read

29. Tusome Tasbihi Kwa Vidole Kwani Vitatoa Ushahidi Wake

Katika tafsiri 'Ruh al-Bayaan, kwa mukhtasari kuwa Mtume Mtukufu s.a.w.w. aliwaambia wanawake kuwa wawe wakisema kwa wingi sana tasbili.

Ipo riwaya nyingineyo isemayo kuwa Mtume mtukufu s.a.w.w. anasema:
"Usiku wa Me'raj nilimwona Malaika mmoja akijenga jengo. Alikuwa akiweka tofali la dhahabu na mara tofali la fedha, na mara nyingine alikuwa akingojea. Mimi nilimwuliza 'je kwa nini unangojea?' Alijibu: "Wakati mja wake Allah swt anapoanza Tasbihi, sisi huwa tunaanza kujenga jengo zuri sana, na mara anyamazapo, nasi pia twangoja.

Katika kipindi cha awali cha Islamu, hapakuwapo na tasbihi bali walikuwa wakihisabia kwa vidole vyao. Kuna vifundo vitatu katika kila kidole na hivyo kuna mafundo thelathini kwa jumla ya mikono yetu miwili. Hivyo tutoe tasbihi kwa kutumia vidole vyetu hivi. Amesema Mtume Mtukufu s.a.w.w."Toeni Tasbihi kwa vidole vyenu kwani siku ya Kiyama vitatoa ushahidi kwa kusema:"Ewe Allah swt! huyu mtu alikuwa akitoa tasbihi pamoja nasi."

Tasbihi kwa mara ya kwanza ilifanywa na binti wake Mtume Mtukufu s.a.w.w. Bibi Fatemah Zahra a.s. Yeye alipokuwa amekwenda kuzuru kaburi la Bwana Hamza, alirudi na udongo mchache na ambao aliutumia katika kutengenezaea Tasbihi.Alitumia hiyo tasbihi katika dhikiri ya Allah swt.

Katika kipindi cha Imam Jaafer as-Sadique a.s. alitilizia mkazo wa kutengeneza tasbihi kwa udongo wa Karbala. Iwapo tasbihi iliyotengenezwa kwa udongo wa Karbala ikizungushwa mkononi tu, basi inayo malipo makubwa kwani udongo wenyewe upo unafanya tasbihi.

Allamah Sheikh Shushtary anasema:"Tasbihi iliyotengenezwa kwa udongo wa Karbala, si tasbihi ya kawaida, bali inayo thawabu nyingi kupita kiasi na inazo khususi kwani ardhi ya karbala ni kipande cha peponi (Jannati)."

Imam a.s. alimwambia Sahaba wa Mtume Ja'abir:
"Ewe Ja'abir ! Uwe ukimzuru Hussein huko Karbala kwani Karbala ni kipande miongoni mwa vipande vya peponi (Jannati)."

Msomaji anombwa kurejea maudhui haya ya kusujudia juu ya udongo. "Kwa nini Mashia husujudu juu ya judongo" cha Bilal Muslim Mission of Tanzania P.O.Box 20033 Dar es Salaam Tanzania East Africa na 'Assujuud' ala turbatil Husseyn Inda As-Shiah al-Imaamiyah' (kiarabu) cha Sheikh Abdul Husseyn al-Amiini.Kilichochapwa na Dar az- Zafra, Beirut Lebanon.