Utangulizi

Sheikh Umar Jumaa Mayunga alikwenda Kenya ambako baada ya mazungumzo ya kidini, alishauriwa na Sheikh Abdallah Nasser (wa Nairobi) na Haji Ali Muhammad Ja'afer (wa Mombasa) kuwa atakaporudi Dar es Salaam aonane nami kwa maelezo zaidi.

Alikuja kuonana nami, na swali lake la kwanza lilikuwa juu ya Taqiyah. Nilimpa jibu lililomtosheleza kutoka kwenye Qur'an Tukufu na Ahadithi.

Baada ya hapo alikuwa akinitembelea mara kwa mara na mambo yote aliyokuwa akiyaelewa vibaya (kutokana na propaganda za kiovu za Wahabiyyah) aliyaelewa vipasikavyo.

Swahili

Pongezi

"Enyi waumini, mkimcha Mwenyezi Mungu atakuongozeni njia ya haki na atawafutieni makosa yenu na atakusameheni." 8:29

Uchamungu ni moja ya pambo lenye thamani kwa binadamu na ni kipimo cha haki na batili na kila ambacho kinamfanya mwanadamu kuwa karibu na Mwenyezi Mungu, kwani uchamungu ni vazi zuri lenye thamani kila ataelivaa, hupata ukunjufu wa moyo na hima ya kutafuta haki hadi kufikia kikomo na kuwa karibu na Mwenyezi Mungu, kando ya neema zake, zikitiririka bila ya hesabu.

Swahili

Hati Ya Nyongeza

Makala hiyo hapo juu (iliyoandikwa kwa lugha ya Kiurdu) ilichapishwa kwanza kwenye gazeti la kila juma liitwalo Sarfaraz (Toleo la Muharram) la mwaka 1354 Masihiya). Makala hii ilichapishwa huko ikiwa imefanyiwa masahihisho fulani fulani na ikaungwa na ile makala yangu ya Kiurdu iitwayo "Karbala Shanasi" (toleo la pili la mwaka 1989, ukurasa wa 199-220).

Swahili

Mwishilizo

Kutokana na mazungumzo haya ni dhamiri kwamba, Mawahhabiya na Wanavyuoni wanaowaunga mkono sio tu kwamba hawauungi mkono msimamo wa Imamu Husayn (a.s.) bali vile vile huyahesabu mauaji yake kuwa ni ya haki kwa sababu kamwasi Yazid na hawapingi kushiriki kwa watu hao kwenye mauaji hayo, na wanaendelea hadi wakathubutu kuyafanya mapokezi ya Ahadith ya watu hawa msingi wa itikadi zao. Wanawasifa wauaji hao. Ingawa watu hawa walihusika kwenye mauaji hayo, wanafanya kuwa Makhalifa kwa makubaliano ya watu.

Swahili

Swali La Tatu

Kwa Mashia, Yazid na wauaji wengine wa Imamu Husayn (a.s.) ni Kafir na hivyo wamejitakia laana ya Allah iwe juu yao na juu ya wote wenye kuyafurahia matendo yao; na huwahesabu wote hao kuwa ni watu wa motoni. Mahanafiya, Mashafii na Mahambaliya wapenda haki nao humchukia Yazid na wauaji wengine wenye kustahili karipio kali zaidi.

Swahili

Swali La Pili

Hebu sasa natuligeukie lile swali la upande wa pili na tuone ni madhehebu ipi inayomchukulia Yazid mwenye nuru ipi. Baada ya kulielezea lile swali la kwanza waziwazi, haipo haja tena ya kueleza kwa kirefu hapa, lakini ili kuzi-imarisha zaidi thibitisho hizo, hapa chini tunatoa maelezo zaidi.

Mashia wanamchukulia mtu huyu aliyelaaniwa (Yazid) kuwa yu adui na kila mtoto wa Kishia humwona Yazid na jadi zake wote kuwa ni kizazi kilicholaaniwa Al-Shajaratul Mal-'unnah kilichotajwa kwenye Qur'ani (kwenye aya isemayo:

Swahili

Swali La Kwanza

Hebu na tufikirie ni madhahebu ipi yenye kumtukuza yule mtu Mtukufu ambaye yu Shahidi wa Karbala na inayozifuata nyayo zake, na ni ipi isiofanya hivyo.

Swahili

Mawahhabiyah na Wauaji wa Imamu Husayn (a.s.)

Mara kwa mara baadhi ya watu wajinga husema kuwa wauaji wa Imamu Husayn (a.s.) walikuwa ni Mashia. Ingawa uwongo huo umekwisha kukomeshwa tangu zamani kwa thibitisho zisizopingika, bado uwongo huu ungali ukitembezwa huko na huko, ili kwenda kuitambua hoja hii yenye nguvu, na kuweza kutofautisha baina ya ukweli na uwongo, tutatoa hapa hakika tatu zitakazoongezea kwenye uamuzi usiopingika. Hakika hizi ni:

1. Ni madhehebu ipi yenye kumheshimu na kumfuata Imamu Husayn (a.s.) na ni madhehebu ipi yenye kumpinga?

Swahili

6. Waliyodai "Wakereketwa"

Sasa tuyajibu yaliyochapishwa na "Wakereketwa wa Sunnah Malindi" kwa jina la "Majibu ya Abdillah Nassir". Makala tunayoyajibu humu ni yale ya "chapa ya kwanza". Sijui kama, baada ya hiyo, wametoa chapa nyengine kwa sababu mimi sijaziona.

Katika makala yao hayo, walianza kwa kusema: "Tunashindwa kukuelewa tukueke wapi …"

Swahili

5. Shirki Ni Nini Na Si Nini

Kwa taarifa tuliyoitoa (na tunaomba tuelezwe kama tumeacha kitu katika taarifa hiyo), kati ya madondoo sita yaliyonukuliwa na ndugu zetu hao, matano yametushinda kuelewa vipi yaweza yakawa ni shirki. Kwa hivyo hatutashughulika nayo kwa leo mpaka hapo tutakapofafanuliwa inshallah. Tutakaloshughulika nalo leo ni moja tu lililobaki ambalo, kwa hujja walizozitoa kulipingia, tumeweza kulifahamu lililowafikirisha wao kuwa ni shirki. Nalo ni lile la Buswiri kusema katika Burdah: "Haukupata kunipiga vita Ulimwengu nikataka nusra kwa Mtume ila huipata tu."

Swahili