Aya 36 – 45: Je, Unaweza Kuwasikilizisha Viziwi
Maana
Anayeifanyia upofu dhikri ya Mwingi wa rehema tutamwekea Shetani kuwa ndiye rafiki yake.
Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni mwadililifu na ni hakimu, hawezi kuwasilitia Shetani waja wake ili awadanganye kuwatia kwenye upotevu na uasi; kisha awaadhibu. Itakuwaje hivyo na hali Yeye ndiye aliyesema:
إِنَّ عِبَادِي لَيْسَ لَكَ عَلَيْهِمْ سُلْطَانٌ إِلَّا مَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْغَاوِينَ {42}
Juz. 14 (15:42).
Akasema tena:
وَمَا رَبُّكَ بِظَلَّامٍ لِلْعَبِيدِ {46}
Kwa hiyo basi maana ya Aya yatakuwa ni mwenye kuitupilia mbali dini ya Mwenyezi Mungu na sharia yake, akafuata matamanio na starehe, Mwenyezi Mungu atamwachia nafsi yake yenye kuamrisha mno uovu na mashetani watu na majini, wamfanye vile watakavyo na kumwongoza kwenye maangamizi. Mwenyezi Mungu hamkatazi mtu mambo maovu kwa nguvu. Umetangulia mfano wake katika Juz. 24 (41:25).
Na hakika wao wanawazuilia Njia.
Yaani hao mashetani wanawazulia watu njia ya uwongofu.
Na wenyewe wanadhani kuwa wameongoka.
Mashetani wanawaongoza wafuasi wao kwenye upotevu na wafuasi wanadhani kuwa wako kwenye uwongofu kwa kuwafuata mashetani. Muovu zaidi katika watu ni yule anayefuata njia ya upotevu na mwenyewe anaitakidi kuwa yuko salama:
قُلْ هَلْ نُنَبِّئُكُمْ بِالْأَخْسَرِينَ أَعْمَالًا {103}
الَّذِينَ ضَلَّ سَعْيُهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَهُمْ يَحْسَبُونَ أَنَّهُمْ يُحْسِنُونَ صُنْعًا {104}
أُولَٰئِكَ الَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِ رَبِّهِمْ وَلِقَائِهِ فَحَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ فَلَا نُقِيمُ لَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَزْنًا {105}
Hata atakapotujia atasema: Laiti ungelikuwako baina yangu na wewe umbali baina ya mashariki na magharibi. Ni urafiki mbaya ulioje?
Yaani kesho mfuasi atamwambia mfuaswa: afadhali ningekuwa mbali sana na wewe, kulikoni urafiki huu mbaya:
إِذْ تَبَرَّأَ الَّذِينَ اتُّبِعُوا مِنَ الَّذِينَ اتَّبَعُوا وَرَأَوُا الْعَذَابَ وَتَقَطَّعَتْ بِهِمُ الْأَسْبَابُ {166}
Na kwa kuwa mlidhulumu, haitawafaa leo kwamba nyinyi mnashirikiana katika adhabu.
Wanaambiwa wafuasi. Maana ni kuwa duniani mtu akipata adhabu na akamuona mwenzake naye anapata adhabu ile basi huwa anapoa kidogo (kifo cha wengi ni arusi), lakini sivyo kwa adhabu ya akhera; inakuwa sawa tu, iwe kwa wafuasi au wafuaswa-kushirikiana kwao hakuwezi kuwapun-guzia chochote wala kuwanufaisha.
Je! Unaweza kumsikilizisha kiziwi, au kumwongoza kipofu na aliyemo katika upotofu ulio wazi?
Starehe zimepiga muhuri kwenye macho yao, nyoyo zao na masikio yao, wataionaje haki na kusikia maneno yao? Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:42), Juz. 20 (27:80) na Juz. 21 (21:52).
Na hata tukikuondoa, Sisi tutalipiza kisasi kwao au tutakuonyesha tuliowaahidi. Nasi bila ya shaka tuna uweza juu yao.
Maneno yanaelekezwa kwa Mtume kuhusiana na washirikina. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hawaachi washirikina walivyo.
Ikiwa mtume atafariki kuelekea kwenye rehema ya Mola wake, kabla ya wao hawajasalimu amri, basi Mwenyezi Mungu atawaadhibu au ikiwa mtume yuko hai basi atampa ushindi juu yao na watanyenyekea amri yake watake wasitake.
Hiyo ilitokea hasa; pale mtume alipoiteka Makka na vigogo wake kusal- imu amri, baada ya kuwa wamemtoa huko kwa hofu na kujificha. Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:46), Juz. 13 (13:40) na Juz. 24 (24:77).
Basi yashike uliyopewa. Hakika wewe uko kwenye Njia iliyonyooka.
Shikamana na Qur’an ewe Muhammad, kwa sababu ni haki, na Mwenyezi Mungu yuko pamoja nawe kwa sababu uko kwenye njia yake iliyo ya sawa. Naye atakutoshea na wanaokufanyia istihzai na inadi.
Na hakika haya ni ukumbusho kwako na kwa kaumu yako.
Yaani Qur’an ni heshima kwako na kwa waarabu, kwa sababu imewainua na ikaeneza utawala wao na lugha yao maghiribi mwa ardhi na mashariki yake; kama tulivyotaja katika Aya ya 4 kwenye Sura hii. Umetangulia mfano wake katika Juz. 17 (21:10).
Na mtakujaulizwa nyinyi waarabu jinsi mlivyoitumia Qur’an; na nyinyi hivi leo mnaipuuza sana; ndio maana mmekua chakula cha kila mwenye tamaa.
Na waulize Mitume wetu tuliowatuma kabla yako: Je! Tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Mwingi wa rehma?
Waulize ewe Muhammad watu wa dini zilizotangulia na mitume kuwa je, wamewahi kumsikia Mtume yoyote aliyeruhusu ushirikina na kuhalisha kuabudiwa masanamu?
Ikiwa mitume wote walilingania Tawhid na kutupilia mbali ushirikina; kama alivyofanya Muhammad, basi kwanini mnanupiga vita mwito wake enyi washirikina?
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا مُوسَىٰ بِآيَاتِنَا إِلَىٰ فِرْعَوْنَ وَمَلَئِهِ فَقَالَ إِنِّي رَسُولُ رَبِّ الْعَالَمِينَ {46}
فَلَمَّا جَاءَهُمْ بِآيَاتِنَا إِذَا هُمْ مِنْهَا يَضْحَكُونَ {47}
وَمَا نُرِيهِمْ مِنْ آيَةٍ إِلَّا هِيَ أَكْبَرُ مِنْ أُخْتِهَا ۖ وَأَخَذْنَاهُمْ بِالْعَذَابِ لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ {48}
وَقَالُوا يَا أَيُّهَ السَّاحِرُ ادْعُ لَنَا رَبَّكَ بِمَا عَهِدَ عِنْدَكَ إِنَّنَا لَمُهْتَدُونَ {49}
فَلَمَّا كَشَفْنَا عَنْهُمُ الْعَذَابَ إِذَا هُمْ يَنْكُثُونَ {50}
وَنَادَىٰ فِرْعَوْنُ فِي قَوْمِهِ قَالَ يَا قَوْمِ أَلَيْسَ لِي مُلْكُ مِصْرَ وَهَٰذِهِ الْأَنْهَارُ تَجْرِي مِنْ تَحْتِي ۖ أَفَلَا تُبْصِرُونَ {51}
أَمْ أَنَا خَيْرٌ مِنْ هَٰذَا الَّذِي هُوَ مَهِينٌ وَلَا يَكَادُ يُبِينُ {52}
فَلَوْلَا أُلْقِيَ عَلَيْهِ أَسْوِرَةٌ مِنْ ذَهَبٍ أَوْ جَاءَ مَعَهُ الْمَلَائِكَةُ مُقْتَرِنِينَ {53}
فَاسْتَخَفَّ قَوْمَهُ فَأَطَاعُوهُ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمًا فَاسِقِينَ {54}
فَلَمَّا آسَفُونَا انْتَقَمْنَا مِنْهُمْ فَأَغْرَقْنَاهُمْ أَجْمَعِينَ {55}
فَجَعَلْنَاهُمْ سَلَفًا وَمَثَلًا لِلْآخِرِينَ {56}