read

Aya 8 – 16: Hawafikirii Nafsi Zao

Maana

Je, hawafikiri katika nafsi zao? Mwenyezi Mungu hakuumba mbingu na ardhi na vilivyomo kati yake ila kwa haki.

Mwenyezi Mungu ni mwenye hekima haumbi kitu chochote isipokuwa kwa haki, na upuuzi kwake ni muhali. Yeye ni Muweza wa kuwarudishia watu uhai baada ya kwisha muda wake uliopangwa.

Mwenye kuangalia vizuri ukuu wa ulimwengu atatambua hekima ya Mwenyezi Mungu katika uumbaji wake na atatambua uweza wake wa kufufua wafu. Kwa sababu kuumba mbingu na ardhi ni kukubwa kuliko kumrudishia uhai mtu baada ya mauti.

“Je! hawaoni kwamba Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi na hakuchoka kwa kuziumba, ana uwezo wa kuwafufua wafu? Ndio! Hakika yeye ni muweza wa kil kitu” (46:33).

Na kwa hakika watu wengi ni wenye kukataa kuwa watakutana na Mola wao.

Wanakataa kuwa ana uweza wa kurudisha uhai na hawajui kwamba anayeweza kuuanzisha anaweza pia kuurudisha? Kwa vile sababu ni moja tu.

Je hawatembei katika ardhi wakaona ulivyokuwa mwisho wa wale waliokuwa kabla yao? Walikuwa wenye nguvu zaidi kuliko wao.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 4 (3:137).

Na wakiilima ardhi na kuistawisha zaidi kuliko walivyoistawisha wao. Na mitume wao wakawajia na dalili zilizo wazi. Basi hakuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wakijidhulumu wenyewe.

Watu wa umma zilizopita walikuwa na maendeleo zaidi ya kilimo na majumba kuliko waarabu, lakini walipodhulumu nafsi zao kwa kufuru yao na kuwakadhibisha kwao mitume, Mwenyezi Mungu aliwapatiliza kwa adhabu na maangamizi. Je, hawaogopi wanaomkadhibisha Muhammad kuwapata yaliyowapata waliokuwa na nguvu zaidi.

Kisha ukawa mwisho wa waliofanya ubaya ni kuzikanusha ishara za

Mwenyezi Mungu na wakawa wanazifanyia stihzai.

Mitume wao waliwajia kwa ubainifu ili wawaokoe na upotevu na kuangamia. Wakawafanyia uovu kwa kuwakadhibisha na kuwafanyia stihizai. Ikawa malipo yao ni adhabu na marejeo mabaya.

Mwenyezi Mungu huaanzisha uumbaji na kisha akaurudisha. Na kisha mtarejeshwa kwake.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 20 (29:19).

Na siku itakaposimama Saa wakosefu watakata tamaa.

Siku hiyo ya Kiyama watajua wenye makosa kwamba hakuna mategemeo wala ujanja kwa aliyetanguliza maasi na kuipa muda toba. Wataonja uchungu wa kukata tamaa kwa sababu walizama kwenye upotevu na wakaung’ang’ania.

Wala hawatakuwa na waombezi miongoni mwa waliokuwa wakiwashirikisha nao watawakana washirika wao.

Walikuwa na wale wanaowashirikisha pamoja na Mwenyezi Mungu duni- ani, wakiwafuata kwenye upotevu na ufisadi kwa ujinga na uigizaji. Walikuwa wakiwatarajia kuwanufaisha na kuwaombea siku ya Kiyama. Lakini watakapokusanyika kwa Mwenyezi Mungu wote na kuiona adhabu na kuhakikisha kuwa hakuna utetezi, basi hapo mfuaswa atajitenga na mfuasi na kiongozi na anayeongozwa.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 2 (2:166 – 167).

Na siku itakaposimama Saa, siku hiyo watagawanyika.

Yaani watagawanyika, wengine ni wa Peponi na wengine ni wa motoni. Yaani wao duniani walikuwa wakikutana sokoni kwenye vyama, masomoni, sehemu za ibada n.k. Lakini siku ya Kiyama hakuna tena makutano.

Ama wale ambao wameamini na wakatenda mema watakuwa katika Bustani wakifurahishwa. Na ama wale ambao wamekufuru na wakazikadhibisha ishara zetu na mkutano wa Akhera, basi hao watahudhurishwa katika adhabu.

Mwenyezi Mungu kesho atawafufua viumbe, awakusanye kwa maswali anayotaka kuwauliza, kisha atawafanya makundi mawili: Kundi la watu wa shirki na la watu wa heri. Hawa atawaneemesha kwa makazi mazuri na Pepo zenye neema; na wale atawaadhibu kwa kuwatia katika moto wa Jahannam.

فَسُبْحَانَ اللَّهِ حِينَ تُمْسُونَ وَحِينَ تُصْبِحُونَ {17}

Basi mtakaseni Mwenyezi Mungu mnapofikia jioni na mnapofikia asubuhi.

وَلَهُ الْحَمْدُ فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَعَشِيًّا وَحِينَ تُظْهِرُونَ {18}

Na sifa njema zote ni zake katika mbingu na ardhi na jioni na mnapofikia mchana.

يُخْرِجُ الْحَيَّ مِنَ الْمَيِّتِ وَيُخْرِجُ الْمَيِّتَ مِنَ الْحَيِّ وَيُحْيِي الْأَرْضَ بَعْدَ مَوْتِهَا ۚ وَكَذَٰلِكَ تُخْرَجُونَ {19}

Hukitoa kilicho hai kutokana na kilichokufa, na hukitoa kilichokufa kutokana na kilicho hai. Na huhuisha ardhi baada ya kufa kwake. Na kama hivyo ndivyo mtakavyotolewa.

وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَكُمْ مِنْ تُرَابٍ ثُمَّ إِذَا أَنْتُمْ بَشَرٌ تَنْتَشِرُونَ {20}

Na katika ishara zake ni kuwa amewaumba kwa udongo; kisha mmekuwa watu mnaoenea.

وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُمْ مِنْ أَنْفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُمْ مَوَدَّةً وَرَحْمَةً ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ {21}

Na katika ishara zake ni kuwaumbia wake zenu kutokana na nafsi zenu. Ili mpate utulivu kwao. Na akajaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya kuna ishara kwa watu wanaofikiri.

وَمِنْ آيَاتِهِ خَلْقُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافُ أَلْسِنَتِكُمْ وَأَلْوَانِكُمْ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِلْعَالِمِينَ {22}

Na katika ishara zake ni kuumba mbingu na ardhi. Na kutofautiana ndimi zenu na rangi zenu. Hakika katika hayo kuna ishara kwa wenye elimu.

وَمِنْ آيَاتِهِ مَنَامُكُمْ بِاللَّيْلِ وَالنَّهَارِ وَابْتِغَاؤُكُمْ مِنْ فَضْلِهِ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِقَوْمٍ يَسْمَعُونَ {23}

Na katika ishara zake ni kulala kwenu usiku na mchana, na kutafuta kwenu fadhila zake. Hakika katika hayo kuna ishara kwa watu wanaosikia.

وَمِنْ آيَاتِهِ يُرِيكُمُ الْبَرْقَ خَوْفًا وَطَمَعًا وَيُنَزِّلُ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَيُحْيِي بِهِ الْأَرْضَ بَعْدَ مَوْتِهَا ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِقَوْمٍ يَعْقِلُونَ {24}

Na katika Ishara zake ni kuwaonyesha umeme kwa hofu na tamaa, na kuwateremshia maji kutoka mbinguni na kwayo akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake. Hakika katika hayo kuna ishara kwa watu wenye akili.

وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ تَقُومَ السَّمَاءُ وَالْأَرْضُ بِأَمْرِهِ ۚ ثُمَّ إِذَا دَعَاكُمْ دَعْوَةً مِنَ الْأَرْضِ إِذَا أَنْتُمْ تَخْرُجُونَ {25}

Na katika Ishara zake ni kusimama mbingu kwa amri yake. Kisha atakapowaita mwito mmoja tu, hapo mtatoka kwenye ardhi.