(10). Bahlul Na Harun Kwenda Kuoga Pamoja
Ilitokea siku moja Bahlul na Harun Rashid kukutana katika Hammam (majumba ya kuogea).
Khalifa alimfanyia mzaha kumwuliza Bahlul:
"Je iwapo ningalikuwa mtumwa, ningalikuwa na thamani gani?"
Bahlul alimjibu:
"Dinar hamsini."
Harun Rashid katika kughadhabika alisema:
"Ewe Mwehu! itawezekanaje hivyo? Mavazi yangu tu yamezidi thamani hiyo!”
Hapo Bahlul alimwambia:
"Kwa hakika mimi nimesema kuwa hiyo ni thamani ya nguo zako tu ama Khalifa hana thamani yoyote!"