Aya 1 – 14
Maana
Haa-miim.
Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:1).
Naapa kwa Kitabu kinachobainisha.
Hiki ni kiapo kutoka kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Qur’an ambayo ndani yake mna ubainifu wa uongofu na upotevu, na halali na haramu.
Hakika tumeifanya Qur’an kwa kiarabu ili mfahamu.
Umetangulia mfano wake katika Juz. 12 (12:2), Juz. 16 (20:113), Juz. 24 (41:3) na kwenye Juzuu hii tuliyo nayo (42:7). Tumekwishaizungumzia sana Aya hii, na hivi sasa hatuna la ziada.
Na hakika hiyo imo katika mama wa Kitabu kilichoko kwetu, ni tuku- fu na yenye hikima.
‘Hiyo’ ni hiyo Qur’an na mama ni asili. Hakuna mwenye shaka kwamba ilimu ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ndio asili ya vitabu vyote mbinguni. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameisifu Qur’an kuwa ni tukufu kwa sababu inainua na kuwatukuza wanayoisikiliza na kuitumia. Tumeona jinsi ilivyowatoa waarabu kwenye ujinga wa wajinga kuwapeleka kwenye maendeleo na jinsi ilivyoeneza utawala wao na lugha mashariki ya ardhi na magharibi yake, pale walipohalalisha halali ya Qur’an na wakaharamisha haramu ya yake.
Vile vile Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameisifu kuwa ina hikima kwa sababu imeweka sawa baina ya watu bila ya kubagua, ikatoa mwito wa kusameheana na ikahimiza kufanya kazi yenye manufaa na kusaidiana kwa masilahi ya watu wote.
Je, tuache kuwakumbusha kwa kuwa ni watu mliopita mipaka?
Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuitaja Qur’an kwamba ni mtoa nasaha mwaminifu, sasa anawaambia wale walioikadhibisha katika washirikina wa kiarabu: Mnaonaje tuache kuwakumbusha Qur’an kwa vile tu nyinyi mmezipitishia kiasi nafsi zenu na mkazidhulumu kwa ujinga na upotevu? Bali nyinyi ndio mnafaa zaidi kukumbushwa kuliko wengineo.
Na Manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani!
Ni wengi tu. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemsimulia Mtume wake habari za manabii kadhaa na akamwambia:
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلًا مِنْ قَبْلِكَ مِنْهُمْ مَنْ قَصَصْنَا عَلَيْكَ وَمِنْهُمْ مَنْ لَمْ نَقْصُصْ عَلَيْكَ ۗ{78}
Na hakuwajia nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli, kama walivyokukejeli wewe ewe Muhammad. Kwa hiyo lisikutie tabu hilo, si mageni hayo. Ni vita baina ya wapotevu na wanaolingania haki na uadilifu, kila mahali na kila wakati.
Na tuliwaangamiza waliokuwa na nguvu kushinda wao.
Mwenyezi Mungu (s.w.t.) aliwaangamiza mataghuti waliokuwa na nguvu katika umma zilizopita kwa kuwanusuru wema walio wanyonge.
Na mfano wa watu wa zamani umekwishapita.
Yaani tumekusimulia katika Qur’an hali ya waongo wa zamani na jinsi walivyoangamia, ili watu wako wapate funzo.
Na ukiwauliza: Nani aliyeumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi.
Umetangulia mfano wake katika Juz. 21 (29:61), (31:25) na Juz. 24 (39:38)
Ambaye amewafanyia ardhi kuwa tandiko, na akawafanyia ndani yake njia mpate kuongoka. Na ambaye ameteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyokufa. Na hivyo ndivyo mtakavyotolewa.
Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:99), Juz. 13 (13:3) na Juz. 16 (20:53).
Na ambaye ameumba aina zote.
Yaani aina zote za waanyama, mimea na vitu vigumu.
Na akawafanyia jahazi na wanyamahowa mnaowapanda.
Baada ya Mwenyezi Mungu kuwatajia neema ya maji na ardhi na kwamba wao wanakula, kuvaa na kunywa humo, sasa anawatajia neema ya mawasiliano. Ametaja jahazi na wanyama kwa njia ya mfano tu sio kuwa ndio hayo tu; kwa sababu magari na ndege hayakuwa maarufu wakati huo.
Ili mkae vizuri migongoni mwao.
Yaani migongoni mwa hao mnaowapanda.
Kisha mkumbuke neema za Mola wenu mnapokaa sawa sawa juu yao hao mnaowapanda na mseme: Ametakasika aliyemfanya huyu atutumikie, na tusingeliweza kufanya haya wenyewe. Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.
Katika Nahjul-balagha amesema: “Ewe Mola wangu! Ninajilinda kwako na mashaka ya safari, na huzuni ya marejeo na ubaya wa mandhari katika watu wa nyumbani na mali.
Ewe Mola wangu! Hakika wewe ni mwenza safarini na wewe ndiwe wa kuachwa nyuma na familia. Wala hawezi kuyakusanya haya mawili isipokuwa wewe. Kwa sababu mwenye kuachwa nyuma hawezi kuwa mwenza na mwenza hawezi kuachwa nyuma.”
Sheikh Muhammad Abduh anaielezea kauli hiyo ya Imam Ali (a.s.), kwa kusema: “Mwanzo wa maneno haya umepokewa kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) na akayatimiza Amirul-muminin kwa kusema Wala hawezi kuyakusanya…mpaka mwisho. Dhati ya Mwenyezi Mungu iko sawa mahali pote na wakati wote. Kwa hiyo kuwa safarini na kuwa mjini kwake ni sawa.”
وَجَعَلُوا لَهُ مِنْ عِبَادِهِ جُزْءًا ۚ إِنَّ الْإِنْسَانَ لَكَفُورٌ مُبِينٌ {15}
أَمِ اتَّخَذَ مِمَّا يَخْلُقُ بَنَاتٍ وَأَصْفَاكُمْ بِالْبَنِينَ {16}
وَإِذَا بُشِّرَ أَحَدُهُمْ بِمَا ضَرَبَ لِلرَّحْمَٰنِ مَثَلًا ظَلَّ وَجْهُهُ مُسْوَدًّا وَهُوَ كَظِيمٌ {17}
أَوَمَنْ يُنَشَّأُ فِي الْحِلْيَةِ وَهُوَ فِي الْخِصَامِ غَيْرُ مُبِينٍ {18}
وَجَعَلُوا الْمَلَائِكَةَ الَّذِينَ هُمْ عِبَادُ الرَّحْمَٰنِ إِنَاثًا ۚ أَشَهِدُوا خَلْقَهُمْ ۚ سَتُكْتَبُ شَهَادَتُهُمْ وَيُسْأَلُونَ {19}
وَقَالُوا لَوْ شَاءَ الرَّحْمَٰنُ مَا عَبَدْنَاهُمْ ۗ مَا لَهُمْ بِذَٰلِكَ مِنْ عِلْمٍ ۖ إِنْ هُمْ إِلَّا يَخْرُصُونَ {20}
أَمْ آتَيْنَاهُمْ كِتَابًا مِنْ قَبْلِهِ فَهُمْ بِهِ مُسْتَمْسِكُونَ {21}
بَلْ قَالُوا إِنَّا وَجَدْنَا آبَاءَنَا عَلَىٰ أُمَّةٍ وَإِنَّا عَلَىٰ آثَارِهِمْ مُهْتَدُونَ {22}
وَكَذَٰلِكَ مَا أَرْسَلْنَا مِنْ قَبْلِكَ فِي قَرْيَةٍ مِنْ نَذِيرٍ إِلَّا قَالَ مُتْرَفُوهَا إِنَّا وَجَدْنَا آبَاءَنَا عَلَىٰ أُمَّةٍ وَإِنَّا عَلَىٰ آثَارِهِمْ مُقْتَدُونَ {23}
قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكُمْ بِأَهْدَىٰ مِمَّا وَجَدْتُمْ عَلَيْهِ آبَاءَكُمْ ۖ قَالُوا إِنَّا بِمَا أُرْسِلْتُمْ بِهِ كَافِرُونَ {24}
فَانْتَقَمْنَا مِنْهُمْ ۖ فَانْظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُكَذِّبِينَ {25}