read

30. Je Tawba Iweje?

Kufanya TAWBA ya Allah swt ni jambo la daraja la juu, na iwapo jambo hili likiandikewa kitabu kwa ufafanuzi zaidi, basi kitatokezea kitabu kikubwa mno, lakini sisi hapa tutajaribu kuelezea vile TAWBA inavyotakiwa kufanywa. Iwapo mtu atatokezea kusema kuwa ,mimi nimefanya TAWBA, nimehuzunikia na kusikitikia madhambi yangu, na vile vile nimeomba msamaha wake Allah swt lakini moyo wake haukusikitika au haukuhuzunika na wala hakuacha kutenda matendo ya madhambi. Basi watu kama hawa hawatafaidika kamwe na faida za TAWBA zisizo za Nasuha.

Al- Imam ar-Ridhaa a.s. amesema:
"Iwapo mtu atatamka 'Astaghfirullah' ya moyoni, basi atambue kuwa amemfanyia mzaha Allah swt."