Hii ni Surah Abasa
Imeteremshwa Makka, ina Aya 42.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.
1. Yeye aliukunja uso akapa mgongo. 1
2. Kwa sababu alijiwa na kipofu. 2
3. Ni lipi kilichokufanya wewe kujua kuwa yeye atajitakasisha,
4. Au akawaidhika ukamfaa waadhi ?
5. Ama kwa yule ajifikiriaye kuwa amejitosheleza (katika utajiri wa mali yake),
6. Na kwa huyo anamshughulikia,
7. Wala haitakuwa lawama juu yako iwapo hatajitakasa.
8. Ama yule anayekuijia kwa jitihada na moyo mnyenyekevu,
9. Na akiwa na khofu (moyoni mwake),
10. Wewe kwake huyo utamshughulikia na kumsikia
11. Sivyo ! Hakika (Quran) hii ni nasaha. 3
12. Basi kila apendaye atawaidhika,
13. (Yameandikwa hayo) Katika Vitabu vilivyohishimiwa.
14. Vilivyotukuzwa, vilivyotakaswa,
15. Vilivyo katika mikono ya wajumbe Malaika
16. Watukufu, watiifu wa Mwenyezi Mungu.
17. Amelaaniwa Mwanadamu ! Namna gani alivyokuwa bila shukrani ?
18. Kwa kitu gani Amemuumba ?
19. Kwa tone la manii, alimuumba, kisha akamwekea vipimo vyake.
20. Kisha akafanyia njia nyepesi.
21. Kisha akamfisha na kumfanya azikwe kaburini.
22. Kisha aendapo atamfufua.
23. La ! Hakutimiza vile alivyokuwa ameamrishwa.
24. Basi mtu na akitazama chakula chake. 4
25. Kuwa ndio sisi tuliomiminisha maji, mmiminiko wa nguvu
26. Kisha tukaipasua ardhi, kwa mipasuko (iliyo lazima),
27. Na tukafanya sisi kuota nafaka humo
28. Na Zabibu na mboga
29. Na Zaituni na Mitende
30. Na mabustani yenye miti mingi
31. Na matunda na malisho
32. Kwa manufaa yenu na wanyama wenu.
33. Basi itakapo kuja sauti kali iumizayo masikio (Sauti ya baragumu la kiyama)
34.. Siku ambayo mtu atakimbia ndugu yake.
35. Na mama yake na baba yake
36. Na mke wake na watoto wake
37. Kila mtu katika wao, siku hiyo atakuwa na jambo la kumshughulisha.
38. (Kutakuwepo) nyuso zing’aazo siku hiyo,
39. Zitacheka na kufurahika 5
40. Na (Zitakuwapo) nyuso katika siku hiyo zenye vumbi,
41. Kiza kitakuwa kimevikwa juu ya nyuso zao. 6
42. Hao ndio makafiri, waliokuwa wakitenda maovu
Kwa kukubali kuwa Mtume s.a.w.w. alikuwa na kasoro, basi ni kupinga na kukana Aya za Quran, 68:4 “Na kwa hakika wewe umesimama kabisa katika tabia njema” (vile vile tazama 2:143,33:45, 33:21). Je itawezekanaje kukubali kwetu kwa uzushi huo wa kasoro wakati ambapo Allah swt anawaamrisha wanadamu wote kufuata mfano wa Mtume s.a.w.w. katika tabia na maadili ?
33:21 “Kwa hakika (kwake) ni kwa ajili yenu katika Mtume wa Allah (Muhammad) Mfano bora kabisa (tabia na maadili) kwa ajili ya yule aliye na matumaini ya Allah na siku ya baadaye (Kiyama) na kumkumbuka mno Mwenyezi Mungu”
Kosa kubwa ni kule kutokutumia na kutokuielewa lugha vile vile ilivyotumika na vile vile kutozitilia maanani riwaya na tafsiri zilizotolewa na Ahli Bayt a.s. ya Mtume Mtukufu s.a.w.w.
Links
[1] https://www.al-islam.org/sw/user/login?destination=node/25375%23comment-form
[2] https://www.al-islam.org/sw/user/register?destination=node/25375%23comment-form
[3] https://www.al-islam.org/sw/tags/surah
[4] https://www.al-islam.org/sw/taxonomy/term/1238
[5] https://www.al-islam.org/sw/library/quran-commentaries