read

22. Tawba Ni Nuru Ya Matumaini

"Ewe uliyekwisha tenda madhambi! Usikate tamaa kwa rehema za Allahs swt, rejeeni katika njia yake, na hataki muendelee kutenda madhambi vile mupendavyo na mutakavyo - tukidhani kuwa atatusamehe tu! La sivyo hivyo! Makusudi ya kutokata tamaa ni kwa wale waliokwisha tenda madhambi wakidhani kuwa hawana la kufanya kusamehewa hivyo wakaendelea na maasi yao, bali inawabidi waitambuw na waombe TAWBA na msamaha wa Allah swt. Hivyo wajue kuwa pale wanapotenda dhambi, waombe Toba mara moja. Inawezekana Allah swt akazikubalia TAWBA zetu.