read

35. Kuiacha Tawba Na Kuendelea Na Madhambi

Imam Muhammad al-Baqir a.s. anaielezea 'kugang'ania hivi; katika Usuli Kafi:

"Iwapo mtu mmoja amefanya madhambi na wala yeye hanuii kuyaacha kabisa na wala hafikirii swala la kufanya TAWBA, basi kwa sababu hiyo itakuwa ni mazoea yake ya kutenda madhambu na hakutakuwa dawa nyingineyo yenye kuponya tabia yake hiyo ila TAWBA tu."

Maulamaa wengi wanaafikiana kuwa ni lazima kufanywa TAWBA papo hapo pale mtu anapotenda dhambi. Sheikh Bahi A.R. anasema kuwa mtu anazidi kujitwisha mzigo wa madhambi kila acheleweshavyo TAWBA kwani hiyo ni faradhi mojawapo na anastahiki kupewa adhabu kamili. Iwapo atafanya TAWBA kwa haraka basi atakuwa mustahiki wa rehema za Allah swt.

Ipo riwaya isemayo kuwa wakati mja anapotenda madhambi na kufanya TAWBA na tena akarejea kutenda madhambi na tena kutubu na kwa mara ya tatu tena akarejea kutenda madhambi na kutubu, basi hapo Allah swt anawaambia Malaika: "Enyi Malaika wangu! Angalieni vile mja wangu asivyoiacha nyumba yangu kwani yeye anatambua kuwa hakuna mwingine awezaye kumsaidia ila mimi tu!"