read

40. Tawba Ya Mauaji

Iwapo mwuaji anataka kufanya TAWBA, basi inambidi kwanza ajisalimishe mbele ya warithi wa marehemu aliyeuawa na hapo ni shauri lao wao iwapo watatekeleza kisasi au watadai fidia au watamsamehe.

Iwapo mtu ataua kwa makosa au kwa kumdhania mtu kimakosa basi ni lazima kwake yeye kulipa fidia kwa familia na warithi wake marehemu. Na iwapo wao watamsamehe, basi ni faradhi juu ya muuaji kumfanya huru mtumwa mmoja, kuwalisha masikini sitini na kufunga saumu kwa siku sitini kwa mfululizo. Kama haweza kumfanya huru mtumwa mmoja, basi avitekeleze vilivyobakia.

Maelezo zaidi juu ya maswala kama hayo yanaweza kupatikana katika vitabu vya Fiqhi na Mafuqahaa wanaweza kutoa maelezo zaidi.

Tahadhari: Ni haramu kabisa kujitolea majibu ya maswala katika fiqhi tukisema: 'Kwa kuwa swala hili liko hivi, basi labda au bila shaka jibu lake litakuwa hivi na hivi.....' Hiyo ni Qiyaas, na qiyaas katika fiqhi ni haramu kwani itakuwa ni uamuzi usiofanyiwa utafiti.