Aya 77 – 87: Je, Umemuona Aliyezikana Ishara Zetu
Maana
Je, umemuona aliyezikana ishara zetu na akasema: Hakika mimi nitapewa mali na watoto.
Imeelezwa katika Hadith na tafsiri kwamaba A’si bin Wail, mzazi wa Amru bin Al’as, aliposikia kuhusu utume, alisema kwa stihzai: Bila shaka mimi huko akhera nitapewa mali na watoto.
Lakini dhahiri ya tamko la Aya linaonyesha kuwa kuna mzandiki fulani aliyesema hivi; ama kuwataja watu majina, hiyo si katika njia ya Qur’an. Mfano wa Aya hii ni kauli ya yule mwenye kitalu aliyesema:
وَلَئِنْ رُدِدْتُ إِلَىٰ رَبِّي لَأَجِدَنَّ خَيْرًا مِنْهَا مُنْقَلَبًا {36}
Ameirudi Mwenyezi Mungu kauli hii kwa kusema:
Kwani yeye amepata habari za ghaibu au amechukua ahadi kwa Mwingi wa rehema.
Amepata wapi habari hizi? Au yeye ana funguo za siri au amechukua ahadi na Mwenyezi Mungu katika hilo?
Hapana! si hivi wala hivyo; isipokuwa yeye ni kafiri muovu. Tutaandika anayoyasema na tutamkunjulia muda wa adhabu Tumezihifadhi kauli zake na tutamzidishia adhabu zaidi ya kufuru yake na uzushi wake.
Na tutamrithi hayo anayoyasema na atatufikia akiwa peke yake, akiwa mtupu na pia tutamnyng’anya mali na watoto alio nao, pale anapokufa na kuangamia na tutamfufua siku ya kiyama akiwa peke yake mtupu; sawa na tulivyomuumba mara ya kwanza.
Na wamechukua miungu mingine ili iwape nguvu. Sivyo kabisa! Kwa sababu mwenye kutaka nguvu kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, basi Mungu humvisha vazi la udhalili.
Wataikataa ibada yao na watakuwa ndio dhidi yao
Yaani hao wanawaabudu wataikataa ibada yao na watakuwa dhidi yao. Tafsiri inayofafanua zaidi Aya hii ni kauli ya Imam Ali (a.s.), katika Nahjulbalagha: Sio mbali anayefuatwa atajitenga na mfuasi na kiongozi na anayeongozwa watafarikiana kwa chuki na watalaaniana watakapokutana.
Mwenyezi Mungu naye amesema:
تَبَرَّأْنَا إِلَيْكَ ۖ مَا كَانُوا إِيَّانَا يَعْبُدُونَ {63}
Kwani huoni kwamba tumewatuma mashetani kwa makafiri wawa- chochee kwa uchochezi.
Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) haingilii kati baina yao na mashetani wanowapa wasiwasi na kuwahadaa na maasi, wala hajiingizi, kwa uweza wake wa kufanya, kumzuia shetani; isipokuwa amewabainishia njia ya kheri na shari na kuwapa uwezo kamili wa kutenda na kuwaacha; anawakataza hili na kuwaamrisha lile; kisha anawaachia hiyari katika watakayoyatenda na kuyaacha.
Kama angeliwanyanyag’anya utashi, basi wangelikuwa wao na miti ni sawa.
Basi usiwafanyie haraka. Sisi tunawahisabia siku.
Yaani, ewe Muhammad, usiwe na haraka ya kuangamia makafiri, kwani maangamizi yao yatakuja tu, lakini Mwenyezi Mungu anawangoja mpaka muda uliotajwa, ili avidhibiti vitendo vyao, kisha aje awalipe, wanayostahili. Kwani hakuna kheri ya kurefuka maisha isipokuwa kwa yule anayeamini na akatenda amali njema, lakini mwenye kukufuru na akafanya maovu, basi maisha yake ni balaa:
وَلَا يَحْسَبَنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا أَنَّمَا نُمْلِي لَهُمْ خَيْرٌ لِأَنْفُسِهِمْ ۚ إِنَّمَا نُمْلِي لَهُمْ لِيَزْدَادُوا إِثْمًا ۚ وَلَهُمْ عَذَابٌ مُهِينٌ {178}
Siku tutakyowakusanya wenye takua kuwa ni wageni wa Mwingi wa rehema
Neno lililotumika katika kufasiri wageni limetokana na neno la kiarabu wafd lenye maana ya wageni wa heshima. Maana ni kuwa wale wanaomtii Mwenyezi Mungu, kesho watakuwa ni wageni wenye kutukuzwa.
Na tutawachunga wahalifu kuwapeleka Jahannam halia ya kuwa na kiu
Waumini watapata makaribisho ya heshima na wahalifu watapata makaribisho ya dharau, kuchungwa kama wanyama wanavyochungwa kwenda kunywa maji; ndivyo wahalifu nao watachungwa kupelekwa kwenye Jahannam.
Hawatakuwa na mamlaka ya uombezi ila wale waliochukua ahadi kwa Mwingi wa rehema.
Kila mwenye kutekeleza ahadi ya Mwenyeezi Mungu na wala asimfanyie hiyana kwenye dogo wala kubwa, basi Mwenyezi Mungu amempa ahadi ya kufuzu na kuokoka na uombezi:
وَأَوْفُوا بِعَهْدِي أُوفِ بِعَهْدِكُمْ وَإِيَّايَ فَارْهَبُونِ {40}
وَقَالُوا اتَّخَذَ الرَّحْمَٰنُ وَلَدًا {88}
لَقَدْ جِئْتُمْ شَيْئًا إِدًّا {89}
تَكَادُ السَّمَاوَاتُ يَتَفَطَّرْنَ مِنْهُ وَتَنْشَقُّ الْأَرْضُ وَتَخِرُّ الْجِبَالُ هَدًّا {90}
أَنْ دَعَوْا لِلرَّحْمَٰنِ وَلَدًا {91}
وَمَا يَنْبَغِي لِلرَّحْمَٰنِ أَنْ يَتَّخِذَ وَلَدًا {92}
إِنْ كُلُّ مَنْ فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ إِلَّا آتِي الرَّحْمَٰنِ عَبْدًا {93}
لَقَدْ أَحْصَاهُمْ وَعَدَّهُمْ عَدًّا {94}
وَكُلُّهُمْ آتِيهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فَرْدًا {95}
إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ سَيَجْعَلُ لَهُمُ الرَّحْمَٰنُ وُدًّا {96}
فَإِنَّمَا يَسَّرْنَاهُ بِلِسَانِكَ لِتُبَشِّرَ بِهِ الْمُتَّقِينَ وَتُنْذِرَ بِهِ قَوْمًا لُدًّا {97}
وَكَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُمْ مِنْ قَرْنٍ هَلْ تُحِسُّ مِنْهُمْ مِنْ أَحَدٍ أَوْ تَسْمَعُ لَهُمْ رِكْزًا {98}