39. Madhambi Yote Yanaweza Kusamehewa
Katika Qurani Tukufu zipo aya nyingi mno na vile vile zipo hadithi ambazo zinazungumzia ukubaliaji wa TAWBA na vile vile zielezeazo kuwa madhambi yote yanaweza kusamehewa. Katika Qurani Allah swt anajisifu kuwa yeye ndiye Msamehevu na mwenye kuzikubalia TAWBA na vile vile anajiita katika Qurani kwamajina tofauti tofauti: Tawwab, Ghaffar, Ghafirudh-Dhunuub..........
Allah swt anawaita wale wote wafanyao madhambi wajirudi na kufanya TAWBA mara moja kabla hawajakumbana na adhabu zake zilizo kali kabisa. Suluhisho la daima la kuvunjika moyo, katika Sura az-Zumar:
Sema ("Ewe Mtume Muhammad!): "Enyi waja wangu! Ambao mumezibadhirisha nafsi zenu, msikate tamaa ya rehema za Mwenyezi Mungu, kwa hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote kwa pamoja, hakika yeye ni Mwingi wa kusamehe, mwingi wa Kurehemu. (39:53)
Katika Aya hii Allah swt anawaita waja wake "Enyi waja wangu' na wala hakuwaita 'Enyi mlio asi' au 'Enyi wenye madhambi!' Na vile vile ametuusia sisi tusikate tamaa na kujidhulumu na badala yake anatupatia mawaidha ya kumrejea yeye ili aturehemu na kutusamehea.
Hivyo sisi tushikamane na imani yetu kwa Allah swt kwa maombi yetu na misaada yetu kwani ni yeye pekee awezaye kutusahilishia matatizo yetu. Yeye tu ndiye Tumaini letu.