Husaini Mwana wa Ali
Naanziliza kwa jina
Lake yeye Subhana
Mola asiye kijana
Wala mke asiliye
Ndie watangu natangu
Kabula ya ulimwengu
Muumba nchi na mbingu
Milele Atabakiya
Asie na mshirika
Na wala hakuzalika
Ameketi pasi shaka
Enzie imetimiya
Sasa penda kuweleza
Kisa chenye kuchukiza
Na moyo nitaukaza
Hadi mwisho kufikiya
Ni rafiki wa Rasuli
Muhammadi mur sali
Husaini mwana wa Ali
Na Fatima Hashimiya