Orodha Ya Vitabu Vitabu Vingine Vinavyohusiana Na Ulinganishaji Baina Ya Uislamu Na Ukristo

• Ahmad, Khurshid. Islam and the West. Lahore, Pakistan: Islamic Publications, Ltd., 1986.

• Ajijole, A.D.A. Myth of the Cross. Chicago: Kazi Publications, 1979.

• Al-Johani, Dr. Maneh Hammad. The Truth About Jesus. Riyadh, Saudi Arabia: World Assembly of Muslim Youth, 1987.

• All Scripture Is Inspired of God and Beneficial. Watch Tower Bible and Tract Society. Brooklyn (NY): WTBTS, 1990.

• Andry, Carl Franklin, Ph. D. Jesus and the Four Gospels. Muncie. IN: Print press, 1978.

Swahili

Hitimisho

Katika kitabu chake "Basic Christianity" (Ukristo wa Msingi) mwandishi John Stott anasema:

"Kimsingi Ukristo ni Kristo. Nafsi na kazi ya Yesu ni jiwe la msingi ambapo juu yake imejengwa imani ya Ukristo. Na kama siye alisema kuwa ni yeye (ikiwa sio yeye aliyejitangaza kuwa ni Yesu kristo). Na kama hakufanya yale aliyosema alikuja kufanya, jengo zima la Ukristo litaporomoka na kuanguka chini".1

Swahili

Madhehebu Katika Ukristo

Japo Uislamu pia umegawanyika katika makundi mawili ya Sunni na Shia, lakini mgawanyiko huu ni wa kisiasa, sio wa kidini. Katika Ukristo mgawanyiko ni wa kidini. Japo wote wanamuamini Mungu, lakini tusimsahau Yesu - - - mambo yanakhitilafiana kuanzia hapa.

Swahili

Ukristo Na Uislamu

Kwa namna yao ya kufikiri, Mungu aliwafanya Wayahudi kuwa ni watu wake wateule. Kwa hadhi hii waliyopewa Wayahudi, ilimanisha kwamba ni wao tu (Wayahudi) waliotengwa na Mungu kwa ajili ya kuteremshia ufunuo na kupata Mitume wa Mungu kutoka miongoni mwao. Kwa hiyo Wakristo wanahisi kwamba wanaweza kumwamini tu Mtume ambaye ni Mwisraeli, na kwamba wengine wote ni walaghai.

Swahili

Imani Halisi Ya Kumuamini Na Kumpwekesha Mwenyezi Mungu Mmoja Imehuishwa

"Kwa hiyo nawaambieni, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, na litapewa taifa jingine lenye kuzaa matunda". (Mathayo 21:43)

Wafuasi wa Yesu walifurahia sana maelezo haya wakiamini kuwa wao ni "Watu wateule" wapya wa Mungu. Hata hivyo, ukristo unaendelea kupotea kutoka katika njia iliyonyooka.

Mpaka kufikia karne ya nne, ukristo ulikuwa umejiimarisha vizuri kama dini, imani na misingi yake ilipangwa vizuri hasa kwa vile ulikuwa ndio Hukumu na mwongozo wa Maandiko kwa wafuasi wake.

Swahili

Uchunguzi Makini Juu Ya Agano Jipya

Ambapo Agano la kale lina umuhimu mkubwa sana kwa Wayahudi, kwa Wakristo halina nafasi muhimu kiasi hicho ambapo wao wanaliona kuwa kwa sehemu kubwa ni mkusanyiko wa utabiri wa manabii juu ya kuja kwa Yesu. Amri na mafundisho yake hayana uthabiti wala umuhimu wowote kwao.

Swahili

Maandiko Matakatifu Ya Kikristo

Dini iliyofunuliwa kutoka kwa Mungu ina nguvu na inakubalika sawa sawa na vile ufunuo ulivyo na nguvu na unavyokubalika. Kwa upande wa ukristo, msingi huu ambao ni mkubwa na mkuu kuliko yote ni dhaifu kabisa kutokana na kuingizwa mikono na akili za watu ndani ya Biblia. Ufunuo hauna mushkeli, tatizo ni juu ya nini kilitokea baina ya muda ufunuo ulipoteremka mpaka kipindi ufunuo huu ulipoandikwa.

Swahili

Uchunguzi Juu Ya Misingi, Mafundisho Na Imani Za Kikristo

Wayahudi walifanikiwa kuyazimisha mafundisho ya Yesu; lakini si Wayahudi tu bali hata dini ya Ukristo tuliyo nayo leo ambayo mafundisho na imani zake zote muhimu zimeanzishwa na Paulo pia imeyafutilia mbali mafundisho na imani zote zilizofundishwa na Yesu. Licha ya hoja zozote zinazoweza kutolewa na mkristo, hatuwezi kupata ushahidi wowote ambapo Yesu amethibitisha au kazitaja imani hizi nne (uungu wa Yesu, Utatu Mtakatifu, kufa kwa Yesu kwa ajili ya dhambi za wanadamu, na uokovu kwa imani peke yake) katika Injili.

Swahili

Mtazamo wa Uislamu

Mungu alimtuma Yesu kwa Wayahudi kwa sababu waliiacha ibada ya Mwenyezi Mungu kwa madai na visingizio kwamba wanafuata sherehe na uchambuzi wa kina wa sheria. Vitabu 63 vya Talmud - ambavyo ni tafsiri na uchambuzi wa sheria ya kiyahudi - ni uthibitisho juu ya jambo hili. Wayahudi waliamini kwamba wokovu unapatikana kwa kutii sheria ya Mungu.

Swahili

Mtazamo wa Uislamu Juu ya Dhambi Ya Asili

Uislamu inaichukulia imani ya dhambi ya asili na kifo cha Yesu kama inavyoaminiwa na Wakristo kama ifuatavyo:

1) Dhana ya Dhambi ya Asili

Imani ya ukristo juu ya dhambi ya asili haina nafasi yoyote katika Uislamu, kwani Waislamu wanaamini kwamba mwanadamu huzaliwa akiwa hana dhambi yoyote. Ndani ya Qur'an, Mwenyezi Mungu anasema:

"Uelekeze uso wako katika dini iliyokuwa sawa ambayo Allah amemuumbia mwanadamu, ambayo inawiana na maumbile ya mwanaadamu". (Qur'an 30.30)

Swahili