Takbir
Mwenyezi Mungu ni Mkubwa
Tarjuma Ya Surat-Al-Hamd
Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehma, Mwenye kurehemu
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe
Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu
Mwenye kumiliki Siku ya malipo
Wewe tu, ndiye tunayekuabudu, na kwako tu tunataka msaada
Tuongoze katika njia iliyonyooka
Njia ya wale uliowaneemesha, siyo ya wale walioghadhibikiwa, wala ya wale waliopotea.
Tarjuma Ya Surat-Ul-Ikhlaas
Kwa Jina la Mweyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu
Sema; Yeye Mwenyezi Mungu ni Mmoja
Mwenyezi Mungu ndiye anayekukusudiwa kwa haja
Hakuzaa wala Hakuzaliwa
Wala hana anayefanana naye hata mmoja.
Tarjuma Ya Dhikr Wakati Wa Rukuu Na Sajidah
Ametakasika Mola wangu aliye Mtukufu na ninamtukuza
Ametakasika Mola wangu aliye Mkuu na ninamtukuza
Kabla Ya Kwenda Sijdah
Amezisikia na kuzikubali Mwenyezi Mungu, sifa za mwenye kumsifu
Istighfari Baina Ya Sajdah Mbili
Ninaomba maghfira kwa Mwenyezi Mungu, aliye Mola wangu na ninarejea Kwake
Wakati Unapokuwa Unanyanyuka
Ninasimama na kukaa kwa msaada na nguvu za Mwenyezi Mungu
Tarjuma Ya Tasbihi Nne
Utukufu ni wa Mwenyezi Mungu, na kila sifa njema ni Zake, na hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa kuliko kila kitu.
Tarjuma Ya Tashahudi Na Salaam
Nashuhudia kwamba hapana apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu, Ambaye ni Mmoja na hana mshirika.
Na ninashuhudia kwamba Muhammad ni mja na Mtume Wake
Ewe Mwenyezi Mungu mshushie rehema na amani, Muhammad na kizazi chake.
Amani iwe juu yako ewe Mtume, na rehema za Mwenyezi Mungu na baraka Zake .
Amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yetu, wale tunaoswali, na juu ya waja wote wema wa Mwenyezi Mungu
Amani, rehema na baraka zake Mwenyezi Mungu ziwe juu yenu, enyi waumini!