32. Mapenzi Ya Ahli Bayt Huelekeza Kwa Tawba
Watu wenye Imani na mapenzi ya Ahli Bayti Toharifu ya Mtume Mtukufu s.a.w.w. wanapotokezewa kufanya dhambi, basi ni rahisi kwao kujaaliwa tawfiki ya TAWBA. Allah swt kwa nuru na baraka za Mtume mtukufu s.a.w.w. na ma-Imam a.s.atawafanyia matokeo yao yawe mazuri.
Iwapo watu waliwafuata viongozi wa sini yetu kwa ukamilifu, wakatekeleza faradhi zao ipasavyo, wakajiepusha na yote yaliyoharamishwa, wakawafuata kikamilifu Ahli Bayt ya Nyumba ya Mtume a.s.na wakawa wakidumisha maulidi ya Husseyn a.s. basi siku ya kiyama Mtume s.a.w.w.atawasaidia wote.Wamebahatika wote wale watakaotetewa na Bibi Fatemah az-Zahra a.s. Wasio na bahati ni wale ambao hawana mapenzi ya Ahli Bayt ya Mtume s.a.w.w..
Pamoja na hayo, faida nyingineyo itokanayo na mapenzi ya Ahli Bayt a.s. ni kuondokana na ubakhili na huingiwa na moyo wa kutoa sadaka na misaada na hiyo ndiyo bakhshishi kubwa (lakini wale wasiotoa khums, zaka au sadaka na ambao hutoa rushwa na kukusanya mali kwa kutumia riba kwa hakika wao si wapenzi wa Ahli Bayt a.s.) Iwapo munataka kufanya mapenzi na Imam Ali a.s. na kumfuata basi muwajue hali mayatima, wajane, wageni na muwasaidie wenye madaris (wingi wa Madrassah au vyuo).
Wale walio wapenzi wa kweli wa Ahli Bayt a.s. kwa hakika hawawezi kufariki bila ya kufanya TAWBA. Tawfiki hiyo Inshaallah watajaaliwa kabla ya mauti kuwafikia, na kuelekea peponi huku wakiwa hawana mzigo wa madhambi yao.