Aya 133 – 135: Na Mola Wako Ndiye Mkwasi
Maana
Na Mola wako ndiye mkwasi, mwenye rehema.
Baada ya Mwenyezi Mungu kutaja kwamba atawahisabu watu kulingana na matendo yao. Ameashiria kuwa yeye ni mkwasi (mwenye kujitosheleza), hawahitajii viumbe.
Haimnufaishi twaa ya mwenye kumtii, wala hayamdhuru maasi ya mwenye kuasi; na kwamba ulimwengu wote una haja ya rehema yake. Kwa sababu, yeye ndiye sababu ya kwanza ya kupatikana huo ulimwengu.
Akipenda atawaaondoa kwa sababu ni Mkwasi, hawahitajii, na kuweka wengine awapendao baada yenu awabadili wengine wawe watiifu zaidi kuliko nyinyi. Lakini amewaacha na kuwapa muda kutokana na fadhila na ukarimu kutoka kwake.
Kama alivyowaanzisha kutokana na uzao wa watu wengine.
Yaani kama ambavyo imekuwa wepesi kwake kuwaleta nyinyi kutokana na kizazi kilichopita, vilevile ni wepesi kwake kuleta kizazi kipya kutokana na nyinyi na wengineo.
Makusudio ya Aya hii ni kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu anawaonya makafiri, wenye inadi, na maangamivu, kama ilivyokuwa kwa kaumu ya Nuh (a.s.), A’d na Thamud.
Hakika mnayoahidiwa yatafika tu.
Baada ya Mwenyezi Mungu kuwahofisha na adhabu ya dunia, sasa anawahofisha na Kiyama na adhabu yake; kwamba Kiyama kitakuja bila ya shaka yoyote, wala hapana pa kukikimbia ila kwake yeye tu, peke yake.
Sema: Enyi watu wangu! Fanyeni vile muwezavyo; na mimi nafanya. Mtakujajua ni nani atakuwa na makazi mema mwishoni.
Baada ya Mtume (s.a.w.) kuwalingania kwenye Uislamu waarabu wa ujahiliya na wakaitikia mwito wake walioitikia na kupinga waliopinga, Mwenyezi Mungu Mtukufu alimwamrisha kuwaambia wenye inadi: Kuweni kama mlivyo na mimi ninafanya kulingana na uongozi wa Mola wangu.
Baada ya muda mtajua mwisho mwema utakuwa wa nani; sawa na kumwambia yule anayepinga nasaha zako: Haya endelea tu utaona!
Hakika madhalimu hawafaulu.
Wale wanaojidhulumu wenyewe au wengineo kwa uadui. Lau angefaulu dhalimu, basi mwadilifu angelikuwa na hali mbaya kuliko dhalimu. Na maneno ya msimamo wa usawa yangelikuwa ni misamiati ya unafiki na ria.
وَجَعَلُوا لِلَّهِ مِمَّا ذَرَأَ مِنَ الْحَرْثِ وَالْأَنْعَامِ نَصِيبًا فَقَالُوا هَٰذَا لِلَّهِ بِزَعْمِهِمْ وَهَٰذَا لِشُرَكَائِنَا ۖ فَمَا كَانَ لِشُرَكَائِهِمْ فَلَا يَصِلُ إِلَى اللَّهِ ۖ وَمَا كَانَ لِلَّهِ فَهُوَ يَصِلُ إِلَىٰ شُرَكَائِهِمْ ۗ سَاءَ مَا يَحْكُمُونَ {136}
وَكَذَٰلِكَ زَيَّنَ لِكَثِيرٍ مِنَ الْمُشْرِكِينَ قَتْلَ أَوْلَادِهِمْ شُرَكَاؤُهُمْ لِيُرْدُوهُمْ وَلِيَلْبِسُوا عَلَيْهِمْ دِينَهُمْ ۖ وَلَوْ شَاءَ اللَّهُ مَا فَعَلُوهُ ۖ فَذَرْهُمْ وَمَا يَفْتَرُونَ {137}
وَقَالُوا هَٰذِهِ أَنْعَامٌ وَحَرْثٌ حِجْرٌ لَا يَطْعَمُهَا إِلَّا مَنْ نَشَاءُ بِزَعْمِهِمْ وَأَنْعَامٌ حُرِّمَتْ ظُهُورُهَا وَأَنْعَامٌ لَا يَذْكُرُونَ اسْمَ اللَّهِ عَلَيْهَا افْتِرَاءً عَلَيْهِ ۚ سَيَجْزِيهِمْ بِمَا كَانُوا يَفْتَرُونَ {138}
وَقَالُوا مَا فِي بُطُونِ هَٰذِهِ الْأَنْعَامِ خَالِصَةٌ لِذُكُورِنَا وَمُحَرَّمٌ عَلَىٰ أَزْوَاجِنَا ۖ وَإِنْ يَكُنْ مَيْتَةً فَهُمْ فِيهِ شُرَكَاءُ ۚ سَيَجْزِيهِمْ وَصْفَهُمْ ۚ إِنَّهُ حَكِيمٌ عَلِيمٌ {139}
قَدْ خَسِرَ الَّذِينَ قَتَلُوا أَوْلَادَهُمْ سَفَهًا بِغَيْرِ عِلْمٍ وَحَرَّمُوا مَا رَزَقَهُمُ اللَّهُ افْتِرَاءً عَلَى اللَّهِ ۚ قَدْ ضَلُّوا وَمَا كَانُوا مُهْتَدِينَ {140}