Aya 1: Hizo Ni Aya Za Kitab
Maana:
Alif Laam Raa.
Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 mwanzo wa Sura Baqara.
Hizo ni Aya za Kitabu.
Yaani Aya za Sura hii ni katika Qur’an Tukufu. Lengo la kutoa habari hii ni kubainisha kuwa sura hii ni haki kwa sababu ni katika Qur’an. Kwa vile Qur’an ni haki basi nayo ni haki. Haya ndiyo makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:
Na uliyoteremshiwa kutoka Mola wako ni haki.
Hapa linakuja swali: Kuna dalili gani kuwa Qur’an ni haki? Jibu utalipata Juz. 1 (2:23-25) Imam Ali (a.s.) anasema : “Hakika Qur’an dhahiri yake ni safi na undani wake ni wa kina, maajabu yake hayaishi wala giza haliondoki ila kwayo.”
Lakini watu wengi hawaamini Qur’an wala kauli nyingine ya haki na uadilifu ila yule anayeona heri yake ni heri ya watu na shari yake ni shari yao pia.
Mtu mmoja katika watu wa Mungu aliambiwa kuwa soko limeungua lakini duka lako halikuungua, akasema: Alhamdullilah. Kisha akatanabahi kuwa ameasi kwa kujitakia yeye binafsi heri kuliko watu wengine, akatubia dhambi yake na akaomba msamaha.
Mfano wa watu hawa ni wachache ambao wanawafikiria wengine, ndio aliowakudia Mwenyezi Mungu kwa kusema: ‘Lakini watu wengi hawaamini”.
اللَّهُ الَّذِي رَفَعَ السَّمَاوَاتِ بِغَيْرِ عَمَدٍ تَرَوْنَهَا ۖ ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ ۖ وَسَخَّرَ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ ۖ كُلٌّ يَجْرِي لِأَجَلٍ مُسَمًّى ۚ يُدَبِّرُ الْأَمْرَ يُفَصِّلُ الْآيَاتِ لَعَلَّكُمْ بِلِقَاءِ رَبِّكُمْ تُوقِنُونَ {2}
وَهُوَ الَّذِي مَدَّ الْأَرْضَ وَجَعَلَ فِيهَا رَوَاسِيَ وَأَنْهَارًا ۖ وَمِنْ كُلِّ الثَّمَرَاتِ جَعَلَ فِيهَا زَوْجَيْنِ اثْنَيْنِ ۖ يُغْشِي اللَّيْلَ النَّهَارَ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ {3}
وَفِي الْأَرْضِ قِطَعٌ مُتَجَاوِرَاتٌ وَجَنَّاتٌ مِنْ أَعْنَابٍ وَزَرْعٌ وَنَخِيلٌ صِنْوَانٌ وَغَيْرُ صِنْوَانٍ يُسْقَىٰ بِمَاءٍ وَاحِدٍ وَنُفَضِّلُ بَعْضَهَا عَلَىٰ بَعْضٍ فِي الْأُكُلِ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِقَوْمٍ يَعْقِلُونَ {4}