Aya 42-50: Kila Umma Ulikanusha Mtume Wake Alipowafikia
Maana
Kisha baada yao tukaanzisha karne niyingine.
Baada yao ni baada ya A'd na karne ni watu. Watu wa kwanza kuja baada ya A'd ni Thamud, kwa dalili ya yaliyoelezwa katika Juz. 8 (7:74)
Hapana umma unaoweza kutanguliza ajali yake wala kuikawiza.
Kila kitu isipokuwa, Mwenyezi Mungu (s.w.t), kina muda wake hauchelewi wala kuja haraka. Miongoni mwa hayo ni kuangamia wale waliokadhibisha mitume yao. Adhabu ilikuwa ikawajia ghafla bila ya kutambua wala kuhisi.
Kisha tukawapeleka mitume wetu mmoja baada ya mmoja.
Mitume walikuwa wakija mmoja baada ya mwingine. Kwa sababu Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alijaalia kila umma uwe na mtume.
Kila umma alipowafikia Mtume wao walimkanusha au kumuua. Si kwa lolote ila ni kwa kuwa amekuja na ambayo matamanio yao yanayakataa; kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Kila alipowajia Mtume kwa yale yasiyoyapenda nafsi zenu, mlijivuna, kundi moja mkalikadhibisha na kundi jingine mkaliua." Juz. 1 (2:87)
Tukawafuatishia baadhi yao wengine.
Yaani Mwenyezi Mungu aliangamiza umma uliomkadhibisha Mtume wake mmoja baada ya mwingine na akajaalia ni mazingatio kwa mwenye kuzingatia na habari watayoinukuu kizazi baada ya kizazi kingine.
Ikapotelea mbali kaumu isiyoamini haki wala kuitumia.
Kisha tukamtuma Musa na nduguye Harun pamoja na ishara zetu, kama vile fimbo kugeuka nyoka na kumeremeta mkono, na hoja zilizo wazi za kunyamazisha.
Kwenda kwa Firaun na wakuu wake, lakini wakajivuna na walikuwa ni kaumu waliojikweza.
Kuna kujikweza gani na majivuno makubwa zaidi ya kauli ya Firaun:
فَقَالَ أَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ {24}
Au pale aliposema:
مَا عَلِمْتُ لَكُمْ مِنْ إِلَٰهٍ غَيْرِي {38}
Watu wengi wana moyo kama wa Firaun, wanaweza kudai uungu kama watakuwa na nyenzo na kupata watakaomwitikia kama alivyopata Firaun.
Wakasema: "Je, tuwaamini watu wawili hawa kama sisi, na ambao watu wao ni watumwa wetu?"
Firauni alidai uungu na akawaadhibu waisrail kwa kuwachinja watoto wao wa kiume na kuwaacha wa kike. Na Musa na Harun ni katika waisrail; vipi watawafuata?
Basi wakawakadhibisha wakawa miongoni mwa walioangamizwa. Kila anayepituka mipaka mwisho wake ni maangamizi tu. Na hakika tulimpa Musa Kitabu ili wapate kuongoka.
Makusudio ya Kitabu hapa ni Tawrat na wanaotakiwa kuongoka ni wana wa Israil, lakini hawakuongoka na wala hawataongoka kamwe baada ya kuipotoa Tawrat, wakafuata matamanio yao na wakaijaza dunia ufisadi na upotevu.
Kisa cha Musa kimekaririka mara nyingi kwenye Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Tumebainisha sababu ya kukaririka kisa katika Juz. 16 (20:9) Kifungu cha 'Kukaririka kisa cha Musa.'
Tukamfanya mwana wa Maryam na mama yake kuwa ni ishara.
Yaani muujiza. Isa ni muujiza kwa sababu amezaliwa bila ya Baba na Mama yake ni mujiza kwa vile amezaa bila ya mume. Tazama Juz. 3 (3:45-51).
Na tukawapa kimbilio kwenda mahali palipoinuka. Makusudio ni Palestina, kwa sababu Bwana Masih alizaliwa hapo, napo ni penye utulivu na chemchem za maji.
يَا أَيُّهَا الرُّسُلُ كُلُوا مِنَ الطَّيِّبَاتِ وَاعْمَلُوا صَالِحًا ۖ إِنِّي بِمَا تَعْمَلُونَ عَلِيمٌ {51}
وَإِنَّ هَٰذِهِ أُمَّتُكُمْ أُمَّةً وَاحِدَةً وَأَنَا رَبُّكُمْ فَاتَّقُونِ {52}
فَتَقَطَّعُوا أَمْرَهُمْ بَيْنَهُمْ زُبُرًا ۖ كُلُّ حِزْبٍ بِمَا لَدَيْهِمْ فَرِحُونَ {53}
فَذَرْهُمْ فِي غَمْرَتِهِمْ حَتَّىٰ حِينٍ {54}
أَيَحْسَبُونَ أَنَّمَا نُمِدُّهُمْ بِهِ مِنْ مَالٍ وَبَنِينَ {55}
نُسَارِعُ لَهُمْ فِي الْخَيْرَاتِ ۚ بَلْ لَا يَشْعُرُونَ {56}