36. Tawba Ndiyo Sababu Ya Kusamehewa
Allah swt anatuambia 'Saabiquu' yaani haraka haraka mtangulie. Je ni wapi huko tena? Basi jibu ni kuelekea kwake Allah swt, hiyo TAWBA inaweza kuwa sababu ya rehema za Allah swt. Faradhi na Sunna zote ni sababu za rehema na Maghfirah za Allah swt. Matendo yote mema ni wasila wa Maghfirah zake Allah swt. Iwapo utauondoa mwiba njiani basi iwe ni kwa ajili ya Allah swt, na ulifanyalo jambo lolote lile, liwe kwa ajili ya Allah swt na yawe yote kwa ajili ya kutaka radhi na maghfirah zake Allah swt.
Katika baadhi ya kazi huwa tunababaika na baadhi huwa tunayo yakini. Lakini TAWBA ni tendo ambalo sisi tunayo yakini ya kutakabaliwa kwake na tukasamehewa madhambi yetu yote papo hapo iwapo tutaifanya kwa masharti na maelezo tuliyoyaelezea hapo awali.
Iwapo ulimdhulumu mtu na unataka msamaha basi lazima kwanza umwombe msamaha huyo mtu na iwapo atakusamehe ndipo hapo ujue kuwa umefaidika kwa kuupata Msamaha wa Allah swt. Allah swt anatuambia katika Qurani Sura al-Baqarah:
Na kuwa nyinyi wenyewe (kwa hiari) musamehe (yote) ni ukaribio kwa ucha Mungu (Taqwa). (2:23)
Msameheni kwa ajili ya Allah swt kwani yeye hupenda sana msamaha!