Aya 90 – 104: Pepo Kwa Wenye Takua Na Moto Kwa Wapotevu
Maana
Na Bustani (Pepo) itasogezwa kwa wenye takua
Bila shaka iko karibu na mwenye kuongoka na akamcha Mungu na iko mbali na mwenye kupotea.
Na Jahannam itadhihirishwa kwa wapotofu.
Ataidhihirisha Mwenyezi Mungu kwa wale walioikana na kuikadhibisha.
Na wataambiwa wako wapi mliokuwa mkiwaabudu badala ya Mwenyezi Mungu? Na mkiwatarajia kwa siku hii, huku mkisema kuwa mliwabudu ili wawakurubishe kwa Mwenyezi Mungu?
Je, watawasaidia au kujisaidia wenyewe?
Hakika wao hawawezi kuwasaidia wala kujisaidia wenyewe.
Basi watavurumizwa humo wao na wapotofu na majeshi ya Ibilisi yote.
Wao ni hao waungu wao na wapotofu ni wale walioabudu. Mwanajeshi wa Ibilisi ni kila mpotofu na mpotoshaji. Mwenyezi Mungu atawachanganya wote kisha awatupe kwenye shimo la Jahannam.
Watasema na hali ya kuwa wanazozana humo: Wallah! Hakika tulikuwa katika upotevu ulio wazi, tulipowafanya sawa na Mola wa walimwengu wote. Na hawakutupoteza ila wakosefu.
Wapotofu kesho watasema, baada ya kupitwa na wakati, kuwaambia waungu wao na mashetani wao, kwamba nyinyi ndio mliokuwa viongozi wetu wa upofu na upotevu, wakati tulipowaabudu na kuwafanya mko sawa na Mwenyezi Mungu. Na wakosefu ndio waliokuwa kikwazo, ambao ni viongozi wa manufaa na masilahi, asili ya ufisadi na balaa.
Basi hatuna waombezi wala rafiki wa dhati.
Kesho hakuna uombezi wala ugombezi. Hakuna kitakachomfaa mtu isipokuwa moyo ulio salama na amali njema. Na muovu ni yule asiyekuwa na mawili hayo.
Laiti tungepata kurejea tena tungelikuwa katika waumini.
Baada ya kukata tamaaa na kila kitu ndio wanatamani kurudi duniani ili waamiini na kutenda. Mwenyezi Mungu anasema:
وَلَوْ رُدُّوا لَعَادُوا لِمَا نُهُوا عَنْهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ {28}
Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
Imetangulia kwa herufi zake, katika Aya 67 na 68 ya sura hii.
كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ الْمُرْسَلِينَ {105}
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ {106}
إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ {107}
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ {108}
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ {109}
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ {110}
قَالُوا أَنُؤْمِنُ لَكَ وَاتَّبَعَكَ الْأَرْذَلُونَ {111}
قَالَ وَمَا عِلْمِي بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ {112}
إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّي ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ {113}
وَمَا أَنَا بِطَارِدِ الْمُؤْمِنِينَ {114}
إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُبِينٌ {115}
قَالُوا لَئِنْ لَمْ تَنْتَهِ يَا نُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ {116}
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ {117}
فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِي وَمَنْ مَعِيَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ {118}
فَأَنْجَيْنَاهُ وَمَنْ مَعَهُ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ {119}
ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ الْبَاقِينَ {120}
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُمْ مُؤْمِنِينَ {121}
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ {122}