Hii ni historia ya vuguvugu la Uislamu ambalo lilianzishwa na Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) mnamo mwaka 610 A.D. huko Makka, na kuendelea alipohamia Madina mpaka alipofarika. Inahusisha kipindi cha miaka tisini kuanzia 570 A.D. wakati yeye Muhammad alipozaliwa huko Makka, hadi mwaka 661 wakati mrithi wake, Ali ibn Abi Talib, alipouawa huko mjini Kufah.

Historia zisizo na idadi zimeandikwa huko nyuma na zitaandikwa wakati ujao. Maendeleo ya kuvutia ya Uislamu katika nyanja ya ulinganiaji katika nyakati zetu wenyewe; kufufuka upya kwa mataifa ya Kiislamu baada ya karne nyingi za usingizi mzito; kujidukiza kwa mafuta kama wakala mpya katika siasa za kidunia katika karne hii; bali juu ya yote na hivi karibuni kabisa, yale mafanikio ya Mapinduzi ya Kiislamu ndani ya Iran, yote haya yanakuwa, kote Mashariki na Magharibi, kama vichocheo vya shauku mpya katika Uislamu.