read

Baadhi ya Dua’ za Imam Ali (a s )

1257. Ewe Allah swt, mbariki yule ambaye hazina yake kuu ni imani na silaha zake ni machozi

1258. Ewe Allah swt, wewe ni mkuu kabisa kwa kumwangamiza yule ambaye umeshakwisha kumtukuza hapo awali

1259. Sala ni silaha ya mumini

1260. Je kuna yeyote yule ambaye anaelewa vyema uwezo wa Allah swt na tena asimwogope Allah swt?

1261. Je kuna yeyote akuelewaye vile wewe ulivyo na tena asiwe na khofu yako?

1262. Ewe Allah swt, ngozi hii yangu hafifu, haitaweza kustahimili moto mkali wa Jahannam

1263. Mishale yote hailengi penye kuheshimiwa na kwa kupatwa na shida na majaribio

1264. Ewe muumba ,wewe upo pekee mwenye kuheshimiwa na mwenye kudumu daima milele na umelazimishia viumbe vyako kwa kifo na kwa kupatwa na shida na majaribio

1265. Ewe muumba, nisamehee madhambi yangu pasipo mimi kujua kwangu

1266. Ewe mola , unisamehe madhambi yangu yale ambayo yanayoweza kuniteremshia juu yangu laana na adhabu na ghadhabu zako

1267. Ewe mola wangu, nisamehee madhambi yangu yale yanayoweza kuwa sababu ya kuharibu na kuzighasi zile baraka zako zilizo juu yangu

1268. Ewe mola, nisamehe madhambi yangu ambayo ndiyo yanayozuia na kuzipoteza ibada zangu kabla ya kukufikia wewe

1269. Ewe mola wangu, nisamehee madhambi yangu yale ambayo inanikatiza mimi katika imani yangu

1270. Ewe mola, mimi nakukaribia wewe kupitia kwa kukukumbuka wewe

1271. Ewe mola, mimi nakuomba wewe uniweke furaha na niwe nimeridhika na yale wewe uliyonijaalia maishani mwangu na katika bahati yangu (kwa ajili yangu)

1272. Ewe mola wewe ni mwepesi sana wa kubariki na kurehemu, msamehe yule ambaye hana chochote ila ni ibada na sala zako tu

1273. Ewe Allah swt !, Je wewe utauachilia Moto uzikumbe nyuso ambazo zimeangukia mbele yako kwa unyenyekevu?

1274. Ewe Allah swt, zipatie nguvu mikono na miguu katika kutekeleza wajibu na huduma katika kazi zako

1275. Na uzipatie nguvu mbavu zangu ili nipate hali ya kukufikia wewe