Aya 31 – 45: Hamtapenya Ila Kwa Madaraka
Maana
Tutawakusudia enyi wazito wawili.
Makusudio ya kuwakusudia hapa ni kuwahisabu, na hicho ni kiaga kwa kila mwenye kufanya dhambi katika wazito wawili ambao ni watu na majini.
Katika Bahru Al-muhit cha Abu hayan Al-andalusi imeelezwa: “Wameitwa watu na majini kuwa ni wazito kwa sababu ya uzito wao juu ya ardhi. Katika Hadith limetumika neno hilo pale iliposemwa: ‘Hakika mimi ninawachia vizito viwili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu, Ahlu bayt wangu,’ vimeitwa hivyo kwa sababu ya utukufu wao.”
Basi ni ipi katika neema ya Mola wenu mnayoikanusha nyinyi wawili?
Je, ni uweza wake wa kufufua na kuhisabu au ni nini? Hisabu na malipo ni katika neema kubwa kwa viumbe; vinginevyo mwenye kudhulumiwa angelikuwa na hali mbaya zaidi kuliko aliyedhulumu.
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa madaraka.
Kabisa hakuna kuokoka na kukutana na Mwenyezi Mungu ila kwa tawfiki inayotoka kwake kwenye toba na kujing’oa kwenye dhambi.
Haya ndio makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘Ila kwa madaraka.’ Kwa sababu toba ni ngome inayomkinga mwenye kutubia kwa ikhlasi na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na adhabu yake.
Basi ni ipi katika neema ya Mola wenu mnayoikanusha nyinyi wawili?
Je, ni uweza wake kwenu au ni hadhari yake au mengine?
Mtapelekewa muwako wa moto na ufukizo; wala hamtanusurika.
Wamesema kuwa muwako hapa, lililofasiriwa kutokana na neno shuwadh, ni muwako wa moto bila ya moshi. Na ufukizo, lililotokana na nuhas ni moshi bila ya moto. Vyovyote iwavyo, maana yanayopatikana kutokana na Aya ni kuashiria vituko vya kiyama na machngu yake, na kwamba mkosefu hataokoka na machungu na vituko hivi kwa uombezi wala usaidizi.
Basi ni ipi katika neema ya Mola wenu mnayoikanusha nyinyi wawili?
Je, ni adhabu ya mwenye kupituka mipaka au ni nini?
Itakapopasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
Mbingu na vilivyomo ndani yake miongoni mwa sayari vitayeyuka kama yanavyoyeyuka mafuta kwenye moto na rangi ya myeyuko huu itakuwa kama wekundu wa waridi.
Lengo la kufananisha huku na mengineyo yaliyokuja katika Aya nyingine ni kuashiria kuharibika ulimwengu na kubomoka kwake Siku ya Kiyama.
Basi ni ipi katika neema ya Mola wenu mnayoikanusha nyinyi wawili?
Je, ninani dhalimu mkubwa na muovu zaidi kuliko yule mwenye kukadhibisha ukweli na akaikalia juu haki?
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
Tukiunganisha Aya hii na ile isemayo: “Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa” Juz. 23 (37:24), inatubainikia kuwa Siku ya Kiyama kuna sehemu watu wataulizwa yale waliyokuwa wakiyafanya na sehemu nyingine hakutakuwa na maswali wala majibu, bali ni kungoja maswali na hisabu. Tazama Juz. 22 (36:55-68).
Basi ni ipi katika neema ya Mola wenu mnayoikanusha nyinyi wawili?
Je, ni kwa kusimama kuonyeshwa hisabu au ni kusimama kuingoja? Yote hayo ni dhiki na uchungu, hilo halina shaka, lakini malipo ni katika neema itokayo kwa Mwenyezi Mungu kwa vile Watajulikana wakosefu kwa alama zao, basi watakamatwa kwa nywele zao za utosi na kwa miguu.
Yaani wakosefu watakuwa na alama za kuwatambulisha na kuwapambanua na watu wema, zaidi ya hayo Malaika wa adhabu watawafunga utosi na miguu pamoja na kuwatupa Motoni kifudifudi.
Basi ni ipi katika neema ya Mola wenu mnayoikanusha nyinyi wawili?
Katika mawaidha na makanyo?
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikadhibisha.
Hili ni jawabu sahihi zaidi kwa mwenye kukadhibisha adhabu ya Mwenyezi Mungu, nalo ni kutumbukizwa ndani yake:
وَنَقُولُ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا ذُوقُوا عَذَابَ النَّارِ الَّتِي كُنْتُمْ بِهَا تُكَذِّبُونَ {42}
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayochemka.
Hiyo ni Jahannam. Maji ya moto ni kinywaji.
Kukisifia kuwa kinachemka ni kuonyesha kuwa kinywaji hiki kitafikia kiwango cha joto kiasi ambacho mnywaji atahisi kama kwamba kiko motoni.
Maana ni kuwa hakuna kazi kwa wakosefu isipokuwa kuzunguka baina ya Moto au kunywa kinywaji cha Moto.
Basi ni ipi katika neema ya Mola wenu mnayoikanusha nyinyi wawili?
Je, ni adhabu ya Moto au ni kinywaji cha Moto? Yote hayo mawili ni katika neema ya Mwenyezi Mungu, kwa sababu ni hukumu ya uadlifu na upanga wa haki.
وَلِمَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ جَنَّتَانِ {46}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {47}
ذَوَاتَا أَفْنَانٍ {48}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {49}
فِيهِمَا عَيْنَانِ تَجْرِيَانِ {50}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {51}
فِيهِمَا مِنْ كُلِّ فَاكِهَةٍ زَوْجَانِ {52}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {53}
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ فُرُشٍ بَطَائِنُهَا مِنْ إِسْتَبْرَقٍ ۚ وَجَنَى الْجَنَّتَيْنِ دَانٍ {54}
yapo karibu.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {55}
فِيهِنَّ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنْسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَانٌّ {56}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {57}
كَأَنَّهُنَّ الْيَاقُوتُ وَالْمَرْجَانُ {58}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {59}
هَلْ جَزَاءُ الْإِحْسَانِ إِلَّا الْإِحْسَانُ {60}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {61}
وَمِنْ دُونِهِمَا جَنَّتَانِ {62}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {63}
مُدْهَامَّتَانِ {64}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {65}
فِيهِمَا عَيْنَانِ نَضَّاخَتَانِ {66}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {67}
فِيهِمَا فَاكِهَةٌ وَنَخْلٌ وَرُمَّانٌ {68}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {69}
فِيهِنَّ خَيْرَاتٌ حِسَانٌ {70}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {71}
حُورٌ مَقْصُورَاتٌ فِي الْخِيَامِ {72}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {73}
لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنْسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَانٌّ {74}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {75}
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ رَفْرَفٍ خُضْرٍ وَعَبْقَرِيٍّ حِسَانٍ {76}
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ {77}
تَبَارَكَ اسْمُ رَبِّكَ ذِي الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ {78}