako, kipawa chenye kuhis­abiwa

رَبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا الرَّحْمَٰنِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًا {37}

Mola wa mbingu na ardhi na viliomo kati yake, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake.

يَوْمَ يَقُومُ الرُّوحُ وَالْمَلَائِكَةُ صَفًّا ۖ لَا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ الرَّحْمَٰنُ وَقَالَ صَوَابًا{38}

Siku atakaposimama Roho na malaika kwa safu. Hawatasema ila atayepewa idhini na Mwingi wa rehema na atasema yaliyo sawa.

ذَٰلِكَ الْيَوْمُ الْحَقُّ ۖ فَمَنْ شَاءَ اتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِ مَآبًا {39}

Hiyo ndiyo siku ya haki. Basi anayetaka na ashike njia kurejea kwa Mola wake.

إِنَّا أَنْذَرْنَاكُمْ عَذَابًا قَرِيبًا يَوْمَ يَنْظُرُ الْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ الْكَافِرُ يَا لَيْتَنِي كُنْتُ تُرَابًا {40}

Hakika tunawaonya na adhabu iliyo karibu; siku mtu atakapoona yaliyotangulizwa na mikono yake; na kafiri aseme: Laiti ningelikuwa mchanga.

Aya 31 – 40: Wenye Takua Watafuzu

Maana

Hakika wenye takua wana pa kufuzu, kwa kupata thawabu za Mwenyezi Mungu na radhi zake na pia kuokoka na dhabu yake na ghadhabu yake. Pakufuzu, ni Peponi.

Mabustani na mizabibu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amehusisha kutaja mizabibu kutokana na umuhimu wake kwa waliokuwa wakiambiwa.

Na wasichana walio marika mamoja. Hurilaini walio na umri mmoja na ambao matiti yao yamesimama. Na bilauri zilizojaa kinywaji kinachoshuka kooni kwa ladha na uzuri wake.

Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo.

Hatasema wala kusikia maneno yasiyokuwa na msingi wala kutokuwa ya kawaida. Hapa kuna ishara kwamba watu wa Peponi ingawaje hawana kazi yoyote, lakini hawatakuwa na upuuzi wa watu wavivu wa duniani.

Malipo kutoka kwa Mola wako, kipawa chenye kuhisabiwa.

Neno malipo linaasharia kuwa thawabu kwa matendo mema ni haki isiyokuwa na shaka, na neno kipawa linaonyesha kuwa Mwenyezi Mungu atawazidishia kwa fadhila yake ziada ya kutosheleza katika yale wanayoy­apendelea na kuyatamani. Umetangulia mfano wake katika Aya kadhaa, ikiwemo ile ya Juz.16 (19:60-63).
Mola wa mbingu na ardhi na viliomo kati yake, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake. Ambao watamiliki ni viumbe ambao wameashiriwa kwa kutajwa mbingu na ardhi; kwa sababu Mwenyezi Mungu ndiye Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake.

Maana ni kuwa hizo bustani na neema nyiniginezo za Mwenyezi Mungu alizowapa wenye takua zinatokana na Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu na ni Mmiliki, ambaye hakuna yeyote atakayemhoji kuhusiana na thawabu na adhabu Siku ya Kiyama. Yeye peke yake ndiye atakayefanya vile atakavyo.

Siku atakaposimama Roho na malaika kwa safu. Hawatasema ila atayepewa idhini na Mwingi wa rehema na atasema yaliyo sawa.

Imesemekana kuwa Makusudio ya Roho hapa ni Jibril, kwa vile Mwenyezi Mungu alimwita Roho mwaminifu katika Juz. 19 (26:194). Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Roho ni katika maumbile ya Mwenyezi Mungu yaliyoghaibu kwetu, ambayo hatukukalifishwa kutafuta uhakika wake.”

Maana ni kuwa Malaika watajipanga safu siku ya Kiyama na wataijaza mandhari kwa kuhofisha na kupendeza, wakiwa kwenye utiifu wao na kujikurubisha kwao kwa Mwenyezi Mungu; hawatakua na harakati yoyote wala kusema lolote wao au mwenginewe isipokuwa kwa ruhusa yake Mwenyezi Mungu Mtukufu; wala Mwenyezi Mungu hatamruhusu isipokuwa ambaye maisha yake yote ni usawa, ukweli, uadilifu na haki. Vile vile atakayeruhusiwa hatasema isipokuwa anayoyapenda na kuyataka Mwenyezi Mungu.

Hiyo ndiyo siku ya haki. Basi anayetaka naashike njia kurejea kwa Mola wake.

Siku ya Kiyama ni haki isiyokuwa na shaka, na watu siku hiyo watakuwa makundi mawili: Kundi la motoni litakalokuwa mbali na Mwenyezi Mungu na rehema yake, na kundi jingine litakuwa karibu na Mwenyezi Mungu na rehema yake. Njia ya kuelekea huko iko wazi na imeandaliwa; nayo ni ukweli wa nia. Kwa hiyo basi, ni juu yake mtu kufanya, kwa ikhlasi, kwa mujibu wa utashi wake na raghaba yake ya kuingia Peponi.

Hakika tunawaonya na adhabu iliyo karibu ambayo ni adhabu ya Siku ya Kiyama, kwa sababu kila lijalo liko karibu. Je, kuna jambo lililo karibu zaidi na mtu kuliko mauti?

Siku mtu atakapoona yaliyotangulizwa na mikono yake katika maisha ya duniani yawe ya kheri au ya shari. Mfano wa Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: Juz. 3 (3:30).

Na kafiri aseme: Laiti ningelikuwa mchanga. Siku ya haki atatamani mkosefu kuwa mchanga unaokanyagwa na nyayo, kutokana na shida atakayokuwa nayo na kukata tamaa na kuokoka. Hivi ndivyo yalivyo majuto!

  • 2980 views

Sura Ya Sabini Na Tisa: An-Naziaa’t

Imeshuka Makka Ina Aya 46.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَالنَّازِعَاتِ غَرْقًا {1}

Naapa kwa zinazotoa kwa nguvu.

وَالنَّاشِطَاتِ نَشْطًا {2}

Na kwa zinazotoa kwa upole.

وَالسَّابِحَاتِ سَبْحًا {3}

Na zinazoogelea sana.

فَالسَّابِقَاتِ سَبْقًا {4}

Na zinazoshindana mbio.

فَالْمُدَبِّرَاتِ أَمْرًا {5}

Zikapangilia mambo.

يَوْمَ تَرْجُفُ الرَّاجِفَةُ {6}

Siku itakapotetemeka mtete­meko.

تَتْبَعُهَا الرَّادِفَةُ {7}

Ifuate ya kufuatia.

قُلُوبٌ يَوْمَئِذٍ وَاجِفَةٌ {8}

Nyoyo siku hiyo zitadundadun­da.

أَبْصَارُهَا خَاشِعَةٌ {9}

Macho yake yatanyenyekea.

يَقُولُونَ أَإِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِي الْحَافِرَةِ {10}

Wanasema: Hivi kweli tutarudishwa hali ya kwanza?

أَإِذَا كُنَّا عِظَامًا نَخِرَةً {11}

Pindi tutakapokuwa mifupa iliyooza?

قَالُوا تِلْكَ إِذًا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌ {12}

Wanasema: Hayo ni marejeo yenye hasara!

فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ {13}

Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu.

فَإِذَا هُمْ بِالسَّاهِرَةِ {14}

Mara watakuwa juu ya ardhi.

Aya 1- 14: Zinatoa Kwa Nguvu

Maana

Naapa kwa zinazotoa kwa nguvu.

Kauli za wafasiri zimekua nyingi kuhusu maneno haya; annazia’t ghar­qa na yanayoyafuatia. Tutaelezea kwa muhtasari kauli ya Sheikh Muhammad Abduh kwa jinsi ya alivyokusudia yeye.

Mwenye kufuatilia Aya za Qur’an yenye hikima, atakuta kuwa Mwenyezi Mungu ameapa kwa nyakati, mahali na vitu vinginevyo. Mwenye kutaa­mali yote yale aliyoyaapia Mwenyezi Mungu atakuta ama ni jambo amba­lo watu wamelikana, au kulidharau au hawakujua dalili zilizomo ndani yake za uweza wake Mwenyezi Mungu na ukuu wake.

Kwa hiyo Mwenyezi Mungu Mtukufu akaapa kwa lile wanalolikana ili kuthibitisha kuweko kwake; akaapa kwa lile wanalolidharau ili kulitukuza au akaapa kwa kutanabahisha lile lenye dalili ya uwezo wake ambaye umetukuka ukuu wake. Hapa ameapa kwa baadhi ya viumbe vyake kudhihirisha ufundi wake wa kuvifanya na faida zake, ili wajue wakadhibishaji kuwa mwenye uwezo wa kuyafanya hayo, basi ana uwezo zaidi wa kufufua wafu.

Makusudio ya zinazotoa, hapa ni nyota zinazotupa kama unavyotupa mshale, kwa vile nyota zinatupa vimondo. Waarabu wanalitumia neno hili nazi” kwa maana ya kutupa kwa mshale na pia gharq kwa maana ya mkazo wa kutupa mshale.

Na kwa zinazotoa kwa upole.

Waarabu wanatumia neno nasht, tulililofasiri kwa maana ya kutoa kwa maana ya upole, kwa mtu anayetoka sehemu moja hadi nyingine. Kwa hiyo maana ni kuwa nyota zinatoka kwenye buruji moja hadi nyingine.

Na zinazoogelea sana; yaani nyota zinaogoelea angani

Na zinazoshindana mbio; yaani zinazokamilisha mzunguko wake kwa haraka kwenye kile zinachokizunguka. Na inaeleweka kuwa kasi ya kila kitu ni kulingana na ukubwa wake.

Zikapangilia mambo; yaani nyota zinadhihirisha athari yake kwa yale wanayonufaika nayo watu; kama vile kujua nyakati, mielekeo, kutofau­tiana majira ya mwaka na mambo mengineyo ya maisha.

Huu ndio muhtasari wa kurasa tatu, kutoka Juzuu Amma ya Sheikh Muhammad Abduh, kuhusiana na maneno haya.

Sisi hatukubaliani naye moja kwa moja wala pia hatukubaliani moja kwa moja na waliosema kuwa makusudio ni malaika; au mengineyo yaliyosemwa; kwa vile hayana mategemezi yoyote. Na waliozama katika ilimu wanakiri kutojua na kushindwa maarifa ya ghaibu, wala hawasemi wasiyoyajua.

Siku itakapotetemeka mtetemeko.

Itakayotetemeka hapa ni ardhi kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

يَوْمَ تَرْجُفُ الْأَرْضُ وَالْجِبَالُ وَكَانَتِ الْجِبَالُ {14}

“Siku ambayo ardhi itatikisika na milima.” Juz. 29 (73:14).

Maana ni kuwa ardhi Siku ya Kiyama itavigonganisha viliomo ndani yake na kuharibika.
Ifuate ya kufuatia.

Hiyo ni mbingu ambayo itafuatia kuharibika na kubomoka. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

إِذَا السَّمَاءُ انْفَطَرَتْ {1}

وَإِذَا الْكَوَاكِبُ انْتَثَرَتْ {2}

“Mbingu itakapopasuka Na nyota zitakapopukutika.” (82:1-2).

Nyoyo siku hiyo zitadundadunda, macho yake yatanyenyekea.

Makusudio ya nyoyo hapa ni nyoyo za wakosefu, pale zitakapotambua adhabu itakazozipata, zitapigapiga kwa hofu na athari yake itajitokeza machoni; ambapo hapo nyuma zilikuwa kama nyoyo za wanyama na kama jiwe kwa kususuwaa kwake.

Wanasema: Hivi kweli tutarudishwa hali ya kwanza?

Maneno ‘hali ya kwanza tumeyafasiri’ kutokana na neno la kiarabu Hafira lenye maana ya kurudia kwenye hali iliyokuwako baada ya kuitoka. Maana ni, vipi tunaweza kuwa hai baada ya kuutoka uhai na kuwa wafu? Ni maa­jabu!

Pindi tutakapokuwa mifupa iliyooza kweli tutapata umbo jipya?

Wanasema: Hayo ni marejeo yenye hasara.

Walipinga ufufuo, Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akawahadharisha na adhabu ya moto; kisha wakasema kwa madharau: basi kama ni hivyo sisi tutakua wenye hasara Siku ya Kiyama. Ndio hivyo hasa, si ajabu hilo, wao watakuwa wenye hasara:

وَيَوْمَ تَقُومُ السَّاعَةُ يَوْمَئِذٍ يَخْسَرُ الْمُبْطِلُونَ {27}

“Na siku itakaposimama saa, Siku hiyo watahasirika wenye batili.” Juz. 25 (45:27).

Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu.

Haya ni maneno ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akiwarudi wakadhabishaji wanaofanya madharau. Maana yake ni kuwa ni jambo jepesi sana kwa Mwenyezi Mungu kuwafufua:

إِنْ كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً  {53}

“Haitakuwa ila ukelele mmoja tu.” Juz. 23 (36:53).

Mara watakuwa juu ya ardhi.

Yaani ukiisha ukelele tu, wao watakusanywa kwenye uwanja.

هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ مُوسَىٰ {15}

Je, imekujia hadithi ya Musa?

إِذْ نَادَاهُ رَبُّهُ بِالْوَادِ الْمُقَدَّسِ طُوًى {16}

Alipomwita Mola wake katika bonde takatifu la Tuwaa:

اذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُ طَغَىٰ {17}

Nenda kwa Firauni. Kwani hakika yeye amepituka mpaka.

فَقُلْ هَلْ لَكَ إِلَىٰ أَنْ تَزَكَّىٰ {18}

Mwambie je, unataka kuji­takasa?

وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ {19}

Na nikuongoze kwa Mola wako upate kumcha?

فَأَرَاهُ الْآيَةَ الْكُبْرَىٰ {20}

Basi akamwonyesha Ishara kubwa.

فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ {21}

Lakini akakadhibisha na akaasi.

ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ {22}

kisha akarudi nyuma na akafanya juhudi.

فَحَشَرَ فَنَادَىٰ {23}

Akakusanya akanadi.

فَقَالَ أَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ {24}

Akasema: Mimi ndiye mola wenu mkuu.

فَأَخَذَهُ اللَّهُ نَكَالَ الْآخِرَةِ وَالْأُولَىٰ {25}

Basi Mwenyezi Mungu akamshika kumwadhibu kwa la mwisho na la kwanza.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبْرَةً لِمَنْ يَخْشَىٰ {26}

Hakika katika hayo kuna mazingatio kwa wenye kuo­gopa.

أَأَنْتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ السَّمَاءُ ۚ بَنَاهَا {27}

Je, ni vigumu zaidi kuwaumba nyinyi au mbingu aliyoijenga?

رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّاهَا {28}

Akainua kimo chake na akaifanya sawa.

وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَاهَا {29}

Akautia giza usiku wake na akautokeza mwanga wake.

وَالْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَاهَا {30}

Na baada ya hapo akaitandika ardhi.

أَخْرَجَ مِنْهَا مَاءَهَا وَمَرْعَاهَا {31}

Akatoa humo maji yake na malisho yake.

وَالْجِبَالَ أَرْسَاهَا {32}

Na milima akaiimarisha.

مَتَاعًا لَكُمْ وَلِأَنْعَامِكُمْ {33}

Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.

Aya 15 – 33: Hadith Ya Musa

Maana

Je, imekujia hadithi ya Musa?

Hii ni hali ya kumfariji Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Mtume wake mtukufu, Muhammad (s.a.w.); kwamba atamnusuru na maadui zake, kama alivy­omnusuru Musa aliyezungumza na Mwenyezi Mungu. Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 16 (20:9).

Alipomwita Mola wake katika bonde takatifu la Tuwaa.

Bonde hilo liko chini ya Mlima Sinai, jina lake ni Tuwaa. Umetangulia mfano wake katika Juz. 16 (20:12).

Nenda kwa Firauni. Kwani hakika yeye amepituka mpaka na kuzidi uasi mpaka akadai uungu. Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 16 (20:25).

Mwambie je, unataka kujitakasa?

Je, unapendelea kujitwaharisha na shirki na uchafu?

Na nikuongoze kwa Mola wako upate kumcha?

Mwenye kumcha Mwenyezi Mungu hawezi kupituka mipaka na kufanya ufisadi katika ardhi.

Firauni alimdharau Musa na kusema: Hivi huyu mpuzi anaweza kuongoza! Basi Musa akamwonyesha Ishara kubwa ya fimbo kugeuka nyoka, laki­ni akakadhibisha na akaasi.

Aliupinga muujiza na kusema kuwa ni uchawi; kisha akarudi nyuma na akafanya juhudi ya kumpangia njama Musa; akakusanya akanadi. Alikusanya wachawi na wasaidizi wake akasema:

Mimi ndiye mola wenu mkuu;’’ wala simjui mungu mwingine kwenu asiyekuwa mimi.
Huu ni ubainifu na tafsiri ya kunadi kwake kwa wachawi wake na wasaidizi wake. Watu wengi leo, kabla yake na baada yake wanadai uungu lau wanapata atakayewasadiki.

Basi Mwenyezi Mungu akamshika kumwadhibu kwa la mwisho na la kwanza.

Alimwadhibu kwa kumgharikisha duniani na kumwunguza Akhera.

Hakika katika hayo kuna mazingatio kwa wenye kuogopa mwisho, hivyo wanajitoa shakani na kujiokoa. Lakini mwenye kupuuza atamwad­hibu kwa kujiamini kwake.

Je, ni vigumu zaidi kuwaumba nyinyi au mbingu aliyoijenga?

Maneno yanaelekezwa kwa wale waliokadhibisha ufufuo. Maana ni lipi lenye ugumu zaidi kati ya kurudishwa mtu kama alivyokuwa mara ya kwanza na kuaanzisha kujenga hii mbingu kwa mpangilio wake na nid­hamu yake?

Mfano wake ni kauli yake:

 أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمْ مَنْ خَلَقْنَا ۚ {11}

“Je, hao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tuliowaumba?” Juz. 23 (37:11).

Sheikh Muhammad Abduh anasema: Kujenga ni kukusanya sehemu tofau­

ti na kuzichanganya pamoja mpaka ziwe jengo moja. Hivi ndivyo alivy­ofanya Mwenyezi Mungu kwa nyota; aliiweka kila nyota mahali pake panapolingana; kila moja ikiwa na kani ya mvutano kwa nyingine. Mkusanyiko huu ndio ukawa jengo moja linaloitwa mbingu.

Na hii ndio maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu: akainua kimo chake na akaifanya sawa; yaani aliinua gimba lake juu ya vichwa vyetu akaliweka sawa kila gimba mahali pake.

Akautia giza usiku wake na akautokeza mwanga wake.

Dhamiri ya wake ni ya mbingu, kwa sababu inakuwa na giza kwa kutua jua na inakuwa na mwanga kwa kutokeza jua.

Na baada ya hapo akaitandika ardhi; yaani aliitandaza kwa namna ya kufaa kukaliwa na kutembea juu yake.

Katika kitabu uhawalatu lifahmi asriy liqur’an, imeandikwa hivi, ninanukuu: “Dahaaha, maana yake ni kuwa ameifanya kama yai, jambo ambalo linaungwa mkono na fikra za sasa za kifalaki kuhusu umbo la ardhi… Na neno hilo pia lina maana ya kutandaza.Hili ni neno la kiarabu pekee lenye maana ya kutandaza na kukunja kwa wakati mmoja. Kwa hiyo linakuwa neno bora kwa ardhi iliyokunjuliwa kwa dhahiri na kukunjwa (kuwa mviringo) kiuhakika... Na huu ni ufundi na uficho wa hali ya juu wa kuchagua tamko la undani lililo wazi.”

Akatoa humo maji yake na malisho yake.

Maji yote yaliyoko ardhini yanatoka mbinguni; Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: “ Juz.18 (23:18). Kisha Mwenyezi Mungu anayabu­ubujiza maji haya kuwa chemichemi na mito; inatoka mimea itakayoliwa na watu na wanayama. Na milima akaiimarisha, ili isiyumbe ardhini wakangona waliomo:

وَأَلْقَىٰ فِي الْأَرْضِ رَوَاسِيَ أَنْ تَمِيدَ بِكُمْ  {15}

“Na akaweka katika ardhi milima ili isiyumbe nanyi.” Juz. 14 (16:15).

Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameiumba ardhi akaitandika na kuiimarisha, kisha akachimbua maji na kutoa mimea; yote hayo ni kwa ajili ya kheri ya mtu na mifugo anayonufaika nayo huyo mtu.

Je, yote haya yamekuja kwa sadfa na bila ya mpango? Au yule aliyeanzisha yote hayo mara ya kwanza atashindwa kuyarudisha mara ya pili?

وَهُوَ الَّذِي يَبْدَأُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ وَهُوَ أَهْوَنُ عَلَيْهِ ۚ {27}

“Naye ndiye ambaye anaanzisha uumbaji kisha ataurudisha.” Juz. 21 (30:27).

فَإِذَا جَاءَتِ الطَّامَّةُ الْكُبْرَىٰ {34}

Basi itakapofika hiyo balaa kubwa.

يَوْمَ يَتَذَكَّرُ الْإِنْسَانُ مَا سَعَىٰ {35}

Siku atakayokumbuka mtu aliyoyahangaikia.

وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِمَنْ يَرَىٰ {36}

Na Moto ukadhihirishwa kwa mwenye kuona.

فَأَمَّا مَنْ طَغَىٰ {37}

Basi ama yule mwenye kupituka mipaka.

وَآثَرَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا {38}

Na akaathirika na maisha ya dunia.

فَإِنَّ الْجَحِيمَ هِيَ الْمَأْوَىٰ {39}

Kwa hakika Moto ndio makazi!

وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ وَنَهَى النَّفْسَ عَنِ الْهَوَىٰ {40}

Na ama mwenye kuogopa kusimama mbele ya Mola wake na akaizuilia nafsi na matamanio.

فَإِنَّ الْجَنَّةَ هِيَ الْمَأْوَىٰ {41}

Basi hakika Pepo ndio makazi!

يَسْأَلُونَكَ عَنِ السَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَاهَا {42}

Wanakuuliza saa itakuwa lini?

فِيمَ أَنْتَ مِنْ ذِكْرَاهَا {43}

Una nini na kuitaja?

إِلَىٰ رَبِّكَ مُنْتَهَاهَا {44}

Ni kwa Mola wako ukomo wake.

إِنَّمَا أَنْتَ مُنْذِرُ مَنْ يَخْشَاهَا {45}

Hakika wewe ni muonyaji tu wa anayeiogopa.

كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوا إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَاهَا {46}

Kama kwamba wao siku watakapoiona hawakukaa ila jioni moja au asubuhi yake.

Aya 34 – 46: Balaa Kubwa

Maana

Basi itakapofika hiyo balaa kubwa.

Kitakaposimama Kiyama ulimwengu, ikiwemo ardhi na mbingu yake, utaharibika na hakuna kitakachobaki isipokuwa Muumba wa kila kitu. Hiyo ndio balaa kubwa. Kuna jambo gani kubwa kuliko hilo? Ndio kuanzia hapa ikasemwa: Hakuna balaa isipokuwa juu yake kuna balaa na Kiyama kiko juu ya balaa zote.

Siku atakayokumbuka mtu aliyoyahangaikia.

Akishagura kutoka kwenye kuisha kwenda kwenye kubakia ataona daftari la matendo yake; yakiwa ni kheri basi ni kheri na yakiwa ni shari basi ni shari. Hapo ndio atakumbuka aliyoyahangaikia katika maisha ya dunia na yaliyochumwa na mikono yake.

Na Moto ukadhihirishwa kwa mwenye kuona.

Hakuna kizuizi cha kuuona wala mlinzi wa kumzuia nao; fauka ya hayo:

وَإِنْ مِنْكُمْ إِلَّا وَارِدُهَا ۚ كَانَ عَلَىٰ رَبِّكَ حَتْمًا مَقْضِيًّا {71}

“Hakuna miongoni mwenu ila ni mwenye kuifikia. Ni hukumu ya Mola wako, ni lazima itimizwe.” Juz. 16 (19:71).

Basi ama yule mwenye kupituka mipaka, na akaathirika na maisha ya dunia, kwa hakika Moto ndio makazi yake. Na ama mwenye kuogopa kusimama mbele ya Mola wake na akaizuilia nafsi na matamanio, basi hakika Pepo ndio makazi yake.

Mwenye kufuata matamanio yake yatamwingiza kwenye maangamizi, na mwenye kuyashinda anakuwa ameona njia na kufikia ukomo wa heri.

Matamnio ni ila ya ila zote; amesema kweli aliyesema; “Mwenye kuyatii matamanio yake amempa adui matakwa yake.”

Mwengine naye akasema: “Hakika ya mtu ni nafsi yake; matamanio yake yakishinda nafsi yake basi atakuwa kiumbe mwingine asiyefanana na mtu katika moyo wake wala akili yake.”

Miongoni mwa aliyoyasema Imam Ali katika wasifu wa anayeipima haki kwa matamanio yake ni: “Hajui mlango wa uongofu akaufuata, wala mlan­go wa upofu akajitanibu nao; huyo basi ni maiti hai.”

Hakika ilivyo, ni kuwa Makusudio ya matamanio ni yale yanayohalifu haki na uadilifu; vinginevyo nikuwa nafsi huwa inatamani mambo ya halali, kama inavyotamani haramu.

Wanakuuliza saa ya Kiyama itakuwa lini? Yaani Kiyama kitakuwa lini? Una nini na kuitaja? Ni kwa Mola wako tu ukomo wake. Hakika wewe ni muonyaji tu wa anayeiogopa.

Wanakutaka wewe Muhammad uwaelezee siku ambayo Kiyama kita­tokea; wala hili halihusiani nawe wala na wadhifa wako.

Linalotakikana kwako ni kuwahadharisha watu na hicho Kiyama na vituko vyake; ama kitakuwa lini, ilimu yake iko kwa Mwenyezi Mungu, na hiki­ma yake imetaka kukificha kwa waja wake; hata manabii na wenye kuku­rubishwa. Umetangulia mfano wake katika Juz. 9 (7:187).

Kama kwamba wao siku watakapoiona hawakukaa ila jioni moja au asubuhi yake.

Walikikana Kiyama mpaka watakapokiona ndio watakuwa na yakini kuwa ni haki isiyokuwa na shaka na kwamba ndio nyumba ya kubakia na dunia ni mapitio ya kukiendea, kikiwakunja watu kwa mauti wataona kuwa umri wao ulikuwa ni sawa na wakati mdogo au saa moja tu ya mchana.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:45).

  • 3316 views

Sura Ya Themanini: Abasa

Imeshuka Makka Ina Aya 42.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰ {1}

Alikunja uso na akageuka.

أَنْ جَاءَهُ الْأَعْمَىٰ {2}

Kwa sababu alimjia kipofu!

وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُ يَزَّكَّىٰ {3}

Na nini kitakujulisha huenda akatakasika?

أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنْفَعَهُ الذِّكْرَىٰ {4}

Au akakumbuka ukamfaa ukumbusho?

أَمَّا مَنِ اسْتَغْنَىٰ {5}

Ama anayejiona amejitosha.

فَأَنْتَ لَهُ تَصَدَّىٰ {6}

Ndio wewe unamshughulikia?

وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ {7}

Na si juu yako asipojitakasa.

وَأَمَّا مَنْ جَاءَكَ يَسْعَىٰ {8}

Ama mwenye kukujia mbio mbio.

وَهُوَ يَخْشَىٰ {9}

Naye anaogopa.

فَأَنْتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ {10}

Ndio wewe unajipurukusha naye?

كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ {11}

Si hivyo! Hakika hizo ni ukumbusho.

فَمَنْ شَاءَ ذَكَرَهُ {12}

Anayetaka amkumbuke.

فِي صُحُفٍ مُكَرَّمَةٍ {13}

Zimo katika kurasa zilizo­hishimiwa.

مَرْفُوعَةٍ مُطَهَّرَةٍ {14}

Zenye kuinuliwa zilizo­takaswa.

بِأَيْدِي سَفَرَةٍ {15}

Zimo mikononi mwa wajumbe.

كِرَامٍ بَرَرَةٍ {16}

Watukufu, wema.

Aya 1 – 16: Alikunja Uso Na Akageuka

Ni Nani Aliyekunja Uso?

Wameafikiana wafasiri kuwa kipofu ni Ibn Ummi Maktum, swahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) mtoto wa mjomba wa Khadija, mke wa Mtume. Na wamehitalifiana kuhusu aliyekunja uso. Ikasemekana kuwa hajulikani. Kauli hii ina mwelekeo kutokana na Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuleta dhamir ya ghaibu (ya asiyekuweko). Mfano huu katika Qur’an ni mwingi; kama vile kauli yake Mwenyezi Mungu : “Kisha akenda kwa watu wake kwa matao.” Juz. 29 (75:33).

Pia imesemekana ni mtu mmoja katika Bani Umayya alikuwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.), basi alipomwona kipofu akaona kinyaa na kugeuka.

Kauli iliyo mashuhuri kwa wafasiri na wengineo ni kuwa aliyekunja uso na kugeuka ni Mtume (s.a.w.); na sababu ni kuwa Ibn Ummi Maktum alimjia Mtume alipokuwa na vigogo wa kikuraishi, wenye jaha na mali, wakiwe­mo Utba na Shaiba-watoto wa Rabiaa, Abu Jahl, Walid bin Al-Mughira na wengineo.

Mtume alikuwa amewaacha wengine akiwakabili hawa akiwapa mawaid­ha ya Mwenyezi Mungu na kuwahadharisha na mwisho mbaya wa shirki na dhulma na kuwaahidi heri ya dunia na Akhera, kama wakisilimu. Alifanya hivyo akitaraji kuongoka kwao na kuwa na nguvu ya uislamu au angalau wazuie shari yao. Wakati huo Uislamu ulikuwa bado haujapata nguvu

Basi kipofu fukara akamkatiza Mtume mazungumzo yake, na kusema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, nifundishe nitakayonufaika nayo kati­ka yale aliyokufundisha Mwenyezi Mungu. Mtume akaendelea na maneno yake pamoja na wale jamaa.

Aliporudia kipofu, Mtume alikirihika na likadhihirika hilo kwenye uso wake; ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia Nabii wake mtukufu kwa dhamiri ya asiyekuweko ghaibu: Alikunja uso na akageuka; kisha kwa dhamiri ya moja kwa moja mukhatab: Ama anayejiona amejitosheleza wewe unamshughulikia?

Haya ndiyo waliyokwenda nayo wafasiri wengi; na yana mwelekeo wenye nguvu zaidi kuliko ule wa kwanza kutokana na dhamiri ya kuelekeza moja kwa moja ukhatab-wewe, ambayo, kwa dhahiri, makusudio ni Mtume, na inakuwa ni ubainifu na tafsiri ya dhamiri ya ghaibu, kwa kugeukia kwenye mukhatab.

Lakini kauli ya wafasiri kuwa Mwenyezi Mungu alimkaripia Mtume, kwa hilo, haina mwelekeo kabisa, kwani hakuna lililowajibisha karipio wala lawama katika tendo la Mtume (s.a.w.); kwa vile yeye alikuwa akipatiliza fursa pamoja na wale vigogo kwa masilahi ya Uislamu na waislamu, sio kwa masilahi yake wala ya familia yake. Kumfundisha Mwislamu hukumu na matawi kuna wakati mrefu usiokuwa na mpaka, bali kunawezekana wakati wowote.

Kwa ibara ya wanafikhi ni: Kusilimu kafiri wakati wake ni finyu sana (inapopatikana fursa ndio wakati wake huo, hakuna mwingine) lakini kum­fundisha Mwislamu hukumu za dini kuna wasaa mkubwa, inawezekana kutekeleza wakati wowote. Kwa hiyo ulio finyu ni muhimu zaidi na wenye wasaa ni muhimu (ahammu na muhimmu), na la muhimu zaidi ndilo linalotangulizwa, kwa hukumu ya akili. Kwa hiyo basi alivyofanya Mtume ni kheri na hikima.

Unaweza kuuliza: Ikiwa ni hivyo basi wakulaumiwa na kukaripiwa ni kipofu, naye Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemsifu na kumtetea, sasa itakuwaje?

Jibu: Hapana lawama wala karipio katika Aya hizi, si kwa Nabii wala kipo­fu; isipokuwa hali halisi ni kuwadharau na kuwatahayariza washirikina waliokabiliwa na Mtume kwa lengo la kuwavutia kwenye Uislamu; kwa Mwenyezi Mungu kumwambia Mtume wake: Una haraka gani ya nusra ya dini ya Mwenyezi Mungu mpaka ukafikia kuwa na tamaa ya kuongoka viumbe hawa waovu zaidi na walio mafisadi na wapotevu? Achana nao! Hawa ni watu duni zaidi wa kuinusuru dini ya Mwenyezi Mungu na hawana nguvu yoyote ya kuuendeleza Uislamu; kwani Mwenyezi Mungu atawadhalilisha maadui zake, hata wakiwa na nguvu kiasi gani, na ataidhi­hirisha dini yake kuwa juu ya dini zote wajapochukia washirikina.

Aya hizi ziko karibu katika maana yake na Aya isemayo:

فَلَا تَذْهَبْ نَفْسُكَ عَلَيْهِمْ حَسَرَاتٍ ۚ  {8}

“Basi roho yako isitoke kwa kuwasikitikia.” Juz. 22 (35:8).

Kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akagura kwenda kwenye ripoti ya kiu­jumla na uhakika ambayo ni ‘Mtukufu wenu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule mwenye takua zaidi katika nyinyi.’ Ameiripoti kwa mfumo mwingine ambao ni yule mwenye kucha akawa anajitakasa na kunufaika na mawaidha ndiye anayestahiki takrima na taadhima, lakini yule anayeikataa haki wala asinufaike na mawaidha, inapasa kumtupilia mbali na kumdharau, hata kama ni tajiri wa matajiri na bwana wa wenye jaha.

Maana

Alikunja uso na akageuka, kwa sababu alimjia kipofu ambaye ni Ibn Ummi Maktum aliyemkusudia Mtume (s.a.w.) ili amuulize maswali ya hukumu ya dini yake, lakini akamuacha kwa kushughulika kwake na jambo muhimu, kama tulivyotaja.

Kipofu huyu ni miongoni mwa wahajiri wa mwanzo mwanzo na ni mwad­hini wa pili wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.). Mara kwa mara alikuwa akimwakilisha Mtume (s.a.w.) kuswalisha watu Madina.

Inasemekana kuwa alizaliwa kipofu na jina lake ni Abdallah. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alimpa wasifu wa kipofu kwa kuashiria udhuru wake wa kuwa na hamu ya kujua masuala.

Na nini kitakujulisha huenda akatakasika au akakumbuka ukamfaa ukumbusho?

Yaani ni jambo gani linalokufanya ujue hakika ya kipofu huyu? Lau ungelijibu matakwa yake na ukamweleza baadhi ya hukumu za dini angelinufaika na kuyatumia yale utakayomfunza.

Ama anayejiona amejitosha, ndio wewe unamshughulikia?

Umemuacha yule aliye na haja na kumkabili yule anayejiona kuwa hana haja na Mwenyezi Mungu na wewe kutokana na mali anayomiliki na jaha; ukitarajia kuongoka kwake na kurejea kutoka kwenye upotevu. Je, unatara­jia uongofu kwa yule aliyepofushwa na matamanio na ujinga?

 أَفَأَنْتَ تَهْدِي الْعُمْيَ وَلَوْ كَانُوا لَا يُبْصِرُونَ {43}

“Je, wewe unaweza kuwaongoza vipofu ingawa hawaoni?” Juz. 11 (10:43).

Na si juu yako asipojitakasa.

Si juu yako wala juu ya Uislamu ukafiri wa kafiri na upotevu wake. Mfano wa Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَإِنْ تُعْرِضْ عَنْهُمْ فَلَنْ يَضُرُّوكَ شَيْئًا ۖ {42}

“Na ukiachana nao, hawatakudhuru chochote.” Juz. 6 (5:42).

Ama mwenye kukujia mbio mbio naye anaogopa ndio wewe unajipu­rukusha naye?

Umejishughulisha na washirikina na ukaghafilika na mumin aliyekukusu­dia wewe kufaidika na ilimu yako akitegemea imani yake na kwamba wakati wa mafunzo ni mpana; kwa hiyo achana na mataghuti na umkabili yule aliyeufungua moyo wake kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake.

Si hivyo! Mwenyezi Mungu hawezi kuinusuru dini yake kwa yule anayejiona amejitosheleza, akiwa hana haja na Mwenyezi Mungu wala wewe; kwa vile ana mali na cheo; isipokuwa nusra ya haki itakuja na watu wema, mfano wa kipofu huyu, hata kama ni fukara na masikini.

Hakika hizo ni ukumbusho, anayetaka amkumbuke.

Hizo ni hizo Aya za Qur’an au inawezekana kuwa ni huo uongofu.

Anayekumbukwa ni Mwenyezi Mungu au inawezekana kuwa ni, na aikumbuke hiyo Qur’an. Maana ni kuwa hakika hii Qur’an inatosheleza kuwa ni mwongozo kwa anayeutaka, na si juu yako ewe Muhammad isipokuwa kufikisha tu na kukumbusha; anayetaka naamini na anayetaka na akufuru; kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akaisifu hii Qur’an na mafun­zo yake na hukumu zake kwa kusema:

Zimo katika kurasa zilizohishimi­wa. Ni shani yake iliyoje na utukufu wake mbele ya Mwenyezi Mungu? Zenye kuinuliwa kwa kutukuzwa kutokana na mafunzo yake yenye kun­ufaisha na hikima yake ya hali ya juu zilizotakaswa zisichezewe na upote­vu.

Zimo mikononi mwa wajumbe, watukufu, wema.

Kurasa hizo za Mwenyezi Mungu ziko katika hifadhi isiyofikiwa wakizinukuu malaika kutoka kwa mtukufu aliye juu hadi kwa manabii wake walio maasumu, kwa umakini na uaminifu.

قُتِلَ الْإِنْسَانُ مَا أَكْفَرَهُ {17}

Ameangamia mtu, si ukafiri wake huo!

مِنْ أَيِّ شَيْءٍ خَلَقَهُ {18}

Kwa kitu gani amemuumba?

مِنْ نُطْفَةٍ خَلَقَهُ فَقَدَّرَهُ {19}

Kwa tone la manii amemuum­ba akamkadiria.

ثُمَّ السَّبِيلَ يَسَّرَهُ {20}

Kisha akamfanyia nyepesi njia.

ثُمَّ أَمَاتَهُ فَأَقْبَرَهُ {21}

Kisha akamfisha akamtia kaburini.

ثُمَّ إِذَا شَاءَ أَنْشَرَهُ {22}

Kisha anapotaka atamfufua.

كَلَّا لَمَّا يَقْضِ مَا أَمَرَهُ {23}

Si hivyo! Bado hajatekeleza aliloamrishwa.

فَلْيَنْظُرِ الْإِنْسَانُ إِلَىٰ طَعَامِهِ {24}

Hebu na atazame mtu chakula chake.

أَنَّا صَبَبْنَا الْمَاءَ صَبًّا {25}

Hakika tumeyamimina maji mminiko

ثُمَّ شَقَقْنَا الْأَرْضَ شَقًّا {26}

Kisha tukaipasua ardhi mpa­suko.

فَأَنْبَتْنَا فِيهَا حَبًّا {27}

Tukaotesha humo nafaka.

وَعِنَبًا وَقَضْبًا {28}

Na zabibu na mboga.

وَزَيْتُونًا وَنَخْلًا {29}

Na mizaituni na mitende.

وَحَدَائِقَ غُلْبًا {30}

Na mabustani yenye miti mingi.

وَفَاكِهَةً وَأَبًّا {31}

Na matunda na ndishwa.

مَتَاعًا لَكُمْ وَلِأَنْعَامِكُمْ {32}

Kwa ajili ya manufaa yenu na ya wanyama wenu.

فَإِذَا جَاءَتِ الصَّاخَّةُ {33}

Utakapokuja ukelele mkubwa.

يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ {34}

Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye.

وَأُمِّهِ وَأَبِيهِ {35}

Na mama yake na baba yake.

وَصَاحِبَتِهِ وَبَنِيهِ {36}

Na mkewe na wanawe.

لِكُلِّ امْرِئٍ مِنْهُمْ يَوْمَئِذٍ شَأْنٌ يُغْنِيهِ {37}

Kila mtu katika wao siku hiyo atakuwa na jambo la kum­tosha.

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ مُسْفِرَةٌ {38}

Siku hiyo kuna nyuso zitaka­zonawirika.

ضَاحِكَةٌ مُسْتَبْشِرَةٌ {39}

Zitacheka, zitafurahika.

وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌ {40}

Na nyuso nyingine siku hiyo zitakuwa na mavumbi.

تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ {41}

Zimefunikwa na giza.

أُولَٰئِكَ هُمُ الْكَفَرَةُ الْفَجَرَةُ {42}

Hao ndio makafiri waovu.

Aya 17 – 42: Ameangamia Mtu Si Ukafiri Wake Huo!

Maana

Ameangamia mtu, si ukafiri wake huo!

Makusudio ya ameangamia hapa ni kuduiwa mtu kwa kuombewa adhabu na maangamizi.

Amesema katika afsir Ar-Razi akinukuu kundi la wafasiri: “Makusudio ya mtu hapa ni kila tajiri aliyejiinua kwa mafukara kwa sababu ya utajiri na ufukara.” Sisi tuko pamoja na kauli hii, kwa sababu hali halisi inashuhudia hilo na kulipa nguvu. Lau si tamaa na ulafi wa kurundika mali angeliishi kila mtu katika raha na amani.

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Hakika kuduiwa huku kwa mtu kwa maduizo mabaya kabisa ni kinaya cha kuwa mtu amefikia ubaya ambao hastahili kuishi. Chimbuko la kinaya hiki ni ni kusahau kwake neema alizo nazo na kughafilika kwake mpaka akikumbushwa haki anakataa.”

Hakuna shaka kuwa kupatikana, kuwa na utambuzi, kusikia na kuona ni neema; bali ni katika neema kubwa, lakini neema hii haimpelekei mtu kujikuza na kupituka mipaka. Linalomtoa mtu mkosefu kwenye mipaka yake na kumpelekea kufanya dhulma na uadui ni kule kuhisi kwake kuwa ni tajiri na kutofautiana kwake na wengine.

Kwa kitu gani amemuumba? Kwa tone la manii amemuumba akamkadiria.

Makusudio ya kumkadiria ni kumtoa kwenye umbo moja hadi jingine na makuzi baada ya makuzi mengine. Maana ni una nini wewe mtu dhaifu mpaka ukawa unajizuia kumtii Mwenyezi Mungu na kujikuza kwa waja wake? Fikiria asili yako jinsi ulivyogura kutoka umbo moja hadi nyingine na mwenendo wako na mwishilio wako. Ni nani aliyekufanya uweko baada ya kutokuweko, na akakuanzisha kwenye tumbo la mama yako kuto­ka hali moja hadi nyingine. Kisha akakutoa katika umbo zuri? Je, sadfa ndio iliyoyafanya yote haya?

Kisha akamfanyia nyepesi njia.

Mtu ameandaliwa njia ya heri kwa mambo mawili: la kwanza ni kumuon­goza kwenye hiyo heri na kumhimiza. La pili, ni akili na uwezo wa kufanya. Vile vile ameandaliwa njia ya maisha kwa mambo mawili: Kwanza, ni maumbile ya heri zinazotosheleza mahitaji yake. Pili, ni nguvu na maandalizi ya kuweza kuzitumia heri hizo vile atakavyo.
Umetangulia mfano wake katika Aya kadhaa ikiwemo ile iliyoko Juz. 29 (76:1-3).

Kisha akamfisha, baada ya kwisha muda wake, akamtia kaburini.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameamrisha kuzikwa mtu baada ya kufa kwake na akakataza kutupiwa wanyama na ndege, kwa kuashiria heshima ya mtu mbele ya Mwenyezi Mungu hata akiwa amekufa; sikwambii tena akiwa hai.

Kisha anapotaka atamfufua.

Amemuumba, akamfisha, akamtia kaburini kisha atamfufua, kama alivyokuwa mwanzo, kwa ajili ya hisabu na malipo. Lau si ufufuo huu ingelikuwa kuwako mtu ni mchezo ndani ya mchezo. Tazama Juz. 11 (10:4) kifungu ‘Hisabu na malipo ni lazima,’ Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Kisha anapotaka,’ inafahamisha kuwa Yeye pekee ndiye anayejua lini utakua ufufuo na mkusanyiko.

Si hivyo! Bado hajatekeleza aliloamrishwa.

Ambaye hajatekeleza hapa ni mtu mwenye makosa anayepuuza. Maana ni kuwa tumempa mtu nishati zote za kufanya heri na mambo mema, wala hatukumwachia visababu vya kutoa, lakini pamoja na hayo watu wengi wamepuuza na kufanya uzembe; bali wengi katika wao wamepituka mipa­ka na kufanya dhulma, wakazifanya neema za Mwenyezi Mungu ni nyen­zo za ufisadi na kuwafanyia uadui waja. Hebu na atazame mtu chakula chake kilicho mbele yake ambacho ni mhimili wa uhai wake na kuweko kwake.

Aangalie na aiulize akili yake ni nani aliyemsahilishia chakula hiki? Je, ni maumbile? Basi ni nani aliyeyaleta hayo maumbile? Je, ni sadfa? Je, sadfa ina akili ya kukadiria na kupangilia kuweza kuleta maumbile yenye sababu za chakula na kinywaji na mengineyo ya ufundi wa hali ya juu?

Hapana! Hakika tumeyamimina maji mmiminiko. Ni Mwenyezi Mungu tu pekee ndiye aliyeyaleta maji na akayateremsha kutoka mbinguni.

Tumewahi kuelezea mara nyingi kwamba dhahiri ya maumbile inatege­mezwa kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu, kwa sababu Yeye ndiye chim­buko la kuweko yote na ndiye msababishi wa sababu.

Kisha tukaipasua ardhi mpasuko, tukaotesha humo nafaka na zabibu na mboga; yaani mimea inapasua ardhi ili itoke; kama kifaranga kinavy­opasua ganda la yai na kutoka mahali alipokuwako.

Na mizaituni na mitende, na mabustani yenye miti mingi; yaani bustani zenye miti na matunda mengi na pia vivuli vyake na uzuri wake.

Na matunda na ndishwa, kwa ajili ya manufaa yenu na ya wanyama wenu.

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Imepokewa kwamba Abu Bakr ali­ulizwa kuhusu neno Abb (tulilolifasiri kwa maana ya ndishwa), akasema: “Ni mbingu gani itakayonifunika na ni ardhi gani itakayonimeza, nikisema katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu sijui?”

Anaendelea kusema Sheikh Muhammad Abduh: “Imepokewa kutoka kwa Umar Bin Al-khattwab, kwamba yeye alisoma Aya hii akasema: “Yote haya tumeyajua, lakini ni nini abb?” Akavunja fimbo iliyokuwa mkononi mwake, akasema: “Naapa kwa Umri wangu! Hii ndio taklifa, huna neno ewe mwana wa mamie Umar kutojua nini abb…’’ Usidhanie kuwa Sayyidna Umar anakataza kufuatilia maana ya Qur’an; isipokuwa anataka kukufahamisha kuwa lililo wajibu kwako, kama mumin ni kufahamu maana kiujumla.”

Utakapokuja ukelele mkubwa unaziba masikio kukaribia kufanya kizi­wi.

Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye, na na mama yake na baba yake, na mkewe na wanawe. Kila mtu katika wao siku hiyo atakuwa na jambo la kumtosha.
Siku ya Kiyama hakuna mapenzi wala nasabu, kwa sababu kila mtu atakuwa anajishughulikia mwenyewe bila ya kumwangalia mwingine. Hii ni kuashiria kwamba wale anaowapupia mtu duniani na kumuasi Mwenyezi Mungu kwa ajili yao, hawatamfaa kitu akhera wala yeye hatawafaa na chochote.

Katika baadhi ya tafsir imeelezwa kuwa, kutajwa ndugu katika Aya kumekuja kwa mpangilio wa kimaumbile yalivyo; kwa kutangulizwa ndugu kisha wazazi na mwisho mke na watoto.

Kwani mapenzi ya mtu kwa wazazi wake yana nguvu zaidi kuliko ya nduguye, na mapenzi kwa mkewe na wanawe yana nguvu zaidi kuliko ya wazazi wake; ni kama kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: Mtu atamkimbia nduguye, hata mama yake na baba yake pia, bali hata mkewe na wanawe.

Siku hiyo kuna nyuso zitakazonawirika, zitacheka, zitafurahika kwa kufurahia malipo makubwa na ya heshima aliyoziandalia Mwenyezi Mungu.

Na nyuso nyingine siku hiyo zitakuwa na mavumbi, zikiwa zimesawiji­ka kwa huzuni. Zimefunikwa na giza la udhalili na uduni. Hao ndio makafiri waovu.

Ukafiri kuupa sifa ya uovu kunaashiria kwamba muovu mwenye kuangamiza yuko sawasawa na kafiri mbele ya Mwenyezi Mungu, hata kama atadumisha swala tano kwa nyakati zake.

Sheikh Muhammad Abduh ana maneno marefu kuhusiana na Aya hii tutayafupiliza kwa namna ifuatayo: Mwenye kuitafuta haki kwa njia ya haki na akaitumia, au akafikiwa na mauti akiwa bado anaitafuta, huyo ndiye atakayecheka na kufurahi Siku ya Kiyama, kwa fadhilia ya Mwenyezi Mungu.

Na mwenye kuidharau akili yake, akajishughulisha na visababu vya kufuata matamanio na akashikamana na ubatilifu, kama walivyokuwa wakifanya maadui wa manabii, basi huyo ndiye ambaye uso wake utafunikwa na giza la huzuni na vumbi la udhalili Siku ya Kiyama.

Hayo ni kutokana na kuwa dini inakataza maovu na yeye anayafanya, dini inaamuru kuchunga masilahi ya umma na yeye anayavunja, dini inawata­ka watu kujitolea mali katika njia ya heri, yeye anaipora ili aitumie katika njia ya shari, dini inaamuru uadilifu na yeye ndiye dhalimu wa madhalimu, dini inaamuru kusema ukweli, yeye anasema uwongo na kuwapenda waon­go… Mwenye kuwa katika hali hii atakuwaje siku atayojitokeza Aliye jabari na kuondoka sitara!

  • 2933 views

Sura Ya Themanini Na Mmoja: At-Takwir

Imeshuka Makka Ina Aya 29.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

إِذَا الشَّمْسُ كُوِّرَتْ {1}

Jua litakapokunjwa kunjwa.

وَإِذَا النُّجُومُ انْكَدَرَتْ {2}

Na nyota zitakapoanguka.

وَإِذَا الْجِبَالُ سُيِّرَتْ {3}

Na milima itakapoondolewa.

وَإِذَا الْعِشَارُ عُطِّلَتْ {4}

Na ngamia wenye mimba watakapotupiliwa mbali.

وَإِذَا الْوُحُوشُ حُشِرَتْ {5}

Na wanyama pori watakapokusanywa.

وَإِذَا الْبِحَارُ سُجِّرَتْ {6}

Na bahari zitakapofurika.

وَإِذَا النُّفُوسُ زُوِّجَتْ {7}

Na nafsi zitakapounganishwa.

وَإِذَا الْمَوْءُودَةُ سُئِلَتْ {8}

Na msichana aliyezikwa hai atakapoulizwa.

بِأَيِّ ذَنْبٍ قُتِلَتْ {9}

Ni kwa dhambi gani aliuawa?

وَإِذَا الصُّحُفُ نُشِرَتْ {10}

Na madaftari yatakapoenezwa.

وَإِذَا السَّمَاءُ كُشِطَتْ {11}

Na mbingu itakapotanduliwa.

وَإِذَا الْجَحِيمُ سُعِّرَتْ {12}

Na moto utakapokokwa.

وَإِذَا الْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ {13}

Na Pepo itakaposogezwa.

عَلِمَتْ نَفْسٌ مَا أَحْضَرَتْ {14}

Itajua kila nafsi ilichokihud­hurisha.

Aya 1 – 14 : Jua Litakapokunjwa Kunjwa

Maana

Katika Aya hizi Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameashiria yatakayotokea Siku ya Kiyama hadi saa ya hisabu; kama ifutavyo:-
Jua litakapokunjwa kunjwa.

Neno kukunjwa tumelifasiri kutokana na neno takwir lenye maana ya kukunja kwa kuviringa, kama kichwa kukiviringa kilemba. Sababu ya kukunjwa kunjwa jua ni uharibifu utakaolipata.

Na nyota zitakapoanguka.

Neno lililotumika ni Inkadar, lenye maana ya kuanguka kichwa chini miguu juu. Makusudio yake hapa ni kuanguka nyota na kutawanyika. Mahali pengine Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

وَإِذَا الْكَوَاكِبُ انْتَثَرَتْ {2}

“Na nyota zitakapopukutika.’’ (82:2).

Na milima itakapoondolewa kutoka sehemu zake na kuwa hewani.

Na ngamia wenye mimba watakapotupiliwa mbali.

Hawa ni mali ya thamani kubwa sana kwa waarabu. Hiki ni kinaya cha shida na vituko vya siku hiyo ambapo mtu atasahau kila kitu.

Na wanyama pori watakapokusanywa.

Watakurupuka kwa hofu. Mwenye Majmaul-Bayan na Razi wanasema kuwa Mwenyezi Mungu atawakusanya wanyama ili walipane visasi. Lakini inavyoeleweka ni kuwa Mwenyezi Mungu hahisabu mpaka akali­fishe, wala hakalifishi mpaka atoe akili. Kwayo hutoa thawabu na kwayo hutoa adhabu. Lau wanyama wangelikuwa na akili wangelijikinga na wanadamu na wangelikuwa sawa nao.

Na bahari zitakapofurika.

Neno kufurika tumelifasiri kutokana na neno sujjira ambalo miongoni mwa maana zake ni kujaa kupita kiasi. Kwa hiyo maana yake ni kuwa maji ya bahari yatafurika huku na huko bila ya kuwa na kizuizi chochote, ikiwa ni natija ya kuharibika ulimwengu mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu: Na bahari zitakapopasuliwa. (82:3).

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Inawezekana kuwa maana ni kuwa­ka moto, kwa sababu moto ulioko ndani ya ardhi huwa unajitokeza inapopasuka, hapo maji ya bahari yatageuka moshi na kuisha na hakutabakia kitu baharini isipokuwa moto. Imepokewa hadith kuwa bahari ni kifuniko cha Jahannam. Utafiti wa ilimu umethibitisha hilo na kushuhudiwa na volkano na matetemeko ya ardhi.”

Na nafsi zitakapounganishwa na viwiliwili; yaani kila nafsi itarudi kwenye mwili wake wa kwanza ilioachana nao. Na msichana aliyezikwa hai atakapoulizwa, ni kwa dhambi gani ali­uawa? Ili liwe ni tukio gumu kwa yule aliyemzika akiwa hai. Tazama Juz.14 (16:59).

Na madaftari yatakapoenezwa.

Kesho kila mtu atapewa kitabu cha matendo yake yawe ya heri au ya shari. Inawezekana haya kuwa ni kinaya cha kuwa Siku ya Kiyama matendo ya waja yatawadhihirikia kwa ukamilifu, kama yalivyokuwa. Vyovyote iwavyo si wajibu kutafiti uhakika wa madaftari hayo.

Na mbingu itakapotanduliwa; yaani zitaondolewa nyota zilizokuwa zimefunika yaliyo nyuma yake; kama inavyoondolewa ngozi ya mnyama aliyechinjwa na kuonekana nyama iliyokuwa imeifunika.

Na moto utakapokokwa uwake.

Na Pepo itakaposogezwa.
Itasogezewa watu wake na wao wataisogelea, kwa sababu imeandaliwa wao na wao wamejiaanda nayo. Mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na Pepo italetwa karibu kwa wenye takua, haitakuwa mbali.” Juz. 26 (50:31)

Itajua kila nafsi ilichokihudhurisha.

Hili ndilo jawabu la mambo yote hayo 12 yaliyopita (jawabushart). Maana ni kuwa yatakapotokea hayo yaliyotajwa, kila mtu ataletwa kwa Mola wake akiwa anajua amechukua matendo gani na amejibebea akiba gani, ya heri au ya shari. Imeelezwa katika Nahjul-balagha imesemwa: “Hakika msafiri anayekwenda ‧ kwa Mola wake ‧ kwa kufaulu au kutofaulu anas­tahiki maandalizi bora. Basi jiandalieni masurufu i mkiwa duniani ambayo mtajihifadhi nafsi zenu kwayo.”

فَلَا أُقْسِمُ بِالْخُنَّسِ {15}

Naapa kwa zinazorejea nyuma,

الْجَوَارِ الْكُنَّسِ {16}

Zinazokwenda kwa kujificha.

وَاللَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ {17}

Na kwa usiku unapopungua.

وَالصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ {18}

Na asubuhi inapopumua.

إِنَّهُ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ {19}

Hakika hiyo bila shaka ni kauli ya mjumbe mtukufu.

ذِي قُوَّةٍ عِنْدَ ذِي الْعَرْشِ مَكِينٍ {20}

Mwenye nguvu, mwenye cheo mbele ya mwenye Arshi.

مُطَاعٍ ثَمَّ أَمِينٍ {21}

Mwenye kutiiwa huko mwaminifu.

وَمَا صَاحِبُكُمْ بِمَجْنُونٍ {22}

Na mwenzenu si mwendawaz­imu.

وَلَقَدْ رَآهُ بِالْأُفُقِ الْمُبِينِ {23}

Hakika alimuona katika upeo ulio wazi.

وَمَا هُوَ عَلَى الْغَيْبِ بِضَنِينٍ {24}

Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.

وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَانٍ رَجِيمٍ {25}

Na wala si kauli ya shetani aliyekufukuzwa.

فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ {26}

Basi mnakwenda wapi?

إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِلْعَالَمِينَ {27}

Haikuwa hiyo ila ni ukum­busho kwa walimwengu wote.

لِمَنْ شَاءَ مِنْكُمْ أَنْ يَسْتَقِيمَ {28}

Kwa anayetaka katika nyinyi kuwa sawa.

وَمَا تَشَاءُونَ إِلَّا أَنْ يَشَاءَ اللَّهُ رَبُّ الْعَالَمِينَ {29}

Na hamtataka isipokuwa atake Mwenyezi Mungu Mola wa walimwengu.

Aya 15 – 29: Kwenda Nyuma Na Kujificha

Maana

Naapa

Tumetangulia kusema huko nyuma kwamba herufi la hii kwa mujibu wa wafasiri wengi ni ziada ya kiirabu, na kwa wengine ni ya kukanusha, kwa misingi ya kuwa jambo liko wazi halihitajii kiapo.

Natija ya kauli zote mbili ni moja tu. Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Ibara hii inaletwa ikiwa inakusudiwa kuadhimishwa kinachoapiwa, na hakika hakiadhimish­wi kwa kuapiwa kwa sababu chenyewe ni adhimu.”

Kwa zinazorejea nyuma, zinazokwenda kwa kujificha

Makusudio yake hapa ni nyota zote. Imesemekana kuwa ni nyota tano tu: Zebaki, Zuhura, Mars Mushtara na Zohali. Nazo zinakwenda kwa sababu zinazunguka kwenye falaki yake.

Wametofautiana kuwa kwa nini zimepewa sifa ya kurudi nyuma na kuji­ficha?

Sheikh Muhammad Abduh anasema kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amezisifu kwa kujificha kwa sababu hazionekani kwenye mwanga wa jua, kama anavyojificha paa kwenye nyumba yake na amezisifu kwa kurejea, kwa vile zinarudi kuonekana baada ya kupotea jua.

Hii inaafikiana na natija ya tafsir ya Tabrasi katika ajmaul-bayan ali­posema, ninamnukuu: “Ni nyota zinazorudi kujificha mchana na kuji­tokeza usiku.”

Tofauti baina ya tafsiri mbili nikuwa kwa Mwenye Majmau kurudi ni kuji­ficha na kwa Muhammad Abduh ni kujitokeza, lakini natija ni moja.

Hali yoyote iwayo ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameapa kwa nyota kutanabahisha utengenezaji wake kwenye dalili ya uweza wa mtengeneza­ji na hikima yake.

Na kwa usiku unapopungua na asubuhi inapopumua.

Neno kupungua tumelifasiri kutokana na neno A’s-a’s lenye maana ya kuondoka na kurudi. Hiki ni kiapo cha pili, kutoka kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kuondoka usiku na kuja mchana, kwa sababu ameunganisha kwenye kiapo. Katika kitabu uhawalatu fahmil Asril lil ur’an anasema: “Unasoma Qur’an nayo inaacha mdundo, athari na picha kwenye masikio. Wakati Mwenyezi Mungu anapoapa kwa usiku na mchana anatumia neno A’s-a’s. Hizi herufi nne ndio usiku, kwa kuleta sura ya kila yaliyomo ndani yake. Na asubuhi inapopumua. Hakika mwanga wa alfajiri hapa unaonekana na kusikikika. Hakika wewe unakurubia kusikia sauti mwanana ya ndege na kuwika jogoo.”

Hakika hiyo bila shaka ni kauli ya mjumbe mtukufu mwenye nguvu, mwenye cheo mbele ya mwenye Arshi.

Hiyo ni Qur’an, imefahamika hivyo kutokana na mfumo wa maneno. Mjumbe ni Jibril, Mwenyezi Mungu ameitegemeza Qur’an kwa Jibril kwa vile yeye ndiye anayeichukua na kuinukuu kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.). Mwenye Arshi ni Mwenyezi Mungu. Jibril ana cheo na heshima mbele ya Mwenyezi Mungu, ni mwaminifu wa uteremsho, ana nguvu kulitekeleza hilo na mengineyo katika kazi anazoziwakilisha. Umetangulia mfano wake katika Juz. 27 (53:5-6).

Mwenye kutiiwa huko mwaminifu.

Huko ni ishara ya mahali anakotiiwa Jibril nako ni ulimwengu wa ghaibu ambao haujui hakika yake isipokuwa Mwenyezi Mungu.

Na huyu mwenzenu si mwendawazimu.

Maneno yanaelekezwa kwa vigogo wa kikuraishi, mwenzao ni Muhammad (s.a.w.) ambaye baadhi yao walimbandika uwazimu: “Na walisema:

يَا أَيُّهَا الَّذِي نُزِّلَ عَلَيْهِ الذِّكْرُ إِنَّكَ لَمَجْنُونٌ {6}

“Ewe uliyeteremshiwa ukumbusho! Wewe ni mwendawazimu.” Juz. 14 (15:6).

Mwenyezi Mungu hapa anamwondelea wanayomzulia. Umetangulia mfano wake katika Juz. 29 (68:2).

Hakika alimuona katika upeo ulio wazi.

Mnamwambia Muhammad ni mwendawazimu wakati anawapa habari ya Pepo na Moto? Hapana! Hakika Qur’an ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu, alioletewa na Jibril alipomuona kwenye upeo ulio wazi akiwa kwenye sura yake na uhakika wake alivyo, alimuona kiukweli usiokuwa na shaka. Umetangulia mfano wake katika Juz. 27 (53:5-12).

Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.

Yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) na ghaibu ni Qur’an. Maana ni kuwa Muhammad hakuwa ni mwenye kuificha Qur’an na kunyamazia kuitangaza haki, kwa kuwahofia nyinyi washirikina kumwambia kuwa ni mwendawazimu; bali anaitangaza waziwazi bila ya kuhofia lawama.

Na wala si kauli ya shetani aliyekufukuzwa.

Hii ni kuyarudi madai yao kuwa anayoyasema Mtume yamepuziwa na shetani kwenye ulimi wake. Shetani kweli anaweza kufahamisha uongofu na heri au haki na uadilifu?

Basi mnakwenda wapi kwenye hukumu yenu na upotevu?

Haikuwa hiyo ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

Qur’an ni yenye kuamarisha heri na kuikemea shari. Zaidi ya hayo yote ndani yake mna ubainifu wa kila kitu, vipi itakuwa ni kauli ya shetani?

Kwa anayetaka katika nyinyi kuwa sawa.

Qur’an ni uongozi na wema kwa yule mwenye kupendelea uongofu na usawa. Ama mwenye kung’ang’ania upotevu hatanufaika na ukumbusho wala kuathirika na mawaidha.

Na hamtataka isipokuwa atake Mwenyezi Mungu Mola wa wal­imwengu.

Razi anasema Aya hii inafahamisha kuwa mtu ni mwenye kuendeshwa hana hiyari. Lakini anajibiwa kuwa maana ya Aya ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anamtakia mja wake kufuata haki na uadilifu, lakini mpin­zani anakataa isipokuwa upotevu tu, wala hawi sawa, ila akilazimishwa na Mwenyezi Mungu na hilo linapingana na uadilifu wa Mwenyezi Mungu na hikima yake.

Kwa maneno mengine ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemuumba mtu akiwa na hiyari, mwenye akili na utashi, na akamtofautisha na mnya­ma kwa hilo. Kutokana na hilo ndio akamkalifisha utiiifu kinyume cha mwenginewe. Lau angelitaka Mwenyezi Mungu angelimnyang’anya mtu utashi wa akili na kumfanya kama mnyama au chini ya mnyama.

  • 2464 views

Sura Ya Themanini Na Mbili: Al-Infitar

Imeshuka Makka Ina Aya 19.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu

إِذَا السَّمَاءُ انْفَطَرَتْ {1}

Mbingu itakapopasuka.

وَإِذَا الْكَوَاكِبُ انْتَثَرَتْ {2}

Na nyota zitakapopukutika.

وَإِذَا الْبِحَارُ فُجِّرَتْ {3}

Na bahari zitakapopasuliwa.

وَإِذَا الْقُبُورُ بُعْثِرَتْ {4}

Na Makaburi yatakapofukuli­wa.

عَلِمَتْ نَفْسٌ مَا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ {5}

Itajua nafsi ilichokitanguliza na ilichokibakisha nyuma.

يَا أَيُّهَا الْإِنْسَانُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ الْكَرِيمِ {6}

Ewe Mtu! Nini kilichokughuri na Mola wako mkarimu?

الَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّاكَ فَعَدَلَكَ {7}

Aliyekuumba, akakuweka sawa, akakulinganisha?

فِي أَيِّ صُورَةٍ مَا شَاءَ رَكَّبَكَ {8}

Katika sura yoyote aliyopenda amekutengeneza.

كَلَّا بَلْ تُكَذِّبُونَ بِالدِّينِ {9}

Si hivyo! Bali mnakadhibisha malipo.

وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَافِظِينَ {10}

Na hakika bila shaka juu yenu kuna walinzi.

كِرَامًا كَاتِبِينَ {11}

Waandishi wenye heshima.

يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ {12}

Wanaojua mnayoyafanya.

إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ {13}

Hakika wema watakua katika nema.

وَإِنَّ الْفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٍ {14}

Na hakika waovu watakuwa katika moto.

يَصْلَوْنَهَا يَوْمَ الدِّينِ {15}

Watauingia siku ya malipo.

وَمَا هُمْ عَنْهَا بِغَائِبِينَ {16}

Na hawatakuwa mbali nao.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ {17}

Na ni lipi lakukujulisha ni ipi siku ya malipo?

ثُمَّ مَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ {18}

Kisha ni lipi la kukujulisha ni ipi siku ya malipo?

يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌ لِنَفْسٍ شَيْئًا ۖ وَالْأَمْرُ يَوْمَئِذٍ لِلَّهِ {19}

Ni siku ambayo nafsi haitakuwa na mamlaka juu ya nafsi nyingine; Na amri siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu.

Maana

Sura hii, kwa ukamilifu wake ni sawa na sura iliyotangulia, inaonyesha picha ya baadhi ya matukio ya Kiyama na yatakayofuatia baadae, ya his­abu na malipo.

Mbingu itakapopasuka.

Itapasuka na nyota kuanguka, mfano wake ni:

فَإِذَا انْشَقَّتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ وَرْدَةً كَالدِّهَانِ {37}

“Itakapopasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.” Juz. 27 (55:37).

Na nyota zitakapopukutika zitawanyike na kuharibika.

Na bahari zitakapopasuliwa.

Mawimbi yatainuka na kuchanganyika mashariki na magharibi. Au maji yake yatafuka moshi na kujitokeza moto kutoka ndani. Tazama mwanzo mwanzo mwa sura iliyo kabla ya hii.

Na Makaburi yatakapofukuliwa.

Neno “kufukuliwa” tumelifasiri kutokana na neno la kiarabu Bu’thira lenye maana ya kukifumua kitu ndani kuwa nje au nje kuwa ndani. Makusudio yake hapa nikwamba Kiyama kitakua tu, hakuna shaka: “Na hakika Mwenyezi Mungu atawafufua walioma makaburini.” Juz. 17 (22:7).

Itajua nafsi ilichokitanguliza na ilichokibakisha nyuma.

Baada ya ufufuo kila mtu atajua kilichofanywa mikono yake, kiwe cha heri au shari, na ilichokiwacha.

Ewe Mtu! Nini kilichokughuri na Mola wako mkarimu aliyekuumba, akakuweka sawa, akakulinganisha?

Kukuweka sawa nikukupa nguvu za dhahiri na batini zilizokufanya uwe mtu kamili. Kukulinganisha ni kujaalia viungo vyako kuwa na uwiano, hakufanya mkono wako mmoja kuwa mrefu na mwingine kuwa mfupi, wala moja ya macho yako kuwa dogo au baadhi ya viungo vyako kuwa vyeusi na vingine kuwa vyeupe n.k.

Wametofautiana kuhusu neno Mkarimu hapa. Wengine wamesema kuwa Mwenyezi Mungu amejisifu kwa ukarimu ili amfundishe mja wake mwenye dhambi jawabu, atakapoulizwa kesho kuhusu dhambi zake aseme: Umenighuri msamaha wako na ukarimu wako.

Sheikh Muhammad Adul amesema kuwa hii ni kuchezea taawili na ni upotevu kwa kuangalia kitabu cha Mwenyezi Mungu. Usawa ni kufasiri ukarimu hapa kwa maana ya utukufu katika sifa zake zote, na kwamba aliye hivyo hatamwacha mja wake, bure bure bila ya swali wala malipo, bali atamuhisabu na kumpa thawabu mwema na kumwadhibu muovu. Kwa hiyo basi inatakikana kwa mtu kutoghurika na dunia na mapambo yake.

Imam Ali (a.s.) ana maneno marefu kuhusiana na Aya hii aliyoyaunganisha pamoja na khutba. Kwa ufupi wa ujumla wake ni kama ifuatavyo:
Ni lipi lililokupa ujasiri ewe mtu mpaka ukamuasi Mola wako na hali wewe unaishi kwenye himaya yake na unaogelea kwenye neema zake? Je, kumekudanga kukupatia wewe neema zake na huku unamtawalisha mwingine asiyekuwa Yeye? Hivi hujui kuwa hii ni fadhila kwako itokayo kwake, na anakupa muda ili urudi kwenye uongofu wako na uache upote­vu wako?

Kwa hiyo basi makusudio ya ukarimu wake Mwenyezi Mungu ni kumpa muda mja wake mwenye dhambi kwamba aharakishe kutubia na kurejea na asighurike na huku kupewa muda bila ya kuadhibiwa haraka.

Katika sura yoyote aliyopenda amekutengeneza.

Baadhi ya wafasiri wamesema yaani hakukufanya nguruwe au punda. Wengine wakasema: Alikuweka kwenye sura kama alivyotaka uwe mrefu au mfupi, mweusi au mweupe. n.k. Tunavyofahamu kutokana na Aya hii ni kuwa: Fikiria ewe mtu katika mpangilio wa maumbile yako ili utambue ukuu wa Mwenyezi Mungu kati­ka kuumba kwake, na kwamba yule aliyekuumba katika umbile zuri anaweza kukurudisha kwenye uhai mara nyingine.

Si hivyo! Bali mnakadhibisha malipo.

Acheni upotevu wenu usiokuwa na chimbuko lolote zaidi ya kukadhibisha ufufuo. Nyinyi mtahisabiwa tu, yale mliyokuwa mkiyafanya.

Na hakika bila shaka juu yenu kuna walinzi, waandishi wenye heshi­ma, wanaojua mnayoyafanya ya kheri au shari wala hakuna linalofichi­ka kwao. Maana ya wenye hishima ni kuwa wao wana nguvu na ni waaminifu katika kutekeleza wajibu wao kwa njia ya ukamilifu.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 25 (43:80).

Ilivyo ni kuwa lililo wajibu kwetu ni kujua tu, kuwa matendo yetu yanahi­fadhiwa na kudhibitiwa. Ama yanahifadhiwa vipi na kwa kitu gani hayo hatuna majukumu nayo.

Hakika wema watakua katika nema na hakika waovu watakuwa kati­ka moto, watauingia siku ya malipo.

Wema ni wale wakweli na wakatenda mema. Malipo yao mbele ya Mola wao ni maghufira na ujira mwema. Waovu ni wale wanaoneza ufisadi katka ardhi na malipo yao ni kuingia motoni.

Na hawatakuwa mbali nao hata kidogo, ni adhabu tu ya kudumu .

Na ni lipi la kukujulisha ni ipi siku ya malipo?

Wewe hujui uhakika wa siku ya malipo. Iko zaidi ya unavyofikira kwa shida na vituko vyake.

Kisha ni lipi la kukujulisha ni ipi siku ya malipo?

Huu ni msisitizo na kuipa uzito siku hiyo.

Ni siku ambayo nafsi haitakuwa na mamlaka juu ya nafsi nyingine.

Hakuna yeyote atakayekuwa na mamlaka ya manufaa wala madhara siku hiyo kwa ajli ya nafsi yake wala ya mwingine.

Na amri siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu.

Yeye ndiye pekee atakayeamuru na kukataza, hakuna mshauri wala mtetezi, bali hakuna muombezi isipokuwa atakayeruhusiwa na Mwenyezi Mungu na akasema kweli.

  • 1575 views

Sura Ya Themanini Na Tatu: Al-Mutaffifin

Imeshuka Makka Ina Aya 36.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu

وَيْلٌ لِلْمُطَفِّفِينَ {1}

Ole wao wanaopunja!

الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ {2}

Ambao wakipimia kwa watu wanakamilisha.

وَإِذَا كَالُوهُمْ أَوْ وَزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ {3}

Na wanapowapimia kwa kipi­mo au mizani wao hupunguza.

أَلَا يَظُنُّ أُولَٰئِكَ أَنَّهُمْ مَبْعُوثُونَ {4}

Hivi hawadhani wao kwamba watafufuliwa.

لِيَوْمٍ عَظِيمٍ {5}

Katika siku kubwa.

يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ {6}

Siku watakaposimama watu mbele ya Mola wa walimwen­gu wote?

كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٍ {7}

Si hivyo! Hakika maadishi wawaovu yamo katika sijjin.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا سِجِّينٌ {8}

Ni lipi la kukujulisha nini Sijjin?

كِتَابٌ مَرْقُومٌ {9}

Ni daftari lililoandikwa.

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ {10}

Ole wao siku hiyo wenye kukadhibisha.

الَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ {11}

Ambao wamekadhibisha siku ya malipo.

وَمَا يُكَذِّبُ بِهِ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ {12}

Na haikadhibishi ila kila mwenye kupituka mipaka mwenye dhambi.

إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ {13}

Anaposomewa Aya zetu huse­ma: Ni ngano za watu wa kale!

كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِمْ مَا كَانُوا يَكْسِبُونَ {14}

Si hivyo! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao waliyokuwa wakiyachuma.

كَلَّا إِنَّهُمْ عَنْ رَبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَمَحْجُوبُونَ {15}

Si hivyo! Hakika wao siku hiyo kwa Mola wao watakingi­wa pazia.

ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُو الْجَحِيمِ {16}

Kisha hakika wao watauingia moto.

ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا الَّذِي كُنْتُمْ بِهِ تُكَذِّبُونَ {17}

Kisha waambiwe haya ndiyo mliyokuwa mkiyakadhibisha.

Aya 1 – 17: Ole Wao Wanaopunja

Maana

Ole wao wanaopunja.

Neno ‘ole’ ni maagamizi na adhabu wanaopunja ni kikundi cha wenye nguvu wakifanya biashara kwa chakula chao na mali yao, wanauza na kununua, lakini wao wananunua kwa thamani ndogo na wanauza kwa bei ghali. Katika hali zote mbili wao wanahakikisha faida kubwa. Wanawakandamiza watu kwa njia ya ulanguzi au kwa njia nyingineyo kufanya dhulma yao; wakitafutia visababu vya jina la uhuru wa kazi au soko huria.

Kutokana na maendeleo ya mifumo ya unyonyaji kila wakati unavyoende­lea, maendeleo ya elimu, ugunduzi wa masoko na upatikanaji wa mafuta na madini mengineyo, kumewafanya walanguzi wapate nyenzo bora za kurundika utajiri kwa hali ya juu.

Historia ya upunjaji inaanza kutokana na aliyoyaashiria Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwa kauli yake:

Ambao wakipimia kwa watu wanakamilisha na wanapowapimia kwa kipimo au mizani wao hupunguza.

Wanapima kwa ujazo au kwa uzani lakini wanachukua zaidi na wanatoa pungufu. Hii inafahamisha kuwa wapunjaji walikuwa na nguvu ya kuwalazimisha watu kufanya wanavyotaka. Inawezekana nguvu hiyo ni ya mali, cheo, ulanguzi au nyingineyo. Muhimu kwao ni faida kwa namna yoyote itakavyokuwa.

Vyovyote itakavyokuwa maana ya kupunja ni kuwa makusudio hapa ni kuchukua kwa watu kwa ubatilifu na dhuluma.
Hivi hawadhani wao kwamba watafufuliwa katika siku kubwa, siku watakaposimama watu mbele ya Mola walimwengu wote?

Tuchukulie kuwa wanaokula mali za watu kwa batili hawaamini kukutana na Mwenye Mungu na moto wake au pepo yake, lakini hata hawadhanii angalau kuweko uwezekano wa hilo?

Kule kudhania tu kwamba mtu atasimama mbele ya Mola wake kwa his­abu, basi kunatosha kumkanya. Vipi mtu anaweza kuchukua hadhari, kwa yale anayodhania au kuyawazia tu kuwa yana madhara kidogo katika maisha ya dunia, lakini hachukui hadhari anapodhania kuwa yeye ataku­tana na Mola wake ambaye haachi dogo wala kubwa ila hulidhibiti? Pengine akiwa amekata kabisa bila ya kuwa na shaka yoyote.

Si hivyo! Wanaokula mali za watu kwa batili hawadhani kwamba wao watafufuliwa, katika siku kubwa, siku wakayosimama watu mbele ya Mwenyezi Mungu kwa hisabu na malipo.

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Hakuna tofauti baina ya anayeikana siku ya mwisho na yule mwenye kuleta tafsiri nyingine ya kujikinga na adhabu na kuokoka na hisabu. Kwa sababu kuleta tafsiri nyingine hakumwepushi mtu na daraja ya kukana, bali yuko pamoja naye motoni palipo na makazi mabaya.

Hakika maadishi wa waovu yamo katika sijjin.

Wametofautina katika maana ya neno ijjin. Kauli iliyo karibu zaidi na ufahamu ni kuwa hilo ni jina la masjala ambapo huthibitishwa majina ya waovu: Rai hii ndiyo aliyokwenda nayo mwenye ajamau aliposema: “Ndio dhahiri ya kisomo” Sheikha Muhammad Abduh amemwafiki hilo.

Imesemekana kuwa makusudio yake ni jela kwa maana ya kufungiwa.

Ni lipi la kukujulisha nini Sijjin.

Ni nani aliyekufanya uijue na ilimu yake iko kwa Mwenyezi Mungu peke yake?

Ni daftari lililoandikwa, ndani yake mkiwa na alama za kujulisha maten­do ya waovu.

Ole wao siku hiyo wenye kukadhibisha, ambao wamekadhibisha siku ya malipo.

Hii ni tahadhari na kiaga kwa wanaopinga Siku ya Mwisho, Umetangulia mfano wake katika aya kadhaa. Tazama Sura Al-Mursalat.

Na haikadhibishi ila kila mwenye kupituka mipaka mwenye dhambi, anaposomewa Aya zetu husema: Ni ngano za watu wa kale.

Makusudio ya Aya zetu ni Qur’an.

Siku ya Mwisho ni adhabu na moto kwa waasi waliopituka mipaka vipi wataweza kuiamini? Sheikh Muhammad Abduh alisema: “Mwenye kupon­dokea kwenye uadilifu katika hulka yake na vitendo vyake, basi ni wepesi zaidi kwake kusadiki siku ya mwisho. Na mwenye kuzipitukia mipaka haki za watu, anakurubuia kujizuia kujua habari za Akhera, kwa vile hilo ni kujihukumu yeye mwenyewe kwa dhulma aliyoifanya.”

Si hivyo! Qur’an na Siku ya Mwisho sio ngano wala uzushi kama wanavy­odai wapinzani.

Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao waliyokuwa wakiyachuma.

Madhambi yamerundikana kwenye nyoyo za wakosefu mpaka zimewapo­fusha kuiona haki. Si hivyo! Jizuieni na dhambi ambazo zimewapofusha na haki.

Hakika wao siku hiyo kwa Mola wao watakingiwa pazia.

Madhambi yamewakingia pazia na Mwenyezi Mungu na yamewawekea pazia baina yao na rehema yake.

Kisha hakika wao watauingia moto. Baada ya kufukuzwa kutoka katika rehema ya Mwenyezi Mungu watain­gizwa kwenye moto kisha waambiwe haya ndiyo mliyokuwa mkiyakadhibisha.

Malaika watawaambia maneno haya kuwazidishia lawama na uchungu.

Umetangulia mfano wake mara nyingi, ikiwemo Juz. 24 (41:20).

كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْأَبْرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ {18}

Si hivyo! Hakika maandishi ya watu wema yako katika ili­iyyin.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا عِلِّيُّونَ {19}

Ni lipi la kukujulishwa nini Illiyyun

كِتَابٌ مَرْقُومٌ {20}

Ni daftari lenye kuandikwa.

يَشْهَدُهُ الْمُقَرَّبُونَ {21}

Watalishuhudia waliokuru­bishwa.

إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ {22}

Hakika watu wema watakuwa katika neema.

عَلَى الْأَرَائِكِ يَنْظُرُونَ {23}

Wakiwa juu ya malili waki­tazama.

تَعْرِفُ فِي وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ النَّعِيمِ {24}

Utatambua mnyiririko wa neema katika nyuso zao.

يُسْقَوْنَ مِنْ رَحِيقٍ مَخْتُومٍ {25}

Watanyweshwa mvinyo wenye kuzibwa.

خِتَامُهُ مِسْكٌ ۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ {26}

Kizibo chake ni miski Na katika hayo na washindane wenye kushindana.

وَمِزَاجُهُ مِنْ تَسْنِيمٍ {27}

Na mchanganyiko wake ni tasnim.

عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا الْمُقَرَّبُونَ {28}

Chemchem watakayoinywa waliokurubishwa.

إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ {29}

Hakika waliokuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walioamini.

وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ {30}

Na walipowapitia wali­konyezana.

وَإِذَا انْقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انْقَلَبُوا فَكِهِينَ {31}

Na waliporudi kwa watu wao walirudi wakishangilia.

وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَضَالُّونَ {32}

Na wakiwaona wanasema: Hakika hawa wamepotea.

وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَ {33}

Na hawakupelekwa wawachunge.

فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ {34}

Basi leo walioamini ndio watakaowacheka makafiri.

عَلَى الْأَرَائِكِ يَنْظُرُونَ {35}

Watakua juu ya malili waki­tazama.

هَلْ ثُوِّبَ الْكُفَّارُ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ {36}

Je, makafiri wamelipwa waliyokuwa wakiyafanya?

Aya 18 – 36: Kizibo Chake Ni Miski

Maana

Si hivyo! Komeni kukadhibisha siku ya mwisho.

Hakika maandishi ya watu wema yako katika iliiyyin.

Masjala yanapothibitishwa majina ya watu wema na matendo yao, yatawekwa mahali pa tukufu panapoafikiana na cheo cha watu wema, kama linavyofahamisha neno Illiyun (mahali pa juu) .

Ni lipi la kukujulishwa nini Illiyyun.

Haiwezi kuwaziwa wala kukadiriwa kwa fahamu.

Ni daftari lenye kuandikwa, ndani yake mkiwa na alama za utukufu wa matendo na sifa kuu.

Watalishuhudia waliokurubishwa.

Daftari hili halina shaka, litaonekana na kila aliye karibu nalo. Imesemekana kuwa makusudio ya waliokurubishwa ni Malaika.

Hakika watu wema watakuwa katika neema.

Huu ni ubainifu wa malipo ya wema na hisani.

Wakiwa juu ya malili wakitazama.

Malili ni viti vya kifahari. Kutazama ni kuburudika macho kwa mandhari mazuri ya kushangaza. Utatambua mnyiririko wa neema katika nyuso zao, unaofahamisha kuwa ni watu wa Peponi.

Umetangulia mfano wake katika Juzuu hii tuliyo nayo (80:38). Watanyweshwa mvinyo wenye kuzibwa, kizibo chake ni miski.

Mvinyo huu ni safi, chombo chake kimezibwa na miski badala ya udon­go.

Na katika hayo na washindane wenye kushindana.

Neema ya Pepo ndiyo inayofaa kushindaniwa, kwa sababu ni ya kubakia, lakini balaa za dunia, zitaondoka na kuisha kila aliye humo ataisha tu.

Na mchanganyiko wake ni tasnim. Chemchem watakayoinywa waliokurubishwa.

Mvinyo huo umechanganywa na maji ya chemchem inayoitwa asnim. Imeitwa hivyo kwa sababu maji yake yanatoka juu, kwa hiyo jina likaafi­ki lilivyoitwa, kama asemavyo Sheikh Muhammad Abduh.

Waliokurubishwa ni wale wema ambao Mwenyezi Mungu amewaandalia hizo neema alizozitaja. Lengo la Aya hizi ni kuhimiza na kuleta mvuto wa Imani na matendo mema.

Hakika waliokuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walioamini.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwataja wenye takuwa, sasa anawataja wakosefu, kwamba wao duniani, walikuwa wakijikuta kwa waumini na wakiwacheka na kudharau, si kwa lolote ila nikushindwa kwao kujibu.

Na walipowapitia walikonyezana kwa kuwadharau, kama ilivyo kawaida ya wapumbavu.

Na waliporudi kwa watu wao walirudi wakishangilia kwa kusen­genya na kutaja uovu.

Na wakiwaona wanasema: Hakika hawa wamepotea.

Hivi ndivyo walivyo wahaini, wanawabandikia mabaya wenye ikhlasi na uovu wale wenye takwa.

Katika afsir Arrazi anasema kuwa Imam Ali (a.s.) pamoja na kundi la waislamu waliwapatia jamaa wa kinafiki, wakawacheka na kukonyezana, kisha wakarudi kwa watu wao na kusema: Leo tumemuona lofa. Basi wakacheka, ndio ikashuka Aya hii kabla ya Ali kufika kwa Mtume (s.a.w.).

Na hawakupelekwa wawachunge; yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakuwapeleka makafiri wawachunge waumini kwenye matendo yao na kudhibiti harakati zao.

Sheikh Muhammad Abduh anasema, maana ni kuwa makafiri walisema: Mwenyezi Mungu hakuwatuma waumini watuchunge na kutuongoza.
Maana haya yanatofautiana na dhahiri ya maneno na yanaweka mbali ufa­hamu.

Basi leo walioamini ndio watakaowacheka makafiri.

Kicheko cha waumini kwa makafiri Siku ya Mwisho ni bora, kwa sababu ni kuwadharau maadui wa Mwenyezi Mungu, lakini kicheko cha wakose­fu kwa waumini duniani ni hatia kubwa, kwa sababu ni kudharau mawalii wa Mwenyezi Mungu.

Watakua juu ya malili wakaitazama alivyowafanya Mwenyezi Mungu maadui zake na maadui wao na jinsi anavyowaadhibu wale waliokuwa wakiwadharau na kuwacheka.

Je, makafiri wamelipwa waliyokuwa wakiyafanya. Makafiri waliwacheka waumini duniani. Mwenyezi Mungu akawecheke­sha waumini kwa makafiri akhera, imekuwa sare, lakini iko mbali mbali.

  • 2521 views

Sura Ya Themanini Na Nne: Al-Inshiqaq

Imeshuka Makka Ina Aya 25.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

إِذَا السَّمَاءُ انْشَقَّتْ {1}

Mbingu itakapochanika.

وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ {2}

Na ikamsikiliza Mola wake na ikafanya ndivyo.

وَإِذَا الْأَرْضُ مُدَّتْ {3}

Na ardhi itakaponyooshwa.

وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ {4}

Na ikatupa vilivyo ndani kuwa tupu.

وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ {5}

Na ikamsikiliza Mola wake na ikifanya ndivyo.

يَا أَيُّهَا الْإِنْسَانُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًا فَمُلَاقِيهِ {6}

Ewe Mtu! Hakika wewe ni mwenye kufanya bidii kwa Mola wako, basi utamkuta.

فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ {7}

Ama atakayepewa daftari lake kwa mkono wake wa kulia.

فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا {8}

Basi atahisabiwa hisabu nyepesi.

وَيَنْقَلِبُ إِلَىٰ أَهْلِهِ مَسْرُورًا {9}

Na atarudi kwa watu wake mwenye furaha.

وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ وَرَاءَ ظَهْرِهِ {10}

Na ama atakayepewa daftari lake nyuma ya mgongo wake.

فَسَوْفَ يَدْعُو ثُبُورًا {11}

Ataomba maangamizo.

وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا {12}

Na atauingia moto.

إِنَّهُ كَانَ فِي أَهْلِهِ مَسْرُورًا {13}

Hakika alikuwa kati ya watu wake ni mwenye furaha.

إِنَّهُ ظَنَّ أَنْ لَنْ يَحُورَ {14}

Hakika yeye alidhani hatare­jea.

بَلَىٰ إِنَّ رَبَّهُ كَانَ بِهِ بَصِيرًا {15}

Kwani? Hakika Mola wake alikuwa akimuona

Aya 1-15: Mbingu Itakapochanika

Maana

Sura hii ni kama sura mbili zilizotangulia (Takwir na Infitar), inabainisha vituko vya siku ya Kiyama na kugawanyika watu, siku ya malipo, kwenye makundi mawili: kundi la peponi na la motoni.

Mbingu itakapochanika.

Mbingu itachanika na kupasuka wakati Mwenyezi Mungu atakapotaka kuuharibu ulimwengu tulio nao.

Na ikamsikiliza Mola wake.

Yaani mbingu itaitikia amri ya Mwenyezi Mungu. Kwa maneno mengine ni kuwa Mwenyezi Mungu ni muweza wa kila kitu.

Na ikafanya ndivyo, yaani ikafanya inavyotakiwa kufanywa kufuata amri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, kwa vile imeumbwa naye na iko mikononi mwake.

Na ardhi itakaponyooshwa.

Kitakaposimama Kiyama ardhi itakosa mshikamano wake na majabali yatang’oka na mengineyo , hapo ardhi itakuwa laini.
Na ikatupa vilivyo ndani, yaani vilivyo ndani ya ardhi wakiwemo wafu na vinginevyo, na kuwa tupu, haina chochote kilichokuwamo.

Na ikamsikiliza Mola wake na ikifanya ndivyo, sawa na ilivyofanya ardhi.

Ewe Mtu! Hakika wewe ni mwenye kufanya bidii kwa Mola wako, basi utamkuta.

Makusudio ya bidii hapa ni mtu anavyojifanyia yeye mwenyewe katika heri au shari. Maana ni kuwa mtu hatakaa milele duniani naye anafanya juhudi kwenda kwa Mola wake na atakutana naye akiwa na matendo yake tu na hakuna kitakachomkutanisha na Mola wake isipokuwa mauti. Maadamu umri unapita na mauti yanakuja, basi mkutano huo uko karibu sana. Kwa hiyo angalie mtu ameandaa nini atakapokutana na Mwenyezi Mungu na hisabu yake?

Ama atakayepewa daftari lake kwa mkono wake wa kulia, basi atahis­abiwa hisabu nyepesi, na atarudi kwa watu wake mwenye furaha.

Kila mwenye kuamini na akatenda mema kesho atapewa maandishi yake kwa mkono wake wa kulia. Makusudioo ya watu wake hapa ni waumini walio wema kama yeye watakapokutana Peponi wakiwa na furaha. Hisabu nyepesi ni ile isiyokuwa na mashaka. Kuna hadithi isemayo: “Mwenye kuihisabu nafsi yake duniani, itakuwa nyepesi kwake hisabu ya akhera.”

Na ama atakayepewa daftari lake nyuma ya mgongo wake, ataomba maangamizo na atauingia moto.

Makusudio ya atakayepewa maandishi yake kwa nyuma ya mgongo wake ni mkosefu mwenye dhambi , angalia katika Juzuu . 18 (25:14).

Unaweza kuuliza! Hapa Mwenye Mungu (s.w.t.) anasema kuwa mkosefu atapewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake na katika Juzuu 29 (69:25) anasema atapewa kwa mkono wake wa kushoto, sasa kuna wajihi gani wa kuonanisha Aya mbili hizi?

Wafasiri wengi wamejibu kuwa mkono wa kulia wa mwenye hatia uta­fungwa shingoni mwake Siku ya Kiyama na wa kushoto utakua nyuma ya mgongo wake na ndio atapokea nao daftari lake.

Sheikh Muhammad Abduh anasema kuwa kupewa daftari kwa mkono wa kulia, kushoto au nyuma ya mgongo ni kufananisha na kuleta picha ya mtu atakavyo yaona matendo yake siku hiyo. Kuna watu watakapoyaona matendo yao watashangilia na kufurahi. Huku ndiko kupokea kwa mkono wa kulia. Kuna wengine watakapofichuliwa matendo yao watakunja uso na kutamani lau wasingefichuliwa.

Huku ndiko kupokea kwa kushoto au nyuma ya mgongo. Kwa hiyo hakuna haja ya kuoanisha Aya mbili hizi kwa kuzua maana yasiyofanana na kitabu cha Mwenyezi Mungu, kama walivy­ ofanya wafasiri wengi.

Hakika alikuwa kati ya watu wake ni mwenye furaha.

Duniani alipokuwa na watu wake alikuwa akicheza wala hafikiri hisabu na malipo.

Hakika yeye alidhani hatarejea.

Yaani hatarejea kwa Mola wake baada ya mauti, wala hakuna yoyote atakayemsaili na dhambi zake. Kwani? Yeye atarejea tu na kuulizwa hilo halina shaka.

Hakika Mola wake alikuwa akimuona.

Hakikufichika kwake chochote katika kauli zake na vitendo vyake, atahis­abiwa ndivyo, ikiwa ni heri basi ni heri na ikiwa ni shari basi ni shari.

فَلَا أُقْسِمُ بِالشَّفَقِ {16}

Naapa kwa wekundu wa machweo.

وَاللَّيْلِ وَمَا وَسَقَ {17}

Na kwa usiku na unavyoviku­sanya.

وَالْقَمَرِ إِذَا اتَّسَقَ {18}

Na kwa mwezi unapotimia.

لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَنْ طَبَقٍ {19}

Bila shaka mtapanda tabaka kwa tabaka!

فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ {20}

Basi wana nini hao hawaami­ni?

وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ الْقُرْآنُ لَا يَسْجُدُونَ ۩ {21}

Na wanaposomewa Qur’an hawasujudu?

بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا يُكَذِّبُونَ {22}

Bali waliokufuru wanakad­hibisha tu.

وَاللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ {23}

Na Mwenyezi Mungu anaya­jua zaidi wanayoyakusanya.

فَبَشِّرْهُمْ بِعَذَابٍ أَلِيمٍ {24}

Basi wabashirie adhabu chungu!

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ {25}

Isipokuwa wale walioamni na wakatenda mema, wana ujira usiokatika.

Aya 16-25:Naapa Kwa Wekundu Wa Machweo

Maana

Naapa kwa wekundu wa machweo.

Yametangulia maelezo mara kadhaa kuhusu la Uqsimu. Tazama Juz. 27 (56:75) na Juzu hii tuliyo nayo (81: 15). Wekundu wa machweo ni ule wekundu unaobakia pambizoni mwa mbingu kutokana athari ya kuchwa jua. Pengine lengo la kuapa huku ni kutanabahisha kwenye wakati huu, kwa sababu ni kipindi cha kugura kutoka mchana na taabu zake hadi usiku na raha yake.

Na kwa usiku na unavyovikusanya.

Yaani unavikusanya vilivyotawanyika mchana na kuviweka pamoja ­wanafamlia wanajumuika usiku baada ya kutawanyika mchana. Vile vile majirani na marafiki wanakusanyika usiku kwa mazungumzo.

Sheikh Muhammad Abduh anasema kuwa si siri kwamba yaliyotawanyika mchana yanakusanyika usiku, hata mikono yako miwili unayoinyoosha kwa kazi mchana, unaikusanya pamoja kwenye ubavu wako usiku. Usiku unawakusanya majike na watoto wao na kuwarudisha waliokwenda machungani kwenye mazizi yao.

Na kwa mwezi unapotimia.

Unakamilika na kutimia nuru yake usiku wa 13,14 na 15. Nyusiku hizi zinaitwa nyusiku nyeupe.

Bila shaka mtapanda tabaka kwa tabaka.

Hili ndilo jawabu la kiapo. Maana ni kuwa mtu hana budi kupitia ngazi nyingi, kuanzia tone la manii hadi kilenge na kuanzia utoto hadi ujana, kisha uzee hadi ukongwe na umri dhalili kabisa.

Vile vile anapambana na hali tofauti katika maisha yake kuanzia afya hadi maradhi, utajiri na ufukara na huzuni na furaha. Vile vile maendelo na kurudi nyuma.

Hivi ndivyo inavyofanya dunia kwa watu wake, kutoka hali moja hadi nyingine, mpaka waje wasimamae wote mbele ya Mwenyezi Mungu kwa ajili ya hisabu na malipo.

Basi wana nini hao hawaamini, pamoja na kuwa sababu za kuamini haz­ina idadi katika pambizo za mbingu na katika nafsi zao?

Na wanaposomewa Qur’an hawasujudu? Hawakiri wala kusalimu amri.

Sheikh Muhammad Abduh anasema kuwa, usifikirie Qur’an haikugonga nyoyo zao wala kufika sauti yake ndani ya dhamiri zao, bali imefikia kiwango cha kukinaisha, lakini inadi tu ndiyo inayowazuia kuamini chan­zo cha ukadhibishaji, sio uzembe wa dalili, isipokuwa ni uzembe wa mwenye kupewa dalili na upinzani wake.

Bali waliokufuru wanadadhibisa tu! Haki kwa kiburi na inadi na Mwenyezi Mungu anayajua zaidi wanayoyakusanya; yaani malengo wanayoyadhamiria katika nyoyo zao si mengine, isipokuwa kupupia vyeo vyao na chumo lao.

Basi wabashirie adhabu chungu ikiwa ni malipo ya waliyoyatenda.

Isipokuwa wale walioamni na wakatenda mema, wana ujira usiokati­ka.

Maana ya yasiyokatika ni kutoisha wala kupungua wala kusimbuliwa.

Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 24 (41:8).

  • 1664 views

Sura Ya Themanini Na Tano: Al-Buruj

Imeshuka Makka. Ina Aya 22.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْبُرُوجِ {1}

Naapa kwa mbingu yenye Buruji!

وَالْيَوْمِ الْمَوْعُودِ {2}

Na kwa siku iliyoahidiwa!

وَشَاهِدٍ وَمَشْهُودٍ {3}

Na kwa shahidi na chenye kushuhudiliwa!

قُتِلَ أَصْحَابُ الْأُخْدُودِ {4}

Wemelaaniwa watu wa mahandaki.

النَّارِ ذَاتِ الْوَقُودِ {5}

Yenye moto wenye kuni nyingi.

إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌ {6}

Walipokuwa wamekaa hapo.

وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِالْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌ {7}

Na wao ni mashahidi wa yale walioyoyafanya waumini.

وَمَا نَقَمُوا مِنْهُمْ إِلَّا أَنْ يُؤْمِنُوا بِاللَّهِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ {8}

Na hapana lililowachukiza kwao ila ni kwamba wal­imwamini Mwenyezi Mungu mwenye nguvu mwenye kusifi­wa.

الَّذِي لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَاللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ {9}

Ambaye ni wake ufalme wa mbingu na ardhi, na Mwenyezi Mungu ni shahidi wa kila kitu.

إِنَّ الَّذِينَ فَتَنُوا الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ الْحَرِيقِ {10}

Hakika wale waliowafitini waumini wanaume na wau­mini wanawake, kisha wasitubie, basi watapata adhabu ya Jahannam na wat­apata adhabu ya kuungua.

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِنْ تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ۚ ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْكَبِيرُ {11}

Hakika waliaomini na waka­tenda mema watapata bustani zipitiwazo na mito chini yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ {12}

Hakika kamato la Mola wako ni kubwa.

إِنَّهُ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ {13}

Hakika yeye ndiye anayeanzisha na anayerud­isha.

وَهُوَ الْغَفُورُ الْوَدُودُ {14}

Na yeye ni mwingi wa maghu­fira Mwenye mapenzi.

ذُو الْعَرْشِ الْمَجِيدُ {15}

Mwenye Arsh, Mtukufu.

فَعَّالٌ لِمَا يُرِيدُ {16}

Mwingi wa kutenda alipenda­lo.

هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْجُنُودِ {17}

Je imekufikia habari ya majeshi?

فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ {18}

(Ya) Frauni na Thamudi?

بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي تَكْذِيبٍ {19}

Lakini waliokufuru wako katika kukadhibisha.

وَاللَّهُ مِنْ وَرَائِهِمْ مُحِيطٌ {20}

Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.

بَلْ هُوَ قُرْآنٌ مَجِيدٌ {21}

Bali hiyo ni Qur’an Tukufu.

فِي لَوْحٍ مَحْفُوظٍ {22}

Katika ubao uliohifadhiwa

Maana

Naapa kwa mbingu yenye buruji.

Kila kilicho juu yako ni mbingu. Ama buruji imesemekana ni nyota nyin­gi kubwa kwa sababu kila nyota katika hizo inaonekana kama buruji kubwa.

Imesamekana ni manazili kumi na mbili yaliyo maarufu ambayo ardhi inayapitia katika mzunguko wake wa jua kwa mwaka mmoja, nayo: Punda, Ng’ombe, Mapacha, Kaa, Simba, Mashuke, Mizani, Nge, Mshale, Mbuzi, Kondoo na Samaki.

Ni sawa makusudio yawe ni maana ya kwanza au ya pili au yote pamoja, lakini lengo ni kutanabahisha usanii wa hali ya juu katika nyota na hikima kubwa, ili kutoa dalili kwa hilo kuwa kuna muumba aliye mkuu.

Na kwa siku iliyoahidiwa ambayo ni siku ya Kiyama.

Na kwa shahidi na chenye kushuhudiliwa.

Kauli zimekuwa nyingi na kugongana kuhusiana na maana ya shahidi na chenye kushuhudiliwa. Baadhi ya wafasiri wameishia kwenye kauli 48; 16 zikiwa katika maana ya shahidi na 32 katika chenye kushuhudiliwa!

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Makusudio ya shahidi ni kila chenye hisia za kushuhudia, na makusudio ya chenye kushuhudiliwa ni chenye kuhisiwa ambacho ushahidi umetokea juu yake.” Ametoa dalili ya kusihi kauli yake kwa mambo mawili:

Kwanza hilo ni hakika dhahiri inayofahamika kutokana na dalii ya tamko.

Pili, kwamba cha kwanza alichoapia nacho Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni nyota za mbingu. Na katika nyota hizi kuna zilizo ghaibu na zina­zoshuhudiwa. Zinazoshuhudiwa ni kuwa nuru ya harakati zake, machim­buko yake na machweo yake, yote yanahisiwa na kushuhudiwa.

Ama zilizo ghaibu ni kuwa hakika yake na nguvu zilizomo ndani yake hazitambuliwi wala kushuhudiwa kwa hisia. Kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akaapa kwa siku ya mwisho ambayo ni ghaibu isiyohusiana na kushuhudiwa kwa karibu wala kwa mbali.

Tena Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akaapa kwa shahidi na chenye kushuhudi­wa. Kwa hiyo Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anakuwa ameapa na ulimwengu wote, ni sawa uwe ni wa ghaibu tu, au wakushuhudiwa tu, au wa yote mawili pamoja.

Lengo la hayo ni kuwa waangaliaji waangalie viumbe kwa aina zake zote, wazingatie hikima na nidhamu inayojitokeza na wafanye juhudi kujua yale yaliyo ghaibu na kujificha.

Wemelaaniwa watu wa mahandaki yenye moto wenye kuni nyingi, walipokuwa wamekaa hapo na wao ni mashahidi wa yale walioyoy­afanya waumini.

Mahandaki ni mashimo yanayochimbwa ardhini kwa umbo la msitatili. Watu wake hapa ni makafiri walio na nguvu na utawala. Imesemekana makusudio yake hapa ni Dhunuwasi na watu wake, aliyekuwa mmoja wa wafalme wa Yemen.

Vyovyote watakavyokuwa wenye mahandaki, muhimu ni kuwa Aya hizi zinaashiria watu waasi waliochimba handaki na wakalikokea moto ndani yake uliowaka sana.

Kisha wakawaleta waumini wenye ikhlasi na kuwaonyesha moto. Mwenye kurudi na kuacha dini yake na kuafikiana nao kwenye kufru na maasi basi walimwacha, na mwenye kushikamana na imaani na ikhlasi, walimuunguza; wenyewe wakiwa wamekaa pembeni mwa haandaki wakiangalia huku wakifurahia na kuburudika kwa kuona miili iliyo hai ikiteketea motoni.

Na hapana lililowachukiza kwao ila ni kwamba walimwamini Mwenyezi Mungu mwenye nguvu mwenye kusifiwa. Ambaye ni wake ufalme wa mbingu na ardhi, na Mwenyezi Mungu ni shahidi wa kila kitu.

Hili ndilo kosa lao la kwanza na la mwisho kwao-kuwa wamemwamini Mwenyezi Mungu mfalme wa wafalme Mwenye uweza, Mwenye kushin­da, Mjuzi wa kila kitu na Mwenye kustahiki sifa njema Yeye peke Yake. Mwenye Mungu (s.w.t.) amejisifu kwa sifa hizi kuashiria kuwa waasi hawana pa kumkimbia Mwenyezi Mungu na adhabu yake, mfano wake ni:

 أَتَقْتُلُونَ رَجُلًا أَنْ يَقُولَ رَبِّيَ اللَّهُ {28}

“Mtamuua mtu kwa kusema Mola wangu ni Mwenyezi Mungu”?: Juz. 24 (40:28).

Hakika wale waliowafitini waumini wanaume na waumini wanawake, kisha wasitubie, basi watapata adhabu ya Jahannam na watapata adhabu ya kuungua.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kudokeza juu ya watu wa mahandaki waliojifanya majabari, hapa anawaelezea vigogo wa kikuraishi waliowaud­hi waumini kwa kuwafitini na dini yao au kuwarudisha kwenye ukafiri baada ya imani yao. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewahadharisha na kuwaahidi adhabu kama hawatakoma.

Kuunganisha adhabu ya kumjua na adhabu ya Jahannam ni katika upande wa kuunganisha tafsir na ufafanuzi, kwa lengo la kusisitiza na hadhari, pia kuzidishia kuhofia.

Hakika waliaomini na wakatenda mema watapata bustani zipitiwazo na mito chini yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

Umetangulia mfano wake katika Aya kadhaa zilizopita. Imetajwa hapa kutokana na njia ya Qur’an Tukufu, kukutanisha maangamizi ya wenye hatia na kufuzu wenye takua, na neema ya hawa na moto wa wale.

Hakika kamato la Mola wako ni kubwa.

Neno “kamato” tumelifasiri kutokana na neno Batsha lenye maana ya kukamata kwa nguvu. Itakuwaje ikiwa kamato hilo ni kubwa, tena kutoka kwa aliye Jabari wa mbingu na ardhi. Maneno hapa yanaelekezwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa lengo la kuwahadharisha wale ambao wanamuudhi Mtume na wale walioamini pamoja naye.

Hakika yeye ndiye anayeanzisha na anayerudisha.

Mwenye kuwa na uwezo wa kuanza kuumba na kurudisha tena, basi ana uwezo zaidi wa kukamata na kudhibiti waasi.

Na yeye ni mwingi wa maghufira Mwenye mapenzi.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alipotaja adhabu kali aliikutanisha na maghufira yake na upole wake, ili waasi warejee kwa toba wala wasikate tamaa na rehema yake. Kwani ghadhabu yake Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa wenye dhambi haimzui na huruma zake kwao.

Mwenye Arsh, Mtukufu, yaani Mwenye ufalme na utawala.

Mwingi wa kutenda alipendalo.

Kutaka kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu kunathibitika kwa mjaradi wa kutaka kwake tu, bila ya kuwa na haja ya kutumia kitu kingine. Imam Ali (as) anasema: “Ni mwenye kufanya sio kwa kutumia vifaa, Mwenye kukadiria sio kwa kuanza kufikiria, Mwenye kutaka bila ya kudhamiria … huliambia analotaka: kuwa, na linakuwa si kwa sauti ya kusikiwa wala kwa mwito unaoitikiwa.”

Hikima yake Mtukufu ilitaka uma zilizotangulia ziangamie zilipowakid­hibisha Mitume, kwa hiyo ikawa ni kama alivyotaka.

Je imekufikia habari ya majeshi ya Firauni na Thamudi?

Hao ni wale ambao Mwenyezi Mungu amewaangamiza kwa kuwakad­hibisha kwao Mitume wao.

Neno “Je” hapo ni la kuthibitisha kama ilivyo katika Juz. 29 (76:1) maana ni umekwishasikia ewe Muhammad na pia kaumu yako wamesikia yaliy­owapitia watu wa Hud ambao ni kaumu ya Swaleh na Firauni na watu wako, jinsi Mwenyezi Mungu alivyomuadhibu walipowakadhibisha Mitume, vile vile Mwenyezi Mungu anaweza kuwaadhibu waliokukad­hibisha wewe wakati wowote anapotaka.

Lakini waliokufuru wako katika kukadhibisha.

Kikundi cha wale waliokufuru, wakiwemo vigogo wa kikuraishi wanaipin­ga haki, si kwa lolote ila ni kwamba wao wanapenda sana kuikadhibisha na kuifanyia inadi popote walipokuwa na watakapokuwa; vinginevyo ni udhuru gani walio nao wa kuipinga haki na hali dalili na ubainifu uko wazi na umejitokeza kama mchana?

Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.

Wao wako mikononi mwa Mwenyezi Mungu, anawageuza vyovyote atakavyo na anaweza kuwangamiza wakati wowote anaotaka. Hapa kuna ishara kwamba wao hawataacha kukadhibisha haki mpaka waione adhabu.

Bali hiyo ni Qur’an Tukufu yenye shani kubwa, kwa sababu kila kili­chomo ndani yake ni haki na uadilifu, pamoja na kusimama hoja na dalili. Na hakuna anayeikadhibisha isipokuwa wakosefu wenye hatia.Katika ubao uliohifadhiwa na upotofu na kulindwa na mageuzo na mabadiliko.

Wafasiri wana maneno marefu na mapana kuhusiana na neno “Ubao ulio­hifadhiwa!” sisi hatutaulizwa hakika yake na ilivyo. Waliozama katika ilimu wanaamini ya ghaibu na yaliyofichika kwao na wanajizuia kuy­achambua.

  • 2802 views

Sura Ya Themanini Na Sita: At-Taariq

Imeshuka Makka Ina Aya 17.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَالسَّمَاءِ وَالطَّارِقِ {1}

Naapa kwa mbingu na kina­chokuja usiku!

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الطَّارِقُ {2}

Ni lipi la kukujulisha nini kinachokuja usiku?

النَّجْمُ الثَّاقِبُ {3}

Ni nyota inayotoboa.

إِنْ كُلُّ نَفْسٍ لَمَّا عَلَيْهَا حَافِظٌ {4}

Hakuna nafsi yoyote ila ina mwenye kuiihifadhi.

فَلْيَنْظُرِ الْإِنْسَانُ مِمَّ خُلِقَ {5}

Basi na atazame mtu ameumb­wa kwa kitu gani?

خُلِقَ مِنْ مَاءٍ دَافِقٍ {6}

Ameumbwa kwa maji yanay­otoka kwa kuchupa.

يَخْرُجُ مِنْ بَيْنِ الصُّلْبِ وَالتَّرَائِبِ {7}

Yanayotoka baina ya uti wa mgongo na kifua.

إِنَّهُ عَلَىٰ رَجْعِهِ لَقَادِرٌ {8}

Hakika yeye ni muweza wa kumrejesha.

يَوْمَ تُبْلَى السَّرَائِرُ {9}

Siku zitakapofunuliwa siri.

فَمَا لَهُ مِنْ قُوَّةٍ وَلَا نَاصِرٍ {10}

Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.

وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الرَّجْعِ {11}

Naapa kwa mbingu yenye marejeo!

وَالْأَرْضِ ذَاتِ الصَّدْعِ {12}

Na kwa ardhi yenye mpa­suko!

إِنَّهُ لَقَوْلٌ فَصْلٌ {13}

Hakika hiyo ni kauli yenye kupambanua.

وَمَا هُوَ بِالْهَزْلِ {14}

Wala si mzaha.

إِنَّهُمْ يَكِيدُونَ كَيْدًا {15}

Hakika wao wanachimba vitimbi,

وَأَكِيدُ كَيْدًا {16}

Nami ninachimba vitimbi.

فَمَهِّلِ الْكَافِرِينَ أَمْهِلْهُمْ رُوَيْدًا {17}

Basi wape muhula makafiri – wape muhula kidogo.

Maana

Naapa kwa mbingu na kinachokuja usiku. Ni lipi la kukujulisha nini kinachokuja usiku? Ni nyota inayotoboa.

Kila kilicho juu yako ni mbingu. Makusudio ya kinachokuja usiku hapa ni nyota kwa sababu haijitokezi isipokuwa usiku. Kutoboa ni kung’aa, kama wanavyolitumia waarabu neno hilo kwa kusema: utoboe moto wako, yaani uwashe uwe na mwanga.

Nyota imepewa sifa hiyo kwa vile mwanga wake unalitoboa giza, kama kwamba giza ni ngozi nyeusi na nyota inaitoboa kwa mwanga wake. eno “ni lipi la kukujulisha” linatambulisha kulikuza jambo na kuliad­himisha. wenyezi Mungu (s.w.t.) ameapa kwa nyota inayong’aa ili kutanabahisha manufaa yake makubwa na kutengenezwa kwake kwa ajabu.

Ama kinachoapiwa, Mwenyezi Mungu (s.w.t.), amekiashiria kwa kusema:

Hakuna nafsi yoyote ila ina mwenye kuiihifadhi kauli zake na vitendo vyake na kudhibiti harakati zake na siri zake, mpaka uishe muda na kuku­tana na Mola wake, hapo itakuta heri iliyoifanya imehudhurisha na shari iliyoifanya pia. Kwa maneno mengine ni:

وَكَفَىٰ بِرَبِّكَ بِذُنُوبِ عِبَادِهِ خَبِيرًا بَصِيرًا {17}

“Na Mola wako anatosha kuwa ni mwenye habari na mwenye kuona dhambi za waja wake.”
Juz. 15 (17:17)
.

Basi na atazame mtu ameumbwa kwa kitu gani? Ameumbwa kwa maji yanayotoka kwa kuchupa, yanayotoka baina ya uti wa mgongo na kifua.

Maji yanayochupa ni manii. eno uti wa mgongo tumelifasiri kutokana na neno ulb lenye maana ya kila mfupa wenye uti wa mgongo. Kifua limetokana na araib lenye maana sehemu inayovaliwa mkufu kifuani.

Makusudio ya uti wa mgongo hapa ni mwanamume na kifua ni cha mwanamke. Sehemu hizi mbili ndio chimbuko la manii yanayotengeneza mtoto. Ni hivi karibuni tu sayansi imepata mwongozo wa hakika hii iliyokuja kutoka kwenye ulimi wa mwarabu mmoja ambaye hakwenda shule.

Maana ya Aya hizi ni kuwa ewe mtu ukishajua kuwa Mwenyezi Mungu anajua siri yako na dhahiri yako, basi ni juu yako kujiangalia na kufikiria kupatikana kwako.

Umeanza kutokana na tone la manii lililotoka mgongo­ni mwa baba yako na kifua cha mama yako, kisha ukawekwa mahali maki­ni penye utulivu mpaka muda maalum, ukawa katika umbo zuri lililokami­lika lilio na uhai, mhemuko na utambuzi.

Hebu fikiria na uzingatie hayo ili ujue kuwa aliyekuanzisha na kukuongoza anaweza kukurudisha mara ya pili kwenye uhai wako.

Haya ndio maana ya kuli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Hakika yeye ni muweza wa kumrejesha.

Kwa hiyo kuumbwa kwa kwanza ni ushahi­di wa kuumbwa kwa pili.

Siku zitakapofunuliwa siri, basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi .

Neno kufunuliwa tumelifasiri kutokana na neno ubla lenye maana ya kufanyiwa mtihani, yaani siri zitafanyiwa mtihani kwa kufichuliwa na kud­hihirishwa.
Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) atawafufua watu katika siku ambayo hakutakuwa na sitara au kificho wala mjadala au hoja, wala haku­takuwa na nguvu kwa yeyote kujisaidia yeye mwenyewe au mwinginewe, isipokuwa nguvu ya imani na matendo mema.

Naapa kwa mbingu yenye marejeo! Na kwa ardhi yenye mpasuko!

Marejeo ni maji ya mvua (kwa vile mvua inanyesha na kurejea) na mpa­suko ni mimea (imepasuka kwa kuchipuka mimea). Mwenyezi Mungu ameapa kwa mbingu yenye kumimina maji na kwa ardhi yenye kuleta heri na vyakula.

Hakika hiyo ni kauli yenye kupambanua wala si mzaha.

‘Hiyo’ ni Qur’an nayo ni ukweli sio mchezo na ni haki isiyofikiwa na batili mbele yake wala nyuma yake. Na hii ni kumrudi aliyesema kuwa ni ngano za watu wa kale.

Hakika wao wanachimba vitimbi nami ninachimba vitimbi. Basi wape muhula makafiri, wape muhula kidogo.

Wao ni wale waliomkadhimisha Mtume Mtukufu (s.a.w). Wanachimba vitimbi ni kufanya njama dhidi ya Mtume na waumini. Nami ninachimba vitimbi ni kubatilisha na kuzipangua njama zao.

Maana ni kuwa: Ewe Muhammad! Mimi ninamuotea yule anayejaribu kubatilisha mambo yako kwa njama, ngoja kidogo utaona hizaya na mate-so yatakayowapata.

Umetangulia mfano wake pamoja na Tafsiri katika Juz. 2. (3:54).

  • 1608 views

Sura Ya Themanini Na Saba: Al-A’ala

Imeshuka Makka Ina Aya 19.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى {1}

Lisabihi jina la Mola wako aliye mtukufu.

الَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ {2}

Ambaye ameumba, na akawe­ka sawa.

وَالَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ {3}

Na ambaye amekadiria, na akaongoza.

وَالَّذِي أَخْرَجَ الْمَرْعَىٰ {4}

Na ambaye ameotesha mal­isho.

فَجَعَلَهُ غُثَاءً أَحْوَىٰ {5}

Kisha akayafanya makavu yenye kupiga weusi.

سَنُقْرِئُكَ فَلَا تَنْسَىٰ {6}

Tutakusomesha hutusahau,

إِلَّا مَا شَاءَ اللَّهُ ۚ إِنَّهُ يَعْلَمُ الْجَهْرَ وَمَا يَخْفَىٰ {7}

Ila akipenda Mwenyezi Mungu, Hakika yeye anayajua yaliyo jahara na yaliyofichika.

وَنُيَسِّرُكَ لِلْيُسْرَىٰ {8}

Tutakusomesha hutusahau

فَذَكِّرْ إِنْ نَفَعَتِ الذِّكْرَىٰ {9}

Basi kumbusha, kwani kukumbusha kunafaa.

سَيَذَّكَّرُ مَنْ يَخْشَىٰ {10}

Atakumbuka mwenye kuo­gopa.

وَيَتَجَنَّبُهَا الْأَشْقَى {11}

Na atajiepusha nako muovu.

الَّذِي يَصْلَى النَّارَ الْكُبْرَىٰ {12}

Ambaye ataingia moto ulio mkubwa.

ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ {13}

Kisha hatokufa humo wala hatakuwa hai.

قَدْ أَفْلَحَ مَنْ تَزَكَّىٰ {14}

Hakika amekwisha faulu aliyejitakasa.

وَذَكَرَ اسْمَ رَبِّهِ فَصَلَّىٰ {15}

Na akalitaja jina la Mola wake, na akaswali.

بَلْ تُؤْثِرُونَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا {16}

Bali mmeathirika na maisha ya dunia!

وَالْآخِرَةُ خَيْرٌ وَأَبْقَىٰ {17}

Na akhera ni bora na yenye kubaki zaidi.

إِنَّ هَٰذَا لَفِي الصُّحُفِ الْأُولَىٰ {18}

Hakika haya yamo katika vitabu vya mwanzo.

صُحُفِ إِبْرَاهِيمَ وَمُوسَىٰ {19}

Vitabu vya Ibrahim na Musa

Maana

Lisabihi jina la Mola wako aliye mtukufu.

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume (s.a.w.) na taklifa inawahusu wote. Maana ni kuwa mtakase Mwenyezi Mungu na ushirika na kuwa na mke na mtoto na kila lisilo laikiana na cheo chake na utukufu wake.

Hakuna kitu kinachofahamisha utakaso wa muumba kuliko neno lailaha illallah (Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu). Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameamrisha kulitakasa jina na wala sio dhati, kwa vile ukomo wa juhudi ya mtu ni kumjua Mwenyezi Mungu kwa majina yake mazuri na sifa zake kuu, lakini kuijua dhati yake hakuwezi kingia kwenye akili wala fahamu.

Ambaye ameumba na akaweka sawa.

Aliumba alivyoumba akaweka kiwango cha kimo chake, akatia sura alivy­otia sura akazifanya nzuri sura zake.

Na ambaye amekadiria na akaongoza.

Kila kitu amekifanyia lengo na kukisahilishia kwenye lengo hilo. Tafsiri nzuri ya Aya hii ni kauli ya Imam Ali (a.s): “Amekadiria alivyoviumba akakadiria na kuimarisha makadirio yake, na amepanga akaufanya mzuri mpango, na akaelekeza mweleko wake wala hakuvuka mpaka wa ngazi yake au kuzembea kwa kutofikia lengo lake.”

Na ambaye ameotesha malisho kwa ajili ya manufaa na riziki ya wanya­ma.

Kisha akayafanya makavu yenye kupiga weusi.

Kimsingi ni kuwa mimea ina manufaa ikiwa mibichi au mikavu kwa mal­isho ya wanyama. Hapa kuna ishara kuwa kila kilicho hai kitaondoka.

Tutakusomesha hatusahau.

Hii ni habari njema kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa Nabii wake Mtukufu, kwamba Qur’an itamshukia moyoni mwake na kujikita humo, haitampita hata herufi moja. Umetangulia mfano wake katika Juz. 28 (75:17).

Ila akipenda Mwenyezi Mungu.

Baadhi ya wafasiri wamesema kuwa maana yake ni kwamba Mwenyezi Mungu hatamsahahulisha mtume wake chochote katika Qur’an isipokuwa Aya za naskh (za kufuta hukumu.).

Sisi tuko pamoja na wale wasemao kuwa lengo la kuvua huku ni kutana­bahisha kuwa kuhifadhi na kutoshau ni fadhila na takrima kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake na wala sio jambo la lazima. Lau Mwenyezi Mungu (s.w.t.) angelitaka kumsahaulisha Nabii wake angeli­fanya na kisingemshinda chochote. mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

خَالِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ إِلَّا مَا شَاءَ رَبُّكَ ۚ {107}

“Watadumu humo muda wa kudumu mbingu na ardhi, isipokuwa apen­davyo Mola wako.”
Juz 12 (11:107).

Yaani kubakia milele ni kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu na utashi wake, lau angelitaka kuwatoa kwenye Jahannam asingelimzuia na hilo mzuiaji yoyote.

Hakika yeye anayajua yaliyo jahara na yaliyofichika.

Hakuna mwenye shaka kwamba Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu. Hapa ameashiria hilo baada ya kutaja kusahau kwa mtume ili kumwambia Nabii wake mtukufu: Sisi tunajua yaliyo katika nafsi yako kwamba wewe ulikuwa unahofia kisikupite kitu chochote. Hapana, hakuna kitaka­chokupita; kuwa katika amani na utulivu.

Tutakasahilisha yawe mapesi.

Makusudio mepesi ni sharia nyepesi. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) atakusahilishia njia ya wahyi kwa ishara zake na hukumu zake ili uzihifadhi na kuzifanyia kazi kama anavyotaka Mwenyezi Mungu.

Basi kumbusha, kwani kukumbusha kunafaa.

Hakuna mwenye shaka kwamba kukumbusha ni wajibu hata kama utajua kuwa hakutanufaisha, ili kuondoa visababu na kuleta hoja, vinginevyo kusingelikuwa na hisabu na adhabu. Mwenyezi Mungu Mtume anasema:

رُسُلًا مُبَشِّرِينَ وَمُنْذِرِينَ لِئَلَّا يَكُونَ لِلنَّاسِ عَلَى اللَّهِ حُجَّةٌ بَعْدَ الرُّسُلِ ۚ {165}

“(Ni) Mitume wabashiri, waonyaji, ili watu wasiwe na hoja juu ya Mwenyezi Mungu baada ya mitume; Juz. 6 (4:165).

Kwa hiyo basi herufi in hapa itakuwa mbali tena mbali sana kuwa ni ya shart (kuifasiri kukumbusha kama kutafaa kukumbusha).

Makusudio hapa ni kubainisha uhalisia; yaani ananufaika na ukumbusho mwenye kutaka uongofu, lakini mwenye kung’ang’ania upotevu hanufaiki na chochote.

Linalofahamisha makusudio ya maana haya ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtume iliyokuja moja kwa moja.

Atakumbuka mwenye kuogopa na atajiepusha nako muovu.

Kwa hiyo ukumbusho unamfaa yule aliyeamshwa na kumwogopa Mwenyezi Mungu wala haupingi isipokuwa muovu aliyepofushwa na matamanio na uovu wake ukamshinda.

Ambaye ataingia moto ulio mkubwa kwa ukali wake na vituko vyake.

Kisha hatokufa humo wala hatakuwa hai.

Tutaifasiri kwa kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَالَّذِينَ كَفَرُوا لَهُمْ نَارُ جَهَنَّمَ لَا يُقْضَىٰ عَلَيْهِمْ فَيَمُوتُوا وَلَا يُخَفَّفُ عَنْهُمْ مِنْ عَذَابِهَا {36}

“Na wale ambao wamekufuru watakuwa na moto wa Jahannam, hawahukumiwi wakafa wala hawatapunguziwa adhabu yake.” Juz: 22 (35:36).

Sheikh Muhammad Abduh anasema katika kufasiri kumbusha, kwani kukumbusha kunafaa: “Jihadhari na kuhadaika na wayasemayo wale wanovaa vazi la ulama na kudai madai ya wapumbavu kwamba si wajibu kukumbusha kwa vile kukumbusha hakufai wakitoa hoja kwa Aya hii.

“Kama ingelikuwa kweli kauli yao hiyo basi isingelikuwa ni wajibu kukumbusha wakati wowote, kwa sababu hakuna wakati usiokuwa na wapinzani wala kusalimika na wanaomlani Mungu. Wengine wanajitamkia kwa hawaa lakini wanajikinga na woga na kutoa hoja kwa uvivu wao na wanapenda kujipamba machoni mwa watu hata kama wataingia kwenye chuki ya Mwenyezi Mungu.

Hakika amekwisha faulu aliyejitakasa.

Makusudio ya kufaulu hapa ni kuokoka na hasira za Mwenyezi Mungu na adhabu yake. Kujitakasa ni kujisafisha na dhambi.

Na akalitaja jina la Mola wake na akaswali.

Makusudio ya kutaja hapa ni yale yanayomkurubisha kwenye heri na kumweka mbali na shari. Ama harakati za ulimi tu peke yake sio lengo. Wala hakuna katika amri ya Mwenyezi Mungu na makatazo yake isipokuwa ni nyenzo ya kufanya heri na kujiweka mbali na shari.

Inatosha kuwa ni dalili ya hakika hii kauli yake Mtume (s.a.w): “Hakika si mengineyo nimetumwa kukamilisha hulka njema” na kauli yake Mwenyezi Mungu:

وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا رَحْمَةً لِلْعَالَمِينَ {107}

“Na hatukukutuma ila uwe ni rehema kwa walimwengu.” Juz. 17 (21:107).

Makusudio ya maswali ni swala tano, kwani ndizo nguzo za dini.

Bali mmeathirika na maisha ya dunia.

Hapa ndio inapatikana siri ya mwanzo na mwisho ya kuikataa haki kwa makusudi. Kuwa mtumwa wa dunia na kuing’ang’ania kama mtoto anavy­oling’ang’ania titi la mama yake, kwa hiyo imemuweka mbali na Mwenyezi Mungu na haki na utu.

Na akhera ni bora na yenye kubaki zaidi; bali hakuna heri yoyote kabisa katika dunia ikiwa sio nyenzo ya heri ya akhera. Kwa sababu uamirishaji wa dunia unaharibika, ufalme wake unaondoka na mali yake inaisha.

Amesema kwenye Nahjul-Balagha: “Kila kitu duniani kusikiwa kwake ni kukubwa kuliko kuonekana kwake, na kila kitu Akhera kuonwa kwake ni kukubwa kuliko kusikiwa kwake. Jueni kwamba linalopungua duniani na kuzidi Akhera ni bora kuliko linalopungua Akhera na kuzidi duniani.”

Hakika haya yamo katika vitabu vya mwanzo vitabu vya Ibrahim na Musa.

‘Haya’ ni ishara ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu : “Hakika amek­wisha faulu aliyejitakasa’ maana ni kuwa mwito wa mitume kwa upande wa kiitikadi ni mmoja kwa sababu aliyewatuma ni mmoja na kauli yake ni moja haipingani.

Tofauti zinakuweko kwenye tanzu ambazo zinaenda na wakati.

Maadamu ni hivyo basi wale wanaomwamini Ibrahim kama waarabu na wanaomwamini Musa kama Mayahudi ni juu yao wamwamni Muhammad (s.a.w.); vinginevyo watakuwa ni katika wale wanaoamini msingi mmoja na kuukataa wakati huo huo.

  • 3137 views

Sura Ya Themanini Na Nane: Al-Ghashiya

Imeshuka Makka Ina Aya 26.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ {1}

Je, imekujia habari ya msiba unaofunikiza?

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ {2}

Nyuso siku hiyo zitadhalilika.

عَامِلَةٌ نَاصِبَةٌ {3}

Zitatumika na kutabika.

تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً {4}

Zitaingia katika moto mkali.

تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ {5}

Zitanyweshwa katika chem­chem inayochemka.

لَيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِنْ ضَرِيعٍ {6}

Hawatakuwa na chakula isipokuwa cha miba.

لَا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِنْ جُوعٍ {7}

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَاعِمَةٌ {8}

Nyuso siku hiyo zitaneemeka.

لِسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ {9}

Zitakuwa radhi kwa mahangaiko yake.

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ {10}

Katika Bustani ya juu.

لَا تَسْمَعُ فِيهَا لَاغِيَةً {11}

Hazitasikia humo upuzi.

فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ {12}

Humo mna chemchem inay­otiririka.

فِيهَا سُرُرٌ مَرْفُوعَةٌ {13}

Mna viti vilivyoinuliwa.

وَأَكْوَابٌ مَوْضُوعَةٌ {14}

Na bilauri zilizowekwa.

وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ {15}

Na mito iliyopangwa.

وَزَرَابِيُّ مَبْثُوثَةٌ {16}

Na mazulia yaliyopangwa huku na huko.

أَفَلَا يَنْظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ {17}

Je, hawamtazami ngamia jinsi alivyoumbwa?

وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ {18}

Na mbingu jinsi zilivyoinuli­wa?

وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ {19}

Na milima jinsi ilivyosi­mamishwa?

وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ {20}

Na ardhi jinsi ilivyotan­dazwa?

فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنْتَ مُذَكِّرٌ {21}

Basi kumbusha hakika wewe ni mkumbashaji tu.

لَسْتَ عَلَيْهِمْ بِمُصَيْطِرٍ {22}

Wewe si mwenye kuwatawalia.

إِلَّا مَنْ تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ {23}

Lakini anayerudi nyuma na akakufuru.

فَيُعَذِّبُهُ اللَّهُ الْعَذَابَ الْأَكْبَرَ {24}

Basi Mwenyezi Mungu atamwadhibu adhabu iliyo kubwa sana!

إِنَّ إِلَيْنَا إِيَابَهُمْ {25}

Hakika ni kwetu marejeo yao.

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُمْ {26}

Kisha hakika ni juu yetu his­abu yao.

Maana

Je, imekujia habari ya msiba unaofunikiza.

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume (s.a.w), lakini sababu inawaenea wote. Msiba unaofunikiza ni Kiyama. Kimeitwa hivyo kwa sababu kinafunikiza watu kutokana na shida yake na vituko. Vyovyote iwavyo, maana yake ni: Je, unajua kitu kuhusu Kiyama? Watu watakuwa makundi mawili.

Kundi la kwanza ni wale ambao nyuso siku hiyo zitadhalilika.

Athari ya udhalili, hizaya na utwevu itajitokeza kwenye hizo nyuso.

Zitatumika na kutabika.

Maana ni kuwa watu wa nyuso hizi walifanya kazi sana duniani, lakini walifanya kwa ajii ya asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo hakuna walichopata kutokana na kazi yao hiyo isipokuwa tabu na kuchoka duni­ani, na Akhera ni hasara na adhabu.

Katika Nahjul-balagha anasema: “Mwenye hasara zaidi ya kupunjika na aliyehangaika bure zaidi ni yule aliyeutumia mwili wake kwa juhudi kati­ka kutafuta mali, lakini majaaliwa hayakumsaidia kwenye matakwa yake, akatoka duniani akiwa na masikitiko na akafika Akhera na majukumu yake.”

Zitaingia katika moto mkali; yaani zitachomwa kwenye moto unaowaka.

Zitanyweshwa katika chemchem inayochemka.

Neno la kiarabu lililotumika kuelezea kuchemka, lina maana ya kufikia nyuzi joto za mwisho. Mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

يَطُوفُونَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ حَمِيمٍ آنٍ {44}

“Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayochemka.” Juz. 27 (55:44).

Hawatakuwa na chakula isipokuwa cha miba.

Mweny Kamusi ya Almuhit anasema: neno dharii (tulilolifasiri kwa maana ya miba) ni mmea usiokurubiwa na mnyama kwa ubaya wake.

Vyovyote iwavyo maana ni kuwa ni chakula kibaya. Ni tosha kuwa ni chakula cha watu wa Motoni.

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa;

Yaani hakiondoi dhara wala hakileti manufaa.

Kundi la pili ni: nyuso nyingine siku hiyo zitaneemeka, zenye uangavu na uzuri.

Zitakuwa radhi kwa mahangaiko yake.

Zitaridhia ujira wake Akhera, kutokana na kazi yake duniani.

Katika Bustani ya juu, iliyo tukufu kwa sifa zake zote; mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Basi yeye atakuwa katika maisha ya kuridhia, katika Bustani ya juu.” Juz. 29 (69:21-22).

Hazitasikia humo upuzi, wala maneno yasiyokuwa na maana. Mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا {25}

“Humo hawatasikia upuzi wala maneno ya dhambi.” Juz. 27 (56-25).

Humo mna chemchem inayotiririka, bustani zipitiwazo na mito chini yake. Mna viti vilivyoinuliwa kuepukana na ardhi.

Na bilauri zilizowekwa pambizoni mwa chemchem, wanazitumia wakita­ka kunywa maji.

Na mito iliyopangwa, ya kuegemea. Na mazulia yaliyopangwa huku na huko.

Kila yaliyoelezwa hapa katika wasifu wa Pepo ni baadhai ya makumi ya Aya zilizopita. Na kila yaliyosmewa au yatakayosemwa katika wasifu wake ni tafsiri na ubainifu wa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 وَفِيهَا مَا تَشْتَهِيهِ الْأَنْفُسُ وَتَلَذُّ الْأَعْيُنُ ۖ {71}

“Vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda, na macho yanavifurahia.” Juz. 25 (43:71).

Je, hawamtazami ngamia jinsi alivyoumbwa?

Unaweza kuuliza: Kwanini Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemuhusu kumta­ja ngamia badala ya wanyama wengine?

Sheikh Muhammad Abduh amejibu kuwa ni mnyama bora na mwenye manufaa zaidi kwa waarabu. Pia ni kiumbe wa ajabu. Kwani pamoja na nguvu zake, lakini anamtii aliye dhaifu; na umbo lake limeandaliwa kube­ba vitu vizito. Huwa anapiga magoti ili abebe, kisha anatembea pole pole na mzigo wake akivumilia kiu, njaa na mengineyo ambayo hayafanani na wanyama wengineo.

Na mbingu jinsi ilivyoinuliwa juu ya ardhi pamoja na nyota zake zenye kumeremeta.

Na milima jinsi ilivyosimamishwa, kuwa vigingi vya ardhi na ikaituliza isitingishike. Lau si milma ardhi ingeliyumba pamoja na watu wake.

Na ardhi jinsi ilivyotandazwa.

Mwenyezi Mungu ameifanya ni tandiko kwa viumbe wake walale humo na watembee. Ilivyo ni kuwa kutandazwa ardhi ni kwa inavyoonekana kwa macho, sio uhalisia wake. Mwenyezi Mungu ameashiria mduara wa ardhi aliposema: “Ameumba mbingu na ardhi kwa Haki. Huuzongazonga usiku kwenye mchana, na Huuzongazonga mchana kwenye usiku.” Juz. 23 (39:5).
Sheikh Muhammad Abduh anasema: Imekuwa vizuri kutajwa ngamia pamoja na mbingu, milima na ardhi, kwa sababu viumbe hivi ndivyo wanavyoviona waarabu katika mabonde yao.

Basi kumbusha hakika wewe ni mkumbashaji tu.

Huu ni ufasaha na uwazi zaidi wa kutaja shughuli ya Mtume - kukum­busha:

 وَمَا عَلَى الرَّسُولِ إِلَّا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ {54}

“Na hapana juu ya mtume ila kufikisha (ujumbe) wazi wazi.” Juz. 18 (24:54).

Wewe si mwenye kuwatawalia, lakini anayerudi nyuma na akakufuru, basi Mwenyezi Mungu atamwadhibu adhabu iliyo kubwa sana. Hakika ni kwetu marejeo yao, kisha hakika ni juu yetu hisabu yao.

Wewe Muhammad si mtawala kwao mpaka uwalazimishe imani, lakini hii haimaanishi kuwa wanaokukadhibisha watachwa burubure. Hapana! wao watarejea kwetu na amali zao na makusudio yao yaliyowekwa rahani, wala hawana malipo isipokuwa adhabu ya fedheha.

  • 1715 views

Sura Ya Themanini Na Tisa: Al-Fajr

Imeshuka Makka Ina Aya 30

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

وَالْفَجْرِ {1}

Naapa kwa alfajiri.

وَلَيَالٍ عَشْرٍ {2}

Na kwa masiku kumi.

وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ {3}

Na kwa shufwa na witiri.

وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ {4}

Na kwa usiku unapopita.

هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِذِي حِجْرٍ {5}

Je, katika hayo mna kiapo kwa Mwenye akili?

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ {6}

Je, hukuona jinsi Mola wako alivyowafanya A’ad?

إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ {7}

Wa Iram wenye maguzo?

الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ {8}

Ambao hakuumba mfano wake katika miji?

وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ {9}

Na Thamud waliopasua maja­bali bondeni?

وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ {10}

Na Firauni mwenye vigingi?

الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ {11}

Ambao walipituka mipaka katika miji?

فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ {12}

Wakakithirisha humo ufisa­di?

فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ {13}

Basi Mola wako akawami­minia kiboko cha adhabu.

إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ {14}

Hakika Mola wako yuko kwenye kuotea.

فَأَمَّا الْإِنْسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ {15}

Na ama mtu Mola wake anapomjaribu na akamkir­imu na akamneemesha, huse­ma: Mola wangu amenikir­imu.

وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ {16}

Na anapomjaribu, akam­punguzia riziki yake, husema: Mola wangu amenitweza.

Aya 1-16:Alfajiri Na Masiku Kumi

Maana

Naapa kwa alfajiri, na kwa masiku kumi, na kwa shufwa na witiri na kwa usiku unapopita.

Makusudio ya Alfajiri hapa ni kila alfajiri, kwa kuchukulia dhahiri ya neno. Ama masiku kumi hakuna dhahiri ya kuwa ni masiku maalum, wala haku­na karina inayoweza kutusaidia. kwa ajili hiyo tunayanyamazia yale aliy­oyanyamazia Mwenyezi Mungu.
Ama kauli ya kwamba ni mianzo ya mwezi wa Dhul-hijja (mfunguo tatu) au Muharram (mfunguo nne) au kuwa ni mwisho wa Ramadhani, inahitajia dalili.

Sheikh Muhammad Abduh amejaribu kuainisha kuwa ni kila masiku ya mwanzo wa mwezi na akaelezea kwa urefu, lakini hakuleta hoja ya kuki­naisha.

Mwanafunzi wake Al-Maraghi naye akamuiga kwa kila alilolisema na akanukuu ibara zake pamoja na urefu wake bila ya kuishiria kwenye chim­buko lake, kama ilivyo desturi yake.

Katika kufasiri shufwa na witiri kuna kauli nyingi; iliyo karibu zaidi na dhahiri ya tamko ni ishara ya kuwa ni hisabu na kudhibiti viwango tu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameapa kwa hisabu ili kutanabahisha kwenye faida zake.

Makusudio ya kupita usiku ni kuondoka. Kwa hiyo hapa Mwenyezi Mungu amechanganya viapo viwili: Kutangulia mchana na kuja usiku, kama alivyosema.

وَاللَّيْلِ إِذْ أَدْبَرَ {33}

وَالصُّبْحِ إِذَا أَسْفَرَ {34}

“Na kwa usiku unapokucha na kwa asubuhi inapopambazuka.” Juz. 29 (74:33-34).

Je, katika hayo mna kiapo kwa Mwenye akili?

Swali hili ni kuripoti uhalisia, kwa maana ya kuwa ndivyo ilivyo hivyo kuwa hakika katika hayo mna kiapo kwa mwenye akili. Makusudio ya kuapia hivi ni hoja na dalili, kwa sababu ndani yake kuna uthibitisho wahaki.

Neno akili tumelitoa kwenye neno Hijr lenye maana nyingi; miongoni mwazo ni majumba ya Thamud, na kizuizi cha Al-kaiba. Limetumika neno hilo kwa maana ya akili kwa vile inamzuia mwenye nayo na mambo mengi.

Maana ni kuwa katika vitu alivyoapia navyo Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuna hoja tosha za kuweko Mwenyezi Mungu, uweza wake na hikima yake. Kwa sababu mazingatio na hikima iliyomo inafahamisha hilo kwa utoaji; sawa na unavyofahamisha ukulima kuwako mkulima.

Je, hukuona jinsi Mola wako alivyowafanya A’ad wa Iram wenye maguzo, ambao hakuumba mfano wake katika miji?

A’d ni kaumu ya Hud. Iram ni jina la kabila la A’d kwa kunasibishwa kwa mmoja wa babu yao, aliyeitwa Iram.

Sheikh Muhammad Abduh anasema, makusudio ya maguzo hapa ni magu­zo ya mahema yao au ni kinaya cha nguvu walizo kuwa nazo. Lililo karibu zaidi na usawa ni kuwa makusudio ya maguzo hapa ni majen­go na ngome kwa sababu Mtume wao aliwaambia kwa kutokubaliana nao:

أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ آيَةً تَعْبَثُونَ {128}

وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ {129}

“Je, mnajenga juu ya kila muinuko ishara ya kufanyia upuzi? Na mnajen­ga ngome ili mkae milele?” Juz. 19 (26:128-129).

Naam! Sisi tuko pamoja na Sheikh Muhamad Abduh katika kauli yake hii: “Hapa wafasiri wamepokea hekaya nyingi katika kuleta picha ya Iram wenye maguzo, ambazo ilikuwa ni wajibu ziepushwe na kitabu cha Mwenyezi Mungu.
Ukiona chochote katika vitabu vyao katika wasifu wa Iram, basi lifumbie jicho lako na ujihadhari na kuchunguza yamepita maelezo kuhusu A’ad na Nabii wao Hud katika Juz. 12 (11:50-56), Juz. 19 (26:123-140) na nyinginezo.

Na Thamud waliopasua majabali bondeni.

Thamud ni kaumu ya Swaleh, kupasua majabali ni ishara ya yaliyosemwa kwenye Aya nyingine isemayo: “Na mnachonga majumba milimani kwa ustadi.” Juz. 19 (26:149).

Na Firauni mwenye vigingi; yaani majengo adhimu, kama ihram (pyra­mids).

Ambao walipituka mipaka katika miji; wakakithirisha humo ufisadi, basi Mola wako akawamiminia kiboko cha adhabu.

Kuanzia neno ambao walipituka mipaka na kuendelea, ni sifa za A’ad, Thamud na Firaun. Mwenyezi Mungu ametaja kiboko kwa sababu kinaashiria kukaririka adhabu; kwani Mwenyezi Mungu aliwaadhibu A’ad kwa upepo, Thamud kwa ukelele na Firauni kwa kuzama majini.

Hakika Mola wako yuko kwenye kuotea.

Hili ni jawabu la kiapo katika mwanzo wa Sura. Imesemekana kuwa jawabu sio hili bali ni la kukadiria, kuwa atawaadhibu wenye hatia. Kwenye makadirio yote mawili natija ni moja.

Maana yako wazi kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu anajua makusudio ya waja na vitendo vyao na atawalipa kulingana navyo.

Na ama mtu Mola wake anapomjaribu na akamkirimu na akam­neemesha, husema: Mola wangu amenikirimu. Na anapomjaribu, akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu amenitweza.

Mtu hapa ni jinsi ya mtu yeyote, kumkirimu na kumneemesha ni wasaa wa riziki na kumjaribu ni kumfanyia mtihani. Maana ya kumfanyia mtihani kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) mja wake, ni kumpa sababu za kudhi­hirisha hakika yake; kama utajiri na ufukara. Akishukuru kwa utajiri na kuwa na subira kwa ufukara, atastahiki thawabu. Akikufuru kwa ufukara na akapituka mipka kwa utajiri atastahili adhabu.

Kwa maneno mengine nikuwa mtihani kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kuweko mgongano ambao utadhihirisha vitendo vya mwema na muovu. Hiyo ni kwa ajili ya maandalizi ya kumlipa wema kwa wema na ubaya kwa ubaya, pamoja na kupatikana hoja.

Hii ni hali ya Mwenyezi Mungu pamoja na mja wake. Ama hali ya mtu mpotevu ni kupima takrima anayoipata kutoka kwa Mwenyezi Mungu ­riziki ikiwa ni kubwa anadhani kuwa yeye ni katika walio karibu zaidi na Mwenyezi Mungu, na kwamba hataulizwa kitu wala hataadhibiwa kwa alilolitenda au kulifanya.

Sambamba na walivyokuwa vigogo wa kishrik­ina, walikuwa wakitoa dalili ya kukirimiwa kwao na Mwenyezi Mungu kwa wingi wa mali na kuwa Mwenyezi Mungu amewatweza waumini kwa ufukara.

Na kama Mwenyezi Mungu akimdhikisha mpotevu kwenye riziki yake ili angalau atubie, hudhania kuwa Mwenyezi Mungu amemtweza.

Inatosha kwa mja kuwa ni jeuri kumdhania muumba wake dhana mbaya .

Imepokewa kutoka kwa Imam Ali (a.s.): “Mwislamu akipata dhiki asimtilie shaka Mola wake, bali ajitilie shaka yeye kwa Mola wake mwenye funguo za mambo yote.” Umetangulia mfano wake katika Juz. katika Juz.17 (21:35).

كَلَّا ۖ بَلْ لَا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ {17}

Si hivyo! bali nyinyi humumkirimu yatima,

وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ {18}

Wala hamuhimizani kulisha masikini;

وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَمًّا {19}

Na mnakula mirathi kula kwa pupa.

وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا {20}

Na mnapenda mali kupenda sana.

كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا {21}

Si hivyo! Ardhi itakapopand­wa pondwa.

وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا {22}

Na akaja Mola wako na malaika safu safu.

وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنْسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ {23}

Na ikaletwa siku hiyo Jahannam, siku hiyo atakum­buka mtu, lakini kutamfaa nini kukumbuka?

يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي {24}

Atasema: laiti ningeutan­gulizia uhai wangu!

فَيَوْمَئِذٍ لَا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ {25}

Basi siku hiyo hataadhibu adhabu yake yoyote.

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ {26}

Wala hatafunga kufunga kwake yoyote.

يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ {27}

Ewe nafsi iliyotua!

ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَرْضِيَّةً {28}

Rejea kwa Mola wako hali ya kuwa radhi umeridhiwa!

فَادْخُلِي فِي عِبَادِي {29}

Basi ingia katika waja wangu.

وَادْخُلِي جَنَّتِي {30}

Na ingia katika Pepo yangu.

Aya 17-30: Mnapenda Sana Mali

Si hivyo! Karama sio mali mbele ya Mwenyezi Mungu, bali ni kwa takua, wala ufukara si utwevu, isipokuwa ni kwa makusudio na matendo mabaya. Bali nyinyi ni washari zaidi, katika viumbe wa Mwenyezi Mungu, kutokana na sababu zifuatazo:

Humumkirimu yatima; hamuwafanyii wema wakimbizi wasiokuwa na wa kuwahami wala kuwatunza kutoka serikalini wala kwao, na nyinyi hamshughulikii mambo yao.

Hamuhimizani kulisha masikini; yaani hamuhimizani kujitolea kwa ajili ya wasio nacho na kuwatengenezea mambo yao.

Na mnakula mirathi kula kwa pupa: Mirathi ni mali inayogura kutoka kwa maiti kwenda kwa warithi wake. Mali nyingi zinazorithiwa huwa mna haki maalum kwa mwenye kuomba na anayejizuia, lakini warithi wanawanyima wenye haki hiyo.

Na mnapenda mali kupenda sana; iwe mirathi au isiyokuwa mirathi; ya halali au haramu.

Si hivyo! Haitakikanii kwa mtu kuifanyia ubahili mali katika njia ya heri; kwa sababu yeye ataulizwa hilo, siku ardhi itakapopandwa pond­wa.

Kukaririka neno kupondwa ni kufuatana yaani kupondwa baada ya kupondwa. Maana ni kuwa kani mvutano itaondoka siku ya Kiyama. Kwa hiyo sehemu moja itaiponda nyingine na utafululiza mpondano mpaka yaharibike yote yaliyo katika ardhi; ikiwemo milima na majengo.

Umetangulia mfano wake katika Juz. katika Juz. 29 ( 69:14).

Na akaja Mola wako na malaika safu safu.

Kuja Mola wako ni kuja amri yake, kadhaa yake, utukufu wake, hukumu yake na utawala wake. Safu safu yaani safu mbali mbali

Na ikaletwa siku hiyo Jahannam.

Itaonekana waziwazi na kuwa katika ulimwengu wa kuonekana baada ya kuwa katika ulimwengu wa ghaibu.

Siku hiyo atakumbuka mtu, lakini kutamfaa nini kukumbuka. Atasema: Laiti ningeliutangulizia uhai wangu.

Waonyaji na watoa nasaha walimwambia mkosefu mwenye jeuri: fanya kwa ajili ya maisha yako ya Akheraa hapa duniani. Akasema Akhera gani? Ni njozi na mawazo tu! Lakini itakapofika siku ya upambanuzi na kuona mahali pake katika Jahannam atasema: haya ndio maisha yangu ya kubakia na makazi ya daima. Kumbe maisha ya dunia yalikuwa ni ya kupi­ta tu, lakini ningeliyatengenezea ya kubakia kwenye yanayopita. Alisahau Akhera alipokuwa duniani kunakofaa toba na ukumbusho; anakumbuka akiwa akhera kutamfaa nini kumbuka.

Basi siku hiyo hataadhibu adhabu yake yoyote, wala hatafunga kufun­ga kwake yoyote.

Pia imesomwa kwa Maf’ul; kwa maana hataadhibiwa na hatafungwa. Maana ya visomo vyote viwili ni kuwa adhabu mbaya zaidi duniani ni nafuu ikilinganishwa na adhabu ya chini Akhera.

Ewe nafsi iliyotua! Rejea kwa mola wako hali yakuwa radhi umerid­hiwa. Basi ingia katika waja wangu na ingia katika Pepo yangu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kutaja nafsi inayoamrisha uovu ambayo haitulii isipokuwa kwa masilahi yake na hawaa yake, sasa anata­ja nafsi iliyotulia, kuwa ni ile ambayo imemwamini Mwenyezi Mungu, ikasikiliza kwa makini mawaidha yake, ikatumia amri yake na makatazo yake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameibanisha nafsi hii kwa kauli yake:

الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ طُوبَىٰ لَهُمْ وَحُسْنُ مَآبٍ {29}

“Wale ambao wameamini na wakafanya mema, raha ni yao na marejeo mazuri.” Juz. 13 (13-29).

Maana ya kuridhia na kuridhiwa ni kuwa itashukuru ujira wake na nafasi yake mbele ya Mwenyezi Mungu kwa sababu ameyashukuru mahangaiko yake na amali yake.

Sheikh Muhammad Abduh anasema katika maana ya kurejea kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na kuingia katika waja wake. “Kurejea kwa Mwenyezi Mungu ni kufananisha takrima kwake; vinginevyo Mwenyezi Mungu yuko pamoja nasi popote tulipo. Na kuingia katika waja wake ni kuwa miongoni mwao. Na waja wanaostahiki kuwa miongoni mwao ni wale wenye takua wenye kutukuzwa.”

  • 2567 views

Sura Ya Tisini: Al-Balad

Imeshuka Makka Ina Aya 20.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

لَا أُقْسِمُ بِهَٰذَا الْبَلَدِ {1}

Naapa kwa mji huu!

وَأَنْتَ حِلٌّ بِهَٰذَا الْبَلَدِ {2}

Nawe unaukaa mji huu.

وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ {3}

Na kwa mzazi na alichokizaa!

لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنْسَانَ فِي كَبَدٍ {4}

Hakika tumemuumba mtu katika tabu.

أَيَحْسَبُ أَنْ لَنْ يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ {5}

Je, anadhani kuwa hapana yeyote atakayemuweza?

يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُبَدًا {6}

Anasema nimeteketeza chun­gu ya mali.

أَيَحْسَبُ أَنْ لَمْ يَرَهُ أَحَدٌ {7}

Je, anadhani kuwa hapana yeyote anayemuona?

أَلَمْ نَجْعَلْ لَهُ عَيْنَيْنِ {8}

Je, hatukumpa macho mawili?

وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ {9}

Na ulimi na midomo miwili?

وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ {10}

Na tukambanishia njia mbili?

فَلَا اقْتَحَمَ الْعَقَبَةَ {11}

Basi mbona hakujitoma njia nzito.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْعَقَبَةُ {12}

Nini la kukujulisha ni ipi hiyo njia nzito?

فَكُّ رَقَبَةٍ {13}

Ni kumwacha huru mtumwa;

أَوْ إِطْعَامٌ فِي يَوْمٍ ذِي مَسْغَبَةٍ {14}

Au kumlisha siku ya njaa.

يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ {15}

Yatima aliye na udugu.

أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ {16}

Au maskini hohe hahe.

ثُمَّ كَانَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا بِالْمَرْحَمَةِ {17}

Kisha akawa miongoni mwa walioamini na wakatenda mema, wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ {18}

Hao ndio watu wa kuliani.

وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا هُمْ أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ {19}

Na wale waliozikana ishara zetu, hao ndio watu wa kushotoni.

عَلَيْهِمْ نَارٌ مُؤْصَدَةٌ {20}

Juu yao ni moto uliokomewa.

Maana

Naapa kwa mji huu.

Herufi la hapa ni kama ya Juz 27 (52:75) na katika Juzuu hii tuliyo nayo (81:15). Makusudio ya mji hapa ni Makka yenye kutukuzwa kwa nyumba tukufu zaidi iliyowekewa watu, yenye kubarikiwa, na kwa utukufu wa Nabii aliyezaliwa humo na kutumwa kuwa rehema kwa walimwengu.

Nawe unaukaa mji huu.

Maneno yanaelekezwa kwa Muhammad (s.a.w.) kwa hiyo kiapo cha kuapia na Makka kimefungwa na ukaaji wa Mtume hapo, kujulisha kuwa Makka imezidi utukufu kwa kuzaliwa kwake na kukaa kwake.

Sheikh Muhammad Abduh amechagua kauli ya anayesema kuwa neno Hillu hapo ni kwa maana ya kuhalalishiwa; yaani watu wa Makka wali­halalisha kumuudhi Mtume katika mji wa amani, mpaka akalazimika kuu­toka.

Maana haya yenyewe ni sahihi, lakini yako mbali na ufahamisho wa tamko. Kwa sababu linalokuja haraka kwenye ufahamu ni kukaa sio kuhalalishiwa.

Na kwa mzazi na alichokizaa.

Jamaa katika wafasiri wamesema makusudio ya mzazi ni Adam na ali­chokizaa ni kizazi chake; kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu hakusema na aliyemzaa, ili kuashria utukufu wa shani wa aliyezaliwa, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Juz:

 وَاللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا وَضَعَتْ {36}

“Na Mwenyezi Mungu anajua sana aliyemzaa.” (3:36).

Wengine akiwemo Ibn Abbas, abariy na Sheikh Muhammad Abduh wanasema makusudio ya mzazi na kilichozaliwa ni kila kitu, awe mtu, mnyama au mmea. Kauli hii iko karibu na dhahiri ya tamko kuliko nyingine. Ama lengo la kuapa kwa mzazi na alichokizaa ni kutambulisha kuanzishwa viumbe hai na kukua kwake kutoka umbo moja hadi jingine; kuanzia tone la manii kwa mtu au mnyama na punje kwa miti na mimea mingineyo.

Hakika tumemuumba mtu katika tabu na mashaka.

Yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameuumba mtu apambane na mapendeleo yake na matakwa yake pamoja na mapambano ya maisha na shida zake; kisha baada ya hapo apambane na uchungu wa mauti, giza la kaburini na upweke, hatimaye kwenye vituko vya Kiyama na kwenda mbele ya Mola kwa ajili ya hisabu ya aliyoyafanya na kuyatenda.
Je, anadhani kuwa hapana yeyote atakayemuweza?

Anayedhani ni mtu kwa kuzingatia baadhi yake sio wote. Maana ni kuwa baadhi ya watu wanadhani kuwa wana nguvu za kutosha kumzuia yeyote vyovyote atavyokuwa na kusahau kwamba wao ni viumbe dhaifu wanaoumizwa na chawa na kufa kwa kupaliwa; kama asemavyo Imam Ali (a.s).

Anasema nimeteketeza chungu ya mali.

Mfumo wa maneno unafahamisha kuwa anayesema hivyo ni tajiri aliyetoa mali yake kwa kutaka umashuhuri na kuzungumzwa vizuri, huku akijizuia kutoa katika njia ya Mwenyezi Mungu ya heri. Maana ni kuwa akiambiwa mbadhirifu huyu, kwa nini hutoi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Atasema nimetoa nyingi sana mpaka inakurubia mali yangu kuisha, lakini sitoi kwa njia mnayonitakia.

Je, anadhani kuwa hapana yeyote anayemuona.

Je, anadhani huyu mwenye kufitiniwa na umashuhuri kwamba Mwenyezi Mungu ameghafilika naye na matendo yake na malengo yake. Kuna hadith isemayo. “Kesho mtu ataulizwa kuhusu mwili wake alivyoutumia na umri wake alivyo umaliza na mali yake alivyoichuma na alivyoitumia.”

Je, hatukumpa macho mawili na ulimi na midomo miwili na tukam­banishia njia mbili?

Katika Tafsir Ar-Razi, kuna maelezo kuwa aliyesema nimeteketeza chun­gu ya mali, vile vile alisema kwa lugha ya maneno au ya kimazingira kuwa ni nani anayenihisabu na mali yangu nikiizuia au nikiitoa? Ndio Mwenyezi mungu (s.w.t) akamjibu. Atakuhisabu yule aliyekupa viungo hivi.

Hii iko karibu sana na hali ilivyo. Vyovyote iwavyo ni kuwa macho maw­ili ni ishara ya neema ya kuona, na ulimi ni neema ya kusema na kubain­isha, na uongofu ni neema ya akili na ufumbuzi.

Makusudio ya njia mbili ni njia ya heri na shari. Kwa akili mtu anajihad­hari na hili na kufuata lile. Anasema kwenye ahjul-balagha: “Inakutosha kuwa una akili, kwamba imekuwekea wazi njia ya kupotea kwako na kuongoka kwako.”

Umetangulia mfano wake katika Juz. 29 (76:3).

Basi mbona hakujitoma njia nzito, nini la kukujulisha ni ipi hiyo njia nzito?

Neno njia nzito tumelitoa kwenye neno Aqaba lenye maana ya njia ngumu kwenye milima. Makusudio yake hapo ni matendo mema, kwa sababu yanahitajia juhudi, subira juu ya mashaka na kudhibiti mapendeleo; hasa kutoa mali katika njia ya heri.

Miongoni mwa matendo mema au yaliyo muhimu ni kumwacha huru mtumwa au kumlisha siku ya njaa yatima aliye na udugu au masikini hohe hahe. Kisha akawa miongoni mwa waliaoamini na wakatenda mema, wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumumiana.

Kuusina kusbiri ni kuusiana waumini kusubri kwenye jihadi ili kuithibitisha haki na kukataa kusalimu amri kwenye batili. Na kuusiana kuhurumian ni kusaidiana na kumpendelea mtu ndugu yake lile analolipen­delea kwa nafsi yake.

Ujumla wa maana nikuwa yule aliyetoa mali yake kwa kutaka umashuhuri, hakupita njia nzito na vikwazo vilivyo baina yake na kuokoka na adhabu na maangamizi, bali yeye ndiye mwenye hasara zaidi na mwingi zaidi wa adhabu.

Lau kama yeye angelitoa katika njia ya Mwenyezi Mungu na akawa katika walioamini na akausiana kusubiri na kuhurumiana, basi angelipituka hiyo njia nzito na kuwa katika amani ya ghadhabu za Mwenyezi Mungu na adhabu yake.

Hao ndio watu wa kuliani.
Hao ni hao walioamini wakatoa na kuusiana. Watu wa kuliani ni watu wema ambao kesho watapewa maandishi ya wema na amani kwa mikono yao ya kulia.

Na wale waliozikana ishara zetu hao ndio watu wa kushotoni juu yao ni moto uliokomewa.

Watu wa kushotoni ni watu waovu ambao watapewa maandishi ya uovu na kiza kwa mikono yao ya kushoto na nyuma ya migongo yao, na watawek­wa kwenye Jahannam makundi makundi, wakifika wanafunguliwa milan­go wakishaingia wanafungiwa kwa muda usiokuwa na kikomo.

  • 1479 views

Sura Ya Tisini Na Mmoja: Ash-Shams

Imeshuka Makka Ina Aya 15.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَالشَّمْسِ وَضُحَاهَا {1}

Naapa kwa Jua na mwangaza wake!

وَالْقَمَرِ إِذَا تَلَاهَا {2}

Na kwa mwezi unapolifuatia!

وَالنَّهَارِ إِذَا جَلَّاهَا {3}

Na kwa mchana unapolidhi­hirisha!

وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَاهَا {4}

Na kwa usiku unapolifunika!

وَالسَّمَاءِ وَمَا بَنَاهَا {5}

Na kwa mbingu na kuzijenga kwake!

وَالْأَرْضِ وَمَا طَحَاهَا {6}

Na kwa ardhi na kuitandaza kwake!

وَنَفْسٍ وَمَا سَوَّاهَا {7}

Na kwa nafsi na kuilingan­isha kwake!

فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَاهَا {8}

Akaifahamisha uovu na takua yake.

قَدْ أَفْلَحَ مَنْ زَكَّاهَا {9}

Hakika amefaulu aliyeitakasa.

وَقَدْ خَابَ مَنْ دَسَّاهَا {10}

Na amepata hasara aliyeitweza.

كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَاهَا {11}

Thamud walikadhibisha kwa kupituka kwao mipaka.

إِذِ انْبَعَثَ أَشْقَاهَا {12}

Alipofanya haraka muovu wao zaidi.

فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ اللَّهِ نَاقَةَ اللَّهِ وَسُقْيَاهَا {13}

Akawaambia Mtume wa Mwenyezi Mungu: Mhadharini ngamia wa Mwenyezi Mungu na
kiny­waji chake.

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُمْ بِذَنْبِهِمْ فَسَوَّاهَا {14}

Wakamkadhibisha na wakamchinja Mola wao akawangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akaifanya sawa.

وَلَا يَخَافُ عُقْبَاهَا {15}

Wala haogopi mwisho wake.

Maana

Katika Sura hii Mwenyezi mungu (s.w.t.) ameapa kwa mwangaza, giza, nyota za mbingu na mpangilio wake, ardhi na utandao wake na nafsi na maandalizi yake. Ameapa na yote hayo, kwamba mwenye takua ndiye mwenye faida na mwenye hatia ndiye mwenye hasara; ufafanuzi ni huu ufuatao:

Naapa kwa Jua na mwangaza wake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameapa kwa jua liwe limejitokeza au limejificha kwa sababu ni kiumbe adhimu, vile vile ameapa kwa mwangaza wake.

Na kwa mwezi unapolifuatia hilo jua.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameaapa kwa mwezi unapoambatana na mwan­ga wake na wa Jua pale linapokosekana giza baina yake. Hilo linakuwa katika masiku meupe mwezi 13,14 na 15.

Na kwa mchana unapolidhihirisha hilo jua.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anaapa kwa mchana ambao unalidhihirisha jua wazi wazi. Lengo la kupa kwa mwanga wa mchana ni kutanabaisha faida zake kubwa ili tumshukuru Mwenyezi Mungu na kumsifu.

Na kwa usiku unapolifunika hilo jua.

Mwenyezi Mungu ameaapa kwa usiku wakati unapofunika mwanga wa jua bila ya kubakia athari yake, si moja kwa moja kama ilivyo kwa mchana, wala kwa mwanga wa mwezi unaotokana na jua.

Na hilo linakuwa katika usiku wa kwanza au wa mwisho au kila mwezi mwan­damo pale ambapo mwezi hauonekani kwa macho au unaonekana kwa udhaifu. Usiku una manufaa kama mchana; miongoni mwa manufaa ya usiku ni utulivu na raha.

Na kwa mbingu na kuzijenga kwake.

Herufi Ma hapa ni ya Masdariya. makusudio ya kujenga ni yaliyomo ndani yake; zikiwemao nyota zinazoelea kwenye falaki zake na kushikama na kwa kuunganishwa na kani mvutano.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 27 (51:47) na (51:6).

Vile vile kwenye Juzuu hii tuliyo nayo (38:12).

Na kwa ardhi na kuitandaza kwake.

Mahali pengine Mwenyezi Mungu anasema: “Na baada ya hapo akaitandika ardhi. (79:30). Kuitandaza na kuitandika yote ni maana moja.

Nafsi Na Usawa Wake

Na kwa nafsi na kuilinganisha kwake .

Nafsi ni kitu ambacho kinamfanya mtu awe mtu na mnyama kuwa mnya­ma Hatujui uhakika hasa wa kitu hiki; bali tunaona athari yake; kama vile kukua, harakati, kusikia, kuona, kuhisi uchungu kwa mtu au mnyama. Pia elimu ya mtu kwa ujumla.

Makusudio ya nafsi hapa ni nafsi ya mtu, kutokana na kauli yale Mwenyezi Mungu Mtukufu. Akaifahamisha uovu na takua yake, kwa sababu uovu na takua ni katika sifa za mtu sio mnyama.

Kwa hiyo maana ya kulinganisha sawa nafsi ya mtu ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.a.w.t) ameiumbia maandalizi kamili ya kufanya heri na shari kwa nguvu sawa; kisha akaikataza shari na akaiamrisha heri. Linalotujulisha kukusudiwa maana haya ni kauli yake Mwenyezi Mungu.

إِنَّا هَدَيْنَاهُ السَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرًا وَإِمَّا كَفُورًا {3}

“Hakika tumemwongoza njia, ama awe ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.”
Juz 29 (76:3)
.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameumba katika nafsi ya mtu maandalizi ya kufanya uovu na wema kwa pamoja kwa vile mtu anakuwa mtu kwa uhuru wake, utashi wake na uweza wake wa kufanya wema na uovu. Lau upande mmoja ungelizidi mwingine angelikuwa kama unyoya tu kwenye mavumo ya upepo; hastahiki sifa wala shutuma au thawabu na adhabu kutokana na aliyoyafanya na kuyaacha.

Hakika amefaulu aliyeitakasa na amepata hasara aliyeitweza.

Hili ndilo jawabu la kiapo. Baada ya Mwenyezi Mungu (s.a.w.t) kuapa kwa mwanga, giza mbingu na kujengwa kwake, ardhi na kutandikwa kwake na nafsi na maandalizi yake, baada ya haya sasa anasema kuwa mwenye kuchagua heri badala ya shari. Akaitwaharisha nafsi yake na uchafu wa madhambi, basi huyo atakuwa amefuzu na kupata takua.

Na mwenye kuichagulia shari na akaichafua kwa madhambi na uovu, basi huyo ni mwenye kupata hasara.

Thamud walikadhibisha kwa kupituka kwao mipaka.

Yaani walimkadhibisha mtume wao Swaleh. Thamud ni jina la kabila.
Alipofanya haraka muovu wao zaidi.

Yaani alifanya haraka kumchinja ngamia. Muovu huyu huwa anapigiwa mfano kwa uovu wake tangu maelfu ya miaka.

Akawaambia mtume wa Mwenyezi Mungu mhadharini ngamia wa Mwenyezi Mungu na kinywaji chake.

Mtume wa Mwenyezi Mungu ni Swaleh; ngamia wa Mwenyezi Mungu ni yule ngamia wa muujiza, na kinywaji chake ni ishara ya kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: ”

Akasema:

 هَٰذِهِ نَاقَةٌ لَهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَعْلُومٍ {155}

وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍ {156}

“Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalum. Wala msimguse kwa ubaya isije ikawashika adhabu ya siku kubwa.”
Juz; 19 (26:155-156)
.

Wakamkadhibisha na wakamchinja. Mola wao akawangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akaifanya sawa.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema wakamchinja na aliyemchinja ni mmoja tu, kwa vile wao waliridhia kitendo chake, bali walimhimiza hasa; kama alivyosema Mwenyezi Mungu“Basi wakamwita mtu wao akaja akamchin­ja.” Juz.27 (54:29). Maana ya kuifanya sawa ni kuwa alivunja majumba yao wote na hakuna aliyepona katika wao, si mkubwa wala mdogo:

وَاتَّقُوا فِتْنَةً لَا تُصِيبَنَّ الَّذِينَ ظَلَمُوا مِنْكُمْ خَاصَّةً ۖ {25}

“Na jikingeni na fitna ambayo haitawasibu wale waliodhulumu miongoni mwenu peke yao.”
Juz. 9 (8:25)
.

Wala haogopi mwisho wake.

Wafasiri wengi wamesema maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ali­wangamiza Thamud wala haogopi kuangamia kwao.

Wengine wamesema hapa kuna maneno yaliyotangulia na yaliyokuja nyuma, kukadiria kwake ni. alipofanya haraka muovu wao zaidi; wala hakuhofia mwisho wake, Mtume wa Mwenyezi Mungu akawaambia mhadharini ngamia na kinywaji chake. Inawezekana pia kuwa maana yake ni Mwenyezi Mungu hana wa kumpinga wala kumtaaradhi katika jambo lake.

قُلْ إِنَّ الْأَمْرَ كُلَّهُ لِلَّهِ ۗ {154}

“Waambie mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu.” Juz. 4 (3:154).
  • 1786 views

Sura Ya Tisini Na Mbili: Al-Layl

Imeshuka Makka Ina Aya 21.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ {1}

Naapa kwa usiku unapofuni­ka!

وَالنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ {2}

Na kwa mchana unapofunuli­wa!

وَمَا خَلَقَ الذَّكَرَ وَالْأُنْثَىٰ {3}

Na kwa kuumba kiume na kike!

إِنَّ سَعْيَكُمْ لَشَتَّىٰ {4}

Hakika mahangaiko yenu ni mbali mbali.

فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَاتَّقَىٰ {5}

Basi Mwenye kutoa na akawa na takua.

وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَىٰ {6}

Na akalisadikisha jema.

فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَىٰ {7}

Tutamsahilishia wepesi.

وَأَمَّا مَنْ بَخِلَ وَاسْتَغْنَىٰ {8}

Na ama mwenye kufanya ubahili na akatoshelezeka.

وَكَذَّبَ بِالْحُسْنَىٰ {9}

Na akalikadhibisha jema.

فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْعُسْرَىٰ {10}

Basi tutamsahilishia uzito.

وَمَا يُغْنِي عَنْهُ مَالُهُ إِذَا تَرَدَّىٰ {11}

Itamfaa nini mali yake atakapodidimia?

إِنَّ عَلَيْنَا لَلْهُدَىٰ {12}

Hakika ni juu yetu kuongoza.

وَإِنَّ لَنَا لَلْآخِرَةَ وَالْأُولَىٰ {13}

Hakika ni wetu mwisho na mwanzo.

فَأَنْذَرْتُكُمْ نَارًا تَلَظَّىٰ {14}

Basi ninawaonya na moto unaowaka!

لَا يَصْلَاهَا إِلَّا الْأَشْقَى {15}

Hatauingia isipokuwa muovu mno.

الَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ {16}

Ambaye amekadhibisha na kupa mgongo.

وَسَيُجَنَّبُهَا الْأَتْقَى {17}

Na ataepushwa nao mwenye takua.

الَّذِي يُؤْتِي مَالَهُ يَتَزَكَّىٰ {18}

Ambaye anatoa mali yake kwa kujitakasa.

وَمَا لِأَحَدٍ عِنْدَهُ مِنْ نِعْمَةٍ تُجْزَىٰ {19}

Wala hapana yeyote aliyem­fanyia hisani ili alipwe.

إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ رَبِّهِ الْأَعْلَىٰ {20}

Isipokuwa ni kwa kutaka radhi ya Mola wake aliye juu kabisa.

وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ {21}

Na hakika ataridhia

Maana

Naapa kwa usiku unapofunika na kwa mchana unapofunuliwa

Kiapo hiki ni kama cha sura iliyopita. Huko tumemebainisha kwamba lengo la kuapa kwa mwanga na giza ni kutanabahisha manufaa yake.

Na kuwa kuumba kiume na kike.

Hii ni kwa kila kiumbe hai; awe mtu, mnyama au mmea. Na kwa kuumba huko ndio kunapatikana kizazi na kuendelea maisha

Hapa kuna maswali yanayojitokeza:

Ni nani aliyefanya kuwe na uhai kwenye ulimwengu huu? Ni nani aliye­andaa uhai kwa wadhifa wa kizazi? Kwa nini anayezaliwa mara anakuwa wa kiume na mara nyingine wa kike, na hali chimbuko lao ni moja tu? Je, mada pofu ndiyo iliyofanya yote haya kwa mpangilio, au ni kwa upande wa sadfu?

Je, ilimu imeweza kugundua kuwa mada moja inakuwa ni sababu ya hali mbali mbali bila ya kuingiliana na vitu vingine? Au tusema ni sadfa? Sadfa nayo ni juhudi ya kushindwa.
Kwa hiyo hakuna jibu lililobaki isipokuwa kuweko mpangiliaji mwenyye ujuzi anayepanga kulingana na hikima ya hali ya juu na nidhamu kamili.

Hakika mahangaiko yenu ni mbali mbali.

Hili ndilo jawabu la kiapo. Maana ni kuwa katika matendo ya mtu kuna ya kheri na ya makosa.

Unaweza kuuliza kuwa kadhia hili ni la kimsingi halihitaji kiapo; kwanini Mwenyezi Mungu (s.w.t) akalisisitiza kwa kiapo?

Jibu: Ndio, nikweli kuwa mahangaiko yenu ni mbali mbali, ni kadhia lililo wazi hilo lenyewe tu, bila ya kuangalia mwisho na natija yake, lakini kama tukiangalia yale yanayofungamana nalo; kama kufanyiwa wepesi mwema na kufanyiwa uzito muovu na mengine mfano wake, hapa itahitajika msisitizo au angalau tuseme hakuna kizuizi cha msisitizo.

Yanayoapiwa hapa ni kuanzia Aya hii tuliyo nayo na zinazofuatia ambazo ni:

Basi Mwenye kutoa katika njia ya heri kwa ajili ya heri na akawa na takua; kwa kujiweka mbali na mambo ya haramu na madhambi. Na akalisadikisha jema yaani akaamini Pepo na Mto, halali na haramu na akafanya kwa mujibu wa imani yake, vinginevyo imani yake itakuwa ni sarabi, kwa sababu imani ni nyezo ya kufikia kwenye lengo na wala sio lengo lenyewe. Basi huyo tutamsahilishia wepesi.

Wametofautiana wafasiri katika maana ya wepesi, kuna anayesema kuwa ni Pepo, mwingine akasema ni heri, na Sheikh Muhammad Abduh akase­ma: “ni mkakati wa kuikamilisha nafsi na kuikuza kwenye ukamilifu.”

Ama sisi tunafasiri wepesi hapa kwa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na anayemcha Mwenyezi Mungu humtengezea njia ya kutokea.” Juz. 28 (65:4) Yaani atampa msaada wake na atampa tawfiki kwenye lile lililo na heri yake na masilahi yake.

Na ama mwenye kufanya ubahili wa kutoa katika njia ya Mwenyezi Mungu, na akatoshelezeka kwa mali yake bila ya kutaka msaada wa Mwenyezi Mungu, akaicha Akhera yake kwa dunia yake, Na akalikad­hibisha jema kwa kusema kuwa hakuna Pepo wala Moto wala halali au haramu, basi tutamsahilishia uzito.

Makusudio ya uzito hapo ni kuingia katika uovu na upotovu. Dalili ya kukusudiwa maana haya ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu inay­ofuatia: ‘Atakapodidimia.’

Makusudio ya kufanyiwa wepesi uzito ni kumwacha na hawa yake wala hakatazwi kwa nguvu yale anayojichagulia mwenyewe ya kudidimia na kuangamia.

Itamfaa nini mali yake atakapodidimia?

Pia inawezekana kufasiriwa: Haitafaa mali yake atakapodidimia.

Makusudio ya kudidimia ni kuanguka kwenye shimo la uchafu na maovu.

Muhtasari wa Aya hizi kuanzia: Ama mwenye kutoa, mpaka, atakapo­didimia, ni kwamba desturi ya Mwenyezi Mungu kwa viumbe wake ni kubainishia njia mbili, ya wema na ya ufisadi, na kuwapa uwezo wa kufu­ata njia yoyote katika hizo mbili au kuacha yoyote, kisha anamchukulia kila mmoja kwa lile alilojichagulia yeye mwenyewe.

Akiathrika na heri na wema, basi humwingiza kwenye tawfiki yake na msaada wake, na akijich­agulia shari na ufisadi hukaa mbali naye na kumwachia nafsi yake na hawa yake imwongoze kwenye shida na maangamizi.

Hakika ni juu yetu kuongoza.

Hili ni jawabu la swali la kukadiria ambalo vipi Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamwachia muovu na kumwakilishia nafsi yake na hawa yake? Je, hii haipingani na upole wake na rehema yake?

Ndio akajibu Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwamba lililo wajibu kwake ni kumpa mja uwezo wa kutenda na akili ya kupambanua kheri na shari, kisha anambainishia, kumwongoza, kumbashiria na kumuonya. Haya yote yamekamilika kwa ukamilifu, nayo ni ukomo wa upole na huruma.

Ama kufanya amali na kuongoka ni juu ya mja mwenyewe peke yake; wala Mwenyezi Mungu hamlazimishi, kwani kulazimisha kunampokonya mtu uhuru na utashi wake, bali hata na utu wake. Kwa sababu mtu ni kwa uhuru wake na matakwa yake.

Neno juu yetu hapo linajulisha wajibu, kinyume na Sheikh Muhammad Abduh na wengineo katika Ashaira. Kwa sababu wajibu ukinasibishwa kwa mtu, maana yake ni kuwa kuna mwingine aliyemwajibishia na kama akiacha kutekeleza ataulizwa. Na ukinasibishwa kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, maana yake ni kuwa yeye mwenyewe amejiwajibishia; yaani kwamba yeye ameahidi na ahadi yake haivunji; Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema Juz:

كَتَبَ عَلَىٰ نَفْسِهِ الرَّحْمَةَ ۚ {12}

“Amejilazimishia rehema” 7 (6:12).

Hakika ni wetu mwisho na mwanzo.

Mwenyezi Mungu peke yake ndiye mfalme wa wafalme, duniani na Akhera wala hana manufaa yoyote kwa twaa ya mtiifu au uasi wa muasi; wala waasi hawatapata pa kuponyokea utawala wake.

Basi ninawaonya na moto unaowaka.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameamrisha akakataza na akahadharisha mwenye kuasi na moto unaowaka ili atubie na kurejea kwa Mola wake.

Hatauingia isipokuwa muovu mno, ambaye amekadhibisha na kupa mgongo.

Imesemekana kuwa muovu mno hapa ni kafiri, Sheikh Muhammad Abduh anasema:” Muovu mno ni yule aliye muovu zaidi ya mwengine.” Usahihi ni kuwa uovu zaidi sio makusudio kwa upande wa kuingia motoni, kwa sababu hakuna muovu yeyote ila atauonja:

فَأَمَّا الَّذِينَ شَقُوا فَفِي النَّارِ لَهُمْ فِيهَا زَفِيرٌ وَشَهِيقٌ {106}

“Ama wale waovu watakuwa motoni watachachatika na kukoroma.” Juz. 12 (11:106).

Tofauti ya muovu na muovu mno iko katika uchungu wa adhabu na shida yake si katika asili ya adhabu. Kwa hiyo itakuwa makusudio ya muovu mno hapa ni yule aliyemuasi Mwenyezi mungu na akaipinga amri yake; ni sawa awe ameipinga kwa vile hamwamini Mwenyezi Mungu na sharia yake, au anamwamini, lakini akazembea na kupuuza.

Hakuna tofauti baina ya wawili hawa, kwa sababu imani ni nyenzo na wala si lengo. Imethibiti kwa nukuu ya Qur’an kwamba mwenye kuamini bila ya maten­do yuko sawa na kafiri. Mwenye Mungu Mtukufu anasema:

 لَا يَنْفَعُ نَفْسًا إِيمَانُهَا لَمْ تَكُنْ آمَنَتْ مِنْ قَبْلُ أَوْ كَسَبَتْ فِي إِيمَانِهَا خَيْرًا ۗ {158} 

“Basi mtu haitamfaa imani yake ambaye hakuamini zamani, au hakuchu­ma kheri kwa
imani yake.” Juz. 8 (6:158).

Na ataepushwa nao mwenye takua.

Maana ya kuepushwa nao ni kujitanibu na sababu zinazopelekea huko; ambazo ni maharimisho ya Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo makusudio hapa ni mwenye mwenye takua.

Ambaye anatoa mali yake kwa kujitakasa.

Yaani anatoa mali yake katika njia ya kheri ili kuitwaharisha nafsi yake na madhambi na kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu; wala hatoi kwa umashuhuri na kujitukuza au kwa biashara na ria.

Wala hapana yeyote aliyemfanyia hisani ili alipwe.

Mara nyingine hisani inakuwa kwa msukumo wa umashuhuri na kujionye­sha, au kwa kulipa hisani uliyofanyiwa; kama kumpa aliyekufanyia wema kwa kumlipa wema wake. Pia inaweza kuwa kutoa ni kwa njia ya nipe nikupe; kama wafanyavyo wanasiasa kwenye miradi ya heri na mingineyo, siku za uchaguzi ili apate kura. Mumin hakusudii hayo wala mengine isipokuwa ni kwa kutaka radhi ya Mola wake aliye juu kabisa, kwa kutaka thawabu zake na kuhofia adhabu yake:

إِنَّمَا نُطْعِمُكُمْ لِوَجْهِ اللَّهِ لَا نُرِيدُ مِنْكُمْ جَزَاءً وَلَا شُكُورًا {9}

“Hakika tunawalisha kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu tu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.” Juz. 29 (76:9).

Na hakika ataridhia.

Mwenyezi Mungu atampa mwenye kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kila analoliridhia na zaidi ya alivyokuwa alifikiria na kutarajia.

Imesemekana kuwa atakayeridhia ni Mwenyezi Mungu sio mwenye takua. Maana ni moja katika makadirio yote mawili, kwa sababu Mwenyezi Mungu akimridhia mja wake na mja naye huwa radhi.

Sheikh Muhammad Abduh anasema kuwa wafasiri wamepokea sababu za kushuka Aya na kwamba Aya hizi zilishuka kwa ajili ya Abu Bakr. Ukipatikana usahihi wa hilo hakuna cha kutuzuia kulisadiki hilo, lakini maana ya Aya bado ni ya ujumla.

  • 1553 views

Sura Ya Tisini Na Tatu: Ad-Dhuha

Imeshuka Makka Ina Aya 11.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَالضُّحَىٰ {1}

Naapa kwa Dhuha!

وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ {2}

Na kwa usiku unapotua!

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ {3}

Hakukuacha Mola wako wala hakukukasirikia!

وَلَلْآخِرَةُ خَيْرٌ لَكَ مِنَ الْأُولَىٰ {4}

Na hakika mwisho ni bora kwako kuliko mwanzo.

وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰ {5}

Na Mola wako atakupa utarid­hia.

أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًا فَآوَىٰ {6}

Je, hakukukuta ni yatima akakuhifadhi?

وَوَجَدَكَ ضَالًّا فَهَدَىٰ {7}

Na akakukuta umepotea akakuongoa?

وَوَجَدَكَ عَائِلًا فَأَغْنَىٰ {8}

Akakukuta mhitaji akaku­tosheleza?

فَأَمَّا الْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ {9}

Ama yatima usimwonee!

وَأَمَّا السَّائِلَ فَلَا تَنْهَرْ {10}

Na ama mwenye kukuomba usimkaripie!

وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ {11}

Na ama neema ya Mola wako izungumze.

Maana

Naapa kwa Dhuha

Makusudio ya dhuha hapa ni mchana wote, kwa dalili ya mkabala wake na usiku. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameuletea mchana ibara ya dhuha kwa sababu dhuha ni chimbuko la mchana, kwa mujibu wa maelezo ya Razi. Au ni ujana wa mchana kwa maelezo ya Sheikh Muhammad Abduh.

Na kwa usiku unapotua.

Makusudio ya kutua usiku ni kutulia watu wake na kuacha harakati. Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameapa na mawili haya kwa sababu ni katika ishara zake kubwa.

Mafakihi wengi wamesema kuwa Nabii (s.a.w) aliswali swala ya dhuha siku ya ushindi wa Makka, nayo ni rakaa mbili kwa baadhi, na wengine wanasema ni zaidi, na ikafanywa Sunna kwa wote.

Shia Imamiya wamesema hakuna kiwango kwa Swala ya Sunna ni Qurbani ya kila mwenye takua, anayetaka ataifanya chache na anayetaka ataifanya nyingi. Kila mtu anaweza kuswali rakaa za kuanzia kila wakati na kila mahali, kwa nia ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu.

Hakukuacha Mola wako wala hakukukasirikia.
Hili ni jawabu la kiapo. Wafasiri na wapokezi wameafikiana kwamba wahyi ulisimama kumfikia Mtume kwa siku kadhaa. Washirikina wakase­ma: Mungu wa Muhamadi amemchukia na Jibril amemkasirikia, ndio akateremsha Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hakukuacha Mola wako wala hakukukasirikia.

Maneno ni yale aliyosema: Sheikh Muhammad Abduh: “Kwenye mfumo wa Sura hakuna kinachoashiria hilo. Washirikina walijua wapi vipindi vya wahyi? Isipokuwa Mtume alitamani wahyi baada ya kuonja Utamu wake na kila mwenye kuonja huwa na hamu na shauku na shauku huleta hofu? Kuna Hadithi katika sahih inayosema kuwa Nabii (s.a.w.w) alihuzunikia sana kwa wahyi kuchukua muda.”

Kwa mnasaba huu ninasema kuwa mimi nimesoma kila chapisho la Sheikh Muhammad Abduh nikagundua kuwa heshima ya mtu huyu na umashuhuri wake, hautokani na ilimu yake tu, wala kwa upeo wa uchun­guzi wake; kwani badhi ya wanafunzi wake, kwa ninavyoona mimi, wana upeo na kujua kauli za waliopita na wapya zaidi yake.

Siri pekee ya heshi­ma ya Sheikh huyu iko katika kuitegemea kwake haki, kuifanyia ikhilasi na ujasiri wake wa kuisema wazi wazi; hata kama inapingana na waliopita na wanaokuja. Kwa njia hii ndio maana vilemba viovu vimemkufurisha, lakini historia imemsafisha na kumweka mbele na kuutupa kapuni ule uovu.

Na hakika mwisho ni bora kwako kuliko mwanzo. Na Mola wako atakupa utaridhia.

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume Mtukufu (s.a.w.). Makusudio ya mwisho hapa ni maisha ya Akhera na mwanzo ni maisha ya dunia kuanzia kushukiwa na wahyi mpaka Siku ya Kiyama. Kwa sababu hakuna Siku yoyote inayopita ila wanazaliwa mamia ya waislamu, kuongezea umma na mataifa yatakayoingia katika dini ya Mwenyezi Mungu. Yote hayo yamepatikana kwa Muhammad na risala ya Muhammad (s.a.w.).

Maana ya Aya ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) atakuzidishia fadhila zake ewe Muhammad siku baada ya siku mpaka Siku ya Kiyama. Fauka ya hayo wewe utakuwa na ukuu na utukufu huko Akhera. Je, yanakutosha haya au unataka mengine?

Kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anamtajia Nabii wake mtukufu neema ali­zomneemesha tangu siku yake ya kwanza na kuendelea bila ya kikomo; zifuatazo ni neema kabla ya utume:­

1. Je, hakukukuta ni yatima akakuhifadhi?

Swali hili ni la kuripoti uhalisia; yaani ulikuwa hivyo. Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Nabii (s.a.w.) alikuwa yatima kwa sababu baba yake alikufa Madina akiwa bado yuko tumboni mwa mama yake, akalelewa na babu yake, Abdul-Mutwalib, kwa malezi bora. Kisha babu yake naye aka­fariki akiwa na umri wa miaka minane.

Akalelewa na ami yake, Abu Twalib, kwa wasia wa Abdul-Mutwalib. Alikuwa akimlinda na akimpenda sana hadi ukubwani mwake. Aliendelea kumhami na kumsaidia, baada ya utume, hadi kufariki kwake, ndio Makuraishi wakasubutu kumghasi, baada ya mauti ya ami yake, mpaka akalazimika kuhamia Madina.

Hiyo ndiyo hifadhi ya Mwenyezi Mungu kwa Nabii wake akiwa ni yatima.

2. Na akakukuta umepotea akakuongoa.

Wafasiri wametofautiana kuhusu makusudio ya kupotea hapa. Razi ameishiliza kauli zao ishirini.

Iliyo karibu zaidi na uhalisia ni ile isemayo kuwa Nabii (s.a.w.) alikuwa amedangana kuhusu watu wake, hajui afanye nini kuhusiana na kupotea kwao katika itikadi zao. Pia ufisadi wa matendo yao, ujinga wao na utengano wao.
Akawa hajui atumie njia gani ya kuwaongoza mpaka akashukiwa na wahyi ambao ndani yake mna ubainifu wa kila kitu, mwongozo na rehema. Kwa hiyo upotevu wa Mtume (s.a.w.) ni kudangana kwake jinsi atakavy­owaongoza makafiri, lakini Qur’an ikamwongoza.

3. Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

Wapokezi wanasema kuwa Mtume (s.a.w.) hakurithi kutoka kwa baba yake isipokuwa ngamia mmoja na mjakazi, lakini Mwenyezi Mungu alimfanya asiwe mhitaji kwa kutunzwa na ami yake, Abu Twalib, mali ya Khadija na ngawira.

Ama yatima usimwonee na ama mwenye kukuomba usimkaripie.

Ambaye amekuwa yatima anakuwa mtunzaji mzuri wa mafukara na may­atima na kuwashughulikia sana. Hakuna mwenye shaka kwamba hii ni kumfunza kila mwenye kujaribu kuwaonea mayatima au kuwakaripa mafukara; ni kuwa tayari Mtume wa rehema ana hulka adhimu na mwenye kuwahurumia wanyonge.

Na ama neema ya Mola wako izungumze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu na kumsifu. Kuna Hadith tukufu isemayo: “Kuzizungumza neema za Mwenyezi Mungu ni kumshukuru. Imam As-Sadiq (a.s.) anasema kati­ka maana ya Aya hii: “Simulia aliyokupa Mwenyezi Mungu, akakufadhili, akakuruzuku, akakufanyia hisani na akaukuongoza.

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Maana ya zungumza ni ongeza kuwapa mafukara.” Mwanafunzi wake Al-Maraghi naye akamfuata katika tafsiri hii, lakini iko mbali na dhairi ya tamko na ufahamisho wake. Linalokuja haraka kwenye ufahamu kutokana na neno zungumza ni kuz­izungumza neema za Mwenyezi Mungu kwa kumshukuru na kumsifu.

  • 3757 views

Sura Ya Tisini Na Nne: Al-Inshirah

Imeshuka Makka Ina Aya 8.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

أَلَمْ نَشْرَحْ لَكَ صَدْرَكَ {1}

Je, hatukukukunjulia kifua chako?

وَوَضَعْنَا عَنْكَ وِزْرَكَ {2}

Na tukakuondolea mzigo wako.

الَّذِي أَنْقَضَ ظَهْرَكَ {3}

Ambao uliuelemeza mgongo wako?

وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ {4}

Na tukakunyanyulia utajo wako?

فَإِنَّ مَعَ الْعُسْرِ يُسْرًا {5}

Basi kwa hakika pamoja na uzito kuna wepesi.

إِنَّ مَعَ الْعُسْرِ يُسْرًا {6}

Hakika pamoja na uzito kuna wepesi.

فَإِذَا فَرَغْتَ فَانْصَبْ {7}

Basi ukishamaliza jitaabishe.

وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَارْغَبْ {8}

Na Mola wako mtake haja.

Maana

Razi anasema: “Imepokewa kutoka kwa Twaus na Umar Bin Abdul-aziz, kwamba Sura hii na Sura Adhuha ni moja na walikuwa wakiisoma katika rakaa moja bila ya kuitenganisha na Bismillah.

Lililowafanya hivyo ni kauli yake Mwenyezi Mungu tukufu: Je, hatukukukunjulia kifua chako? Ni kama inaungana na kauli yake: Je, hakukukuta ni yatima akakuhifadhi?

Mwenye ajamul-bayan anasema: “Wamepokea watu wetu ‧ yaani Shia Imamiya ‧ kuwa hizo ni sura moja kutokana na kufungamana na wamezi­soma pamoja katika rakaa moja, vile vile Sura Fiyl na Quraysh.

Sheikh Almaraghi anasema: “Sura hii ilishuka baada ya Dhuha na ime­fungamana sana nayo.” Mwenye Dhilal anasema: Sura hii imeshuka baada ya Sura Adhuha, kama kwamba inaikamilisha.

Je, hatukukukunjulia kifua chako?

Mtume aliona dhiki sana kutokana na ufisadi wa jamii aliyokuwa akiishi nayo. Akawa hajui afanye nini, huku akitafuta njia ya kuwatengeneza watu wake na kuwaongoza, mpaka aliposhukiwa na Qur’an ikamwangazia njia anayoitaka ‧ kuleta utangamano na wema. Ndipo moyo wake ukatulia na kifua chake kikakunjuka.

Na tukakuondolea mzigo wako, ambao uliuelemeza mgongo wako?

Makusudio ya mzigo unaolemea hapa ni hamu na ghamu yake Mtume kwa ushirikina na upotevu waliokuwa nao watu wake, ndio Mwenyezi Mungu akampa raha Mtume wake kwa Qur’an Tukufu.

Kwa hiyo basi, makusudio ya kukuondolewa mzigo ni sawa na kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘Je, hatukukukunjulia kifua chako.’ Hakuna tofauti isipokuwa katika mfumo wa maneno na ibara. Lengo ni kuzidisha ufafanuzi na kusisitiza.

Na tukakunyanyulia utajo wako?

Kuna kitu gani cha juu na kitukufu zaidi kuliko kukutanishwa jina la Muhammad na jina la Mwenyezi Mungu na kutiiwa yeye kuwa ndio kuti­iwa Mwenyezi Mungu? Juz. 5 (4:80) na Juz, 22 (33:36).

Basi kwa hakika pamoja na uzito kuna wepesi. Hakika pamoja na uzito kuna wepesi.

Maana yako wazi, ni kuwa baada ya dhiki ni faraji, kwa haraka au kwa kuchelewa. Kwa sababu makusudio ya pamoja hapa ni kusisitiza matu­maini ya kupata wepesi hata kama muda utarefuka, na wala sio kusuhu­biana na kwenda pamoja.

Unaweza kuuliza: Nini makusudio ya kukaririka huku?
Jibu: Hatuoni wajihi wowote zaidi ya kusisitiza kadhia hili katika nafsi na kulimakinisha katika nyoyo, kwani watu wengi wanakuwa na shaka nalo. Ama riwaya inayosema: Uzito mmoja hautashinda wepesi mbili, tume­ichunguza na tukafahamu kuwa wepesi wa kwanza ni kuondokewa na uzito, lakini hatukufahamu wepesi wa pili. Imesemekana kuwa ni thawabu za Akhera, lakini hii ni mbali ya umbali zaidi wa dhahiri ya tamko na mfumo wa Aya, kwa sababu inazungumzia uzito wa dunia na wepesi wake, si Akhera na thawabu zake.

Vile vile imesemekana kuwa uzito wa pili ndio ule ule uzito wa kwanza, kwa sababu zote mbili zina heruf alif na lam ya jinsi, lakini wepesi umerudiwa bila, ya alifu na lam (nakira), na likirudiwa hivyo neno basi makusudio ya kwanza yanakuwa sio ya pili.

Kauli hii kwa hakika, haina mategemzi ya hoja yoyote isipokuwa ni kucheza na matamshi tu, kwa sababu, kwa mfano ukimwambia unayem­dai: ninakudai shilingi mbili naye akasema: unanidai shilingi moja, unanidai shilingi moja, haina maana kuwa amekubali kuwa unamdai shilingi mbili.

Sheikh Muhammad Abduh amejaribu kutofautisha baina ya uzito, sio wepesi, akasema: Makusudio ya uzito wa kwanza ni ule uzito uliozoeleka. Ama uzito wa pili ni wa kiujumla. Sheikh Muhammad Abduh amerefusha na kubainisha ili kuipa nguvu rai yake, lakini hakuleta kitu cha kutuliza nafsi, kwani linalokuja haraka akilini ni kuwa uzito uliotajwa kwanza ndio ule ule uliotajwa mara ya pili, wala hakuna tofauti baina yake.

Swali la pili: Tumeona watu wengi wanaendelea kuwa na uzito hadi mauti; na hili haliafikiani na mtazamo wa Aya hii; sasa je, kuna wajihi gani?

Jibu: Hukumu katika Aya ni ya kiujumla na uaghlabu, sio kuenea na kuchanganya wote. Zaidi ya hayo ni kuwa inaleta matumaini katika nafsi na kuipa msukumo wa kufanya kwa ikhlasi - jambo ambalo linasaidia kushikamana na Mwenyezi Mungu na kumtegemea Yeye tu.

Basi ukishamaliza jitaabishe.

Yaani ewe Muhammad, ukishamaliza kazi ya kutafuta maisha, jitaabishe na ufanye juhudi kwa ajili ya maisha ya Akhera.

Kuna baadhi ya mamluki walioajiriwa kwa ajili ya kueneza fitna katika madhehebu za kiislamu, wamewazulia Shia Imamiya kuwa eti wanafasiri neno fanswab, tulilolifasiri kwa maana ya jitaabashe, kwa maana ya msi­mamishe Ali kuwa khalifa.

Inatosha kuurudi uzushi huu, yale aliyoyasema mwenye ajmaul-bayan, ambaye ni miongoni mwa masheikh wafasiri katika Shia Imamiya, amese­ma katika kufasiri Aya hii, ninamnuku: “Maana ya neno fanswab ni jitaabishe; usijishughulishe na raha.”

Na Mola wako mtake haja.

Usiuelekeze moyo wako kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, wala usimtake msaada yoyote asiyekuwa Yeye. Mtume (s.a.w.) anasema: “Ukiomba muombe Mwenyezi Mungu, ukitaka msaada mtake msaada Mwenyezi Mungu. Jua kwamba lau watu na majini wataungana kukunufaisha na cho­chote, hawawezi kukunufaisha na chochote ila kile alichokuandikia Mwenyezi Mungu na kama wataungana kukudhuru, basi hawawezi kukud­huru ila kwa kile alichokuandikia Mwenyezi Mungu.”

  • 3608 views

Sura Ya Tisini Na Tano: At-Tin

Imeshuka Makka Ina Aya 8.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَالتِّينِ وَالزَّيْتُونِ {1}

Naapa kwa tini na zaituni!

وَطُورِ سِينِينَ {2}

Na kwa mlima Sinai!

وَهَٰذَا الْبَلَدِ الْأَمِينِ {3}

Na kwa mji huu wenye amani!

لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنْسَانَ فِي أَحْسَنِ تَقْوِيمٍ {4}

Hakika tumemuumba mtu katika hali nzuri mno.

ثُمَّ رَدَدْنَاهُ أَسْفَلَ سَافِلِينَ {5}

Kisha tukamrudisha chini ya walio chini!

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ فَلَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ {6}

Isipokuwa wale walioamini na wakatenda mema, wana ujira usiokwisha.

فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعْدُ بِالدِّينِ {7}

Basi ni kipi baadaye kitaka­chofanya ukadhibishe dini?

أَلَيْسَ اللَّهُ بِأَحْكَمِ الْحَاكِمِينَ {8}

Kwani Mwenyezi Mungu si hakimu bora wa mahakimu wote?

Maana

Naapa kwa tini na zaituni.

Wametofautiana kuhusu makusudio ya tini na zaituni, kwenye kauli nyin­gi. Iliyo mbali zaidi na dhahiri ya tamko na ufahamisho wake, ni ile aliy­oisema Sheikh Muhammad Abduh:

“Tini ni ishara ya Adam na Hawa wakiwa Peponi, ulipofunuka uchi wao walianza kujibandika majani ya mtini na mzaituni kuashiria zama za Nuh na kizazi chake.”

Hatuoni sababu ya kuleta taawili hii, kwa sababu yanayokuja kwenye ufa­hamu ni kuwa tini ni ile ya kawaida tu na zaituni ni ile ile inayokamuliwa mafuta; wala hakuna kizuizi cha kuapa Mwenyezi Mungu kwa chochote anachotaka katika viumbe vyake, na hii ni kwa kukiri kwake yeye mwenyewe Sheikh Muhammad Abduh, na mara nyingi amekuwa akitege­mea yanayokuja haraka akilini katika Aya za Qur’an yenye hikima.

Ama hikima ya kuapia nazo inawezekana kuwa ni kutanabahisha faida ilizo nazo na inawezekana kuwa ni mengineyo. Ni mengi ambayo hatuya­jui.

Na kwa mlima Sinai.
Mlima hapa ni ule ambao Mwenyezi Mungu alizungumza na Musa.

Na kwa mji huu wenye amani, ambao ni Makka iliyo na heshima kwa kuzaliwa Muhammad (s.a.w.) na kuweko nyumba takatifu; mfano wake ni kama “Naapa kwa mji huu.” (90:1).

Hakika tumemuumba mtu katika hali nzuri mno.

Hili ni jawabu la kiapo na ndilo lililokusudiwa katika sura yote. Hali nzuri ni mpangilio na nidhamu. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameapa kwa upole wake na ulinzi wake wakati alipomfanya aweko; akaumba mwili wake katika sura ya ajabu na shepu nzuri; na roho yake akaipa nguvu na utashi ambao anaweza kuwapita viumbe wote akitaka; au kuanguka chini kabisa akipotoka na hawa na matamanio yake.

Ikiwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemshughulikia mtu, kwa umuhimu huu na akamuandaa kwenda juu na ukamilifu, basi mtu mwenyewe, ndio anatakikana ajishughulikie yeye mwenyewe wala asipotoke akaacha lile aliloumbiwa nalo, la ukamilifu na uzuri. Mfano wa Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 وَصَوَّرَكُمْ فَأَحْسَنَ صُوَرَكُمْ {64}

“Na akawatia sura, na akazifanya nzuri sura zenu.”Juz. 24 (40:64).

Kisha tukamrudisha chini ya walio chini; yaani huyo mtu kwa kuzinga­tia baadhi sio kila mtu. Makusudio ya chini ya walio chini hapa, ni Jahannam. Lau si mfumo wa maneno tungelisema makusudio ni uzee na ukongwe, lakini kauli yake Mwenyezi Mungu ‘isipokuwa wale walioami­ni na wakatenda mema,’ ni wazi kuwa makusudio ni Jahannam. Maana ni kuwa tumemuumba mtu katika uzuri wa umbo, kimwili na kiro­ho, lakini baadhi au wengi wao wanamuasi Mwenyezi Mungu na kuziku­furu neema zake, ndio akawarudisha kidato cha chini katika Moto.

Isipokuwa wale walioamini na wakatenda mema, wana ujira usiok­wisha; yaani walioamini wakatenda kwa mujibu wa imani yao kwa ikhlasi, wataneemeka Peponi na kudumu humo milele. Kwa Mwenyezi Mungu kuna malipo makubwa.

Umetangulia mfano wake kwa herufi zake katika Juz. 24 (41:8).

Basi ni kipi baadaye kitakachokufanya ukadhibishe dini?

Tamko ni la kuuliza, lakini maana yake ni kukanusha; yaani hakuna kitaka­chokufanya ukadhibishe dini ya Mwenyezi Mungu baada ya kusimama hoja na dalili juu yake, zikiwa ni kuumbwa mtu katika umbo zuri.

Kwani Mwenyezi Mungu si hakimu bora wa mahakimu wote?

Kwanini isiwe hivyo? Yeye ni mpangiliaji bora zaidi ya wote na mwadlifu zaidi kwa kauli na vitendo; naye atamhukumu kwa haki yule atakayemkad­hibisha kwa kiburi na inadi.

  • 2976 views

Sura Ya Tisini Na Sita: Al-A’laq

Imeshuka Makka Ina Aya 19.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

اقْرَأْ بِاسْمِ رَبِّكَ الَّذِي خَلَقَ {1}

Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba.

خَلَقَ الْإِنْسَانَ مِنْ عَلَقٍ {2}

Amemuumba mtu kwa pande la damu.

اقْرَأْ وَرَبُّكَ الْأَكْرَمُ {3}

Soma! Na Mola wako ni Karimu zaidi!

الَّذِي عَلَّمَ بِالْقَلَمِ {4}

Ambaye amefundisha kwa kalamu.

عَلَّمَ الْإِنْسَانَ مَا لَمْ يَعْلَمْ {5}

Amemfundisha mtu aliyokuwa hayajui

كَلَّا إِنَّ الْإِنْسَانَ لَيَطْغَىٰ {6}

Si hivyo! Hakika mtu bila ya shaka hupituka mipaka.

أَنْ رَآهُ اسْتَغْنَىٰ {7}

Kwa kujiona amejitosheleza.

إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ الرُّجْعَىٰ {8}

Hakika ni kwa Mola wako marejeo.

أَرَأَيْتَ الَّذِي يَنْهَىٰ {9}

Je, umemwona yule anayemkataza.

عَبْدًا إِذَا صَلَّىٰ {10}

Mja anaposwali?

أَرَأَيْتَ إِنْ كَانَ عَلَى الْهُدَىٰ {11}

Je, umeona kama yuko juu ya uwongofu?

أَوْ أَمَرَ بِالتَّقْوَىٰ {12}

Au anaamrisha takua?

أَرَأَيْتَ إِنْ كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ {13}

Je, umeona kama yeye akikanusha na kurudi nyuma?

أَلَمْ يَعْلَمْ بِأَنَّ اللَّهَ يَرَىٰ {14}

Hajui kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

كَلَّا لَئِنْ لَمْ يَنْتَهِ لَنَسْفَعًا بِالنَّاصِيَةِ {15}

Si hivyo! Kama hatakoma, tutamburuza kwa nywele za utosi!

نَاصِيَةٍ كَاذِبَةٍ خَاطِئَةٍ {16}

Utosi wa uwongo, wenye makosa!

فَلْيَدْعُ نَادِيَهُ {17}

Basi na awaite wanachama wenzake!

سَنَدْعُ الزَّبَانِيَةَ {18}

Nasi tutawaita Mazabania!

كَلَّا لَا تُطِعْهُ وَاسْجُدْ وَاقْتَرِبْ ۩ {19}

Si hivyo! Usimtii! Nawe suju­du na ujikurubishe.

Maana

Imesemekana kuwa Sura ya mwanzo kumshukia Mtume ni sura A-lfatiha. Kauli hii inanasibiana na na jina la Sura yenyewe (ufunguzi), lakini kauli hii ni nadra. Ikasemekana kuwa ya kwanza kushuka ni Muddathir. Waliosema hivi ni wachache. Wafasiri wengi, wapokezi na ulama wame­sema ya kwanza iliyoshuka ni mwanzo wa Sura hii tuliyo nayo.

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Imesihi katika Hadith kwamba mwanzo wa malaika aliyekuwa akimpa wahyi ni pale alipomwambia: Soma kwa jina la Mola wako, mpaka kufikia, amemfundisha mtu asiyoya­jua.”

Vyovyote iwavyo lilio wajibu kwa mwislamu ni kuamini pasi na kuwa na shaka kwamba yote yaliyo katika Qur’an ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu, wala halazimiki kufanya utafiti wa wakati na tarehe ya kushuka Aya. Ambalo halina shaka ni kuwa wahyi ulimshukia Mtume mtukufu (s.a.w.), akiwa na miaka arubaini katika umri wake mtukufu; na kwamba kabla

yake alikuwa akiamini Mungu mmoja bila ya kumshirikisha na chochote, na hakuwa akitetereka hata kidogo katika kumtegemea kwake. Chimbuko la imani hii ni mambo mawili: Kwanza ni dhati ambayo ni akili yake na umbile lake. Pili urithi wa kutoka kwa babu yake Ibrahim Al-Khalil (a.s.).

Mwenye kufuatilia maisha ya Nabii (s.a.w.) na sera yake, atapata ushahi­di mwingi wa kumwamini Mungu mmoja; miongoni mwayo ni kwamba yeye katu hakuwahi kusujudia sanamu udogoni mwake na ukubwani.

Wapokezi wamenukuu kwamba mmoja wa washirikina siku moja, kabla ya kufikia umri wa utu uzima alimwambia: “Ewe kijana ninakuomba kwa Lata na Uzza uniambie jambo fulani.” Muhammad (s.a.w.) akamwambia: “Usiniombe kwa lata na Uzza: Wallah hakuna kitu ninachokichukia kama hivyo viwili.” Na siku nyingine alitofautiana na mshirikina katika jambo fulani, kabla ya utume. Yule mshirikina akamwambia: “Apa kwa Lata na Uzza,” akasema: “Siapi kwa hao katu na mimi nawapinga.”
Vile vile kauli ya mkewe, Bibi Khadija wakati alipomwelezea yaliompata wakati wa kushukiwa na wahyi: Wallah Mwenyezi Mungu hatakuhizi milele, wewe utaunga udugu, utachukua taabu, utawakaribisha wageni na utasaidia upande wa haki’’. Katika ibara hii ya kihistoria. Wallah Mwenyezi Mungu hatakuhizi, inatuonyesha njia isiyo na mjadala wa fikra ya Mungu mmoja ndani ya familia ya Muhammad kabla ya utume. Tumeyanukuu haya kutoka kitabu Adhahiratul ur’aniyya cha Malik bin Nabiy.

Wakati wowote ule, hata wakati wa wajinga, wamepatikana watu waliomwamini Mungu mmoja kwa msukumo wa akili zao na maumbile yao; miongoni mwao ni Waraqa bin Nawfal, Zaid bin Amr, Uthman bin Al-Huwayrith na wengineo. Tazama Juz. 15 (17: 105-111) kifungu cha ‘Wanyoofu.’ Sasa je, itakuwa ni ajabu kwa bwana wa duniani na Akhera na mtukufu wa viumbe kuanzia wa kwanza hadi wa mwisho, kuongoka kwa akili yake kwenye Mungu mmoja Mwenye nguvu?

Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba.

Hii ni Aya ya kwanza kushuka katika Qur’an, kama tulivyoashiria. Hilo linatiwa nguvu na amri ya kuanza kwa jina lake Mwenyezi Mungu Mtukufu. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amesema aliyeumba, bila ya kutaja alichoumba, kwa ajili ya kuenea, kwamba Yeye ni muumba wa vyote. Maulama wa Kiarabu wanasema: Kutotajwa kinachofanywa kunafa­hamisha kuenea kote.

Unaweza kuuliza: Nabii (s.a.w.) alikuwa hasomi wala haandiki, na Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anajua hilo, sasa ilikuwaje kumpa amri ya kuso­ma? Hii sio kukalifisha asiloliweza?

Sheikh Muhammad Abduh amejibu swali hili kwa kusema: “Soma kwa jina la Mola wako ni amri ya kimaumbile ya kukiambia kitu ‘kuwa’ na kikawa na wala sio amri ya taklifa; mfano swali na utoe zaka. Tazama Juz. 1 (2:26-27) kifungu cha ‘Kuumba na kuweka sharia.’ Kwa hiyo maana ni: kuwa msomaji hivi sasa, hata kama hapo mwanzo hukua hivyo, kwani Mwenyezi Mungu ambaye ameumba mbingu na ardhi anaweza kukufanya wewe Muhammad kuwa msomaji bila ya kujifundisha kusoma.

Amemuumba mtu kwa pande la damu,

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kutaja kuwa Yeye ni muumba wa kila kitu, hapa amemhusisha mtu, kwa kumtukuza:

وَلَقَدْ كَرَّمْنَا بَنِي آدَمَ {70}

“Hakika tumewatukuza wanaadamu.” Juz. 15 (17:70).

Vile vile kutanabahisha uweza wake mkuu ambao umefanya pande la damu liwe mtu huyu wa ajabu jinsi alivyopangiliwa, ili atoe dalili kwa hilo kuweko muumba mwenye uweza:

أَوَلَا يَذْكُرُ الْإِنْسَانُ أَنَّا خَلَقْنَاهُ مِنْ قَبْلُ وَلَمْ يَكُ شَيْئًا {67}

“Je hakumbuki mtu kwamba tulimuumba kabla na hali hakuwa chochote?” Juz. 16 (19:67)

Soma! Na Mola wako ni Karimu zaidi! Ambaye amefundisha kwa kalamu.

Soma, ni kusisitiza amri ya kwanza. Na Mola wako ni karimu… hii ni jumla nyingine; maana yake ni Mwenyezi Mungu ni mkarimu wala haku­na kiwango cha ukarimu wake; kama ulivyo uweza wake na ilimu yake. Hakuna kitu kinachofahamisha zaidi ukarimu na fadhila yake kuliko kuwa yeye amemtoa mtu kutoka chini-pande la damu-hadi juu, kuandika kwa kalamu ambayo ina faida zisizokuwa na idadi; kama vile kuunganisha yaliyopita na yatakayokuja na kuanganisha mashariki ya ardhi na magharibi yake; hasa baada ya kugunduliwa mtambo wa kuchapisha ambao umefanya ilimu ienee hata kwa vipofu wanaosoma kwa herufi zao. Ulimi unatoa yaliyo moyoni, lakini maneno yanakwenda na upepo. Ndio maana ikasemwa kalamu ni naibu wa ulimi na ulimi ni naibu wa kalamu.

Amemfundisha mtu aliyokuwa hayajui.
Mwenyezi Mungu haitii ilimu moyoni isipokuwa anampa mtu akili ambayo ni chimbuko la ilimu. Akili haina mpaka, si kupanda mwezini wala Mars. Vile vile ilimu, huwa inazidi siku baada ya siku bila ya kikomo.

Wafasiri wameafikiana mpaka kufikia hapa kuanzia Aya ya kwanza ndizo Aya za kwanza kushuka na zilishuka mara moja zote. Ama zilizobakia zil­ishuka baadae

Mali Na Kupituka Mipaka

Si hivyo! Hakika mtu bila ya shaka hupituka mipaka, kwa kujiona amejitosheleza.

Mtu hapa ni kwa kuzingatia aghalabu ya watu. Watu wengi wanatoa ushahidi kwa Aya hii kwamba mtu anajikuza na kudhulumu anapomiliki mali na utajiri. Fikra hii wamekwenda nayo jamhuri ya wafasiri. Anasema Arrazi: “Ni Sura ya kwanza inayosifu ilimu na ya mwisho kuishutumu mali.”

Mwenye ajmaul-bayan anasema: “Yaani mtu akijiona hana haja na Mola wake, kwa sababu ya familia yake, mali yake na chakula chake.” Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Yaani pale anapojihisi yeye mwenyewe bila ya kuangalia yaliyo kabla yake, ambayo ni kufundishwa asiyoyajua.”

Tukiangalia mkusanyiko wa Aya mbili hizi, zikiwa ziko kwenye sentesi moja bila ya kitenganisho kati yake, na hapana budi kuwa na mtazamo huu, tukifanya hivyo maana yatakuwa, mtu hupituka mipaka ya sharia pale anapojiona amejitosheleza kielimu na nyenzo zake; kama vifaa vya upelelezi na viwanda na kumdhulumu aliye chini yake kwa nguvu.

Tafsiri hii, mbali ya kutiliwa nguvu na mfumo wa Aya, lakini pia ndio hali halisi ya sasa anayoishi nayo mtu. Wale walio na ilimu wanajaribu kuu­fanya ulimwengu wote uwanyenyekee wao na ukandamizaji wao, baada ya kuielekeza ilimu kuwa ni natija ya vita na viwanda vya silaha; wamekuwa na silaha zinazoweza kuimaliza dunia yote na vilivyomo ndani yake, kwa masaa machache tu.

Hii ndio tafsiri sahihi ya kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘Kwa kujiona ame­jitosheleza.’ Hata hivyo tuna uhakika ulioenea: “Mtu akijitosheleza, huji­faharisha na kuwa na kiburi, na akifukarika hukata tamaa na kuwa mny­onge.” Lakini hakika ya dhati ya kitu ni jambo jingine na ufahamisho wa tamko na mfumo wa maneno ni jambo jingine.

Hakika ni kwa Mola wako marejeo, usighurike na dunia na mapambo yake ewe mpetuka mipaka, wala pia na ilimu na makombora yake au mali na hadaa yake. Kwa sababu nguvu ya haki inasonga kuliko makombora ya nyuklia. Mapinduzi dhidi ya ukandamizaji na utumwa yaliyotokea India, China na kwengineko, yametoa somo kubwa kwa wenye viwanda vya sila­ha katika Amerika; kisha watarudishwa kwa mjuzi wa ghaibu na dhahiri awaambie yale waliyokuwa wakiyafanya.

Je, umemwona yule anayemkataza mja anaposwali?

Hii ni kumkana kila anayekataza mema kwa njia moja au nyingine.

Je, umeona kama yuko juu ya uwongofu? Au anaamrisha takua?

Niambie kuhusu huyo mpotevu ambaye anakataza mema na kuamrisha uovuje, yuko kwenye haki katika makatazo yake na amri yake?

Je, umeona kama yeye akikanusha na kurudi nyuma? Hajui kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

Mpotevu huyu ameikanusha haki na akaipinga; hivi haogopi adhabu ya Mwenyezi Mungu ambaye anajua siri yake na dhahiri yake?

Si hivyo! Kama hatakoma, tutamburuza kwa nywele za utosi! Utosi wa uwongo, wenye makosa!

Waarabu walikuwa wakizingatia kuburuta huku kuwa ni upeo wa idhlali na dharau, kwa sababu ni kwa wanyama si kwa watu. Utosi wa uwongo maana yake ni wa mwenye kusema uwongo. Maana ni akome huyu mpote­vu na upotevu wake, vinginevyo tutamkokota kwa utosi wake kwenda kwenye adhabu ya kuungua.

Basi na awaite wanachama wenzake!

Hapa kuna maneno ya kukadiria kuwa mpotevu na awaite watu wa baraza lake wamzuie na adhabu. Makusudio ya wanachama wenzake ni wasaidi­zi wake na jamaa zake; mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu:

قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُمْ مِنْ دُونِهِ فَلَا يَمْلِكُونَ كَشْفَ الضُّرِّ عَنْكُمْ وَلَا تَحْوِيلًا {56}

“Sema: Waombeni hao mnaodai badala Yake. Hawawezi kuwaondolea madhara wala kuyabadilisha.”Juz. 15 (17:56) .

Nasi tutawaita Mazabania!

Ambao ni malaika wa adhabu. Neno zabania lina asili ya maana ya kusukuma; yaani malaika watawasukuma wapituka mipaka kwenye moto wa Jahannam.

Si hivyo! Usimtii! Nawe sujudu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake, na ujikurubishe kwa Mwenyezi Mungu kwa vitendo vya kheri; bora yake zaidi ni jihadi.

Mafakihi wamezigawanya sijda kwenye vigawanyo vifuatavyo: Sijda ya Swala iliyozoeleka, sijda ya kusahahu inayotokana na ziada au upungufu katika Swala, sijda ya kushukuru, kwa kupata neema au kuondoka balaa na sijda ya kisomo.

Shia Imamiya wameifanya wajibu sijda ya kisomo katika sura 32, 41, 53 na 96 (Sajda, Hamim Sajda, Najm na A’alaq). Zisizokuwa hizo ni sunna.

  • 3372 views

Sura Ya Tisini Na Saba: Al-Qadr

Imeshuka Makka Ina Aya 5.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

إِنَّا أَنْزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ {1}

Hakika tumeiteremsha katika Laylatul Qadri.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا لَيْلَةُ الْقَدْرِ {2}

Na nini cha kukujulisha nini Laylatul Qadri?

لَيْلَةُ الْقَدْرِ خَيْرٌ مِنْ أَلْفِ شَهْرٍ {3}

Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu.

تَنَزَّلُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِمْ مِنْ كُلِّ أَمْرٍ {4}

Hushuka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao kwa kila jambo.

سَلَامٌ هِيَ حَتَّىٰ مَطْلَعِ الْفَجْرِ {5}

Ni amani huo mpaka mapam­bazuko ya alfajiri.

Maana

Hakika tumeiteremsha katika Laylatul Qadri,

Iliyoteremshwa ni Qur’an kwa kuingia kwake akilini. Laylatulqadr ni usiku mmojawapo katika mwezi mtukufu wa Ramadhani kutokana na Hadith nyingi, na pia kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Ni mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa ndani yake Qur’an.” Juz. 2 (2:185). Tukiunganisha Aya hii na hii tuliyo nayo, natija inakuwa laylatulqadr iko ndani ya mwezi wa Ramadhani.

Kauli zimekuwa nyingi kuhusu tarehe ya usiku huo, kutokana na hadith mbali mbali. Kitabu cha Mwenyezi Mungu kimelinyamazia hilo ili kuhimiza kuyashughulikia masiku yote ya Ramadhani kwa ibada, kama ilivyosemekana.

Kuna riwaya ya Imam Jafar As-Swadiq (a.s.) inayosema kuwa muulizaji alimuuliza kuhusiana na huo, akasema: “Utafute kwenye mwezi 19, 21 na 23,” imekuwa desturi kwa Sunni kuuadhimisha kwenye mwezi 27.

Maajabu niliyoyasoma, kuhusu kuuainisha usiku huu, ni yale yaliyoko kwenye kitabu AhkamulQur’an cha Abu Bakr, aliye maarufu kwa jina la Ibn Al-arabi Almua’firi Al-andalusi Almaliki, ninamnukuu: “Huo ni usiku wa 27, kwa sababu maulama wamehisabu herufi za sura mpaka walipofikia neno ‘huo,’ wakakuta ni 27, ndio wakauhukumia hivyo. Hilo ni jambo lililo wazi na baada ya kulijua ni jepesi, wala hawezi kulifuata ila mwenye fikra ya ukweli na mazingatio ya sawa.”

Wala ugwiji huu katika kutafuta natija na huku kujichunga sana katika kufafanua maneno ya Mwenyezi Mungu kuwa ni jambo jipya kwa yule aliyesema akiongezea juu ya fatwa ya Imam Shafi. Kwa kusema: “Haya ni maneno ya ambaye hajaonja ladha ya fiqh.” Vile vile aliyesema akiongezea fatwa ya Imam Abu Hanifa: “Hii ni fiqh dhaifu.” Tazama Kitabu Ahkamul ur’an Juz. 2 chapa ya 331 AH.

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Laylatulqadr ni usiku wa ibada, kunyenyekea na kukumbuka neema ya haki na dini, lakini waislamu siku hizi wanazungumza yale ambayo Mwenyezi Mungu hayaangalii kwao, na wanasikiliza kitu katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu bila ya kuchunguza yaliyomo wala kuzingatia maana yake; bali kama watasikiliza basi watazingatia sauti tamu tu ya anayesoma Qur’an, nao wana njozi nyingi, kuhusu laylatulqadr, zisizoingia hata kwenye akili za watoto, sikwambii za watu wazima.”

Wametofautiana kuhusu kushuka Qur’an kwamba ilishuka mara moja kwa ujumla au ilishuka kidogo kidogo? Ilivyo ni kuwa ilishuka kidogo kidogo na kwamba maana ya tumeiteremsha katika aylatulqadr ni kuanza kushu­ka kwake kwenye usiku huo. Hayo tumeayazungumza kwa ufafanuzi zaidi katika Juz. 15 (17:106).

Vile vile wametofautiana kuwa kwanini usiku huu ukaitwa laylatulqadr: kuna waliosema kuwa ni usiku wa makadirio, kwa vile Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anakadiria na kugawanya riziki na muda wa kufa baina ya waja wake katika usiku huu. Kuna aliyesema kwamba makusudio ya neno adr hapa ni cheo na heshima, kwa maana ya usiku wa heshima. Kauli hii iko karibu zaidi na neno adr na inatiliwa nguvu na Mwenyezi Mungu alivy­ousifu usiku huu kuwa ni wa Baraka: “Hakika tumekiteremsha katika usiku uliobarikiwa.” Juz. 25 (44:3).

Baraka ni wema na kukua. Hakuna mwenye shaka kuwa utu unakua na kuwa wema kama utaenda na sera ya Qur’an iliyoteremsha kwenye usiku wa heshima.

Na nini cha kukujulisha nini Laylatul Qadri?

Hii ni kuadhimisha shani yake na utukufu wa cheo chake na kwamba hau­fikiriki.

Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu isiyokuwa na laylatulqadr;

vinginevyo ingelazimika kujiweka chini huo wenyewe. Maana yake ni kuwa mwenye kukesha kwenye aylatulqadri ni kama aliyemwabudu Mwenyezi Mungu kwa miezi elfu moja.

Arrazi anasema: “Aya hii ina bishara kuu na tahadhari kubwa. Bishara ni kuwa Mwenyezi Mungu ametaja kuwa usiku huu ni bora lakini hakubain­isha kiwango cha ubora wake.

Hii ni kama kauli ya Mtume (s.a.w.) kwa Ali (as): kupambana Ali na Amru bin Wudd ni bora kuliko amali ya umma wangu mpaka siku ya Kiyama. Hakusema mfano wa amali yake, bali ame­sema ni bora zaidi; kama kwamba anasema: inatosha hii kuwa ni kipimo vilivyo baki ni vya kubahatisha.”

Hushuka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao kwa kila jambo.

Tafsiri na kauli zimekuwa nyingi kuhusiana na Aya hizi. Kwanza tutataja maana ya misamiati yake kisha ujumla wa maana.

Neno ‘Hushuka,’ hali­hitaji tafsiri, lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakutaja hao malika wanashukia wapi huo usiku wa layalatulqadr? Je, wanashukia kwenye ardhi yetu au nyingineyo? Au mahali popote? Roho ni Jibril. Idhini ya Mola ni amri. Kila jambo ni kila kitu mbinguni na ardhini.

Ujumla wa maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) katika laylatulqadr anawaamuru Malaika washuke mahali fulani kwa ajili ya kila jambo.

Kama tukiulizwa nini maana ya kwa ajili ya kila jambo? Je, ni kupangilia vitu na mkakati wa mwenendo wake, kuudhibiti au mengineyo? Tutajibu: Mwenyezi Mungu ndiye mjuzi zaidi. Sheikh Muhammad Abduh anasema: “makusudio ni kuwa mwanzo wa Mtume (s.a.w.) kushuhudia malaika ilikuwa usiku wa laylatulqadr.” Kauli hii iko mbali na dhahiri ya tamko.

Ni amani huo mpaka mapambazuko ya alfajiri.

Je, makusudio ya amani mpaka mapambuzo inakuwa katika masiku yote ya laylatulqadr, kwamba hakuna shari wala maafa katika usiku wowote wa laylatulqadr, au amani mpaka mapambuzoko ilikuwa maalum tu ya usiku ulioshukia Qur’an kwenye moyo wa Mtume?

Dhahiri, kutokana na ibara ya wafasiri, ni kuenea kwenye masiku yote ya laylatulqadr. Na kwa ibara ya Sheikh Muhammad Abduh ni kuhusika na usiku ule tu, anasema: “Ulikuwa ni usiku uliosalimika na kila shari na adha…Mwenyezi Mungu alimfariji Nabii wake na akamfungulia njia ya uwongofu akampa yale aliyokuwa anamtakia.”

  • 2505 views

Sura Ya Tisini Na Nane: Al-Bayyina

Imeshuka Makka Ina Aya 8 Imesemekana imeshuka Madina na ikasemekana imeshuka Makka.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

لَمْ يَكُنِ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ مُنْفَكِّينَ حَتَّىٰ تَأْتِيَهُمُ الْبَيِّنَةُ{1}

Hawakuwa waliokufuru mion­goni mwa Watu wa Kitabu na washirikina ni wenye kuachana na walio nayo mpaka iwajie hoja.

رَسُولٌ مِنَ اللَّهِ يَتْلُو صُحُفًا مُطَهَّرَةً {2}

Mtume atokaye kwa Mwenyezi Mungu awasomee kurasa zili­zotakaswa.

فِيهَا كُتُبٌ قَيِّمَةٌ {3}

Ndani yake mna vitabu vilivy­onyooka.

وَمَا تَفَرَّقَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ إِلَّا مِنْ بَعْدِ مَا جَاءَتْهُمُ الْبَيِّنَةُ {4}

Wala hawakufarikiana waliopewa Kitabu ila baada ya kuwajia hoja.

وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَ ۚ وَذَٰلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ {5}

Nao hawakuamrishwa ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, wawe wanyoofu, na wasimamishe Swala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini iliyonyooka.

إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ أُولَٰئِكَ هُمْ شَرُّ الْبَرِيَّةِ {6}

Hakika waliokufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina watakua katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu.

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَٰئِكَ هُمْ خَيْرُ الْبَرِيَّةِ {7}

Hakika walioamini na waka­ tenda mema hao ndio bora wa viumbe.

جَزَاؤُهُمْ عِنْدَ رَبِّهِمْ جَنَّاتُ عَدْنٍ تَجْرِي مِنْ تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ۖ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ ۚ ذَٰلِكَ لِمَنْ خَشِيَ رَبَّهُ {8}

Malipo yao kwa Mola wao Mlezi ni Bustani za milele, zip­itiwazo na mito chini yake. Wakae humo milele. Mwenyezi Mungu yuko radhi nao, na wao wako radhi naye. Haya ni kwa anayemuogopa Mola wake.

Maana

Hawakuwa waliokufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirik­ina ni wenye kuachana na walio nayo mpaka iwajie hoja.

Makusudio ya watu wa Kitabu ni mayahudi na wanaswara, na washirikina ni waabudu masanamu katika waarabu. Watu wa Kitabu walikuwa wame­soma katika vitabu vyao kwamba Mwenyezi Mungu atapeleka Mtume atakayeongoza kwenye haki. Vile vile washirkina walimsikia Nabii huyu.

Yakawa makundi mawili haya ni kama mfano wa maelewano ya kutumwa Nabii aliyeahidiwa. Mara nyingi ikitokea uhasama baina ya watu wa Kitabu na washirikina, kila kundi likidai lina haki; kisha wanaafikiana kumngojea Nabii aje awaaamue na kwamba akija watamwamini na wata­fuata hukumu yake. Huyo ndiye aliyekusudiwa kuwa ni hoja aliyoibainisha Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwa kauli yake:

Mtume atokaye kwa Mwenyezi Mungu awasomee kurasa zilizo­takaswa, Ndani yake mna vitabu viliyonyooka.

Makusudio ya Mtume hapa ni Muhammad (s.a.w.); na kurasa ni Qur’an, na ni nyingi kwa kuzingatia Sura zake au kurasa zake. Zilizotakaswa maana yake ni zilizotakaswa na ubatilifu na kupotolewa.
Na makusudio ya vitabu ni kuwa Qur’an ndani yake mna ubainifu mwingi wa aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu katika vitabu vya mbinguni vilivy­otangulia kama vitabu vya Ibrahim, Tawrat, Injil na Zaburi, bali mna ubainifu wa yote yaliyoteremshiwa manabii, ukiwemo mwongozo na misingi ya dini. Makusudio ya kunyooka ni kuwa kwenye njia ya haki.

Maana ni kuwa Muhammad (s.a.w.) alipokuja na Qur’an ambayo ndani yake mna ubainifu wa kila kitu, washirikina na watu wa Kitabu walimpin­ga, na wakavunja ahadi waliyoiweka kuwa watahukumiwa na Nabii aliyeahidiwa.

Wala hawakufarikiana waliopewa Kitabu ila baada ya kuwajia hoja.

Hoja hii iliwajia watu wa Kitabu kupitia kwenye ndimi za manabii wao. Kwa hiyo makusudio ya hoja hii sio ile ya Aya iliyotangulia. Maana ni kuwa watu wa Kitabu waliendelea na upotevu kwa kupinga kwao mwito wa Muhammad (s.a.w.), aliyewajia na hoja waziwazi, kama walivyoende­lea na usafihi na upotevu baada ya manabii wao kuwajia na dalili na hoja.

Na hilo ni kwamba mayahudi waligawanyika kwenye vikundi baada ya kujiwa na Musa, vile vile wanaswara wakagawanyika baada ya Isa. Tofauti sio kuwa ilisababishwa na kutojua dini; isipokuwa hawaa na manufaa ndiyo yaliyowafarikisha.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 4 (3:105) na Juz. 25 (45:17).

Nao hawakuamrishwa ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kum­takasia Dini, wawe wanyoofu, na wasimamishe Swala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini iliyonyooka.

Neno unyoofu tumelitoa kwenye neno ‘hunafaa’, lenye maana ya kuwa na msimamo wa haki kwa kuepuka kila batili. Maana ni kuwa watu wa Kitabu walifarikiana katika dini yao pamoja na kuwa dini ya Mwenyezi Mungu ni moja na iko wazi, nayo ni kumfanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu peke yake, msimamo wa haki na uongofu, kusimamisha swala na kutoa Zaka. Hii ndio dini ya mbinguni iliyonyooka kwenye njia ya sawa; sasa zimetoka wapi idadi za dini mataifa na madhehebu?

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Haya ndio anayowasikitikia Mwenyezi Mungu watu wa Kitabu. Je, na sisi tusemeje kuhusu hali yetu? Si Kitabu chetu kinatusikitikia kwa kukushudia ubaya wetu katika kufarikiana kwetu kwenye dini, baada ya kuwa makundi na tukaijaza dini bid’a na uzushi? Tazama Juz. 1 (2:111-113) kifungu cha ‘Waislamu vile vile wanakufurishana.’

Hakika waliokufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina watakua katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu.

Makusudio ya makafiri hapa ni kila mwenye kuipinga haki iliyo na dalili; ni sawa aipinge kwa inadi baada ya kuijua au kukataa kuitafuta haki na kuichunguza pamoja na dalili zake.

Maulama wa kiislamu wameafikiana kuwa asiyejua na akazembea kuitafuta haki, hukumu yake ni sawa na anayeijua kisha akaiacha kwa makusudi. Hakuna shaka kwamba mwenye kuipinga bila ya sababu za kutosha, huyo ni mshari zaidi katika watu wa ardhini; sawa na aliyemfanyia washirika Mwenyezi Mungu. Hakuna malipo ya huyu na yule isipokuwa fedheha na adhabu.

Hakika walioamini na wakatenda mema, yaani walioiamini haki na wakatenda kwa mujibu wa imani yao, hao ndio bora wa viumbe.

Kila mwenye kuitafuta haki na akaitumia kwa njia ya haki bila ya kuogopa lawama, basi hakuna yeyote aliye bora kumshinda; isipokuwa aliyechag­uliwa na Mwenyezi Mungu kufikisha risala yake na kumwamini na wahyi wake.

Malipo yao kwa Mola wao Mlezi ni Bustani za milele, zipitiwazo na mito chini yake. Wakae humo milele. Mwenyezi Mungu yuko radhi nao, na wao wako radhi naye.

Amewaridhia kwa vile walifanya kwa mujibu wa radhi yake, ndio akawali­pa miliki ya daima; na wao wako radhi naye kwa neema alizowamiminia.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (5:119) na Juz. 11 (9:100).

Hayo ni kwa anayemwogopa Mola wake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemwandalia malipo mema yule anayem­wogopa Mwingi wa rehema, na akawa mkwelii. Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amekusudia kwa matamshi matukufu, kuondoa fikra mbovu iliyoenea, kwamba kiasi cha imani tu ya kurithi kutoka kwa wazazi na kujua baadhi ya dhahiri za hukumu na kutekeleza baadhi ya ibada huwa inatosha kumfanya mtu apate aliy­owaamdalia Mwenyezi Mungu waumini; hata kama moyo umejaa chuki, hasadi, kiburi na ria; na mdomoni kumejaa uwongo, fitina na uzushi; na moyoni kumejaa utumwa.

Hapana! hatapata malipo mema, kwa sababu moyoni mwake hamkuingia hofu ya Mwenyezi Mungu wala nafsi haikuwa safi. Hilo haliwi ila kwa anayemwogopa Mola wake na akihisi hofu ndani ya moyo wake.

  • 1939 views

Sura Ya Tisini Na Tisa: Az-Zilzala

Imeshuka Makka na imesemekana imeshuka Madina Ina Aya 8.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

إِذَا زُلْزِلَتِ الْأَرْضُ زِلْزَالَهَا {1}

Itakapotetemeshwa ardhi huo mtetemeko wake!

وَأَخْرَجَتِ الْأَرْضُ أَثْقَالَهَا {2}

Na ikatoa ardhi mizigo yake!

وَقَالَ الْإِنْسَانُ مَا لَهَا {3}

Na mtu akasema: Ina nini?

يَوْمَئِذٍ تُحَدِّثُ أَخْبَارَهَا {4}

Siku hiyo itahadithia habari zake.

بِأَنَّ رَبَّكَ أَوْحَىٰ لَهَا {5}

Kwa sababu Mola wako ameipa wahyi!

يَوْمَئِذٍ يَصْدُرُ النَّاسُ أَشْتَاتًا لِيُرَوْا أَعْمَالَهُمْ {6}

Siku hiyo watu watatoka kwa mtawanyiko ili wakaonywesh­we vitendo vyao!

فَمَنْ يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ {7}

Basi anayetenda chembe ya wema, atauona!

وَمَنْ يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ شَرًّا يَرَهُ {8}

Na anayetenda chembe ya uovu atauona!

Maana

Itakapotetemeshwa ardhi huo mtetemeko wake!

Hii ni kutoa hadhari ya vituko vya siku ya Kiyama ambapo ardhi itagongana na kutingishika kwa mtingishiko mkali. Mfano wa Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمْ ۚ إِنَّ زَلْزَلَةَ السَّاعَةِ شَيْءٌ عَظِيمٌ {1}

“Enyi watu! Mcheni Mola wenu. Hakika tetemeko la saa ni jambo kubwa.” Juz. 17 (22:1).

Na ikatoa ardhi mizigo yake!

Itatoa kila kilichomo ndani yake wakiwemo wafu, hazina, madini na maen­deleo.

Na mtu akasema: Ina nini?

Vipi hii ardhi inakwenda bila ya desturi yake? Imetokewa na nini?

Siku hiyo itahadithia habari zake.

Kuhadithia kwa mtu ni kutoa yaliyo katika nafsi yake na kuhadithia kwa ardhi, Siku ya Kiyama, ni kudhihirisha nje yale maajabu yote iliyoyameza wakati wote. Sijui wataalamu wa mambo ya kale watayaona maonyesho haya ya kutisha?

Kwa sababu Mola wako ameipa wahyi!

Kila litakalotokea kwenye ardhi Siku ya Kiyama ni kwa amri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Hakuna kitakachozuia kuharibika ardhi katika mwisho wa umri wake, kwa kuvunjika jengo lake na kuifanya vumbi linalotifuka.”

Kama kwam­ba anaashiria, kwa kauli yake hii, kwenye mlipuko wa nyuklia kwenye uso wa ardhi na ndani yake, ingawaje haikuwako wakati wake. Kauli yake hii iko karibu sana, kwa sababu umri wa ardhi hauishi kwa kupita nyakati kama ilivyo katika viumbe vingine hai; bali ni kwa kuharibi­ka yote au sehemu zake za msingi.

Siku hiyo watu watatoka kwa mtawanyiko ili wakaonyweshwe viten­do vyao!

Siku ya Kiyama Mwenyezi Mungu ataubadilisha ulimwengu usiokuwa ulimwengu huu na kiumbe wa kwanza atakutana na wa mwisho na wote watakwenda pale kila mmoja aone jaza ya matendo yake.

Basi anayetenda chembe ya wema, atauona! Na anayetenda chembe ya uovu atauona!

Katika Tafsir Arrazi na nyinginezo imesemwa neno dharra, tulilolifasiri kwa maana ya chembe, kuwa lina maana ya mdudu chungu aliye mdogo zaidi ya wengine. Katika kitabu Al-ur’an wal-ilmulhadith cha Nawfal anasema: “Neno dharra ni sehemu ndogo ambayo umbo lake halifiki sehe­mu ya kumi chini ya milimita bilioni moja.” Vile vile imesemwa kuwa dharra haiwezi kuonekana hata kwa hadubini kubwa, isipokuwa inaju­likana kwa athari yake tu.

Maana ni kwamba kila mtu kesho atakuta malipo ya matendo yake kwa Mwenyezi Mungu, yakiwa ni heri basi ni heri na yakiwa nishari basi ni shari, kwa kiasi chochote cha udogo kitakachofikia. Kimsingi ni kuwa malipo ya kitu yanahisabiwa kwa kiwango na kiaina.

Unaweza kuuliza: Je, mumin na kafiri ni sawa katika hilo, au ni kuwa mwenye kumkufuru Mwenyezi Mungu hayatakubaliwa matendo yake ya heri wala kulipwa, hata kama ameyafanya kwa njia ya heri ya ubinadamu?

Jibu: Kila kitu kina hisabu yake. Ikiwa kafiri atafanya heri, ataadhibiwa adhabu ya ukafiri wake na atalipwa matendo ya heri kulingana na vile hiki­ma ya Mwenyezi Mungu itakavyoona; iwe ni kumlipa duniani au kumhafi­fishia adhabu ya Akhera. Tumeyazungumzia maudhui haya kwa ufafanuzi zaidi katika Juz. 4 (3:176­178) kifungu cha ‘Kafiri na amali njema.’

Swali la pili: Aya nyingi zimefahamisha kuwa kufuru inaporomosha matendo yote hata kama yote ni mema?

Baadhi ya maulama wamejibu kuwa maana ya kuporomoka matendo ni kuwa mema ya kafiri yahayamuokoi na adhabu ya kufuru, na wala sio kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hamlipi kabisa hata duniani.

  • 2191 views

Sura Ya Mia: Al-A’diyat

Imeshuka Makka na imesemekana ni Madina Ina Aya 11.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَالْعَادِيَاتِ ضَبْحًا {1}

Naapa kwa wanokwenda mbio wakihema.

فَالْمُورِيَاتِ قَدْحًا {2}

Wakitoa moto kwa kupiga kwato.

فَالْمُغِيرَاتِ صُبْحًا {3}

Wakishambulia wakati wa asubuhi.

فَأَثَرْنَ بِهِ نَقْعًا {4}

Wakatifua vumbi wakati huo.

فَوَسَطْنَ بِهِ جَمْعًا {5}

Wakaliingilia kati wakati huo kundi.

إِنَّ الْإِنْسَانَ لِرَبِّهِ لَكَنُودٌ {6}

Hakika mtu ni mtovu wa shukrani kwa Mola wake!

وَإِنَّهُ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌ {7}

Na hakika yeye bila ya shaka ni shahidi wa hayo!

وَإِنَّهُ لِحُبِّ الْخَيْرِ لَشَدِيدٌ {8}

Naye hakika ana mapenzi sana na mali!

أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِي الْقُبُورِ {9}

Kwani hajui watakapofufuliwa waliomo makaburini?

وَحُصِّلَ مَا فِي الصُّدُورِ {10}

Na yakadhihiirishwa yaliy­omo vifuani?

إِنَّ رَبَّهُمْ بِهِمْ يَوْمَئِذٍ لَخَبِيرٌ {11}

Hakika Mola wao siku hiyo bila ya shaka atakuwa na habari sana!

Maana

Katika Tafsir Majmau-lbayan na nyinginezo imeelezwa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) alituma kikosi cha wapiganaji kwenye kitongo­ji kimoja cha Bani Kinana, kikachelewa. Basi wanafiki wakasema wameuliwa, ndio ikashuka Sura hii kumpa habari Nabii (s.a.w.) kuwa wako salama, na kuwakadhibisha wanaoneza uvumi.

Naapa kwa wanokwenda mbio wakihema.

Makusudio ya wanokwenda mbio hapa ni farasi. Imesemekana kuwa ni ngamia. Kuhema hapa ni kutuo pumzi mbele ya adui.

Wakitoa moto kwa kupiga kwato.

Yaani farasi wanatoa cheche za moto kwenye kwato zao zinapopiga mawe mbele ya adui.

Wakishambulia wakati wa asubuhi.

Farasi waliwashambulia maadui ghafla wakati wa asubuhi.

Wakatifua vumbi wakati huo, wakaliingilia kati wakati huo kundi.

Makusudio ya kundi hapa ni kundi la maadui. Maana ni kuwa farasi wali­washambulia maadui wakati wa asubuhi.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameapa kwa farasi wa vita. Kwa ufasha zaidi ni kuwa ameapa kwa nguvu na kuandaa maadui, ili awahimize waumini kufanya jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu na kuwa na silaha ya kumkemea adui wa Mwenyezi Mungu na wa ubinadamu.

Mwenye kufu­atilia Aya za Qur’an yenye hikima atakuta kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewahimiza waumini kwenye Aya kadhaa na kwa mifumo mbal­imbali, wawe na silaha za kuwaogofya wapituka mipka ambao hawafahamu lugha isipokuwa nguvu; miongoni mwa Aya hizo ni hizi zifuatazo:

وَأَعِدُّوا لَهُمْ مَا اسْتَطَعْتُمْ مِنْ قُوَّةٍ وَمِنْ رِبَاطِ الْخَيْلِ تُرْهِبُونَ بِهِ عَدُوَّ اللَّهِ وَعَدُوَّكُمْ {60}

“Na waandalieni nguvu kama vile muwezavyo na kwa farasi waliofungwa ili mumtishe adui wa Mwenyezi Mungu na adui yenu.” Juz. 10 (8:60).

 وَدَّ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْ تَغْفُلُونَ عَنْ أَسْلِحَتِكُمْ {102}

“Wanataka wale waliokufuru lau kama nyinyi mwasahau silaha zenu.” Juz. 5 (4:102).

وَلَا تَكُونُوا كَالَّتِي نَقَضَتْ غَزْلَهَا مِنْ بَعْدِ قُوَّةٍ أَنْكَاثًا {92}

“Wala msiwe kama mwanamke ambaye ameufumua uzi wake baada ya kuusokota na
kuwa mgumu.” Juz. 14 (16:92).

Na Aya nyinginezo zisizokuwa hizo zinazoamuru kila jambo la kufanya tamko la haki liwe juu na la batili liwe chini. Hapa inatubainikia kwamba kutajwa farasi na kuhema kwake, kupiga kwato na kushambulia ni kinaya cha kuandaa nguvu za kuihifadhi haki na watu wake. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ametumia farasi kuelezea nguvu, kwa vile ndio waliokuwa wakitu­mika zaidi wakati huo.

Sheikh Muhamad Abduh akiwa anafasiri Aya hizi anasema: “Si ni jambo la kushangaza kwamba watu, wanadai kuwa Qur’an ni Kitabu chao na wao ndio walioko mbali zaidi na ukakamavu na sifa zake.

Nimezungumza na Mwalimu katika wao kuhusu kunufaika na baadhi ya ilimu ili zifundishwe kwenye chuo cha Al-azhar, akasema: ‘kwa hiyo ni lazima tuwafundishe wanafunzi kupanda farasi?’ Alisema hivi ili aninyamazishe. Je, kauli yake hii inaafikiana na kuamini Kitabu cha Mwenyezi Mungu? Pima na uamue.”

Hakika mtu ni mtovu wa shukrani kwa Mola wake!

Hukumu ya Aya ni kuzingatia aghalabu ya watu sio watu wote. Maana ni kuwa watu wengi wanamsahau Mwenyezi Mungu kwenye neema wala hawamshukuru kwa kujitolea kwenye njia yake. Amesema Mtume (s.a.w.): “Mtovu wa shukrani ni yule anayekula peke yake, anampiga mtumishi wake na anazuia msaada wake.”

Na hakika yeye bila ya shaka ni shahidi wa hayo!

Yaani vitendo vya mtovu wa shukrani vinashuhudia kwa lugha ya mazin­gira kwamba yeye anazikufuru neema za Mwenyezi Mungu. Aina kubwa kabisa ya kumkufuru Mwenyezi Mungu na neema yake ni kuwakandamiza waja wa Mwenyezi Mungu kwa neema hiyo.

Naye hakika ana mapenzi sana na mali.

Neno mali hapa tumelifasiri kutokana na neno khair, kama walivyosema wafasiri. Hakuna mwenye shaka kwamba ambaye penzi lake kwa mali limezidi sana basi atakuwa amejivua na utu na kupinga misimamo yote isipokuwa kama ni nyenzo ya kukusanya mali. Na kama tutatafuta sababu zinazoleta maafa ya ubinadamu tutaona kuwa yanatokana na kushindania mali na kuikusanya. Harbert Marcuse ambaye alikuwa ni mwalimu katika vyuo vikuu vya Columbia, Harvad na Brandeis huko Amerika anasema katika kitabu chake ne dimensional man: “Itatoka wapi heri kwenye zama ambazo hakuna ila shari; ambapo mambo ya kimaada yamemtawala mtu kwa namna ambayo imemfaya mtu kuwa ni mtumwa na hiyo ndiyo bwana mkubwa mwenye nguvu na kutawala.”

Kwani hajui watakapofufuliwa waliomo makaburini? Na yakadhi­hirishwa yaliyomo vifuani? Kuwa hakika Mola wao siku hiyo bila ya shaka atakuwa na habari sana!

Anaelezewa mtu au mtovu wa shukrani, kuwa hajui mwisho wake? kudhi­hirishwa waliomo makaburini ni kufufuliwa. Kuwa na habari ni ishara yakuwa anayajua makusudio na matendo yao na atawalipa wanavyostahi­ki.

Aya hizi zinamhadharisha na kumpa kiaga kila mwenye kuzikufuru neema za Mwenyezi Mungu na kuzitumia kuwakandamizia waja wake mfano wa Aya hizi uko kwenye Aya kahaa zilizopita; ikiwemo ile ya Juz. 2 (2:235).

  • 2041 views

Sura Ya Mia Na Mmoja: Al-Qari’aa

Imeshuka Makka Ina Aya 11.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

الْقَارِعَةُ {1}

Inayogonga!

مَا الْقَارِعَةُ {2}

Nini inayogonga?

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْقَارِعَةُ {3}

Na nini cha kukujuilisha nini inayogonga?

يَوْمَ يَكُونُ النَّاسُ كَالْفَرَاشِ الْمَبْثُوثِ {4}

Siku ambayo watu watakuwa kama panzi waliotawanyika.

وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِ الْمَنْفُوشِ {5}

Na milima itakuwa kama sufi zilizochambuliwa!

فَأَمَّا مَنْ ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ {6}

Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito.

فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَاضِيَةٍ {7}

Huyo atakuwa katika maisha ya kuridhiwa.

وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ {8}

Na yule ambaye mizani yake itakuwa hafifu.

فَأُمُّهُ هَاوِيَةٌ {9}

Basi mama yake atakuwa Hawiya!

وَمَا أَدْرَاكَ مَا هِيَهْ {10}

Na nini kitachokujuilisha nini hiyo?

نَارٌ حَامِيَةٌ {11}

Ni Moto mkali!

Maana

Inayogonga!

Hilo ni mojawapo ya majina ya siku ya Kiyama. Kwa sababu kinagonga nyoyo; mfano wake ni Tukio la haki, Ukelele, Balaa kubwa n.k.

Nini inayogonga?

Ni swali lenye lengo la kulikuza jambo.

Na nini cha kukujuilisha nini inayogonga?

Ni jambo gani la kukujulisha kuwa siku hiyo iko zaidi ya inavyofikiriwa.

Siku ambayo watu watakuwa kama panzi waliotawanyika.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amefananisha hali ya viumbe Siku ya Kiyama na hali ya panzi katika kutojua wafanye nini na wengi wao kuanguka motoni.

Na milima itakuwa kama sufi zilizochambuliwa kwa kutawanyika. Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito.

Yaani yule ambaye matendo yake yatakuwa mema, Huyo atakuwa katika maisha ya kuridhiwa; yaani atayaridhia na kuyafurahia.

Na yule ambaye mizani yake itakuwa hafifu; yaani matendo yake yaki­wa mabaya.

Tumelizungumzia hilo kwa ufafanuzi katika Juz. 17 (21:45-50).

Basi mama yake atakuwa Hawiya!

Makusudio ya mama hapa ni mahali atakapofikia na patakapomkumbatia. Hawiya ni Jahannam. Neno hili lina maana ya kuangukia. Imeitwa hivyo kwa sababu mwenye hatia ataaangukia hapo.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amelibainisha hilo kwa kusema:

Na nini kitachokujuilisha nini hiyo Hawiya? Ni Moto mkali!

Haya ndiyo unayoweza kuyafahamu kuhusiana na Jahannam. Ama kuijua hakika yake, utashindwa kufahamu, kwa sababu shimo lake liko ndani sana na adhabu yake ni kali.

  • 1891 views

Sura Ya Mia Na Mbili: At-Takathur

Imeshuka Makka, na imesemekana ni Madina Ina Aya 8.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

أَلْهَاكُمُ التَّكَاثُرُ {1}

Kumewashughulisha kujifa­harisha kwa wingi!

حَتَّىٰ زُرْتُمُ الْمَقَابِرَ {2}

Mpaka mkayazuru makaburi!

كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ {3}

Si hivyo! Mtakuja jua!

ثُمَّ كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ {4}

Tena si hivyo! Mtakuja jua!

كَلَّا لَوْ تَعْلَمُونَ عِلْمَ الْيَقِينِ {5}

Si hivyo! Lau mngelijua kwa ujuzi wa yakini.

لَتَرَوُنَّ الْجَحِيمَ {6}

Hakika mtauona Moto!

ثُمَّ لَتَرَوُنَّهَا عَيْنَ الْيَقِينِ {7}

Kisha, hakika, mtauona kwa jicho la yakini.

ثُمَّ لَتُسْأَلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ النَّعِيمِ {8}

Kisha hakika mtaulizwa siku hiyo juu ya neema.

Maana

Kumewashughulisha kujifaharisha kwa wingi, mkaacha haki na maten­do mema na kujifaharisha kwa wingi wa mali na mengineyo mfano wake; kama kusema: Mimi nina mali nyingi au nina cheo kikubwa kuliko wewe.

Mpaka mkayazuru makaburi.

Mmepita kwenye mghafala mpaka yakawafikia mauti. Imam Ali (a.s.) ana maneno marefu aliyoyasema baada ya kusoma Aya hii; miongoni mwayo ni: “Hivi wanajifaharisha kwa wazazi wao walio wafu, au wanajifaharisha kwa wingi wa idadi ya walioangamia? …. Ilitakikana hayo yawe mazinga­tio badala ya kujifaharisha.”

Si hivyo!

Acheni kujifaharisha kwa wingi, kwani hakuwafai chochote.

Mtakuja jua!

Adhabu itakayowapata.

Tena si hivyo! Mtakuja jua!

Huu ni msisitizo wa kutoa hadhari.

Si hivyo! Lau mngelijua kwa ujuzi wa yakini.

Yaani lau mngelikuwa mnajua kwa ujuzi wa uhakika matokeo ya kujifa­harisha kwa wingi, basi mngelikoma kufanya hivyo. hapo kuna ishara kwamba ilimu bila ya matendo ni sawa na ujinga. Katika hilo Imam Ali (a.s.) anasema: “Ilimu inatoa mwito wa kufanya, asipouitikia inamwondo­ka.”

Hakika mtauona Moto!

Hii ni kumhadharisha mwenye kuukadhibisha huo Moto, au akauamini lakini asifanye kwa mujibu wa imani yake. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameleta kinaya cha kuona kwa maana ya kuuingia.

Kisha, hakika, mtauona kwa jicho la yakini.

Hii ni kusisitiza kuwa wataujua na kwamba wataujua kwa macho.

Inaonyesha kuwa nadharia yoyote isiyotegemea kuonekana na kushuhudi­wa na macho moja kwa moja au kwa kupitia kitu kingine, basi hiyo sio ilimu. Kwa hiyo ilimu ya kweli ni kuliona jambo lenyewe au kuona athari yake inayolifahamisha. Ya kwanza inaitwa ilimu ya uoni na ya pili ni ilimu ya dalili.

Kisha hakika mtaulizwa siku hiyo juu ya neema.

Makusudio ya neema hapa ni mali wanayojifaharisha nayo, kwa lugha ya kusema au ya hali. Wataulizwa mbele ya Mwenyezi Mungu: wameipata wapi? Wameitumia vipi? Je, waliipata kwa jasho lao au kwa kupora? Je, wameitumia katika njia ya halali au haramu?

Ama mahitaji ya kawaida, kama chakula, mavazi na makazi, sio neema inayokusudiwa hapa.

  • 2528 views

Sura Ya Mia Na Tatu: Al-A’sr

Imeshuka Makka Ina Aya 3.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَالْعَصْرِ {1}

Naapa kwa Zama!

إِنَّ الْإِنْسَانَ لَفِي خُسْرٍ {2}

Hakika mtu bila ya shaka yumo katika hasara.

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَتَوَاصَوْا بِالْحَقِّ وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ {3}

Ila wale walioamini, na waka­tenda mema, Na wakausiana haki, na wakausiana kusubiri.

Maana

Naapa kwa Zama!

Neno zama tumelifasiri kutokana na neno A’sr, ambalo wafasiri wameto­fautiana katika makusudio yake kwa kauli mbali mbali:

Ya kwanza, ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameapa kwa Swala ya alasiri, kwa lengo la kutanabahisha ubora wake kama ilivyo katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

حَافِظُوا عَلَى الصَّلَوَاتِ وَالصَّلَاةِ الْوُسْطَىٰ {238}

“Angalieni sana Swala na ile Swala ya katikati.” Juz. 2 (2:238).

Kauli hii iko mbali na ufahamu wa kiujumla.

Kauli ya pili, ni kwamba makusudio ni zama za Mtume (s.a.w.). Kauli hii iko mbali zaidi kuliko ile ya kwanza.

Kauli ya tatu, ni wakati wa alasiri, mwisho wa mchana. Kwamba Mwenyezi Mungu hapa ameapa na mwisho wa mchana, kama alivyoapa na mwanzo wa mchana kwenye Juzuu hii tuliyo nayo (91:1). Kauli hii haiko mbali sana na ufahamisho wa tamko.

Kauli ya nne, kwamba makusudio ya Al-a’sr ni wakati wowote ambao unatukia matukio na matendo. Mfumo wa maneno unaashiria kwenye kauli hii; kwani kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Hakika mtu bila ya shaka yumo katika hasara,’ iliyokuja moja kwa moja bila ya kuweko kati maneno mengine, inatambulisha kuwa mtu ndiye aliye katika hasara na wala sio zama.

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Ni desturi ya waarabu kukusanyika wakati wa alasiri na kuzungumza mambo yao. mara nyingine mazungum­zo yao yanapelekea yale yanayowachukiza, watu wakaushutumu wakati huo. Ndio Mwenyezi Mungu akaapia nao ili kuwabainishia kuwa wakati haushutumiwi; isipokuwa vinavyoshutumiwa ni vitendo vya kuchukiza na wakati ni wa mambo mema na maovu na utukufu na udhalili.

Hakika mtu bila ya shaka yumo katika hasara; ila wale walioamini, na wakatenda mema.

Hili ndilo jawabu la kiapo. Makusudio ya mtu ni yule mwenye majukumu ya kauli yake na vitendo.

Mtu huyu, kwa hukumu ya Qur’an, ni mwenye hasara, hata kama ni tajiri aliye na mamilioni, au mtaalmu anayejua siri za maumbile na kuzitumia kwa masilahi yake, au mwenye nguvu za kuwatawala watu, au mwenye ufasaha anayeweza kutengeneza maneno na mawaidha.

Huyu atakuwa hana kitu na ni mwenye hasara tu, isipokuwa akimwamini Mwenyezi Mungu, halali yake na haramu yake, Moto wake na Pepo yake; na imani yake hii iakisi kwenye kauli yake na vitendo vyake; vinginevyo imani bila ya matendo ni kiasi cha fikra tu na nadharia.

Miongoni mwa niliyoyasoma, ni kuwa wanaanga watatu wa kimarekani waliorusha bomu la nyuklia kule Hiroshima Japan, kila mmoja wao alikuwa na nakala ya ‘Biblia takatifu’ pembeni mwa kombora la maangamizi!!

Unaweza kuuliza: kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Hakika mtu bila shaka yuko katika hasara,’ si inafahamisha kwa dhahiri yake, kuwa mtu ni mwenye hasara kwa maumbile yake; na kwamba watu wako sawa kwenye hasara? Ikiwa ni hivyo basi haifai kuwagawanya watu kwenye wema na uovu, hasara na faida. Kwa sababu dhati haiwezi kubadilika; hati­mae kuna haja gani ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Ila wale walioamini na wakatenda mema?

Jibu: Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakuhukumu maumbile ya mtu kwenye hasara, kama mtu; isipokuwa ni kwa uaghlabu. Mfano huu kwenye Qur’an ni mwingi; kama vile kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 إِنَّ الْإِنْسَانَ لَظَلُومٌ كَفَّارٌ {34}

“Hakika mtu ni dhalimu mkubwa mwingi wa kukufuru.” Juz. 13 (14:34)

Pia kauli yake:

 وَكَانَ الْإِنْسَانُ قَتُورًا {100}

“Mtu ni mchoyo sana.” Juz. 15 (17:100).

Kwa hiyo basi mtu kwa maumbile yake hahisabiwi kuwa ni mwenye hasara wala mwenye faida, kwa sababu yeye ana uwezo na maandalizi ya yote mawili. Hivyo kumchukila kwenye moja wapo itakuwa ni kutia nguvu bila ya nguvu. Atachukuliwa, kwa moja wapo ya sifa mbili, kwa kuangalia itikadi yake na matendo yake; sio kuangalia dhati yake na maumbile yake.

Mara nyingi tumeeleza kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amempa mtu akili na uwezo wa kufanya shari na heri, akamwamrisha hili, wa akamkataza lile na akamwachia hiyari bila ya kumlazimisha dini na matendo kwa kuyaum­ba kama anavyoumba viumbe. Kama angelifanya hivi angeliuondoa utu wa mtu; kwa kuwa hakuna utu bila ya uhuru na utashi.

Kwa hiyo mtu hawi na hasara ila kwa itikadi yake na matendo yake. Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Hakika mtu bila ya shaka yumo katika hasara ila wale walioamini, na wakatenda mema,’ inamaanisha kuwa wale ambao hawakuamini au wameamini lakini wasitende, basi hao ndio walio na hasara, lakini walioamini na wakatenda hao ndio wenye faida na wenye kufuzu.

Na wakausiana haki, na wakausiana kusubiri.

Maneno haya yanaungana na walioamini na wakatenda. Maana ni kuwa wenye kufuzu kesho ni wale waliomwamini Mwenyezi Mungu na sharia yake, wakatenda kwa mujibu wa imani yao hiyo na wakausiana kushika­mana na haki na subira.

Sheikh Muhammad Abduh ameielezea haki kuwa: “Ni ile inayoongoza kwenye dalili mkataa au kuonekana na kushuhudiwa.”

Hii ni taarifa ya hakika sio ya haki. Tofauti iliyoko ni kwamba hakika ni mtoto wa dalili, ama haki inajisimamia hiyo yenyewe; ni sawa iwe imefa­hamishwa na dalili au haikufahamishwa. Watu wengi huwa wanashindwa kuithibitisha haki yao kwa dalili mkataa na ushahidi.

Vyovyote iwavyo ni kuwa kila tendo lililo na radhi ya Mwenyezi Mungu na masilahi kwa watu basi hiyo ni haki, heri na uadilifu. Ama subira ni kuthibiti kwenye haki na kumwambia anayeivunja: La! Kwa namna yoy­ote yatakavyokuwa matokeo.

Kwa ufupi ni kuwa kubwa lilio kwa mtu na neema muhimu aliy­oneemeshwa na Mwenyezi Mungu mtu, ni kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu amempa mtu uwezo wa kutosha kuwa malaika au shetani, mwenye faida au hasara; na kwamba hikima yake Mtukufu, imempa uhuru mtu peke yake kujichagulia mwenyewe analolitaka; uovu na hasara au faida na wema, na kwamba Mwenyezi Mungu atamchukulia kwa lile alilo­jichagulia mwenyewe - faida au hasara, baada ya kumpa mwongozo wa njia mbili. Kuna fadhila gani kuu kuliko hii na uadilifu gani mkubwa kuliko huu.

  • 2328 views

Sura Ya Mia Na Nne: Al-Humaza

Imeshuka Makka Ina Aya 9.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَيْلٌ لِكُلِّ هُمَزَةٍ لُمَزَةٍ {1}

Ole wake kila msingiziaji, msengenyaji!

الَّذِي جَمَعَ مَالًا وَعَدَّدَهُ {2}

Aliyekusanya mali na kuyahis­abu.

يَحْسَبُ أَنَّ مَالَهُ أَخْلَدَهُ {3}

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

كَلَّا ۖ لَيُنْبَذَنَّ فِي الْحُطَمَةِ {4}

Si hivyo! Bila shaka Atavurumishwa katika Hutwama.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْحُطَمَةُ {5}

Ni nini cha kukujulisha ni nini Hutwama.

نَارُ اللَّهِ الْمُوقَدَةُ {6}

Ni Moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa?

الَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى الْأَفْئِدَةِ {7}

Ambao unapanda nyoyoni.

إِنَّهَا عَلَيْهِمْ مُؤْصَدَةٌ {8}

Hakika huo utafungiwa juu yao.

فِي عَمَدٍ مُمَدَّدَةٍ {9}

Kwenye maguzo marefu.

Maana

Ole wake kila msingiziaji, msengenyaji!

Msingiziaji na msengenyaji tumeyafasiri kutokana na maneno humaza na lumaza. Imesemekana pia maana ya lumaza ni kutumia jicho, kubinua mdomo na mkono, na lumaza ni kutumia ulimi.

Ni sawa sifa mbili ziwe na maana moja au mbalimbali, lakini yote yanashirikiana katika kuudhi watu na kuwavunjia heshima kwa kauli au kwa vitendo. Mazoewa haya mabaya huwa yanatokana na kujihisi mtu kuwa na upungufu, ndio anajaribu kuu­funika upungufu wake kwa kuwatia ila wenzake.

Imam Ali (a.s.) anasema: “Muovu zaidi wa watu ni yule asiyewamwamini yeyote kwa dhana yake mbaya na asiyeaminiwa na yeyote kwa vitendo vyake vibaya.”

Aliyekusanya mali na kuyahisabu.

Ameyakusanya mali kutokana na halali na haramu na kuyahisabu kila mara kwa kuipenda sana. Hii ndiyo iliyomfanya kuwasingizia na kuwasengenya wengine; akiwa amesahau kwamba haya yote atayaacha muda mchache ujao na atabakiwa na hisabu yake itakyomfuatia.

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

Hivi anadhani kwamba mali hii aliyoikusanya na kuihisabu itamkinga na mauti au kumwokoa na hisabu ya Mwenyezi Mungu na adhabu yake?

Si hivyo! Bila shaka Atavurumishwa katika Hutwama ambayo ni Jahannam itakayowapondaponda wakosefu, (kama linavyofahamisha neno hutwama). Kuvurumishwa ni neno linalotambulisha udhalili.

Ni nini cha kukujulisha ni nini Hutwama, iko zaidi ya unavyofikiria. Ni Moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa. Ni moto wa Mwenyezi Mungu sio moto wa watu na ni moto wa ghadhabu sio moto wa kuni.

Ambao unapanda nyoyoni.

kupanda tumelifasiri kutokana na neno tatwaliu. Imesemekana makusudio ni kujua na maarifa. Lakini kauli hii iko mbali na ufahamu wa kiujumla. Nyoyo ni kinaya cha kuwa Moto utakaopanda na kuunguza kila kiungo katika viungo vya wakosefu. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amehusisha kutaja nyoyo kwa sababu ndio tumbo la ukafiri na lawama.

Hakika huo utafungiwa juu yao, hakuna kukimbia.

Kwenye maguzo marefu. Hiki ni kinaya cha umadhubuti wa kufunikwa.

Umetangulia mfano wake katika Juzu hi tuliyo nayo (90:20).

  • 2178 views

Sura Ya Mia Na Tano: Al-Fil

Imeshuka Makka. Ina Aya 5.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصْحَابِ الْفِيلِ {1}

Je, hukujua namna gani alivy­owafanya Mola wako wenye ndovu?

أَلَمْ يَجْعَلْ كَيْدَهُمْ فِي تَضْلِيلٍ {2}

Je, hakuvifanya vitimbi vyao ni vyenye kupotea?

وَأَرْسَلَ عَلَيْهِمْ طَيْرًا أَبَابِيلَ {3}

Na akawapelekea ndege makundi makundi.

تَرْمِيهِمْ بِحِجَارَةٍ مِنْ سِجِّيلٍ {4}

Wakawatupia mawe ya udon­go mkavu.

فَجَعَلَهُمْ كَعَصْفٍ مَأْكُولٍ {5}

Akawafanya kama majani yaliyoliwa!

Kisa Kwa Ufupi

Kisa cha ndovu kilitokea mwaka aliozaliwa Mtume mtukufu (s.a.w.). Kwa ufupi ni: Baada ya wahabeshi kuishinda Yemen waliikusudia Makka kwa nia ya kuivunja Al-Ka’aba. Basi wakaenda huku wakimtanguliza au kuwatanguliza ndovu.

Walipofika karibu na Makka mahali panapoitwa Al-Mughammas, walishuka na wakampeleka raisi wao, Abraha, kama wanavyomwita wapokezi, kwa makuraishi awape habari kuwa wao hawakuja kupigana nao isipokuwa wamekuja kuivunja Al-Ka’aba, na kama hawatawasumbua na vita basi nao hawana haja na damu yao.

Kabla ya Abrah kutekeleza lengo lake, Mwenyezi Mungu alimtumia jeshi la ndege wakiwatupia vijiwe vidogo, kila kinayempata basi anashikwa na maradhi ya ndui na nyama humpukutika na kuanguka chini, jeshi likaogo­fywa na likakimbia. Abraha naye pia alipatwa na ugonjwa huo, akafia Sanaa.

Dkt Twaha Hussein, katika Kitabu ir-atul-slam, anasema: “Katika tukio hili Abdul Muttwalib, alionyesha subira, ushujaa na uimara kwa namna ambayo hajawahi kuionyesha yeyote katika watukufu wa kikuraishi. Hilo ni kwa kuwa aliwashauri makuraishi waikimbie Makka na watu wake wakamsikiza, lakini yeye alibakia Makka bila ya kuondoka na akasimama mbele ya Al-Ka’aba, akimuomba Mwenyezi Mungu na kumtaka nusra.

Wapokezi wanasema kuwa jeshi liliteka ngamia wa makuraishi, akaja Abdul-Muttwalib kwa Abrah. Alipofika hakumwambia lolote zaidi ya madai ya ngamia wake. Abrah akamdharau na kumwambia: “Mimi nad­hani umekuja kuzungumza nami kuhusu Makka na hii nyumba ambayo mnaitukuza?” Abdul-Muttwalib akamwambia: “Mimi ninakuzungumzia mali yangu ninayoimiliki, lakini hiyo nyumba ina Mlezi wake, ataihami akitaka.”

Basi Mwenyezi Mungu akampelekea, Abraha na jeshi lake, ndege hao waliowatupia mawe ya udongo mkavu ukawafanya kama majani yaliyoli­wa. Makuraishi wakarudi Makka na wakazidi kumtukuza Abdul­Muttwalib, kwa ushujaa, uthabiti na uimara wake.

Maana

Je, hukujua namna gani alivyowafanya Mola wako wenye ndovu?

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.), na swali ni kuelezea hali halisi ilivyo; yaani unajua ewe Muhammad vile Mwenyezi Mungu alivyowafanya wenye ndovu. Hii ni kumtuliza Mtume kwamba aliyewaangamiza watu wa ndovu ana uwezo pia wa kuangamiza wakadhibishaji.

Je, hakuvifanya vitimbi vyao ni vyenye kupotea?

Makusudio ya vitimbi ni kupanga njama. Maana ni kuwa Wahabeshi wali­panga njama mbaya dhidi ya nyumba ya Mwenyezi Mungu tukufu, lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alivipoteza vitimbi vyao na juhudi yao ikaenda bure.

Na akawapelekea ndege makundi makundi.

Wafasiri na wapokezi wanasema yalikuja makundi kwa makundi ya ndege wadogo kutoka baharini, wakawatupia mawe ya udongo mkavu, uliokuwa jiwe.

Akawafanya kama majani yaliyoliwa.

Neno majani tumelitoa kwenye neno Asf ambalo maana yake ni kupeperu­ka. Yameitwa hivyo kwa vile yanapeperushwa. Makusudio ya kuliwa hapa ni kama kuliwa na wadudu.

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Inawezekana uamini kuwa ndege hawa walikuwa ni mbu au nzi waliochukua viini vya magonjwa na kwam­ba mawe haya yalikuwa ni udongo ulio na sumu inayopeperushwa na upepo na kushika kwenye miguu ya wanyama hawa, ikifika kwenye mwili wa mtu mtu kumwambukiza sumu hiyo na kuathiri mwili na kuanguka nyama zake.”

Ilivyo ni kuwa kauli yake, inawezekana uamini kuwa ndege hawa walikuwa ni mbu au nzi... na kwamba mawe haya yalikuwa ni udongo ulio na sumu, kauli hii haiwezi kuwa ni sawa ila ikitegemea kwenye dalili mkataa au ushahidi wa kuonekana, kulingana na maneno yake huyo huyo Sheikh Muhammad Abduh.

Lau angelisema: Inawezekana uone kuwa kuna uwezekano, angalau inge­likuwa iko karibu na usawa.

Ama sisi tunachukua dhahiri ya matamko, kama walivyofanya waislamu wa mwanzo, maadamu akili hailikatai hilo.

  • 2452 views

Sura Ya Mia Na Sita: Quraysh

Imeshuka Makka Ina Aya 4.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu

لِإِيلَافِ قُرَيْشٍ {1}

Kwa ajili ya kuzowea maku­raishi.

إِيلَافِهِمْ رِحْلَةَ الشِّتَاءِ وَالصَّيْفِ {2}

Kuzowea kwao safari ya kusi na kaskazi.

فَلْيَعْبُدُوا رَبَّ هَٰذَا الْبَيْتِ {3}

Basi wamwabudu Mola wa nyumba hii.

الَّذِي أَطْعَمَهُمْ مِنْ جُوعٍ وَآمَنَهُمْ مِنْ خَوْفٍ {4}

Ambaye amewalisha wasipate njaa na akawasalimisha na hofu.

Maana

Wametofautiana kuhusu Sura hii kuwa je, inajitegemea kama Sura moja peke yake, au inaungana na Sura Fiyl na kuwa sura moja?

Anasema Al-hafidh Al-Kalabiy katika afsir Attashil: “Kauli ya kuwa hizo ni Sura moja inatiliwa nguvu kwamba, kwenye msahafu wa Ubayya bin Kaa’b, hazikutengenishwa. Vile vile Umar alizisoma pamoja katika rakaa moja kwenye Swala ya maghrib.

Hii inaafikiana na kauli ya Shia Imamiya. Na amesema mwenye Dhilal: “Sura hii inaonyesha kuwa ni mwendelezo wa sura iliyo kabla yake, kwa maudhui yake na mazingira yake.

Mwenye kuifanya Sura hii kuwa inaungana na ya kabla yake anasema maneno ‘Kwa ajili ya kuzowea Makuraishi yanaungana na akawafanya kama majani yaliyoliwa, kwa ajili ya kuzowea Makuraishi.
Na mwenye kusema kuwa ni sura inayojitegemea, anasema: Kwa ajili ya kuzowea Makuraishi, basi wamwabudu Mola….
Kwa ajili ya kuzowea makuraishi.

Kuraishi ni jina la kabila la waraabu wa kizazi cha Nadhr bin Kinana. Katika baadhi ya tafsiri imesemwa kuwa neno Kuraishi limetokana na neno qarash lenye maana ya biashara. Waliitwa hivyo kwa vile walikuwa wafanyibiashara; hilo likiashiriwa na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukukufu:

Kuzowea kwao safari ya kusi na kaskazi.

Katika karne ya sita (A.D.) wakazi wa Makka walikuwa makundi matatu: La kwanza likuwa ni Makuraishi waliokuwa na haki zote. La pili ni marafi­ki wa Makuraishi, lililokuwa la waarabu wengineo. Na la tatu lilkuwa la watumwa waliokowa hawamiliki chochote hata nafsi zao pia.

Makuraishi walikuwa na misafara miwili ya kibiashara kila mwaka: msa­fara wa kwenda Yemen katika majira ya baridi na msafara wa kwenda Sham katika majira ya joto.

Walikuwa wakienda na kurudi kwa amani kwenye misafara yao, bila ya kuguswa na yeyote kwa uovu, kwa vile walikuwa ni wakazi wa Makka walio jirani na nyumba ya Mwenyezi Mungu, tukufu; kama walivyosema wafasiri au kama tunavyodhania sisi, kwamba waarabu ni lazima waje wahiji Makka; wakiogopa kama watauchokoza msafara wa makuraishi basi watakuja walipizia kisasi watakapokuja kwenye mji wao.

Wapokezi wanasema kuwa ni katika misafara hii ndio Muhammad (s.a.w.) aliwahi kusafiri na ami yake Abu Twalib kwenda Sham. Wakati huo umri wake mtukufu ulikuwa ni miaka 12, lakini hakuwahi kufika naye Sham, bali walirudi haraka Makka kutokana na ushauri wa mtawa wa kinaswara (mkiristo) aliyemuusia kumlinda na njama za Mayahudi na wanaswara.

Vile vile wanasema wapokezi kuwa Muhammad (s.a.w.) alitoka na ami yake Zubeir kwenda Yemen katika msafara wa kusi, wakati akiwa na umri wa miaka ishirini na kidogo; na msafara huo ulikuwa kabla ya kwenda Sham na mali ya Khadija.

Basi wamwabudu Mola wa nyumba hii.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anawaamuru waache kuaabudu masanamu na wamwabudu mmoja aliye pekee, ambaye amewalisha wasipate njaa na akawasalimisha na hofu.

Katika Aya hii Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anawakumbusha waasi wa kiku­raishi, wanaoabudu masanamu, badala ya Mwenyezi Mungu, na kumkad­hibisha Nabii wake mtukufu Muhammad (s.a.w.), tukio la ndovu jinsi alivyowaokoa Mwenyezi Mungu na Abrah na jeshi lake. Lau si fadhila zake Mwenyezi Mungu wangelikuwa wao ndio kama majani yaliyoliwa badala ya watu wa ndovu.

Vile vile anawakumbusha jinsi alivyowaneemesha Mwenyezi Mungu kwa riziki kwa sababu ya misafara miwili, ambayo kama si hiyo wangelikufa na njaa; kwa sababu wao wako katika bonde lisilokuwa na mimea. Fauka ya hayo amewafanya wawe na amani na utulivu kwa mali yao na roho zao katika misafara yao.

Lau si fadhila yake Mwenyezi Mungu Mtukufu. Watu wangeliwapora kila mahali. Hivi baada ya yote haya wanaweza kuabudu masanamu, kuzikufuru neema za Mwenyezi Mungu na kumkadhibisha Mtume wake mtukufu? Kweli mtu ni dhalimu mkubwa wa nafsi yake na mjinga sana.

  • 3146 views

Sura Ya Mia Na Saba: Al-Maa’un

Imeshuka Makka. Imesekana si hivyo. Ina Aya 7.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu

أَرَأَيْتَ الَّذِي يُكَذِّبُ بِالدِّينِ {1}

Je, umemwona ambaye anakadhibisha dini?

فَذَٰلِكَ الَّذِي يَدُعُّ الْيَتِيمَ {2}

Huyo ni ambaye humsukuma yatima.

وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ {3}

Wala hahimizi kumlisha mask­ini.

فَوَيْلٌ لِلْمُصَلِّينَ {4}

Basi ole wao wanaoswali.

الَّذِينَ هُمْ عَنْ صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ {5}

Ambao wanasahau Swala zao.

الَّذِينَ هُمْ يُرَاءُونَ {6}

Ambao wanafanya ria.

وَيَمْنَعُونَ الْمَاعُونَ {7}

Na wanazuia msaada.

Maana

Je, umemwona ambaye anakadhibisha dini?

Maana ya kumuona ni kumjua. Tamko ni la swali na maana yake ni kukanusha yaliyotokea. Maneno yanaelekezwa kwa wote; kwa sababu Sura hii kwa ujumla wake inajulisha udugu baiana ya dini na matendo na kuzingatia kuwa ni sehemu yake isiyoachana. Kisha dini inawakana wale wanaosifika na uovu ufuatao:

Huyo ni ambaye humsukuma yatima.

Makusudio ya kumsukuma hapa ni kumzuilia haki yake iwe ni kwa nguvu au bila ya nguvu, kumdharau au kumuudhi au kwa kumkalia kwa namna yoyote ya dhulma. Makusudio ya yatima hapa ni kila mdhaifu asiyejiweza; awe mdogo au mkubwa. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amehusisha kumtaja yatima kwa vile ni mdhaifu zaidi ya wadhaifu.

Maana ni kuwa kila dhalimu ni kafiri mwenye kukadhibisha dini ya Mwenyezi Mungu; hata kama ataswali na kufunga. Kwa sababu dini ya Mwenyezi Mungu haitosheki na mambo ya dhahiri na nembo; isipokuwa pamoja na takua na kujizuia na yaliyo haramu.

Ni kweli kuwa kila mwenye kusema: ailaha illa llah uhammadur-rasulullah, anachukuliwa kuwa ni mwislamu duniani, lakini hukumu yake Akhera ni ya kafiri. Tazama Juz. 19 (25:55).

Wala hahimizi kumlisha maskini.

Makusudio ya kuhimiza hapa ni kusaidiana na wengine kuwashughulikia wasiojiweza. Makusudio ya masikini ni kila asiyemiliki sababu za riziki na kutekeleza mahitaji. Umetangulia mfano wake katika Juz. 29 (69:34) na Juzuu hii tuliyo nayo (89:18).

Basi ole wao wanaoswali, ambao wanasahau Swala zao.

Kusahau hapa sio makusudio, kwa sababu mwenye kusahau hana majuku­mu kiakili na kisharia. Mtume mtukufu (s.a.w.) anasema: “Umma wangu umeondolewa kukosea na kusahau.” Kwa hiyo basi hapana budi kuchuku­lia kusahau kwa maana nyingine. Maana yenyewe Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anayabainisha kwa kusema:

Ambao wanafanya ria na wanazuia msaada.

Yaani hawasaidii kwa kujikurukubisha kwa Mwenyezi Mungu bali wanafanya kwa kujionyesha kwa watu. Ujumla wa maana ni kuwa wenye kusahau Swala zao wanaswali, lakini kwa ria na unafiki na kuwahofia watu sio kumhofia Mwenyezi Mungu. Wao wanadhihirisha uzuri na kuficha ubaya.

Hivi ndivyo walivyo katika matendo yao yote; wanajikurubisha kwayo kwa waja wa Mwenyezi Mungu na kujiweka mbali kwayo na Mwenyezi Mungu Mtukukufu na radhi zake; hata msaada pia hawautoi ila kwa ria na unafiki.

Hii inatufichulia kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ametaja msaada kufanan­isha ria yao katika kila kitu, sio katika swala tu, bali hata kwenye mambo madogo kama kuazima.

  • 2204 views

Sura Ya Mia Na Nane: Al-Kawthar

Imeshuka Makka Ina Aya 3.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

إِنَّا أَعْطَيْنَاكَ الْكَوْثَرَ {1}

Hakika tumekupa wingi sana.

فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ {2}

Basi swali kwa ajili ya Mola wako na uchinje.

إِنَّ شَانِئَكَ هُوَ الْأَبْتَرُ {3}

Hakika mwenye kukubughud­hi, yeye ndiye mwenye kuishi­wa.

Maana

Hakika tumekupa wingi sana.

Neno wingi sana tumelitoa kwenye neno kawthar lenye maana ya uzaidi wa wingi. Wametofautiana kuhusu wingi huu wa zaidi. Lililo karibu zaidi na ufahamu ni lililonukuliwa na wafasiri, kutoka kwa Ibn Abbas na Said bin Jubayr, kwamba makusudio ya wingi sana ni yote yale aliyomneeme­sha Mwenyezi Mungu Mtume wake mtukufu. Kwa sababu neno kawthar linatumika kwa wingi wa wingi usiokuwa na ukomo wala udhibiti.

Saidi aliambiwa kwamba watu wanasema kuwa kawthar ni mto katika Pepo.
Akasema: “Hakika mto huu ni katika heri nyingi alizompa Mwenyezi Mungu Muhammad (s.a.w.), lakini waasi wapenda anasa wanadharau heri hizi nyingi na hawezioni ni chochote; huku wakasema kuhusiana na Mtume mtukufu:

 لَوْلَا أُنْزِلَ عَلَيْهِ كَنْزٌ {12}

“Mbona hakutermshiwa hazina?” Juz. 11 (11:12).

Basi swali kwa ajili ya Mola wako na uchinje.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kumkumbusha Nabii wake mtukufu, neema alizompa, sasa anamwamrisha kushukuru na kwamba swala yake na dhabihu zake ziwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake.

Kuna riwaya nyingine inayosema kuwa makusudio ya neno wanhar tulilo­lifasiri kwa maana ya uchinje, hapa lina maana kuinua mikono hadi kufika mkabala wa shingo wakati wa kuelekea Qibla kwenye Swala.

Hakika mwenye kukubughudhi, yeye ndiye mwenye kuishiwa.

Hii ni jumla nyingine inayoanza upya. Wametofautiana kuhusu aliyeishi­wa. Kauli iliyo karibu zaidi ni kuwa adui wa Muhammad (s.a.w.) ni bure tu asiyekuwa na athari yoyote wala utajo wowote. Lakini utajo wake Mtume una athari na utabakia kwa kubakia Mwenyezi Mungu.

Wafasiri wengi wamesema kuwa mmoja wa washirikina alisema: “Muhammad ameishiwa hana mtoto,” ndio Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akampa habari Mtume wake kuwa mwenye kusema hivi ndiye aliyeishiwa hata kama ana watoto. Hakuna kizuizi cha kuchanganya maana zote mbili.

Sheikh Muhammad Abduh anasema: “Mwenye kumbughudhi Muhaammad hakuubughudhi utu wa Mtume (s.a.w.) kwa sababu alikuwa ni kipenzi cha nyoyo; isipokuwa waliobughudhi walichukia uongofu aliokuja nao…Na walioishiwa wanaingia wale walioacha Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kushikamana na dhana na kauli za wasiokuwa maa­sumu… wakijiambatanisha na bid’a katika dini.

Wanapotajiwa Qur’an wanapeta vichwa vyao…si ajabu kuwa ghadhabu ya Mwenyezi Mungu inawafuata kila mahali na wanapatwa na udhalili baada ya udhalili wakiwa hawatambui; bali wanacheka.”

  • 3786 views

Sura Ya Mia Na Tisa: Al-Kafirun

Imeshuka Makka Ina Aya 6.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu

قُلْ يَا أَيُّهَا الْكَافِرُونَ {1}

Sema: Enyi makafiri!

لَا أَعْبُدُ مَا تَعْبُدُونَ {2}

Siabudu mnachokiabudu.

وَلَا أَنْتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ {3}

Wala nyinyi si wenye kuabaudu ninayemwabudu.

وَلَا أَنَا عَابِدٌ مَا عَبَدْتُمْ {4}

Wala mimi si mwenye kuabudu mlichokiabudu.

وَلَا أَنْتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ {5}

Wala nyinyi si wenye kuabudu ninayemwabudu.

لَكُمْ دِينُكُمْ وَلِيَ دِينِ {6}

Mna dini yenu nami nina dini yangu.

Maana

Sema: Enyi makafiri! Siabudu mnachokiabudu, wala nyinyi si wenye kuabaudu ninayemwabudu.

Inasemekana kuwa watu katika makafiri wa Kikuraishi walimwendea Nabii (s.a.w.) na kumwambia: wewe ni bwana wa Bani Hashim na mwana wa mabwana wakubwa wao, haitakikani wewe kuzisafihi fikra za watu wako, lakini tutaabudu sisi Mungu wako kwa muda wa mwaka na wewe uabudu mungu wetu mwaka mmoja; ndio ikashuka Aya hii.

Unaweza kuuliza nini makusudio ya kukaririka huku? Kwani kauli yake wala siabudu mnachokiabudu si ni sawa na kauli yake: wala mimi si mwenye kuabudu mlichokiabudu?

Hakuna tofauti isipokuwa ile ni jumla ya isimu na hii ni jumla ya kitendo. Tena kuna jumla nyingine imerudiwa kwa herufi zake.

Wala nyinyi si wenye kuabudu ninayemwabudu.

Sasa itakuwaje?

Wamelijibu hilo kwa jawabu mbali mbali; ikiwemo ile ya mwenye ajmaul bayan kwamba ya kwanza ni ya muda wa sasa na ya pili ni ya muda ujao. Lakini ieleweke kuwa zote mbili zinakubaliana na hali ya sasa na ya baadae, kwa hiyo inahitajia dalili.

Jibu jingine ni lile alilolisema Abu Muslim na akalichagua Sheikh Muhammad Abduh, kwamba ya kwanza ni anayeabudiwa na ya pili ni ibada yenyewe; yaani muabudiwa wangu sio muabudiwa wenu na ya pili iwe ibada yangu sio ibada yenu. Pia hapa ieleweke kuwa hakuna ibada bila ya muabudiwa na kwamba kuta­ja moja kunatosheleza kutaja nyingine.

Jibu jingine ni kuwa kukaririka huku kunafahamisha msisitizo, na kila inapohitajika kusisitiza basi kukaririka ni vizuri zaidi. Sisi tuko pamoja na rai hii.

Mna dini yenu nami nina dini yangu.

Yaani nyinyi mna kufuru na shirki na mimi nina ikhlasi na tawhid, wala sina mfungamano wowote na kile mnachokiabudu, na nyinyi ni hivyo hivyo kwangu. Hili ni kemeo na hadhari; mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukukufu:

 أَنْتُمْ بَرِيئُونَ مِمَّا أَعْمَلُ وَأَنَا بَرِيءٌ مِمَّا تَعْمَلُونَ {41}

“Nyinyi hamna jukumu kwa ninayoyatenda, na mimi sina jukumu kwa mnayoyatenda.”
Juz. 11 (10:41).
  • 3008 views

Sura Ya Mia Na Kumi Na Moja: An-Nasr

Imeshuka Madina. Ina Aya 3.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu

إِذَا جَاءَ نَصْرُ اللَّهِ وَالْفَتْحُ {1}

Itakapokuja nusra ya Mwenyezi Mungu na ushindi.

وَرَأَيْتَ النَّاسَ يَدْخُلُونَ فِي دِينِ اللَّهِ أَفْوَاجًا {2}

Na ukawaona watu wanaiingia katika dini ya Mwenyezi Mungu makundi makundi.

فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَاسْتَغْفِرْهُ ۚ إِنَّهُ كَانَ تَوَّابًا {3}

Basi zisabihi sifa za Mola wako na umtake maghufira; hakika yeye ni Mwingi wa kukubali toba.

Maana

Itakapokuja nusra ya Mwenyezi Mungu na ushindi.

Jamhuri ya wafasiri imesema kuwa hii ni bishara kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwa Nabii wake mtukufu ya ushindi wa kuiteka Makka na kuwashinda maadui wa Mwenyezi Mungu na wake.

Na ukawaona watu wanaiingia katika dini ya Mwenyezi Mungu makundi makundi.

Dini ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu. Makabila mengi ya waarabu yalikuwa yakingojea kutekwa Makka ndio yaingie kwenye Uislamu. Basi Mwenyezi Mungu alipompa ushindi huo Mtume wake, Uislamu ulienea Bara arabu yote kwa muda mchache, na Uislamu ukaleta maadili mapya kwa waarabu, ukawaunganisha baada ya kuwa wametengana na ukawapa nguvu baada ya kuwa na udhalili. Ukawafanya wawe ni umma unaooneka na ukiwa na mwelekeo wa heri na utengeneo.

Basi zisabihi sifa za Mola wako na umtake maghufira.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alimwamrisha Mtume wake amsabihi na kumsi­fu baada ya kuona ushindi, kuwa ni shukrani kwa neema za Mwenyezi Mungu Mtukukufu na kuitakasa nafsi isilewe na ushindi na furaha. Hakuna mwenye shaka kwamba lengo la hilo ni kujipamba kwa maadili ya Qur’an na kupata mawaidha yake. Imam Ali (a.s.) anasema: “Ukimmudu adui yako, kufanye kumsamehe ni shukrani ya huko kummudu.”

Hakika yeye ni Mwingi wa kukubali toba.

Kumkubalia toba Mwenyezi Mungu maasumu maana yake ni rehema kwake na radhi, na kumkubalia toba mwenginewe ni kumsamehe. Yametangulia maelezo kuhusiana na hilo katika Juz. 11 (9:117).

Kuna mapokezi yanayosema kuwa Mtume (s.a.w.) alisema iliposhuka Sura hii: “Ni tanzia yangu mimi mwenyewe.” Binti yake Fatima, aliposikia hivyo akalia. Akamwambia: usilie, kwani wewe ni wa kwanza kuungana nami. Basi akacheka. Kama kwamba Mtume (s.a.w.) alijua kutokana na Sura hii kuwa muda wake wa kuishi umeisha na kazi yake imekwisha baada ya kupatikana ushindi na kuingia watu katika dini ya Mwenyezi Mungu makundi kwa makundi.

  • 2981 views

Sura Ya Mia Na Kumi Na Mbili: Al-Lahab

Imeshuka Makka Ina Aya 5.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

تَبَّتْ يَدَا أَبِي لَهَبٍ وَتَبَّ {1}

Imeangamia mikono ya Abu Lahab na yeye ameangamia.

مَا أَغْنَىٰ عَنْهُ مَالُهُ وَمَا كَسَبَ {2}

Haitamfaa mali yake na ali­chokichuma.

سَيَصْلَىٰ نَارًا ذَاتَ لَهَبٍ {3}

Atauingia moto wenye miali.

وَامْرَأَتُهُ حَمَّالَةَ الْحَطَبِ {4}

Na mkewe mchukuzi wa kuni.

فِي جِيدِهَا حَبْلٌ مِنْ مَسَدٍ {5}

Shingoni mwake mna kamba iliyosokotwa.

Maana

Imeangamia mikono ya Abu Lahab na yeye ameangamia.

Mikono ya Abu Lahab ni kinaya cha mwenyewe hasa; kama inavyosemwa: Mikono ina majukumu ya ilichokichukua mpaka itekeleze. Kwa sababu mikono ni udhihirisho wa nguvu na ni chombo cha kazi.

Jina kamili la Abu Lahab ni Abdul Uzza bin Abdul-Muttwalib bin Hashim. Ni ami yake Mtume (s.a.w.), lakini alikuwa ndiye adui yake mkubwa zaidi.

Wafasiri na wapokezi wamesema kuwa Mtume (s.a.w.) siku moja alipanda kilima cha swafaa akawaita watoto wa kuraishi, wakakusanyika akiwemo Abu Lahab. Akasema: Hivi nikiwaambia kuwa jeshi la wapanda farasi liko hapo bondeni linataka kuwashambulia mtanisadiki? Wakasema: ndio huja­jaribu kutuambia uwongo.

Akasema: Basi mimi ninawaonya na yule ambaye ana adhabu kali. Abu Lahab akasema: Hivi umekutukusanya kwa hili? Uangamie wewe. Ndipo ikashuka Sura hii.

Haitamfaa mali yake na alichokichuma.

Kesho kwenye hisabu na malipo haitafaa mali wala cheo au watoto. Yote hayo yatakuwa ni hoja juu yake na maangamizi.

Atauingia moto wenye miali.

Haya ndiyo malipo yake na makazi yake ni Jahannam, mwishilio mbaya.
Na mkewe mchukuzi wa kuni.

Mke wa Abu Lahab ni Ummu Jamil bint Harb, dada yake Abu Sufyani na shangazi yake Mua’wiya. Kuni ni kinaya cha shari na dhambi zitakazom­peleka motoni. Alikuwa na uadui na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) kwa hali ya juu sana; akitembea kumfitini na watu ili kuzima mwito wake.

Uhusiano wa moto na kuni unajulikana. Zaidi ya hayo waarabu walikuwa wakimpa jina la mbeba kuni mtu aliyekuwa mfitini, kwa sababu anawasha moto wa fitina. Na imesemekana alikuwa akikusanya miba na kuitawanya kwenye njia anayopita Mtume.

Shingoni mwake mna kamba iliyosokotwa.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kumpa sifa ya mbeba kuni, sasa anam­pa picha hii ya ajabu. Anafunga kuni kichwani mwake kwa ncha moja ya kamba na ncha nyingine iko shingoni mwake. Kama kwamba kuni ndio taji na kamba ni mkufu.

Unaweza kuuliza: waliompiga vita na kumuudhi ni wengi katika mataghuti wa kikuraishi; kama Uqba bin Abi Mui’t, Abu Jahl, Walid Bin Almughira, A’si bin Wail na wengineo, lakini Qur’an haikuyataja majina yao; kwanini basi hapa ikamuhusu kumtaja Abu Lahab na kumteremshia sura nzima kinyume na wengine?

Sheikh Muhammad Abduh amejibu kuwa Abu Lahab alikuwa ni mpinzani mashuhuri zaidi wa Mtume (s.a.w.) na alikuwa ndiye mwakilishi wa madui. Nabii aliathirika na harakati zake; ndio maana Mwenyezi Mungu akamuhusu kumtaja kinyume na wengine.

Sheikh Muhammad Abduh alimalizia kuifasiri sura hii kwa kusema: Mwenye kukuambia kuwa haifai kuitegemeza hukumu yoyote kwenye kitabu cha Mwenyezi Mungu na sunna ya Nabii wake kwa kiwango cho­chote cha ilimu uliyofikia, bali unatakikana umrudie fulani kwenye kauli yake, basi huyo ni Abu Lahab. Na kila mwanamke anayeenda kuwafitini watu na kufanya ufisadi baina ya watu basi huyo ni mchukuzi wa kuni, shingoni mwake mkiwa na kamba ya kusokotwa.

  • 4173 views

Sura Ya Mia Na Kumi Na Tatu: Al-Ikhlas

Imeshuka Makka Ina Aya 4.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ {1}

Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni mmoja.

اللَّهُ الصَّمَدُ {2}

Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kukusudiwa kwa haja.

لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ {3}

Hakuzaa wala hakuzaliwa.

وَلَمْ يَكُنْ لَهُ كُفُوًا أَحَدٌ {4}

Wala hana anayefanana naye hata mmoja.

Maana

Misingi ya Uislamu ni mitatu: Tawhid, Utume na Ufufuo. Ya kwanza inazalisha sifa zake Mwenyezi Mungu Mtukufu, ya pili inazaa Qur’an na sharia na ya tatu inazaa malipo na hisabu. Sura hii tukufu inaeleza hii ya kwanza.

Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni mmoja katika dhati yake, sifa zake na vitendo vyake.

Hana mshirika katika chochote, wala hafanyi kitu kwa kujiletea manufaa au kujikinga na madhara. Tumezungumzia kwa ufafanuzi zaidi kuhusu Tawhid katika Juz. 5 (4:48-50), kwa anuani ya ‘dalili ya umoja na utatu.’

Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kukusudiwa kwa haja.

Makusudio yake hapa ni kujitosheleza na kila kitu, si mhitaji bali kila kitu kinamhitajia Yeye, kwa sababu yeye ndiye muumba wa kila kitu na ndiye chimbuko.

Hakuzaa.

Hii ni kuwarudi wale wanaodai kuwa Mwenyezi Mungu ana watoto wa kiume au mabinti Maulamaa wa theolojia wanasema: “Lau Mwenyezi Mungu angelikuwa na mtoto, basi angelikuwa na mafungu na kila mwenye mafungu anakuwa na mwisho kwa kuisha mafungu yake. Usawa zaidi ni kusema: Lau Mwenyezi Mungu angelikuwa na mtoto angelikuwa na wa kufanana naye na wa kumrithi.

Kwa sababu mtoto anashabihiana na mzazi wake na anam­rithi: Imam Ali (a.s.) anasema: “Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakuzaliwa akawa na mshirika katika utukufu, wala hakuzaa akawa na mrithi na kufa.”

Wala hakuzaliwa.

Hii ni kumrudi mwenye kudai kwamba kuna miungu waliozaliwa. Lau angelikuwa Mungu amezaliwa angelikuwa na tarehe ya kupatikana kwake. Imam Ali (a.s.) anasema: “Hakuzaa akawa naye ni mwenye kuzaliwa, wala hakuzaliwa akawa na kiwango cha wakati.” Yaani kuweko kwake kuanzia tangu alipozaliwa.”

Wala hana anayefanana naye hata mmoja, si katika kuweko kwake wala dhati yake au sifa zake wala vitendo vyake.

Nilipokuwa nikifasiri Sura hii nilisoma rejea nyingi kuanzia Asfar cha Mulla Sadra hadi tafsiri za kawaida, kama Al-baydhawi.

Nikachunguza sana humo ili nichague kauli zilizo bora zaidi; sikupata kauli ya ufupi zaidi na yenye kuweka wazi kuliko kauli ya Imam Husein (a.s.) alipoulizwa na watu wa Basra kuhusu maana ya neno Swamad, (mwenye kukusudiwa kwa haja) akasema: Mwenyezi Mungu amelifasiri neno hilo kwa kusema: hakuzaa wala hakuzaliwa wala hana anayefanana naye hata mmoja.”

Kutokana na tafsiri hii fupi iliyokusanya maana, inafaa tuseme kuwa maana ya Mwenyezi Mungu ni mmoja ni Mwenye kukusudiwa kwa haja, na maana ya Mwenye kukusudiwa kwa haja ni hakuzaa wala hakuzaliwa, na maana ya hakuzaa wala hakuzaliwa ni hana anayefanana naye hata mmoja.

  • 5439 views

Sura Ya Mia Na Kumi Na Tatu: Al-Falaq

Imeshuka Makka Ina Aya 5.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ {1}

Sema: Najikinga kwa Mola wa asubuhi.

مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ {2}

Na shari ya alivyoviumba.

وَمِنْ شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ {3}

Na shari ya giza la usiku liin­giapo.

وَمِنْ شَرِّ النَّفَّاثَاتِ فِي الْعُقَدِ {4}

Na shari ya wanaopulizia mafundoni.

وَمِنْ شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ {5}

Na shari ya hasidi anapo­husudu.

Maana

Sema: Najikinga kwa Mola wa asubuhi.

Neno asubuhi tumelifasiri kutoka na neno falaq lenye maana ya kupasua. Neno hili hutumika kwa maana ya viumbe wote, kwa sababu Mwenyezi Mungu amevitoa kutoka kutokuwepo; kama kwamba vilikuwa vimefichi­ka akavifunua.

Pia hutumika, neno hili, kwa maana ya asubuhi, kwa sababu asubuhi inaondoa giza. Hayo ndiyo makusudio yake hapa kama walivyose­ma wafasiri wengi. Kauli hii inatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu pale aliposema kwa kulitumia neno hili falaq:

فَالِقُ الْإِصْبَاحِ {96}

“Ndiye mpambazuaji wa asubuhi.” Juz. 7 (6:96).

Vyovyote iwavyo ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni Mola wa asubuhi na Mola wa viumbe wote, na amemwarisha Mtume wake kumtaka hifad­hi.

Na shari ya alivyoviumba; yaani na shari ya kila chenye shari; awe mtu au asiyekuwa mtu. Hakuna kiumbe chochte ila kina maandalizi kamili ya kufanya heri au shari - nguvu chanya na hasi.

Wala hakuna katika vilivy­opo kilicho na heri tupu, isipokuwa muumba wa vilivyoko. Tazama Juz. 5 (4:78-79) kifungu cha ‘Haiwezekani kuongeza zaidi ya ilivyo.’

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kumwamuru Mtume wake mtukufu kujihifadhi na shari ya kila mwenye shari, hapa amehusisha kuyataja aliy­oyaashiria, kama ifuatavyo:

Na shari ya giza la usiku liingiapo.

Makusudio ya shari ya usiku hapa ni mambo ya kuchukiza yanatokea usiku; kama kupanga njama, kuiba, kuua, ufasiki na mengineyo.

Na shari ya wanaopulizia mafundoni.

Makusudio ya kupuliza hapa sio uchawi au wachawi wanaume wala wanawake; kama walivyosema wafasiri wengi. Isipokuwa makusudio ni kila mwenye kuifanyia mazingaombwe misingi na misimamo, ni sawa awe atafanya kiini macho kwa kudai kuwa anawatumia majini, kwa uwongo na unafiki au asifanye hivyo. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amehusisha kutaja hivyo hapa, kwa sababu mazingaombe na mauzauza ni anuani ya unafiki.

Wapokezi wamepokea kutoka kwa Aisha kwamba myahudi aliyeitwa Labid bin Al-asam alimroga Mtume (s.a.w.) na akaathirika mpaka akawa anaona anafanya kitu kumbe hafanyi, na kwamba Sura hii ilishuka kwa sababu hiyo.

Riwaya hii ni wajibu kuitupilia mbali kisharia na kiakili. Kiakili ni kuwa Nabii ni maasumu, hatamki isipokuwa wahyi, kwa hiyo itakuwa muhali kwake kufikiria kuwa anapewa wahyi kumbe hapewi wahyi. Ama kisharia ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameukadhibisha uchawi na watu wake, pale aliposema:

 فَإِذَا حِبَالُهُمْ وَعِصِيُّهُمْ يُخَيَّلُ إِلَيْهِ مِنْ سِحْرِهِمْ أَنَّهَا تَسْعَىٰ {66}

 وَلَا يُفْلِحُ السَّاحِرُ حَيْثُ أَتَىٰ {69}

“Mara kamba zao na fimbo zao zikaonekana, kwa uchawi, kuwa zinak­wenda mbio... na mchawi hafanikiwi popote aendapo.” Juz. 16 (20:66,69).

Vile vile amewakadhibisha washirikina waliompa Mtume sifa ya uchawi:

 إِذْ يَقُولُ الظَّالِمُونَ إِنْ تَتَّبِعُونَ إِلَّا رَجُلًا مَسْحُورًا {47}

“Wanaposema hao madhalimu: Nyinyi hamfuati isipokuwa mtu aliyerog­wa.” Juz. 15 (17:47).

Tazama tuliyoyaandika kuhusu uchawi na hukumu yake katika Juz. 1 (2:102) na Juz. 9 (7:113) kwa anuani ya ‘Uchawi.’

Ya kushangaza ni yale aliyoyanukuu Sheikh Muhammad Abduh kutoka kwa waigaji wengi, kama alivyowaita mwenyewe, pale waliposema: “Imekua sahihi habari ya kuwa uchawi uliathiri nafsi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) na mwenye kukana hivyo atakuwa ameleta bid’a katika dini, kwa sababu Qur’an imeelezea usahihi wa uchawi.”

Sheikh Muhammad Abduh aliongezea kwenye kauli hiyo kwa kusema: “Angalia jinsi waigaji wanavyoibadilisha dini sahihi kwenye bid’a, waki­toa hoja kwa Qur’an, iliyoukana uchawi, kwa kuthibitisha uchawi uliomwathiri Mtume wa Mwenyezi Mungu, sawa na walivyosema washirikina: Huyo ni mtu aliyerogwa.

Na shari ya hasidi anapohusudu.

Hasidi ni yule anayetamani neema aliyo nayo mwingine imwondokee na awe nayo yeye. Hadith inasema: “Hasidi anahusudu na mumin anakuwa na ari.” Yaani anatamani awe na neema kama aliyo nayo mwenzake, lakini hatamani imwondokee huyo mwenzake.

Husuda ni mama wa maovu mengi; kama chuki, lawama, uwongo, kusen­genya, fitina, vitimbi na hadaa, kwa kujaribu kila njia ili mwingine aon­dokewe na neema aliyo nayo. Ndio maana Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akamwamuru Mtume wake mtukufu ajilinde na shari ya hasidi.

Hapa inatubainikia kuwa makusudio ya shari ya hasidi na makusudio yake mabaya pamoja na kauli na vitendo vyake, sio jicho; kama walivyosema wafasiri wengi. Ya kushangaza ni yale waliyoyaandika baadhi yao katika tafsiri kuwa kulikuwa na mtu mmoja aliyekuwa mashuhuri kwa kuwadhu­ru watu kwa jicho lake mpaka ikawa watu wanamkodisha kwa lengo hilo.
Siku moja alikodishwa na mwanamke ili amhusudu hasimu wake na amuue kwa jicho lake. Akaenda naye hadi kwa huyo mtu na kumwambia ndiye huyu basi mhusudi. Hasidi akamwambia: “Macho yako ni mazuri sana!” Basi alipomaliza tu maneno yake yule mwanamke akapofuka.

  • 5058 views

Sura Ya Mia Na Kumi Na Nne: An-Nas

Imeshuka Madina Ina Aya 6.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ 

Kwa jina Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ {1}

Sema: Najikinga kwa Mola wa watu.

مَلِكِ النَّاسِ {2}

Mfalme wa watu.

إِلَٰهِ النَّاسِ {3}

Mungu wa watu.

مِنْ شَرِّ الْوَسْوَاسِ الْخَنَّاسِ {4}

Na shari ya mwenye kutia wasiwasi mwenye kurejea nyuma.

الَّذِي يُوَسْوِسُ فِي صُدُورِ النَّاسِ {5}

Anayetia wasiwasi katika vifua vya watu.

مِنَ الْجِنَّةِ وَالنَّاسِ {6}

kutokana na majini na watu.

Maana

Sema: Ninajikinga kwa Mola wa watu, Mfalme wa watu Mungu wa watu

Maneno yanaelekezwa kwa Nabii (s.a.w.), lakini wanakusudiwa watu, kwa sababu Nabii hakimbilii wala hatakimbilia isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu peke yake.

Neno Mola linatumika kwa mfalme, bwana mwenye kuneemesha, neno mfalme linatumika kwa maana ya mtawala na mwenye uweza, na neno Mungu linatumika kwa Muumbaji, mwanzilishi mwenye kudhibiti na mwenye kutoa.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni Muumba wa watu, Mwenye kuneemesha Mwenye kuangilia mambo yao. Kwa hiyo ndiye mwenye kus­tahiki kuabudiwa na kumtaka hifadhi Yeye peke yake.

Unaweza kuuliza: Si Mwenyezi Mungu ni Muumba na Mfalme wa kila kitu, kwa nini amehusisha kutaja kuwa ni wa watu?

Jibu: kwa sababu watu ndio waliomtilia shaka Muumba wao, wakazikufu­ru neema zake na wakamtaka msaada mwinginewe, au wamekuwa ni wenye kupituka mipaka zaidi kuliko viumbe wengine kwa ujumla; ndio akawahusu wao kuwataja, ili waongoke.

Na shari ya mwenye kutia wasiwasi.

Wasiwasi ni sauti ya ndani inayojificha. Makusudio yake hapa ni wahaka wa moyo kutokana na fikra mbovu zinazopinga haki na njia yake. Hakuna yeyote asiyekuwa na mazungumzo ya nafsi na wasiwasi, isipokuwa aliye­hifadhiwa na Mwenyezi Mungu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hamchukulii mja kwa wasiwasi ila kama utaji­tokeza kwenye kauli au kitendo. Mtume (s.a.w.) amesema: “Kila moyo una wasiwasi, ukipasua hijabu ya moyo na kutamkwa na ulimi, basi mja atachukuliwa hatua, na kama hautapasua hijabu ya moyo wala usitamkwe na ulimi, basi hakuna ubaya.”

Mwenye kurejea nyuma.

Makusudio ya wasifa huu ni kwamba mtu akitanabahi wasiwasi wa kishetani na kumtaka hifadhi Mwenyezi Mungu kwa ikhlasi, basi hum­wondokea na kujificha.

Anayetia wasiwasi katika vifua vya watu, kutokana na majini na watu.

Dhahiri ya Aya inafahamisha kwa uwazi kuwa wenye kutiwa wasiwasi ni aina moja nao ni watu tu, lakini wanaotia wasiwasi ni aina mbili: majini na watu. Wasiwasi unaotoka kwa mtu ni kama kumpambia kosa na kumhadaa. Hili liko wazi na linakuwa mara nyingi.

Ama vipi jinni anavy­omtia wasiwasi mtu, Mwenyezi Mungu ndiye anayejua zaidi. Inawezekana kuwa makusudio ya wasiwasi wa jini kwa mtu ni mazungumzo ya ndani ya nafsi yake mwenyewe ambayo hayakutokana na wengine.

Vyovyote litakavyokuwa chimbuko la wasiwasi, lakini muhimu ni mja kumkimbilia Mola wake na kumtaka hifadhi na kila shari ya wasiwasi; iwe imetokana na yeye mwenyewe au na mwinginewe.

Imemalizika tafsiri hii jioni ya mwezi 15 Jamadil-Akhar 1390 (A.H.) sawa na 18 April 1970 (A.D.) Kazi hii imenichukua miaka mine mfululizo wa usiku na mchana.

Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu aliyenisaidia kuifasiri Qur’an yake, na kunifanyia wepesi ufafanuzi na ubainifu wake. Ni Yeye pekee mwenye kuombwa kunifanya niwe katika wenye kushikamana na kamba yake na kuifanya ni akiba siku ya kufanyiwa akiba na kufunuliwa siri, na anizidishie fadhila zake na hisani yake… Hakika yeye ni Manani aliye mkarimu.

Na rehema na amani zimshukie Muhammad na kizazi chake kitakatifu. Nami namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kukamilisha tarjuma hii kutoka kwenye lugha ya Kiarabu, leo Mwezi 20 Dhulhijja 1430 AH (8-12-2009) -Mtarjumu

  • 4963 views

Source URL: https://www.al-islam.org/al-kashif-juzuu-ya-thalathini-muhammad-jawad-mughniyya#comment-0

Links
[1] https://www.al-islam.org/person/muhammad-jawad-mughniyya
[2] https://www.al-islam.org/organization/al-itrah-foundation
[3] https://www.al-islam.org/printpdf/book/export/html/36558
[4] https://www.al-islam.org/printepub/book/export/html/36558
[5] https://www.al-islam.org/printmobi/book/export/html/36558
[6] https://www.al-islam.org/person/hassan-mwalupa