Aya 32 -34: Na Akateremsha Maji Kutoka Mbinguni
Maana
Ayazotehizitatuumepitamfanowakekamaifuatavyo:
Kuumbwa mbingu na ardhi: Juz. 7 (6:73).
Kutermshwa maji kutoka mbinguni: Juz. 1 (2:22) na Juz. hii tuliyo nayo (13:18).
Kupita majahazi: Juz. 2 (2:164).
Kunufaika na Jua na Mwezi: Juz. hii (13:2). Usiku na mchana Juz. 11(10: 67).
Mwenyezi Mungu ameweka idadi ya neema nyingi kwa waja wake katika Juz. hii na Juz. 8 (6:143144) na nyinginezo nyingi zilizokwisha tangulia pamoja na tafsiri yake na ufafanuzi wake. Mwenyezi Mungu amerudia hapa au kuzidokeza kwa mnasaba wa kubadilisha neema kwa kufuru.
Kwa ufupi Aya hizi tatu zinamaanisha kuwa neema za Mwenyezi Mungu hazihisabiki; kama vile kuumbwa mbingu na ardhi, kuteremshwa maji kuenda majahazi faida za jua, mwezi, usiku na mchana. Vile vile kuwafadhili watu kwa waliyoomba na wasiyoomba, lakini pamoja na neema zote hizo wengi wanamkufuru na kuzikufuru neema zake huku wakiabudu yasiyowanufaisha wala kuwadhuru.
Je Mtu Ana Maumbile Ya Hatia?
Kwa mnasaba wa kauli yake Mwenyezi Mungu: Hakika mtu ni dhalimu mkubwa mwingi wa kukufuru, tunadokeza kwamba wataalamu wa saikolojia wametofautiana kuhusu binadamu, kuwa je, ana maumbile ya kufanya hatia, kwamba yeye amezaliwa kumfanyia uadui ambaye hajamfanyia uadui na kukufuru neema za aliyemfanyia wema (hana shukrani)
Mnamo mwaka 1832 watalamu 528 walikutana huko Amerika wakilijadili suala hili. Wengi wakaonelea kuwa hakuna dalili kuwa mwanadamu anaweza kuepuka kufanya makosa, lakini kundi jingine likapinga.
Sisi tunaamini kuwa binadamu hakuzaliwa kuwa ni mwenye kufanya makosa; vinginevyo angelikuwa hana taklifa yoyote na kuhisabiwa kwake na kuadhibiwa ingelikuwa ni dhulma na uonevu. Vile vile dini na sharia ingelkiuwa ni upuzi na mchezo; kama vile unyoya kwenye mavumo ya upepo. Isipokuwa anakuwa ni mwenye hatia kwa sababu nyingine za nje; kama vile njaa inayofanya awe mwizi, hadaa zinazomfanya awe na hiyana na kuwa kibaraka n.k.
Hapa ndio unapata tofauti baina ya watu katika nafsi zao. Wengine wanakuwa dhaifu mbele ya hadaa na kushindwa na matamnio; kama vile mwenye chakula lakini bado anataka ziada tena kwa hali yoyote; au mwenye mke anayemtosheleza, lakini anazini; au anayeificha haki kwa kupupia cheo au manufaa yoyote katika starehe za dunia. Hakuna mwenye shaka kwamba huyu amefanya dhambi kwa kutaka kwake sio kwa maumbile yake. Hayo ndiyo aliyoyakusudia Mwenyezi Mungu aliposema:
‘Hakika mtu ni dhalimu mkubwa mwingi wa kukufuru.’
Ni wazi kuwa kupondokea haramu hakuifanyi kuwa ni halali, madamu iko nafasi ya kuweza kufanya subira na kushinda mapondokeo haya. Tumetangulia kueleza yanayoambatana na utafiti huu katika kufasiri Juz. 12 (11:9).
وَإِذْ قَالَ إِبْرَاهِيمُ رَبِّ اجْعَلْ هَٰذَا الْبَلَدَ آمِنًا وَاجْنُبْنِي وَبَنِيَّ أَنْ نَعْبُدَ الْأَصْنَامَ {35}
رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضْلَلْنَ كَثِيرًا مِنَ النَّاسِ ۖ فَمَنْ تَبِعَنِي فَإِنَّهُ مِنِّي ۖ وَمَنْ عَصَانِي فَإِنَّكَ غَفُورٌ رَحِيمٌ {36}
رَبَّنَا إِنِّي أَسْكَنْتُ مِنْ ذُرِّيَّتِي بِوَادٍ غَيْرِ ذِي زَرْعٍ عِنْدَ بَيْتِكَ الْمُحَرَّمِ رَبَّنَا لِيُقِيمُوا الصَّلَاةَ فَاجْعَلْ أَفْئِدَةً مِنَ النَّاسِ تَهْوِي إِلَيْهِمْ وَارْزُقْهُمْ مِنَ الثَّمَرَاتِ لَعَلَّهُمْ يَشْكُرُونَ {37}
رَبَّنَا إِنَّكَ تَعْلَمُ مَا نُخْفِي وَمَا نُعْلِنُ ۗ وَمَا يَخْفَىٰ عَلَى اللَّهِ مِنْ شَيْءٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ {38}
الْحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي وَهَبَ لِي عَلَى الْكِبَرِ إِسْمَاعِيلَ وَإِسْحَاقَ ۚ إِنَّ رَبِّي لَسَمِيعُ الدُّعَاءِ {39}
رَبِّ اجْعَلْنِي مُقِيمَ الصَّلَاةِ وَمِنْ ذُرِّيَّتِي ۚ رَبَّنَا وَتَقَبَّلْ دُعَاءِ {40}
رَبَّنَا اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِلْمُؤْمِنِينَ يَوْمَ يَقُومُ الْحِسَابُ {41}