28. Mbele Ya Allah Swt Miguu Na Mikono Vitasema
Baadhi ya Mufassirina wanasema kuwa siku ya Kiyama kitakachoweza kusema ni mdomo tu, je viungo kama mikono na miguu vinaweza kusema?Wao wanasema kuwa hali ya udhahiri wa mwanadamu tu ndio utakaodhihirisha hali yake huyo mtu, na wala si mikono au miguu. Basi hao tunamwambia kuwa 'matamshi' si mahitajio ya ulimi bali ni Allah swt anayejaalia uwezo wa mdomo kutamka maneno. Kutamkwa kwa maneno ni Sifa ya Allah swt na wala si kasoro. Iwapo ingalikuwa hivyo, basi ng'ombe na punda pia wanayo midomo na ulimi hata mirefu kuliko wanaadamu. Basi imetuwia dhahiri kuwa mwanadamu amefadhilishwa na Allah swt kwa kumjaalia 'uwezo wa kutamka.' Katika neema kubwa kabisa za Allah swt kwa mwanadamu ni akili, hivyo ulimi ni tafsiri ya akili ili aweze kusema. Wanyama hawajajaaliwa neema hiyo.
Watu wenye akili watambua kuwa 'utamkaji' hauna uhusiano hasa na ulimi, bali ni Allah swt tu aliyezijaalia ndimi za wanaadamu ziweze kutamka maneno. Siku ya kiyama, hata vidoke vyetu vitafanya kazi hiyo hiyo na kusema kuwa huyu mtu alimnyooshea kidole muumin fulani kwa dharau au aliandika kwa kalamu yake mambo dhidi ya muumin. Zipo riwaya zisemazo kuwa hata nywele za mtu pia zitatoa ushahidi wao dhidi ya mtu mwenyewe.
Dalili ya pili ni kule ambapo mtu hatakaporidhika pale viungo vyake na sehemu za mwili wake zitakapotoa ushahidi dhidi yake.Lakini hivyo navyo vitasema kwa kuwa vimejaaliwa Allah swt uwezo huo wa kusema.
Malaika wote wanao uwezo wa kuzungumza na vile vile viumbe vyote tusivyoviona pia vinao uwezo wa kusema:
.Na hakuna chochote ila kinamsabihi yeye (Allah swt ). (17:44)
Baada ya kifo cha mtu, huwa anaelekea katika sehemu za Malaika.
Iwapo ungalikuwa nauwezo wakuyasikia yaliyoghaibu (yasiyoonekana machoni mwetu) Basi hata viungo vyako pia vinamtukuza allah swt, lakini hauyasikii.Mwanadamu hawezi kutambua kwa kuhisi tu kwani sisi tupo humu duniani na wala hatuna uwezo huo wa ziada. (Jikumbushe kisa cha Mtume Suleyman a.s.alipokuwa akipita penye makazi ya mdudu sisimizi).
Kinaadhimisha utukuzo wa Mwenyezi Mungu chochote kile kilicho mbinguni na chochote kile kilicho ardhini. (62:1)
Kesho siku ya Qiyama, Allah swt atakijaalia kila kiungo 'uwezo wa kusema,' na vyote vitasema kama kawaida.Dhambi hata moja halitafichika hata kama kikiwa kidogo kiasi gani, lakini iwapo tutakuwa tumeisha fanya Toba maishani mwetu, basi viungo na sehemu zetu zote za mwili hazitatamka chochote dhidi yetu wala kutushitaki.
Kwa kifupi, itakuwa ni aibu na udhalilisho mkubwa kwetu sisi kushitakiwa na viungo vyetu sisi wenyewe.Hivyo, ili kuepukana na udhalilisho kama huo inatubidi tuwahi kufanya Toba ya madhambi yetu yaliyokwisha tendwa kabla hatujafariki na kukosa fursa hiyo.